Hii ndio (CV) Wasifu ya Nape Moses Nnauye

Hii ndio (CV) Wasifu ya Nape Moses Nnauye

Naelewa kabisa kulinganisha elimu ya Nape na Mnyika hakutusaidii lolote hapa wakati tukiwa kwenye msiba mkali wa watoto wetu kufeli kupita maelezo. Lakini cha kushangaza ni jinsi gani mtu anakula MSWAKI (F) wa Civics kisha anakuwa katibu mwenezi wa chama cha siasa....lol, maendeleo ya JK. Huu ushuhuda uko Tanzania ambako ndege ilifunga breki angani na kutoa vumbi ikiwa angani.

Civic inamhusu nini? Anaiujua na kuielewa katiba ya CCM na ilani za uchaguzi za CCM kwetu inatosha sana na anatekeleza majukumu yake ipasavyo mna lazaidi????????????????????
 
Hao wana athari kuliko Pro.Majembee cjui maghembe au Pro.WichDoctor maji mafup
 

Asante, lakini hii Masters ya juzi 2011 wakati akiwa kigogo tayari haina mvuto, vyeti vyake vya form four na form six vipo wapi?? kama alifeli akaghushi, au alienda chuo kikuu pasipostahili basi ana la kujibu. Na ukimya wake hauna ishara nzuri....weka hii karatasi pembeni, leta za sekondari na hata hizo certificate, diploma...kama zile zina migogoro basi hata hii ni haina maana.
 
Sasa jaman ukimaliza form six halaf ukaenda kusoma diploma maana yake uliliwa kichwa katika matokeo! Then ukaenda india kwa digrii, huko ndo kweny digrii za vyuo feki vya kitaa, kuna vyuo vya kata kama zilizovyo sekondary zetu za kata!
 
tehe...tehe...tehe.Nape kasoma EGM BUTIMBA TTC.kwa walio kiona cheti cha Nape fm4 na cha Myika mtajua nani ni Genius na nani MLOPOKAJI.in short MNYIKA ANA A 7. shule alizosoma tunazijua.si wenye digrii za nyumbani kwa watu huko INDIA.
 
hovyo kabisa! Mie naomba nape afanye paper ya form four 2012, akipata above 25% kwa kila somo mods mnipe lIfe ban,

Sent from my nokia 3310 using JamiiForums
 
Tarehe za kwenye CV na cheti haziendani.
CV 2009-2010; Cheti 2011 (December).

Alimaliza lini Mzumbe?

hii inawezekana kwa sababu ceremony ya kukabidhiwa hiyo degree ndio ilifanyika 2011 kama ilivyoandikwa hapo kwenye cheti...tatizo lipo kwenye tuhuma za kughushi vyeti darasa la 7, form 4 na six na hizo diploma za mwaka mmoja mmoja etc.. mimi kwa upande wangu hata kama alifeli simlaumu sana kwa hilo, wapo waliofeli waka re seat, wakapass wakaendelea mbele. Mi naona tatizo ni hizi tuhuma za kughushi vyeti na kuingia kwenye digrii ya kwanza bila kuwa na vigezo halafu kufukia hayo yote chini ya carpet la Masters degree....kama ni kweli basi ana la kujibu.
 
Civic inamhusu nini? Anaiujua na kuielewa katiba ya CCM na ilani za uchaguzi za CCM kwetu inatosha sana na anatekeleza majukumu yake ipasavyo mna lazaidi????????????????????

Sasa kama hivyo kwa nini alikuwa anamkalia kooni Mnyika, ambaye anatekeleza majukumu yake pia??
mkuki kwa nguruwe...
 
Kumekuwepo na habari ambayo inavumishwa katika mitandao ya kijamii hasa hapa Jamiiforums kuhusu Elimu ya Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, Itikati na Uenezi, Ndugu Nape Moses Nnauye. Taarifa hiyo kwa kiasi kikubwa inapotosha na kueleza yale ambayo si sahihi kuhusiana na CV ya Kiongozi huyo wa Chama cha Mapinduzi; Kutokana na Hilo, nimeona ni jambo la busara kuwasaidia wanajamvi kwa kuwapa CV iliyo sahihi ya Nape Moses Nnauye kama ifuatavyo;

  • Kati ya mwaka 1987-1989 alianza elimu yake ya msingi katika shule ya Msingi Mwanga-iliyopo Iramba Singida (ambapo alianza darasa la 1 mpaka 3)
  • Mwaka 1989-1993 aliendelea na kumalizia elimu ya msingi katika shule ya Bukumbi iliyopo misungwi Mwanza.(ambako alikuwa ni kati ya wanafunzi watatu “3” kati ya 120 waliochaguliwa sekondari.
  • Mwaka 1994-1995 alianza elimu ya Sekondari katika shule ya kutwa ya Ngudu Sekondari.(ambapo alisoma kidato cha kwanza mpaka cha pili)
  • Mwaka 1995-1997 aliendelea na elimu ya sekondari katika shule ya Bweni ya Sekondari Nsumba iliyopo Mwanza (ambapo aliendelea kidato cha pili mpaka cha nne)
  • Mwaka 1998-2000 alisoma elimu ya juu ya sekondari (advanced level), mchepuo wa EGM na kuhitimu Butimba TTC
  • Mwaka 2001-2002 alisoma Diploma ya sayansi ya jamii katika Chuo Cha sayansi ya Jamii-Kivukoni.
  • Mwaka 2002-2003 alisomea Diploma ya Diplomasia na uhusiano wa Kimataifa –Chuo cha Diplomasia Dar es salaam.
  • Mwaka 2005-2008 alisomea digrii ya Saikolojia, Lugha na Habari katika Chuo Kikuu cha Bangalore-India
  • Mwaka 2009-2010 alisoma digrii ya pili ya utawala (Masters in Public Administration-MPA) katika chuo cha Mzumbe
NB: Ndugu Nape Nnauye akiwa Kivukoni aliandika “thesis” iliyohusu ; VIKWAZO VINAVYOZUIA VIJANA KUSHIRIKI KATIKA SIASA. Na pia akiwa Mzumbe University aliandika kuhusu ; SABABU ZINAZOCHANGIA USHIRIKI WA WAPIGAKURA (ni ipi sababu ya kutojitokeza wapigakura siku ya Kura)

Tupia na matokeo yake ya form four basi.
Somo kwa somo
 
acha wivu. mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni. mbona mnyika amekiri kuwa hana degree!? afadhali huyu an masters

Bora kutokuwa na degree kuliko kuwa na CV ya nepi.A-level EGM Butimba Teacher's Training College?
 
Bora kutokuwa na degree kuliko kuwa na CV ya nepi.A-level EGM Butimba Teacher's Training College?

Hii kitu haipo.
Zaman walikuwa wanasoma half comb.
Miaka ya 1980s.
Halafu jamaa alikuwa na F ya Basic Maths. TandaleOne
Kajipange upya
 
Last edited by a moderator:
mkuu tandale one,wewe ndio umeanzisha mada ya utetezi hapa ingekuwa busara sana kama ungekuwa unajibu na maswali yanayoulizwa hapa.
kama vipi huu uzi hauna tija kama hamna anayetoa ufafanuzi
 
Hivi nyinyi viijana wa Kitanzania ni nani aliewaloga?
Hivi degree ya Mnyika ama matokeo ya form four ya Nape yana uhusiano gani na maisha haya 'magumu' yanayowakabili?
Ni aibu kushinda mitandaoni kujadili matokeo ya Mnyika na Nape wakati mkitoka hapa mnaenda kuvizia chakula majumbani mwa baba zenu, pamoja na kumaliza shule/ vyuo miaka mitatu/minne/mitano iliyopita.
Shallow minds always discuss people, angalieni msije kuta na nyinyi ni kundi hilo.
Mbona kuna mengi ya kujadili kama vile ukosefu wa ajira, matokeo ya kidato cha nne, kuhamia digitali, uhuru wa habari na mengine mengi tu yanayogusa maisha yetu?
MUNGU IBARIKI TANZANIA!
 
Mwenyekiti wao form 4 ya kubuma wanauliza mtu mwenye Masters kweli maajabu yapo Chadema
 
TandaleOne Master of Business Administration na sababu zinazochangia ushiriki wa wapiga kura zina uhusiano gani? Angefanya "Reasons lead to poor performance of public corporations" hii kidogo ingelandana na hiyo master yake @Nnauye Jr

@nape maskini kumbe ni product la Kata na Yeboyebo, ndo maana sijawahi kumsikia hata siku moja akivunja mayai, lugha ni tatizo kwake TandaleOne tuambie nani alikuwa supervisor wake wa MBA lakini akafanya dissertation ya political science?. Ndo maana watu wanahoji uadilifu na uwezo wa Mzumbe kwenye kutoa MBA degree, hiyo topic haiusini kabisa na core course aliyosoma, kwa kifupi alinunua tu cheti cha MBA,
 
Last edited by a moderator:
Tandale One= Nape, swali linabaki pale pale matokeo ya Form four Division 4 point 29 uliwezaje kupata Masters?
 
Back
Top Bottom