Hiki ni nini? Naombeni ushauri nachanganyikiwa. Nimekopa Milioni 14 natakiwa kurudisha Milioni 39

Hiki ni nini? Naombeni ushauri nachanganyikiwa. Nimekopa Milioni 14 natakiwa kurudisha Milioni 39

MaAfisa mukopo wahun sana[emoji23]....wana take advantage za shida za watu, hawatoi maelezo ya kujitosheleza..ni wabinafsi.

Ila wako baadhi, ni very innocent.
Wahuni sana....kuna mmoja yupo ABC Bank kweli yule very innocent yani hadi anakushauri jinsi ya kufanya mkopo usikuumize big up sana kwake ila hawa wengine mbuzi kabisa
 
Waalimu kabla ya kukopa uliza riba ni asilimia ngapi? Kama huwezi kujua hilo ,waambie rejesho kwa mwezi litakuwa kiasi gani uzidishe kwa idadi ya miezi uliyekopa halafu jumla yake utoe kwenye mkopo waliokupitishia.Mara nyingi huwa Wana take advantage ya umbumbumbu wa waalimu kwenye elimu ya fedha kwani wao huuluza tuu watapata kiasi gani na kwa muda gani tuu, suala la riba, garama za mkopo kama loan processing fee , bima nk hawajui, na ukiuliza riba kichwa kichwa badala ya kukuambia riba kwa mwaka , anaigawanya kwa 12 anakuambia riba ya mwezi wewe ukiona digit ni ndogo inaingia mkenge
Aende BOT wataweza msaidia- BOT wana mashart kwa wanaotoa Mikopo watamsaidia kwa kutoa interest inayotakiwa hawa ni wezi sio haki kwa interest kubwa kama hii
 
Mimi NMB walinipa 14.6 wanapita na 254k miaka hiyo 8 na deni pamoja na riba lilikuw 24 mln nikalaumiwa sawa na wadau vil nilikuwa na dharula sikuwa na namna,kampuni Sasa limeshuka mpaka 19.


Wewe Kuna namna itakuwa imefanyika anajua afisa wako wa mkopo na meneja wake,kwa makato ya laki nne hicho kimkopo ungekirejesha miaka 4 tu.
 
Umeongea kama vile muelewa kumbe hamna kitu,

Sasa Apo NMB na CRDB ndo unadhani mkopo kwa kipindi cha miaka 8 utakua tofauti?

Nenda bank nyingine waombe waununue mkopo wako na ubadilishe vigezo uombe kulipa ndani ya miaka miwili au mitatu. Riba itakua ndogo ila makato yatakua makubwa

Mfano, ukitaka kuilipa deni lote ndani ya mwaka, utalipa makadirio ya 16,240,000 utakua umeshamaliza kila kitu. Ila ndo ujue kila mwez marejesho yatakua mil 1 laki 3 na ushee..

Ongea na afisa mkopo wako akupe elimu zaidi na huduma zingine za mikopo zilizopo.
Ha ha ha taratibu.

Sawa sijui kila kitu ila ninachokijua

1. Ndio, kwa NMB au CRDB Kwa makato hayo na Muda huo Mkopo hauwezi kuwa Milioni 14. Ni zaidi ya Milioni 20
( Nimetaja hizo benki kwa sababu walimu wengi wanatumia benki hizo kupokea mishahara yao )

2. Hata huo Mkopo ukinunuliwa na benki nyingine hauwezi kutoka Milioni 39 mpaka Milioni 16.

3. Na hayo marejesho ya Milioni moja na laki tatu. Unajuaje kama 1 ya 3 ya mshahara wake kama itahimili?
 
Kuna wapuunye wengine wanaitwa M pawa,***** sitakaa niwakope tena!!!!!Picha linaanza riba ni more than 40%,ila hawakwambiii,Kwa harakaharaka utadhani ni 20%na wanapokukopesha inatakiwa uwagawie walichokupa Kwa asilimia 20% then si utadhani umemaliza right? No way Kuna asilimia nyingine 20% ambayo nayo unatakiwa ulipe sambamba na mkopo na Kila ukichelewesha imoo.Imagine nilikopa 500k,ila kumaliza mkopo Napiga hesabu nimetoa zaidi ya M na nusu,yaani kidogo nijinyonge.Yaani kifupi ni kwamba Hawa matakoooo wanatumia madhaifu ya serikali yetu mbovu kutunyonya maskini,nshasema.
 
Waalimu kabla ya kukopa uliza riba ni asilimia ngapi? Kama huwezi kujua hilo ,waambie rejesho kwa mwezi litakuwa kiasi gani uzidishe kwa idadi ya miezi uliyekopa halafu jumla yake utoe kwenye mkopo waliokupitishia.Mara nyingi huwa Wana take advantage ya umbumbumbu wa waalimu kwenye elimu ya fedha kwani wao huuluza tuu watapata kiasi gani na kwa muda gani tuu, suala la riba, garama za mkopo kama loan processing fee , bima nk hawajui, na ukiuliza riba kichwa kichwa badala ya kukuambia riba kwa mwaka , anaigawanya kwa 12 anakuambia riba ya mwezi wewe ukiona digit ni ndogo inaingia mkenge
Umenena vyema. Usiangalie utakachopata leo. Angalia utakacholipa katika kipindi chote cha mkopo.
 
Ila wafanyakazi [emoji119]

Mimi mfanyabiashara nikitaka kukopa lazima nikae chini na Loan officer anidadavulie kiunagaubaga mambo yote yaliyopo kwenye karatasi..

Yaani unaendaje kukopa bila kujua unarudisha nini? Interest rate yako na mwisho wa marejesho ni kiasi gani!
Faida ya ulichokopa itakua yako au ya Bank?

Pole una namna ilipe tu
Yaani hata mimi nashangaa sana. Ndo maana hata biashara wakifungua zinaishia kufa tu. Ila hawa waalimu wakiwa chuo huwa wanafundishwa SOMO LA UJINGA kwa siri?
 
Watu ukiwaambia saccoss na vikoba hata hawaelewi

Mimi Nina vicoba viwili kila kimoja ninaweza kukopa 10M
Riba inarudishwa kwenye account yangu japo muda wa marejesho siyo mrefu sana ila napunguza stress Za kuneemesha mabank
Kuna uzi wa shoga mmoja huku anasema Vicoba ni vikundi vya kike. Kuna watu wameamua kuwa maskini kilazima.
 
Niliwahi kopa B blue zamani nikitakiwa ndani ya wiki niwe nimelipa ada na si wa kumuendea nilikopa laki nne nakarejesha laki tisa kwa muda wa miezi sita
 
Kila siku tunatoa ushauri humu acheni kukopa kwenye taasisi uchwara za kifedha hamsikiii..hawa ABC,Platinum sijui..Bayport ni kausha damu haswa..
Sio hao tu, hata hizi bank kama CRDB, NMB, NBC na zingine zinanyonya sana wakopaji katika process za mwanzoni za mchakato wa kupata mkopo na pia kwa kupitia riba

Ni vizuri kusoma mkataba na kufuatilia mchanganuo wote wa mkopo na makato
 
Sikufanikiwa kusoma mapema. Lakii kupitia quotes nimeona una deni kubwa balaa.

Kimsingi hilo deni ni kubwa mno. Wakili wa bank aliyeidhinisha huo mkopp anastahili mashtaka
Hakuna cha shtaka lolote hapo iko hivi nenda bank yoyote hata pbz inayotoza 13% kwa mwaka kopa then rudisha kwa mwaka 1 au maximum miwili isizidi hapo hata benki watakuchukia maana in total utalipa riba kidogo, ila mteja anapofanya kosa la kurejesha kwa miaka kuanzia mitatu na kuendelea ndipo mwisho wa siku makato yanapoanza ataona makubwa na ni kweli ni makubwa kwa kuwa unakaa na deni la benk muda mrefu na ndicho kilichomkuta mleta bandiko amefanya kosa kubwa sana la kukopa mkopo wa kurejesha kwa muda mrefu. Personal loan kwenye taasisi za fedha za Tz ili uinjoy maximum period ya kurudisha huwa ni mwisho mwisho kabisaa miaka 2 na humu ishajadiliwa sanaaaaa. Sasa mteja anakopa mkopo wa kurejesga miaka mitano anategemea nini kama sio maumivu ni nani atakukopesha kwa miaka mitano then asikupige na kitu kizito kwenye marejesho obvious hamna.
 
Wahuni sana....kuna mmoja yupo ABC Bank kweli yule very innocent yani hadi anakushauri jinsi ya kufanya mkopo usikuumize big up sana kwake ila hawa wengine mbuzi kabisa
Evelyn Salt mojawapo ya KPI ya Loan officer ni kupata wateja wengi wanaoiingizia kampuni mihela mingi, so mwisho wa siku akiweza kukapitalize kwenye ignorance ya mteja atafanya tu labda umkute afisa mikopo mtumishi mtumishi hivi😂 kama huyo wa abc otherwise....kosa kubwa tunalofanya sie wataka mikopo hatunaga muda wa kupata all detail ili tufanye informed decision, juzi kuna mtu akawa ananiambia anaenda chukua mkopo wa gari kwenye kampuni inaitwa orbit nikamuuliza riba ni asilimia ngapi ni kwa muda gani akaniambia 3.5% kwa mwaka nikambishia nikamwambia asilani abadan katu haiwezekani hiyo 3.5 ni kwa mwezi nikamwambia nipe no. yao ya simu nipige then namweka loud basi nikawapigia kuwauliza riba wakasema 3.5% kuwauliza muda Loan Officer anajibu kingine ohh ni reducing riba ndogo sana hiyo nikamchachamalia kuhusu muda kinyooooonge ndo kusema ni 3.5 kwa mwezi🤣😤😬😟 jamaa yangu alivyosikia kwa nini matusi ya nguoni yasimtoke......
 
Back
Top Bottom