Hii style nimeiona kwa wengi mjini

Hii style nimeiona kwa wengi mjini

Hapo unaenda wapi na hiyo barabara ina Mashimo njia nzima au?!

Huwa natoka bunju 39km kuja Posta, kama ni usiku inachukua dakika 27 tu kufika home sababu hakuna foleni...... But mchana inachukua hata lisaa kufika.
 
Hivi mwendo wa nusu saa kwa gari, zinaweza kuwa KM ngapi best?

Sent from my TECNO KA7 using JamiiForums mobile app
Sasa unapimaje umbali kwa kutumia muda mkuu?! Sehemu ambayo unaweza kwenda kwa passo kwa nusu saa Subaru itachukua dakika 10 au 15.


Unaweza tumia umbali kukadilia muda ila sio muda kukadilia umbali.
 
Kupata kiwanja cha kujenga nyumba hasa katika prime area ni changamoto kubwa kwa sisi tunao safiri kuelekea uchumi wa kati. Unakuta pango la mwezi unapokaa ni 350, 000, ukipiga hesabu kwa miaka miwili unaona ni kheri ujenge ya kwako.

Umepata kiwanja kwa milioni 20. Bahati nzuri ulikua na akiba ya milioni 5, benki wakakupa milioni 20 mkopo. Rafiki zangu wengi walichofanya ni kujenga nyumba ya kujistiri nyuma ya kiwanja. Ina basic needs tu na kuhamia.

Mbele ya kiwanja anaweka banda la kuku hawa wa kienyeji na matuta manne ya mchicha. Hapo amepiga mahesabu ya kurudisha mkopo. Watoto wakilalamika wamechoka kula mchicha wanapozwa na kuku. Maharage ndiyo kubadilisha menu.
Sishauri mtu utumie pesa ya mkopo kujenga nyumba ya kuishi ambayo aghalabu pesa hiyo haiwezi kumaliza hiyo nyumba in anyway.

Kopa pesa kafanye biashara, faida ya biashara utarudisha mkopo, itajenga italipa pango la nyumba na kukufanya uishi.
 
Sishauri mtu utumie pesa ya mkopo kujenga nyumba ya kuishi ambayo aghalabu pesa hiyo haiwezi kumaliza hiyo nyumba in anyway.

Kopa pesa kafanye biashara, faida ya biashara utarudisha mkopo, itajenga italipa pango la nyumba na kukufanya uishi.
Mwagona?!
 
Sishauri mtu utumie pesa ya mkopo kujenga nyumba ya kuishi ambayo aghalabu pesa hiyo haiwezi kumaliza hiyo nyumba in anyway.

Kopa pesa kafanye biashara, faida ya biashara utarudisha mkopo, itajenga italipa pango la nyumba na kukufanya uishi.
My point exactly boss...... Unajua nyumba ni investment nzuri only kama ipo town center na kuna wapangaji unaweza pata.... But kama ni ya kuishi tu..... Haina haraka ya kutumia hela ya mkopo kujenga
 
Sishauri mtu utumie pesa ya mkopo kujenga nyumba ya kuishi ambayo aghalabu pesa hiyo haiwezi kumaliza hiyo nyumba in anyway.

Kopa pesa kafanye biashara, faida ya biashara utarudisha mkopo, itajenga italipa pango la nyumba na kukufanya uishi.
Miaka 20 ijayo deni la milioni 20 atakua amemaliza kulilipa na thamani ya kiwanja itakua milioni 200.

Biashara ilifungwa kwa kushindwa kulipa tozo la TRA.
 
Akili kumkichwa kama una uwezo kidogo nunua kiwanja hata porini jenga baada ya miaka 5 unaweza kuta kiwanja ulichonunua kwa 1.5m kinauzwa 15m. Kwa wakati huo utakua mjini. Kuna watu wanajidai kua hawawezi kuhama katikati ya mji but wana vyanzo vizuri vya hela. Wengine wana support toka kwenye familia zao.
Naungana na wewe mia mia,
Mwaka 2010 nilinunua eneo Moshono Barabara ya Moshi-Arusha zamani. Eneo nilipata kwa milioni 4.5.

Nikaanza ujenzi mdogo mdogo hatimaye nikamaliza nikahamia. Miaka 5 baadae rneo lenye ukubwa wa 20x20 bei ni 20M ikipungua sana 15M.

Sasa nimehamishiwa kazi Dar, nafikiria kwenda ndanindani huko Kigamboni nikapate eneo kwanza then mambo mengine yafuate.
 
hakuna sehemu mbali..mbali kutokea wapi...huo ni umaskini wa fikra zako a uchumi wako....uaishi sehemu ambayo utafeel peace of mind...ukiwa na usafiri wako hupati tabu..
 
kwani kulea vizuri ni lazima wewe uteseke,,,point yangu ni kwamba siwezi kujitesa ili nijenge au nijitese ili watt waje waish vizut tutaishi vizur wote uku uku mjini kikiisha bas tutateseka wote
sawa broh
 
Inategemea na eneo ulipo maeneo yenye foleni lolote linaweza kutokea... Ila huku kwetu ukitembea nusu saa barabara ipo clear gari za kuhesabu dakika 30 unaweza kwenda hata kilomita 35... Mbali umehama hadi mji
 
Hapo unaenda wapi na hiyo barabara ina Mashimo njia nzima au?!

Huwa natoka bunju 39km kuja Posta, kama ni usiku inachukua dakika 27 tu kufika home sababu hakuna foleni...... But mchana inachukua hata lisaa kufika.
Inategemea upo wapi, huku kwetu barabara clear, hakuna foleni ukitembea nusu saa unaenda kilomita zaidi ya hizo... Wewe utakuwa unasafiri sasa
 
Hahahhaaa...

Hapo kwenye bia umenigusa.

Imebidi nipunguze sana unywaji ili kuondoa kero ndogo ndogo za hapo kwenye mji wangu.

Unaweza kuacha kunywa bia mbili siku hiyo ukapata nyama robo(mlo mmoja) au sangara nusu watoto wakajilamba.

Unaweza potezea bia kwa wiki moja ukapata pesa ya kujiunga bando.

Yaani ni wewe kucheza na hesabu zako tu alimradi pa kulala papo na hubudhiwi na mtu.
yani hili swala nina imani ipo siku nami ntaweza kuacha
 
Sishauri mtu utumie pesa ya mkopo kujenga nyumba ya kuishi ambayo aghalabu pesa hiyo haiwezi kumaliza hiyo nyumba in anyway.

Kopa pesa kafanye biashara, faida ya biashara utarudisha mkopo, itajenga italipa pango la nyumba na kukufanya uishi.
Biashara za Sahiv umeziona kweli? Uchukue pesa ya mkopo upeleke kwenye biashara siku hizi ni hatari zaidi, unakaribisha ugonjwa wa moyo na kisukari
 
Kupata kiwanja cha kujenga nyumba hasa katika prime area ni changamoto kubwa kwa sisi tunao safiri kuelekea uchumi wa kati. Unakuta pango la mwezi unapokaa ni 350, 000, ukipiga hesabu kwa miaka miwili unaona ni kheri ujenge ya kwako.

Umepata kiwanja kwa milioni 20. Bahati nzuri ulikua na akiba ya milioni 5, benki wakakupa milioni 20 mkopo. Rafiki zangu wengi walichofanya ni kujenga nyumba ya kujistiri nyuma ya kiwanja. Ina basic needs tu na kuhamia.

Mbele ya kiwanja anaweka banda la kuku hawa wa kienyeji na matuta manne ya mchicha. Hapo amepiga mahesabu ya kurudisha mkopo. Watoto wakilalamika wamechoka kula mchicha wanapozwa na kuku. Maharage ndiyo kubadilisha menu.
Wengine tumefanya hivi bila kuwa na kiasi hicho Cha pesa.

Ukishapata kiwanja hata Cha uridhi ukawa na milioni nne au tano tayari umeishi.
 
Nakosa logic kwanini ninunue kiwanja kwa mill 20 nibaki na akiba mil 5 kisha tena nikope mil 20 nijenge banda la uwani,kwamba nilikuwa na cash mil 25 kwanini basi nisingenunua kiwanja kwa 8million (nadhani popote Tanzania hivi viwanja vinapatikana) nikabaki na 17 nikafanya ujenzi wa nyumba kubwa nzima kwa hela hiyo nikainua boma na kupauwa kisha kidogo kidogo kwa ile riba nilikuwa niipeleke bank nikafanya finishing nikiwa humo humo?

Au labda mleta mada sijamuelewa maana maisha ni ya ajabu sana,unaweza kuingia kwenye madeni ya riba za bank ukiwa bado kwenye chumba na sebule yako na ukazeekea humo humo ukiwa hujafanya chochote.
Ndugu 17Mil katika ujenzi wa nyumba kubwa ni ndogo mno. Ukiisikia ujenzi siyo tofali na mchanga na kokoto, ujenzi ni vitu vidogovidogo vingi vinavyotafuna hela kama mchwa kwenye ubao wa mwembe.

Inafikia mahali unatembea unaokota misumari,😂 fundi unamkusanyia ndoo ya udongo wa plasta uliomwagika!

Everyday is Saturday............................... 😎
 
Back
Top Bottom