ibanezafrica
JF-Expert Member
- Oct 23, 2014
- 7,261
- 6,553
Ni ligi ambayo ulaya waliikataa na ikashindikana kule,sasa hawa wakubwa wa Fifa wameileta huku Afrika kwakua bara hili kwa kiasi kikubwa linakabiliwa na uchumi mbovu na njaa,haraka haraka wamelipitisha lakini ukiangalia muundo mzima wa ligi hii na uendeshaji wake unaona umekaa kibaguzi zaidi.
Mfano
1)kwenye ushiriki.
Wanapendekeza washiriki wawe timu zilizo kwenye rank ya Caf ambapo wanachukua timu 24 tu
Sasa unajiuliza hiyo Caf ranking ina validity ipi? Maana mfano mara ya mwisho kwa nchi ya Tanzania timu ambazo zilikua jirani jirani katika rank hiyo ni Simba na Namungo kitu ambacho Unaona si sahihi kwani tokea timu hizo zipewe rank umepita muda mrefu na timu zimeporomoka sana tofauti na pale walipopewa rank lakini Caf bado anatambua rank ambayo imepitwa na wakati hili haliko sawa.
2)Timu shiriki zinaenda kulipwa mabilioni ya pesa ambayo yanakwenda kujenga tabaka kubwa kati ya timu shiriki na zile ambazo hazishiriki anyway si jambo baya mzigo ukiwa mnono lakini limo ndani ya huohuo mfumo ubaguzi wa ushiriki.
3)Kasoro nyingine eti hao washiriki hizo timu 24 ndio hizo hizo zitashiriki miaka yote mpaka pale mmoja wao apigiwe kura ya kuondolewa kwenye ligi hiyo.
Kiufupi ni mfumo mbovu unaokuja kudhoofisha soka la afrika,na ndio kisa unaona hata akina barbara wameomba kueleweshwa zaidi juu ya vigezo na masharti ya hii super ligi.
Hii kitu haifai,wangetaka labda wangefanya katika kila ligi afrika wachukue timu mbili mbili au moja yaani bingwa wa ligi wacheze ligi hiyo na iwepo kila mwaka na upande wa pesa kibaki hivyo hivyo hapo sasa kila timu itapigana ili iwe bingwa ligi ya nyumbani,kulikoni wafanye watakavyo wao.
Wazungu waliikataa hii kitu,njaa zitatuponza wa afrika.
Sent from my SM-A205F using JamiiForums mobile app
Mfano
1)kwenye ushiriki.
Wanapendekeza washiriki wawe timu zilizo kwenye rank ya Caf ambapo wanachukua timu 24 tu
Sasa unajiuliza hiyo Caf ranking ina validity ipi? Maana mfano mara ya mwisho kwa nchi ya Tanzania timu ambazo zilikua jirani jirani katika rank hiyo ni Simba na Namungo kitu ambacho Unaona si sahihi kwani tokea timu hizo zipewe rank umepita muda mrefu na timu zimeporomoka sana tofauti na pale walipopewa rank lakini Caf bado anatambua rank ambayo imepitwa na wakati hili haliko sawa.
2)Timu shiriki zinaenda kulipwa mabilioni ya pesa ambayo yanakwenda kujenga tabaka kubwa kati ya timu shiriki na zile ambazo hazishiriki anyway si jambo baya mzigo ukiwa mnono lakini limo ndani ya huohuo mfumo ubaguzi wa ushiriki.
3)Kasoro nyingine eti hao washiriki hizo timu 24 ndio hizo hizo zitashiriki miaka yote mpaka pale mmoja wao apigiwe kura ya kuondolewa kwenye ligi hiyo.
Kiufupi ni mfumo mbovu unaokuja kudhoofisha soka la afrika,na ndio kisa unaona hata akina barbara wameomba kueleweshwa zaidi juu ya vigezo na masharti ya hii super ligi.
Hii kitu haifai,wangetaka labda wangefanya katika kila ligi afrika wachukue timu mbili mbili au moja yaani bingwa wa ligi wacheze ligi hiyo na iwepo kila mwaka na upande wa pesa kibaki hivyo hivyo hapo sasa kila timu itapigana ili iwe bingwa ligi ya nyumbani,kulikoni wafanye watakavyo wao.
Wazungu waliikataa hii kitu,njaa zitatuponza wa afrika.
Sent from my SM-A205F using JamiiForums mobile app