OKW BOBAN SUNZU
Platinum Member
- Aug 24, 2011
- 53,868
- 121,001
Msikilize Sunday Manara Computer
FT Yanga 1 - Ken Gold FC kutoka Chunya
Goli la penati
Nimejutia muda wangu,nimetazama mchezo mbovu kabisa wa timu inayoiita timu kubwa dhidi ya timu ndogo kutoka Chunya.
Siku ya jana msemaji wao Nugaz Antonio aliwaambia mashabiki hii timu itakula nyingi. Achana na idadi ya goli nazungumzia kiwango kibovu cha timu ikiwa full mkoko. Kama ndio mara ya kwanza kuiona Yanga unaweza kudhani ni timu ya mkoa.
Jana watazamaji wa Azam walishuhudia kiwango safi Simba Sc ikitumbuiza dhidi ya African Lyon. Licha ya kuweka kikosi cha pili lakini ilikuwa show show.
Ndugu zangu Yanga mjiandae kisaikolojia. Lolote likitokea msishikane uchawi.
Kiufupi ni timu inayohitaji huruma ya marefa