Asalaam Aleykum wana jamvi,
Ama baada ya salamu hizo nidondoke kwenye mada tajwa hapo juu.
Kiukweli suala la kubinafisha (??!kumilikisha) Bandari zetu, ni suala ambalo limeibua hisia za Watanzania wengi wazalendo wa dhati (na wasio na uzalendo wa dhati).
Ni suala ambalo kwa kweli kwa kila Mtanzania anayejielewa, lazima ahoji au awe na maswali mawili matatu ( hata kama ni ya kujihoji au kujiuliza mwenyewe; kikubwa hoja au maswali).
Hili suala linakuwa tata zaidi hasa kutokana na usiri unaoambatana na mkataba wenyewe na terms and conditions ambazo haziko wazi. Mojawapo ya vipengele ambavyo binafsi naona kingekuwepo, basi kingenipunguzia maswali na wasiwasi, ni kipengele cha muda wa kubinafsisha (kumilikisha) itakuwa ni miaka mingapi?
Maana wanaotetea wamekuwa wakiwashambulia wale ambao wanasema tunaenda kumilikisha/kubinafsisha kwa miaka 100 (karne!) kwa madai kwamba hicho kipengele hakipo kwenye mkataba. Sasa swali langu na Watanzania wenzangu wenye mtizamo kama wangu tunahoji, Je, tutamilikisha/kubinafsisha kwa miaka mingapi? Au ndo tunawapa waimiliki milele (kwa muda usio na kikomo)?
Swali la pili, ukiupitia kwa makini mkataba, utagundua tayari ulishasainiwa, Je, bungeni umepelekwa ili kupewa tu baraka za wabunge? Swali la nyongeza, wabunge watakataaje mkataba ambao tayari ulishasainiwa toka mwaka jana; 2022?
Je, usalama wetu kama nchi utakuwa katika hali gani endapo jamaa wakiamua hakuna Mtanzania yeyote kutia mguu wake kwenye himaya yao?
Kwa nini huo Mkataba uhusu tu Bandari za ukanda wa bahari na maziwa ya Tanzania bara tu na wala siyo Tanzania visiwani (Zanzibar).
Anyway, hayo ni maswali machache ambayo nimeamua kujiuliza binafsi.
Pamoja na hayo, nawaomba Watanzania wenzangu, tuviamini vyombo vyetu vya ulinzi na usalama.
Tanzania ni moja ya nchi zenye vyombo bora kabisa duniani katika medani za Kiulinzi na Usalama. Hii huenda ni kwa sababu ya misingi imara waliyoiweka waasisi wa Taifa hili.
Kwa hiyo,, kutokana na ubora huo, na uzalendo wa viongozi wanaoviongoza na viapo walivyoapa kulinda na kutetea maslahi ya nchi hata ikiwezekana kwa kulipia gharama ya maisha (kifo), nina imani kabisa kwamba tuko katika mikono salama.
Ee, Mwenyezi Mungu, naomba kwa niaba ya Watanzania wenzangu, uwaongoze na uwape hekima viongozi wetu wa vyombo vya ulinzi na usalama. Wape ujasiri wa kukabiliana na wanasiasa wenye tamaa. Wape uwezo wa kutambua kwamba, wamewekwa kwenye nafasi zao kwa ajili ya kuwalinda wananchi wenzao pamoja na nchi yao na wala siyo viongozi waliowateua tu.
Nawapenda sana Watanzania wenzangu. Nina amini Mungu anaipenda sana nchi yetu na kamwe hawezi kuruhusu kutupeleka tena Utumwani. Hata hivyo Tanzania imechangia kwa kiasi kikubwa sana kuleta uhuru wa nchi nyingi za Kiafrika. Ee, Mwenyezi Mungu, tunaomba fadhila hata kwa hilo tu.
Ahsanteni sana.
AMIN.
Ama baada ya salamu hizo nidondoke kwenye mada tajwa hapo juu.
Kiukweli suala la kubinafisha (??!kumilikisha) Bandari zetu, ni suala ambalo limeibua hisia za Watanzania wengi wazalendo wa dhati (na wasio na uzalendo wa dhati).
Ni suala ambalo kwa kweli kwa kila Mtanzania anayejielewa, lazima ahoji au awe na maswali mawili matatu ( hata kama ni ya kujihoji au kujiuliza mwenyewe; kikubwa hoja au maswali).
Hili suala linakuwa tata zaidi hasa kutokana na usiri unaoambatana na mkataba wenyewe na terms and conditions ambazo haziko wazi. Mojawapo ya vipengele ambavyo binafsi naona kingekuwepo, basi kingenipunguzia maswali na wasiwasi, ni kipengele cha muda wa kubinafsisha (kumilikisha) itakuwa ni miaka mingapi?
Maana wanaotetea wamekuwa wakiwashambulia wale ambao wanasema tunaenda kumilikisha/kubinafsisha kwa miaka 100 (karne!) kwa madai kwamba hicho kipengele hakipo kwenye mkataba. Sasa swali langu na Watanzania wenzangu wenye mtizamo kama wangu tunahoji, Je, tutamilikisha/kubinafsisha kwa miaka mingapi? Au ndo tunawapa waimiliki milele (kwa muda usio na kikomo)?
Swali la pili, ukiupitia kwa makini mkataba, utagundua tayari ulishasainiwa, Je, bungeni umepelekwa ili kupewa tu baraka za wabunge? Swali la nyongeza, wabunge watakataaje mkataba ambao tayari ulishasainiwa toka mwaka jana; 2022?
Je, usalama wetu kama nchi utakuwa katika hali gani endapo jamaa wakiamua hakuna Mtanzania yeyote kutia mguu wake kwenye himaya yao?
Kwa nini huo Mkataba uhusu tu Bandari za ukanda wa bahari na maziwa ya Tanzania bara tu na wala siyo Tanzania visiwani (Zanzibar).
Anyway, hayo ni maswali machache ambayo nimeamua kujiuliza binafsi.
Pamoja na hayo, nawaomba Watanzania wenzangu, tuviamini vyombo vyetu vya ulinzi na usalama.
Tanzania ni moja ya nchi zenye vyombo bora kabisa duniani katika medani za Kiulinzi na Usalama. Hii huenda ni kwa sababu ya misingi imara waliyoiweka waasisi wa Taifa hili.
Kwa hiyo,, kutokana na ubora huo, na uzalendo wa viongozi wanaoviongoza na viapo walivyoapa kulinda na kutetea maslahi ya nchi hata ikiwezekana kwa kulipia gharama ya maisha (kifo), nina imani kabisa kwamba tuko katika mikono salama.
Ee, Mwenyezi Mungu, naomba kwa niaba ya Watanzania wenzangu, uwaongoze na uwape hekima viongozi wetu wa vyombo vya ulinzi na usalama. Wape ujasiri wa kukabiliana na wanasiasa wenye tamaa. Wape uwezo wa kutambua kwamba, wamewekwa kwenye nafasi zao kwa ajili ya kuwalinda wananchi wenzao pamoja na nchi yao na wala siyo viongozi waliowateua tu.
Nawapenda sana Watanzania wenzangu. Nina amini Mungu anaipenda sana nchi yetu na kamwe hawezi kuruhusu kutupeleka tena Utumwani. Hata hivyo Tanzania imechangia kwa kiasi kikubwa sana kuleta uhuru wa nchi nyingi za Kiafrika. Ee, Mwenyezi Mungu, tunaomba fadhila hata kwa hilo tu.
Ahsanteni sana.
AMIN.