Hii ndo Tanzania: Kumbe Hawa wa nitarejea anaumwa moyo sio INI kama madaktari wa Tanzania walivyosema

TRUE KWA 100%. Hilo nami lilipita akilini mwangu lakini naamua kukausha. Sisi Wabongo ni wanafiki kwa viwango vya SGR! Nilikuwa naangalia zile comment kwenye post ya Tale halafu likanijia hilo wazo,nikaogopa!
mana wabongo sisi Nyerere sijui alitulisha nini? hatupendani kabisaaa😁
 
Madaktari wanapiga ramli, wanakutizama usoni wanakuuliza unakunywa gongo unawaambia ndio, wanakuuliza unasikia maumivu wapi unawaambia hapa, wanatizama miguu na tumbo imevimba aaah... wanakonkuludi! INI limeunguzwa na pombe.
😂😂😂😂😂😂😂
 
Acha tu wengi wanakufa kwa kutibiwa kitu ambacho hawaumwii
Nyie kuleni matango pori ya babu tale wenu, hamjaugua nyie kama mnataka kuthibitisha kuwa madaktari wako vzuri ugueni sasa, ana nenda hospitali uombe wagonjwa watoe shuhuda zao, huyo babutale wenu anajua chochote kuhusu udaktari? Subiri mgonjwa arudi baada ya hiyo operasheni mkague na figo kabla ya kurudi, kama hamjaacha figo huko
 
Case kama hiyo ya operation ilifanyika pia kenyata hospital kenya nao unata kusema hawajui?
Nakumbuka kipindi kile mgonjwa wa kichwa alikatwa mguu na yule wa mguu akapasuliwa kichwa! Huko kwenye vizahanati ndio balaa
 
Kweli tuache ujinga kama ni kweli aweke na taatifa za daktari za hapa aache kupotosha umma, la sivyo huyo banu tale wenu akirudi, airport atadakwa kwa kosa la kupottosha umma
Kwahiyo reference yako ni huyo babu Tale sio? Je kabla ya kwenda alikuwa anaudhuria matibabu hospitali gani? Weka report ya Dr
 
Hapo umenena ila wananchi wawe makini na taarifa za hao akina babu tale
 
Hii ilimtokea Mzee wangu mdogo madaktari wa bongo wengi vimeo
 
Ndio maana madaktari wa Tanzania wao hawaandamani kwa kuongezewa mishahara, kwasababu wanajijua ni vilaza.


Ndukiiiii [emoji2089][emoji2089][emoji2089]
[emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Katafute intvw aliyomfanyia Soudybrown, Hawa wakati akijiandaa kwenda India ndio utamuelewa babutale, hajajiropokea kwani Hawa aliongea mwenyewe. Alafu mbona kawaida mimi Kuna kipindi tumbo lilikuwa linauma, nikienda chooni najisaidia kwa shida, nimeenda Amana nikapelekwa wodi ya KIPINDUPINDU (kama ushawahi kukaa kule ndio utaelewa) bahati nzuri mjomba wangu alikuwa mtata, nikatolewa lkn nililala siku moja na nusu na Mshukuru Mungu sikupata maambukizi kwani kule kinyesi unakiona live . Hii kitu isikie sometime wanakosea, wataalam wetu hawapendi kujisomea, wao wakimaliza chuo wanaamini wanajua kila kitu, wanashindwa hata nakuwa na Library ndogo home kwao kujisomea hata masaa mawili kwa siku yanatosha.
 


Ndiyo tatizo la kliniki ama hospitali za uswahilini (private)…..hata Muhimbili unaweza ukaenda ukakutana na daktari kishoka, hajaenda shule wala nini ila yuko tu pale anafanya kazi na watu wanamuangalia tu akipiga hela ndefu na kumuhamkia.
 
Tumuombe Hawa apone ila tusiwashambulie sana madaktari badala yake tuzikumbushe mamlaka zisisahau kuipa kipaumbele hii sekta ya afya hasa vifaa,mafunzo,wataalamu na maslahi bora.
 
Mimi mara nyingi hua nikiumwa nikienda hospital hua wakinipa medicine, situmii kwasababa hua nawaona madaktari na manesi ni vilaza sana kwahiyo hua naona ni waongo...
Kuna jamaa yangu ni foreigner mwanae alikuwa anaumwa madakrari wakawa wanasema ana uvimbe kwenye jia ya haja kubwa kwa ndani wakasema wataptisha sijui nini waukate, akawauliza swali mkishaukata bleeding mtaizuiaje wakabaki wanatazamna. akawambia nyote ni vilaza akaondoka na mwanae huwezi amini mwanae alikuja pona kwa dawa toka over the counter kwa mdada flani tu.
Kuna rafiki yangu mwingine mdogo wake alizaliwa akiwa na jicho kama limevilia madaktari wakasema eti ana kansa walitoe wakampeleka nairobi wakaambiwa hapana hana kansa divyo lilivyo it was in 2007 mpaka leo jamaa mtu mzima hana tatizo.
Madaktari wa TZ wanaua sana watu
 
mana wabongo sisi Nyerere sijui alitulisha nini? hatupendani kabisaaa😁
Yani sijui kwanini wewe angalia tu bei ya korosho mnadani ilivyoshushwa maksudi kutoka kilo 4000 hadi 2100. Yani Mijitu ina wivu kwasababu eti watu wa kusini tutatoka. Yani iliwauma kutuona mambo yetu safi hadi tunawanywesha mbuzi bia
 
Huwa wanasisitiza kupima mara kwa mara ila mimi huwa naogopa sana kupima maana inaweza ikawa ndio mwanzo wa matatizo kwangu
Madr wetu ni shida, watu wa dawa shida zaidi, watu wa mahabara mazingaombwe matupu
 
madaktari wa tanzania sijui wanasoma vyuo gani,maana hata ommy dompos anasema aliambiwa ana cancer ya koho alivyokwenda s.africa anaambiwa ni tatizo la mfumo wa chakula.,tunauana hivi hivi
 
Siku hizi ugingwa mkuu ni UTI, hapo kitambo ilikuwa maralia hata bila kupima. Ndio maana wengine tunaenda hospital mbili mbili kupata opinion. Ukiona majibu hayaja tally unaenda ya tatu🙈
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…