Hii ndio (CV) Wasifu ya Nape Moses Nnauye

Hii ndio (CV) Wasifu ya Nape Moses Nnauye

Matokeo ya Nape Nnauye ya Ordinary level secondary education ni Division TWO..,kwa anayetaka kujiridhisha anaweza ku-google mwenyewe NECTA matokeo ya Nsumba Secondary 1997. na hata kwa matokeo mengine pia ambayo Ni ya ndani ya Nchi na kuhusu matokeo ya chuo cha bangalore nayo yapo TCU.,ni jambo la kuuliza na kujibiwa.

Mkuu wangu, kama ungetaka watu wa "google", hata hiyo CV ya huyo mheshimiwa ilikuwa haina sababu ya wewe kuileta humu ndani ya JF. Yeye ni kiongozi mkubwa sana ndani ya CCM. Hivyo taarifa zake naamini lazima zitakuwemo katika tovuti yao ya chama.

Lakini kwa ubinadamu na wema wako kwa wana JF ukataka kuwarahisishia kuupata wasifu wa Bw. Nape, na ukauleta humu ndani ya JF. Basi endelea kuyajibu na hayo mengine kuhusu ufaulu wake.

Wahenga walisema "maji ukiisha yavulia nguo huna budi kuyaoga". Yaoge mkuu, usiyaogope kwani ninaamini unazo taarifa sahihi za huyo mheshimiwa.
Kwa mantiki hiyo, ondoa utata huu mkuu. Weka kila kitu wazi kuwakomesha hao wanaotaka kumchafua Mhe. Nape.
 
Akili ndogo (Nape Nnauye) inajaribu kutawala Akili kubwa (John J Mnyika) tunapelekwa pabaya na CCM
 
hii inawezekana kwa sababu ceremony ya kukabidhiwa hiyo degree ndio ilifanyika 2011 kama ilivyoandikwa hapo kwenye cheti...tatizo lipo kwenye tuhuma za kughushi vyeti darasa la 7, form 4 na six na hizo diploma za mwaka mmoja mmoja etc.. mimi kwa upande wangu hata kama alifeli simlaumu sana kwa hilo, wapo waliofeli waka re seat, wakapass wakaendelea mbele. Mi naona tatizo ni hizi tuhuma za kughushi vyeti na kuingia kwenye digrii ya kwanza bila kuwa na vigezo halafu kufukia hayo yote chini ya carpet la Masters degree....kama ni kweli basi ana la kujibu.

Mwanzoni nilifikiri hivyo - kwamba ni tarehe ya Graduation- lakini kwa historia ya mtajwa, iliyojaa umagumashi, ni vema na hilo likatolewa ufafanuzi. Hata jina tunaambiwa si lake. Kadhulumu haki ya mtanzania - masikini- ya kupata elimu kwa sababu tu ana uwezo. Hii ni kinyume kabisa na haki za binadamu, na ingefaa amefidie huyo kijana na Kinyirimba kwa wizi huu wa kihistoria.
 
Magumashi ya chaguzi yana mwanzo wake! Sasa huyu bwana alimiss qlf lakini akafanya exams za f six! kwenye fsix fake!
 
Acheni kutudanganya bana, hii sio CV hebu kajipange ndo uje upya... kama shule ya msingi tuu alisoma miaka 8 itakuwa sekondary??? alisomea digrii ya Saikolojia, Lugha na Habari katika Chuo Kikuu cha Bangalore-India mh hii degiriii atakuwa nayo peke yake duniani Mwaka 2001-2002 alisoma Diploma,Mwaka 2002-2003 alisomea Diploma, hizi ni diploma au short cources......JIPANGE
Jaribu tena hapo umekwama li...CCM, Unadanganya cv we hujui kudanganya ni kosa kisheria!:nono:
 
hapo ndio watu wanapodondokewa na kitu chenye ncha kali.. tunaomba na wengine mnapokuja na siasa za elimu zenu msisahau kuonyesha kipengele hicho yaani KIWANGO CHA JUU CHA ELIMU YAKO, HATA KAMA STD SEVEN NDIO MAJAALIWA YAKO

Na aliifeka Masters yake in flat 1 year. Very sharp!
 
Akikupa hayo matokeo utakutana na kiambatanisho hapo chini, sasa jiulize F ya Maths na bado amesoma EGM
NAPE NNAUYE
DIV IV-29
KISW D, HIST D, GEOG D, ENG F, B/MATH F, BIOL D, CHEM D, PHY D, CIV F
Hivi anaruhusiwa mtu kusoma form 6 wakati ufaulu wake wa form 4 ulikuwa na average ya minus D?

Tanzania haiishi kunishangaza.
 
Jamani huyu mtu mpaka kusoma vidiploma inamaana matokeo yake hayakumruhusu kwenda digrii moja kwa moja! Kama anaweza aweke tokeo la form 4 na 6
 
Butimba TTC ni shule ya sekondari???????
Na hizo Diploma za mwaka mmoja mmoja ni certificates ama?????
Haya matango hamna kitu kajipange nae mje tena
 
napegwe jitu patel....
ahahahhhhhhahah......euuuuuuwiiiiiii.........napegwe j.p. ahhhhhhhhhhhhhhhhj....
 
Ukweli imebidi nisome mara mbili mbili kujiridhisha Butimba TTC,halafu kuna EGM:nono:

hamjamuelewa..ni hv katika vyuo vingi vya ualimu kuna kua na vituo vya private candidate(credit fighters) so mheshiwa alikwenda ku resit pepa alivyopata credt akafanya tena mtihani wa 4m6 kama private hapo butimba ttc...
 
Kumekuwepo na habari ambayo inavumishwa katika mitandao ya kijamii hasa hapa Jamiiforums kuhusu Elimu ya Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, Itikati na Uenezi, Ndugu Nape Moses Nnauye. Taarifa hiyo kwa kiasi kikubwa inapotosha na kueleza yale ambayo si sahihi kuhusiana na CV ya Kiongozi huyo wa Chama cha Mapinduzi; Kutokana na Hilo, nimeona ni jambo la busara kuwasaidia wanajamvi kwa kuwapa CV iliyo sahihi ya Nape Moses Nnauye kama ifuatavyo;

  • Kati ya mwaka 1987-1989 alianza elimu yake ya msingi katika shule ya Msingi Mwanga-iliyopo Iramba Singida (ambapo alianza darasa la 1 mpaka 3)
  • Mwaka 1989-1993 aliendelea na kumalizia elimu ya msingi katika shule ya Bukumbi iliyopo misungwi Mwanza.(ambako alikuwa ni kati ya wanafunzi watatu “3” kati ya 120 waliochaguliwa sekondari.
  • Mwaka 1994-1995 alianza elimu ya Sekondari katika shule ya kutwa ya Ngudu Sekondari.(ambapo alisoma kidato cha kwanza mpaka cha pili)
  • Mwaka 1995-1997 aliendelea na elimu ya sekondari katika shule ya Bweni ya Sekondari Nsumba iliyopo Mwanza (ambapo aliendelea kidato cha pili mpaka cha nne)
  • Mwaka 1998-2000 alisoma elimu ya juu ya sekondari (advanced level), mchepuo wa EGM na kuhitimu Butimba TTC
  • Mwaka 2001-2002 alisoma Diploma ya sayansi ya jamii katika Chuo Cha sayansi ya Jamii-Kivukoni.
  • Mwaka 2002-2003 alisomea Diploma ya Diplomasia na uhusiano wa Kimataifa –Chuo cha Diplomasia Dar es salaam.
  • Mwaka 2005-2008 alisomea digrii ya Saikolojia, Lugha na Habari katika Chuo Kikuu cha Bangalore-India
  • Mwaka 2009-2010 alisoma digrii ya pili ya utawala (Masters in Public Administration-MPA) katika chuo cha Mzumbe
NB: Ndugu Nape Nnauye akiwa Kivukoni aliandika “thesis” iliyohusu ; VIKWAZO VINAVYOZUIA VIJANA KUSHIRIKI KATIKA SIASA. Na pia akiwa Mzumbe University aliandika kuhusu ; SABABU ZINAZOCHANGIA USHIRIKI WA WAPIGAKURA (ni ipi sababu ya kutojitokeza wapigakura siku ya Kura)
tujulishe basi alipata ngapi form four
 
Nadhani alifanya kama private candidate butimba ttc hakukuwa na a level
 
Ili kukata mzizi wa fitna, tunaomba mdahalo kati ya mh.J .J mnyika na ndugu Nape. Nina uhakika hapo tutapata kujua mbivu na mbichi!
 
Kumekuwepo na habari ambayo inavumishwa katika mitandao ya kijamii hasa hapa Jamiiforums kuhusu Elimu ya Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, Itikati na Uenezi, Ndugu Nape Moses Nnauye. Taarifa hiyo kwa kiasi kikubwa inapotosha na kueleza yale ambayo si sahihi kuhusiana na CV ya Kiongozi huyo wa Chama cha Mapinduzi; Kutokana na Hilo, nimeona ni jambo la busara kuwasaidia wanajamvi kwa kuwapa CV iliyo sahihi ya Nape Moses Nnauye kama ifuatavyo;

  • Kati ya mwaka 1987-1989 alianza elimu yake ya msingi katika shule ya Msingi Mwanga-iliyopo Iramba Singida (ambapo alianza darasa la 1 mpaka 3)
  • Mwaka 1989-1993 aliendelea na kumalizia elimu ya msingi katika shule ya Bukumbi iliyopo misungwi Mwanza.(ambako alikuwa ni kati ya wanafunzi watatu "3" kati ya 120 waliochaguliwa sekondari.
  • Mwaka 1994-1995 alianza elimu ya Sekondari katika shule ya kutwa ya Ngudu Sekondari.(ambapo alisoma kidato cha kwanza mpaka cha pili)
  • Mwaka 1995-1997 aliendelea na elimu ya sekondari katika shule ya Bweni ya Sekondari Nsumba iliyopo Mwanza (ambapo aliendelea kidato cha pili mpaka cha nne)
  • Mwaka 1998-2000 alisoma elimu ya juu ya sekondari (advanced level), mchepuo wa EGM na kuhitimu Butimba TTC
  • Mwaka 2001-2002 alisoma Diploma ya sayansi ya jamii katika Chuo Cha sayansi ya Jamii-Kivukoni.
  • Mwaka 2002-2003 alisomea Diploma ya Diplomasia na uhusiano wa Kimataifa –Chuo cha Diplomasia Dar es salaam.
  • Mwaka 2005-2008 alisomea digrii ya Saikolojia, Lugha na Habari katika Chuo Kikuu cha Bangalore-India
  • Mwaka 2009-2010 alisoma digrii ya pili ya utawala (Masters in Public Administration-MPA) katika chuo cha Mzumbe
NB: Ndugu Nape Nnauye akiwa Kivukoni aliandika "thesis" iliyohusu ; VIKWAZO VINAVYOZUIA VIJANA KUSHIRIKI KATIKA SIASA. Na pia akiwa Mzumbe University aliandika kuhusu ; SABABU ZINAZOCHANGIA USHIRIKI WA WAPIGAKURA (ni ipi sababu ya kutojitokeza wapigakura siku ya Kura)

Tuambie hapo form 4 ulipata grade gani zilizokupeleka form 5??? Tujuze vizuri tuondoe ile tuhuma ya ufisadi wa elimu

 
Kama Nchi imefikia kuwa na vyuo mpaka vya kata ni kusema imefikia pazuri hivyo ni mfano mwema kwa Nchi kama Tanzania! Tukubaliane kwamba ndio ni vyuo vya kata, ila ni vya kata huko India na sio Tanzania! Lau chadema wakichukua nchi, wakafanikiwa kuufanya mfumo wetu wa elimu kuwa kama India yaani vyuo vikuu mpaka vya kata! Wakazalishwa kina Nape chekwaa mtaani katika vyuo hivo hapa hapa Tanzania haitakuwa jambo la kujivunia kweli kwa CDM? Au ndio yaleyale ya akutukanae hakuchagulii tusi? Binafsi sioni faida yoyote kuendelea kujadili Elimu ya Nape wala Mnyika! Ingekuwa vyema wasomi wetu mngejikita katika kujadili ni kwa namna gani jinamizi hili (la kufeli kwa vijana wetu) litaondoka hapa kwetu nyumbani Tanzania kwa kuchukua hatua hizi na zile! Hizi siasa zisitufanye tuwe wavivu wa kufikiri hata tukakosa muda wa kujadili mambo ya msingi yenye faida kwa Taifa letu!

Sasa jaman ukimaliza form six halaf ukaenda kusoma diploma maana yake uliliwa kichwa katika matokeo! Then ukaenda india kwa digrii, huko ndo kweny digrii za vyuo feki vya kitaa, kuna vyuo vya kata kama zilizovyo sekondary zetu za kata!
 
Back
Top Bottom