Tangu nianze kushabikia YANGA miaka ya 90's sijawahi ona shabiki wa Yanga akiwa na furaha bila kunyanyua VPL....
Hizo nyingine ni story zako!
Hujaelewa
Sijasema washabiki wa Yanga hawafurahii kuchukua ubingwa wa VPL
Nimesema haijawahi kutokea mshabiki wa timu hizi akafurahi kwa kiwangi cha juu hadi kifo kikamchukua kwa ajiri ya furaha ya kuchukua ubingwa wa ligi.
Siku zote tunaona pale Taifa kwa Chichi Somboko au kwa Kipara Shop, Yanga wanapochukua ubingwa wa ligi, ngoma zinachezwa, wadada wanacheza mwanzo mwisho kwa furaha.
Lakini hajawahi kufa mshabiki kwa furaha ile.
Wala haijawahi kutokea kwa mpenzi yeyote, Yanga inapokosa kuchukua ubingwa wa Ligi,, akahuzunika hadi kifo kikamchukua
Nimesema huzuni au furaha ya kiwango cha juu inatokea pale ambapo mbili hizi zinapofungana.
Bosi, unaninikuu sehemu ndogo ya mada halafu unatoa hitimisho
Unapoteza maudhui ya mada husika.
Kila timu ikichukua ubingwa wa ligi inafurahi.