Hii ni moja ya picha ambazo Waingereza hawapendi kuziona

Hii ni moja ya picha ambazo Waingereza hawapendi kuziona

Kwani ni nani haui wapinzani wake?
Kiongozi halisi. Kama kuanzia Mandela maraisi wa Afrika Kusini (hata yule mbaya) hawakuanza kuua. Katika Umoja wa Ulaya simjui aliyeua mpinzani. Vilevile nchi nyingine kote duniani zilizoendelea. Hata Trump....
 
Hii si kweli hata kidogo. Tamasha hii ilipangwa na Bob Astles. Astles alikuwa Mwingereza aliyebaki Uganda baada ya ukoloni akashiriki na serikali ya Obote na kuendesha biashara zake. Alimwoa Mganda kutoka ukoo wa kifalme. Alikuwa na shamba la mananasi. Amin aliposhika utawala 1971 akamtupa gerezani, akamwachisha baadaye. 1975 Amin alimtaka mshauri kwa mawasiliano na nchi za nje akamchagua Astles. Astles alijitahidi sana kumbembeleza Amin kwa kila namna.

Wakati Amin alichaguliwa mwenyekiti wa Umoja wa Afrika (aibu juu ya madikteta wote wa Afrika waliompa kura!) kulikuwa na party. Kwenye nafasi hii Astles alitisha wafanyabiashara Waingereza walioishi Uganda wambebe Amin mbele ya wageni wa Umoja wa Afrika. Baadaye aliamuru idadi ya Waingereza waliokuwa wafanyabiashara Uganda wapige magoti mbele ya Amin. (kwa nini waliitikia? ).

Astles alikuwa hodari kumbembeleza Amin. Alihukumiwa naye hadi mauti mara nne lakini alifaulu kila safari kumbembeleza tena. Baada ya uvamizi wa Tanzania pale Uganda na kurudishwa kwa Obote Astles alitupwa tena jela kwa miaka 4 au 5, hatimaye aliachishwa akarudi Uingereza....

Kuhusu siku zile ambako Astles alipowalazimisha Waingereza wenzake kumbeba Amin, askofu Mwanglikana Mganda Festo Kivengere aliandika: "At the very moment the heads of state were meeting in the conference hall, talking about the lack of human rights in southern Africa, three blocks away, in Amin torture chambers, my countrymen's heads were being smashed with sledge hammers and their legs being chopped off with axes."
Bado unataka kusheherekea picha hii???

(halafu: si kweli Waingereza hawataki kuona picha hii jinsi unavyodai kwenye kichwa cha habari. Bila shaka ilionyeshwa zaidi huko kuliko Tanzania)
Hakika kaka umesoma, unazitetea hoja kwa ushahidi na nukuu
 
Hio Cip yake ilimuudhi wakwanza mzee mnafik Nyerere kwasbb alijikomba saana kwa waingereza,***** Iddi Amin alikuwa mwanaume lkn kwa unafik wa kamzee mchonga wakaanza kumpakazia “Oohh dikteta’” Oohh anaua wananchi wake “ohh anatawala kimabavu
Hakujuona yeye Huyo mzee mchonga alitawala miaka mingapi Tz[emoji38]hadi kakaambiwa mzee achia vingenevyo,,,,[emoji3]
Wakati Amini hakutawala hata miaka mi5
Papo hapo kamzee mchonga hakakujiona kalivotaifisha mali za wananchi wake na kuidudimiza uchumi wa nchi yake kwa kuwatuhumu watu wake wahujumu wa uchumi
Tena kawashkuru hao wazungu vingenevyo vita vya Uganda maji yalikua shingoni[emoji3]kalishazidiwa saana lkn mabeberu A,k,A Wahisani wakampiga tafu[emoji3]
Habari yako imejaa hisia za chuki na upande mwingine mapenzi.

Kwa andiko lako, unaonekana kufurahishwa na Amini na kuchukizwa sana na mwalimu.

Labda ni uzuri upi wa amini uliokufurahisha na kumuona mtu wa kuigwa katika jamii?
 
Habari yako imejaa hisia za chuki na upande mwingine mapenzi.

Kwa andiko lako, unaonekana kufurahishwa na Amini na kuchukizwa sana na mwalimu.

Labda ni uzuri upi wa amini uliokufurahisha na kumuona mtu wa kuigwa katika jamii?
Andiko lake ni kipimo cha ujinga uliojaa kichwani mwake.
 
JINA LA dada ni lake au sia ya udada
Udada? Kumbe. kuna uhusiano wa siri na "Dadaism" ?🙂😵
(Dadaism is closely associated with the concepts of the grotesque, the absurd and the macabre that were communicated through the arts slightly later in the twentieth century. The idea of ridiculing the absurdity of existence finds its most poignant expression through the dramatic art of Samuel Beckett and the so called Paris school of dramatists that included Arthur Adamov, Jean Genet, and Eugene O'Neill. ) https://simple.wikipedia.org/wiki/Dadaism
 
Basi hujadili Amin (aliyechezea pia ngoma ya uzalendo... km alipowapora na kufukuza Waganda Wahindi), unalilia wengine.
Nenda kamsome tna Amin akuwai kucheza uzalendo alichukua maduka na biashara za wahindi kuwapa wezi wenzie...
 
Huyu mwamba nilikuwa namkubali sana sema historia ya uongo inamchafua nyuma ya pazia
Binafsi nilikuwa na mawazo kama yako kuwa Nduli Amini alikuwa anachafuliwa kumbe sivyo. Tafuta kitabu kinachoitwa 'State Of Blood' by Henry Kyemba ndiyo utajua kuwa Amini alikuwa katili na alitafuna nyama za watu.
Henry Kyemba aliwahi kuwa Waziri wa Afya pia Makamu wa rais ktk serikali ya Obote pamoja na serikali ya Amini.
 
Tupo tofauti Binafsi namkubari sna huyu mtu sifa yke kubwa akuwai kuwa Mnafiki alisimamia anacho kiamini. sio tumeibiwa sna tumechezewa sna hlf hakuna lolote Chukua Chako Mapema Ni ile ile...View attachment 1132267
Pole, inaelekea hujui historia nzima ya huyu Nduli Amin. Ktk watu wanafiki sana enzi zake ni pamoja na huyu. Watu walio differ naye, aliwaita ktk ikulu yake na kushikana mikono as if mambo yameisha. Duuh, wakishatoka ikulu walikuwa hawafiki mbali, vijana wa The State Research Bureau lazima wafanye yao; Kesho yake utasikia yeye mwenyewe Amin akihutubia taifa kuwa Askofu Mkuu wa Anglikan - Arch bishop Janan Luwuum na wenzake wamepata ajali mbaya ya gari.
 
Ipi sasa, kwamba hakuvamia Kagera na kudai ni sehemu ya Uganda? kwamba hakuua Wapinzani wake?

labda kama zile za kuua mwanaye ndio hata mimi huwa kama siziaminiamini.

idd amin hakuvamia kagera
sisi ndio tulimvamia ,yeye alifanya kujihami tu kwa kuleta vikosi vyake TZ , lengo lake ilikua ni kumtoa nyerere madarakani kwa sababu nyerere alifadhili vikosi vya kumpindua idd amin zaidi ya mara 2 kwa pesa ya watanzania


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Back
Top Bottom