Hii style ya Harmonize kuchukua beat na kurudia nyimbo atakuwa ametoka nayo huko alikotoka?

Hii style ya Harmonize kuchukua beat na kurudia nyimbo atakuwa ametoka nayo huko alikotoka?

Salama wakuu!

Ipo hivi najua kila mtu ashasikiliza ile album yake sasa mle naona kama kuna nyimbo nyingi nyingi kachukua beat mfano wimbo wa "body" harmonize ft burna boy, kachukua beat na neno "Show me the way" wa kwake Papa wemba, tuje wimbo wa Hainistui kachukua beat ya Mr nice na huyo hawakukubaliana chochote.

Bado subiri tena bado kuna ule wimbo wa Q chilla "Mabu" bado tena maneno yamerudiwa mule,. Sijamaliza kwanza kuna hii mpya ya Rosa lee kachukua beat tena, mpaka nyimbo ikafutwa kule YouTube,. Bado bado zipo ila tuishie hapo.

Ndo maana nikasema hiyo tabia inawezekana katoka nayo huko alikotoka kama alikuwa hamuoni boss wake akifanya hivyo maana mtoto lazima aige kwa baba, maana anaona jinsi anafanya na mbinu zote anajua[emoji41]

Yeye sio wakwanza wala wa mwisho... ukisikiliza nyimbo ya Diamond baba lao ni copy and paste ya nyimbo ya Naira malley wa Nigeria nahisi alimlipa maana ka copy Kila kitu mpaka video
 
Yeye sio wakwanza wala wa mwisho... ukisikiliza nyimbo ya Diamond baba lao ni copy and paste ya nyimbo ya Naira malley wa Nigeria nahisi alimlipa maana ka copy Kila kitu mpaka video
Yas ndo maana hiyo ametoka nayo huko maana wasafii ambao wako nje ya wasafi huskii ama ni nadra sana kusikia ama wamekocopy sijui kutoka wapi!
 
Mh kuhusu wimbo wa Mr Nice, My Boo na Bachela mimi sioni kama ni ishu as kusample beat za nyuma inafanywa dunia nzima rejea wimbo wa No Love wa Eminem na Lil Wayne. I'll be missing you wa P Didy, Shauri yako wa Kenzo.

Kurudia maneno pia siyo ishu rejea wimbo wa Rangi ya Chungwa wa FM Academia, Georgina wa FM Academia, Loser wa Raje ila kashirikishwa Lil Wayne na verse yake yote imetoka katika wimbo wa Run Away.

Ishu ni kama hana makubaliano na wenye mali zao.
Fm academia hawana hizo nyimbo..ila waliimba kama request maalum kwa mashabiki wao katika live show zao
 
Fm academia hawana hizo nyimbo..ila waliimba kama request maalum kwa mashabiki wao katika live show zao
Rangi ya Chungwa na Georgina zimeimbwa na wengi tangu orijino zake zitoke. Miongoni mwa walioimba ni academia. Of course ni live hata kwenye hard drive yangu hizo nyimbo ni live.

Sasa swali, waliimba hawakuimba?
 
Rangi ya Chungwa na Georgina zimeimbwa na wengi tangu orijino zake zitoke. Miongoni mwa walioimba ni academia. Of course ni live hata kwenye hard drive yangu hizo nyimbo ni live.

Sasa swali, waliimba hawakuimba?
Mtoa mada hakumaanisha hivo. Kuna live, kuna cover, remix, mashup na kuna copy paste (kujimilikisha) kama anazoongelea mtoa mada
 
Rangi ya Chungwa na Georgina zimeimbwa na wengi tangu orijino zake zitoke. Miongoni mwa walioimba ni academia. Of course ni live hata kwenye hard drive yangu hizo nyimbo ni live.

Sasa swali, waliimba hawakuimba?
Rangi ya chungwa=marijani og
rangi ya chungwa ya fm ni live sio official song ya fm..huwezi kuikuta popote kwenye maktaba yao... Tena wanaweza hata wasikumbuke waliimba ukumbi gan....hapo ukute camera man aliivujisha tu wakati anarecord shoe

ngoja nimalizie k vant yangu hapa
 
Unawezaje kujua kila mtu ameshasikiliza hiyo Album....binafsi sijaisikiliza
 
Back
Top Bottom