Hii ni timu bora ya wakati wote, nipinge kwa hoja


[emoji1316]
 
Hi Barca ilikuwa tishio Sana..nikiwakumbuka INIESTA NA XAVI..walikuwa wanakichafua katikati sijapata kuona..laikini walikuwa na tatizo la kubebwa na ma refa..pia kujiangusha angusha.. lakini kwa mpira mzuri walikuwa kiboko kwakweli..
Lakini sisi Chelsea tuliwapa tabu..na mpira wetu wa hovyo hovyo..
 
Brasil 1970
Jairzinho, Tostao, Pele, Carlos Alberto inatajwa kama timu bora ya wakati wote katika fainali za kombe la dunia.

japo kuna wengine wanadai Brazil ile ya 1982 iliyoshiriki fainali za kombe la dunia pale Spain, ilikuwa bora sana ingawa ilishindwa kutwaa ubingwa, iliundwa na mafundi kama Socrates, Zico (Pele Mweupe), Falcao, Eder
 
Hawa jamaa ulikuwa wakijiangusha tu, kuna mtu anaweza kula kadi ya kubandikizwa hapo! 🀣 🀣 🀣 Walidekezwa sana...
 
Kwangu mimi hii ni timu bora ya wakati wote kwa ngazi ya klabu. Walifanya kila kitu katika mchezo wa soka, walinyanyasa timu zote kubwa, ilikuwa ushafungea kabla ya kuingia uwanjani. Unakubaliana na mimi? Karibu kwa hoja
View attachment 1800256
Hii ndio ile barca ambayo Mourinho alimwambia Guardiola "husishangilie subiri filimbi ya mwisho"
Ilikuwa timu nzuri ila walishindwa kumnyanyasa Mourinho.
 
Naunga mkono hoja ila namashaka pale unaposema wakati wote,kivipi wakati wote?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…