Aulizaye anataka kujua... Dude la namna hiyo nililiona mara ya kwanza kwa mchungaji mmoja kutoka Australia. Nilikuwa na miaka sita wakati huo na nilihitaji kuitika wito wa kulenga shabaha kwenye matundu tuliyoyzoea. Hamad!... Kufika chooni dude la chuma limening'inizwa kwa juu huku mnyororo wa kuvutia ukiwa pembeni yake. Baada ya kuona sielewi somo nilimvaa baba yangu anieleweshe nafanyaje sasa? Mwenyeji wetu akatoa somo nikalielewa. Baada ya kushusha mzigo na kutawadha, nikavuta mnyororo pembeni...Lahaullah! Dude liliunguruma kwa presha kali huku maji yakisafisha mzigo wote kwenda kuzimu, mimi mbio... kwa hofu niliyoipata. Mpaka napata Akili sawa sawa nilikiwa naviogopa sana vyoo vyenye madude ya aina hiyo..... Angalau siku hizi vimeboreshwa ukilinganisha na vilivyo kuwapo miaka ya sitini.[emoji41]