Uchaguzi 2020 Hii ndiyo fursa pekee kwa wapinzani kuidai Tume mpya ya uchaguzi iliyo huru hadi ipatikane

Uchaguzi 2020 Hii ndiyo fursa pekee kwa wapinzani kuidai Tume mpya ya uchaguzi iliyo huru hadi ipatikane

Mystery

JF-Expert Member
Joined
Mar 8, 2012
Posts
15,843
Reaction score
31,057
Wakati dunia nzima ikishuhudia uhuni wa hali ya juu, unaofanywa na serikali ya CCM katika kuekekea uchaguzi wa serikali za mitaa unaotarajiwa kufanyika tarehe 24 mwezi huu, vyama vya upinzani nchini, wananchi walio wengi pamoja na viongozi wa dini, wameendelea kutoa mwito kwa Serikali, kuuahirisha uchaguzi huo, ili kutoa fursa ya kukaa pamoja, kutafuta maridhiano kwa uchaguzi huo ambao umevuruguka kwa kiasi kikubwa sana.

Vyama vya upinzani vilivyojitoa kwenye kinyanganyiro hicho, wanadai kuwa kulikuwa na ukiukwaji mkubwa sana, wa kanuni zinazoendesha uchaguzi ulio huru, kuanzia wakati wa zoezi la uandikishaji wa wapiga kura, zoezi zima la uchukuwaji wa fomu za kugombea, hadi wakati wa kuzirejesha fomu hizo, ambapo wagombea zaidi ya asilimia 95, kutoka vyama vya upinzani, waliambiwa na hawa wasimamizi wa uchaguzi, ambao ni makada kindakindaki wa CCM, kuwa hawana sifa za kugombea.

Wakati huo huo hao wasimamizi wa uchaguzi, wakionyesha upendeleo wa wazi kabisa kwa wagombea wa chama chao chao cha CCM, ambapo wagombea wake wote, kwa asilimia 100, wakapitishwa kuwa wagombea halali wa chama chao.

Hivi katika mazingira hayo, ubabe huu unaoonyeshwa na utawala huu wa CCM wa awamu ya tano, wa kutotaka kuwasikiliza wapinzani.hoja zao, hakika unaweza leta machafuko makubwa sana ndani ya nchi hii.

Ifahamike pia kuwa, uchaguzi ulio huru na haki, kwa kutumia sanduku la kura ndiyo njia pekee na iliyo salama zaidi ya kudumisha hali ya amani na utulivu katika nchi yetu.

Inaonekana wazi kuwa watawala wetu wamelewa waadaraka na wameamua kuweka pamba masikioni na kutotaka kusikiliza maridhiano ya aina yoyote na vyama vya upinzani yanafikiwa na badala yake wamekuwa wakitoa vitisho vya hali ya juu, kuwa yeyote atakayeleta fujo wakati wa uchaguzi, Jeshi la Polisi nchini "limeagizwa" na watawala wetu, wawashughulikie kikamilifu.

Hivi ni kwanini watawala wetu wameamua kulewa madaraka kiasi hicho?

Katika uchaguzi ambao dunia nzima inauona kuwa wapinzani wa nchi hii wamefanyiwa hila nyingi, ni kwanini hawataki kuuahirisha na kukaa meza moja na wapinzani na kuwasikiliza wapinzani hao ili kufikia maridhiano?

Hivi huu utawala utaendelea kulitumia hilo Jeshi "lao" la Polisi kukandamiza haki za msingi za raia hadi lini?

Ndiyo maana nikasema vyama vya siasa vya upinzani ni vyema vikaitumia hii fursa bila ya kukata tamaa kudai hiyo Tume ya uchaguzi iliyo huru.

Siyo vyema hata kidogo kukata tamaa na kutishwa na hilo Jeshi "lao" la Polisi nchini, kwani mamilioni ya Umma wa watanzania yapo nyuma yenu, katika kudai Tume hiyo iliyo huru, hadi ipatikane.
 
Niko na wewe, THEN, HOW DO WAPINZANI MOVE FORWARD? Hujatoa suluhisho, hizo ni well wishes ambazo ni nzuri, lakini siyo suluhisho. Nafasi ya kudai tume huru ni hii kwa vipi? Iko wapi? waitumieje?

Mfano, during independence strugle, vyama vya kupigania uhuru vili opt armed strugle na wakaweka modalities za kuanzisha armed strugle. Ndio wakaja say Tanzania kupata misaad etc. Sasa wewe nafasi hiyo ni ipi na itumikeje?
 
Hivi inakuwaje kwa Jeshi letu la Polisi ambalo uendeshaji wake unatokana na kodi zetu watanzania wote, wakiwemo wanaccm na wana Chadema, litumike visivyo kwa kukandamiza haki za msingi wa raia wa nchi hii??
 
Niko na wewe, THEN, HOW DO WAPINZANI MOVE FORWARD? Hujatoa suluhisho, hizo ni well wishes ambazo ni nzuri, lakini siyo suluhisho. Nafasi ya kudai tume huru ni hii kwa vipi? Iko wapi? waitumieje?
Mfano, during independence strugle, vyama vya kupigania uhuru vili opt armed strugle na wakaweka modalities za kuanzisha armed strugle. Ndio wakaja say Tanzania kupata misaad etc. Sasa wewe nafasi hiyo ni ipi na itumikeje?
Ni wazi kuwa kwa utawala huu ulioamua kutumia ubabe na vitisho kwa wananchi wake, kwa kulitumia Jeshi letu la Polisi, inakuwa ni ngumu sana kuidai hiyo Katiba, ambayo hao watawala wa CCM hawataki kabisa tuipate

Hata hivyo ngoja nikujibu swali lako kuwa tutaipataje hiyo Katiba mpya??

Jibu lake ni kuwa haitakuwa rahisi kuipata, lakini ikiwa tutaji-organize kwa kutumia People's Power, basi hiyo Tume mpya ya Katiba ni lazima itapatikana. Full Stop
 
Hivi inakuwaje kwa Jeshi letu la Polisi ambalo uendeshaji wake unatokana na kodi zetu watanzania wote, wakiwemo wanaccm na wana Chadema, litumike visivyo kwa kukandamiza haki za msingi wa raia wa nchi hii??
Uoga wa waTanganyika ni mtaji kwa watawala hawa wasio na vision. Watu wakikubali kutoa uoga na kukubali kufia haki, kila kitu kinapatikana ikiwemo tume huru, katiba mpya ya wananchi na heshima kwa raia. Otherwise ni huu ushenzi
 
People's Power. Full Stop
People's power ni kwa watu wasiooogopa KUFA, si watanzania... mimi na wewe! Tatizo liko hapo. Inabidi kujenga ujasiri wa kuface RISASI, anapigwa mtu anakufa mbele yako, mnasonga mbele! Tanzania, peoples power tuko tayari? Si leo au kesho!
 
Naunga mkono hoja, japo mimi ni miongoni mwa wale tunaosema NEC ni Tume huru ila sio Shirikishi.

P
 
People's power ni kwa watu wasiooogopa KUFA, si watanzania... mimi na wewe! Tatizo liko hapo. Inabidi kujenga ujasiri wa kuface RISASI, anapigwa mtu anakufa mbele yako, mnasonga mbele! Tanzania, peoples power tuko tayari? Si leo au kesho!
Mimi naamini itafika mahali kutokana na huu ushenzi unaofanywa na hawa watawala wetu, watanzania watajengewa ujasiri na kutoogopa hizo bundiki za hilo Jeshi "lao" la Polisi

Tufahamu kuwa ni lazima watu "wa-sacrifice" kuusaka huo ukombozi
 
NEC ni Tume huru
We need to have a common base of our definition of words! Tukikubaliana hapo, then tutakuja kuona kama kweli tume ni huru au siyo huru!
Mfano: Is a whale a fish? Tukikubaliana characteristics of FISH, then tutakuja kuangalia kama WHALE ana characteristics za fish na tutafikia unambiguous answer!
 
Mimi naamini itafika mahali kutokana na huu ushenzi unaofanywa na hawa watawala wetu, watanzania watajengewa ujasiri na kutoogopa hizo bundiki za hilo Jeshi "lao" la Polisi

Tufahamu kuwa ni lazima watu "wa-sacrifice" kuusaka huo ukombozi
Exactly, lazima kukipenda kifo, then ukombozi utakuja!
 
We need to have a common base of our definition of words! Tukikubaliana hapo, then tutakuja kuona kama kweli tume ni huru au siyo huru!
Mfano: Is a whale a fish? Tukikubaliana characteristics of FISH, then tutakuja kuangalia kama WHALE ana characteristics za fish na tutafikia unambiguous answer!
Naunga mkono hoja, to start with, neno huru ni "independent", bila kuingiliwa. Muundo wa NEC ni independent, haipaswi kuingiliwa, japo sheria yetu ya uchaguzi is a bad law, na hili niliisha lizungumza sana humu
Sheria ya Uchaguzi Ni Bad Law! Kuendelea Kuitumia ni Ujinga ...
lakini kanuni za uchanguzi zimeweka utaratibu mzuri kabisa, very open na transparent kama ifuatavyo
  1. Kabla ya uchaguzi kuanza, mawakala wote wanakagua transparent balot boxes kuwa ni empty na kusaini fomu kuwa wameridhika, na kama kuna mwenye mashaka yoyote anatakiwa kujaza fomu.
  2. Baada ya kujiridhisha they are empty, yanafungwa na lakiri mbele ya mawakala na mawakala wote kusaini.
  3. Kura zinapigwa mbele ya mawakala
  4. Baada ya kukamilika kwa zoezi la upigaji kura, mawakala wote wanajaza fomu, na kuweka any anomalities, na kusaini.
  5. Zoezi la uhesabuji kura linaanza mbele ya mawakala, kila wakala anapewa fomu ya matokeo signed na mawakala wote zoezi likikamilika kila wakala anasaini kuyakubali matokeo, yanabandikwa ukutani, hadi matokeo ya kura za urais.
  6. Mawakala wanayasindikiza matokeo kwa msimamizi wa uchaguzi, anatangaza matokeo ya jumla ambayo kila wakala anayo, mshindi anatangazwa. Hivyo kwa matokeo ya udiwani, yanatangaziwa kwenye kata, kisha wakala anakwenda kwenye jimbo kushuhudia tallying. Kote huku anasaini fomu kila hatua.
  7. Ndipo matokeo ya urais yanapelekwa kwenye national tallying center, huku sasa hakuna mawakala, wale mawakala wa vituoni, bali sasa wanaingia kwenye national taliying ni mawakala wa wagombea urais, kwa vile vyama vyote vinakuwa na matokeo yote ya vituo vyote hivyo kila chama kiko huru kufanya its tallying, kisicho ruhusiwa ni kutangaza national taliying. Kilichofanya zile independent tallying kuvamiwa ni kitendo chao cha kutangaza.
  8. Baada ya national tallying kukamilika, wagombea wanapewa matokeo na kutakiwa kusaini fomu kukubali au kukataa, kisha matokeo ya urais yanatangazwa. Na yakiisha tangazwa, there is nothing anybody can do!.
  9. Masikini Ben Saanane, baada ya kutangazwa matokeo ya NEC, akafanya simple arithmetic ya idadi ya waliojiandikisha, idadi ya waliopiga kura, kura zilizoharibika na jumla ya kura halali za kila mgombea, akakuta numbers didn't tally, idadi ya kura halali ni kubwa kuliko idadi ya wapiga kura, akaanza kuhoji na kutumia iteligensia yake akamtaja mhusika, kilichofuatia is history.
My Take, vyama vya upinzani vilikuwa too poor kuweka mawakala nchi nzima, it was as simple as ABC, mawakala wenye smart phone na zote zinawekwa similar scanning program, hivyo kila wakala anatuma scanned copy ya matokeo ya kila kituo, hivyo kila chama kinakuwa na matokeo yote nchi nzima, na tallying inaweza kufanywa hata na Samsung note phone, kama kuna udanganyifu unakwenda na hard evidence.
Haya yote yalifafanuliwa vizuri na Ramadhani Kailima hapa

P
 
Masikini Ben Saanane, baada ya kutangazwa matokeo ya NEC, akafanya simple arithmetic ya idadi ya waliojiandikisha, idadi ya waliopiga kura, kura zilizoharibika na jumla ya kura halali za kila mgombea, akakuta numbers didn't tally, idadi ya kura halali ni kubwa kuliko idadi ya wapiga kura, akaanza kuhoji na kutumia iteligensia yake akamtaja mhusika, kilichofuatia is history.
Mayalla, utawala wako ukisha kuwa na vitu kama hivi, LOSS OF LIFE, you lose any legitimacy , whatever the so called "maendeleo" unayojidai kuyafanya, go down by the TRENCH!. sasa kama huyaoni hayo basi either na wewe ni muuaji au you are moved na u-home boy (kama ninavyokwambia siku zote). Ukishaua watoto wako ili uweze kumuoa mama yao, basi hufai in all aspects on earth!
 
Back
Top Bottom