Hili la Jonas Mkude kuingia kambini akiwa kapendeza sio poa kabisa

Hili la Jonas Mkude kuingia kambini akiwa kapendeza sio poa kabisa

kwani ni wachezaji wengine hawanywi pombe mkuu? Au hujawahi kutana nao! Nachojua asilimia kubwa Wachezaji wanavuta sigara na kunywa pombe
Nadhani huenda ika moja wapo ya sababu hawafiki mbali kimafanikio kama wenzao wa Magharibi. Wengi wao wanaishia Uarabuni na kurudi nyumbani.
 
Jana nilipata nafasi ya kuzama Kambini kwa timu ya Taifa.

Nikiwa Bongo mara nyingi napenda kujibanza na watu wa soka ili kujua mambo mbalimbali ambayo kwa namna moja au nyingine siyatambui.

Kwa bahati nzuri/mbaya mwamba mmoja hivi kutoka pande za Msimbazi akaingi akiwa amependeza kinoma. Nadhani aliutumia vyema ule wakati wa alasiri wa siku ya jana kufanya yake.

Labda huenda alidhani ameonja kidogo na hakuna mtu angeshindwa kumtambua, kwa bahati mbaya mwana alionekana dhahiri hata na wachezaji wenzake kuwa Jey yuko pombe. Mwalimu hakuweza kulitambua hilo mapema ila baadhi ya maafisa wa benchi la ufundi la Stars waliligundua hilo. Nikaona Nadir Cannavaro akimuita kando na kuzungumza na mkude kwa dakika kadhaa kabla drill ya kupasha misuli haijaanza.

Baadaye nikapewa taarifa kuwa Nadir alikuwa anamsaidia Jey ili hadha ili isije kujulikana kwa Kocha, Nadir akamshauri kuwa ajifanye kama anaomba ruhusa ya kwenda nyumbani ya kuwa kumetokea na dharura.

Jey akasaidiwa na baadhi ya maafisa wengine hadi akapata ruhusu ya kuondoka.

Ni kocha pakee ambaye mpaka sasa hajafahamu kuwa Mkude alikuja kambini amelewa. Baadhi ya viongozi wengine wa benchi hilo hilo hawakupendezewa kabisa kwa Jey kuja amelewa, waliona kama ni kitendo cha dharau na ukosefu wa heshima kwa kazi.

Leo Nikiwa naongea kwa simu na mmoja wa afisa niliyekutana naye jana kambini jana, akanitaarifu kuwa Kocha ameambiwa mchezo wote ulio tokea. Huenda ametonywa na lile kundi dogo ambalo walichukizwa na lile tukio.

Akaongeza zaidi kwa kuniambia kuwa Kocha ameanza kujenga "kutokuwa" na uaminifu na baadhi ya watu katika benchi la Ufundi. Akasema nisisangae kama baada ya game ya Benin kukawa na mabadiliko katika benchi hilo.

Nashauri:- Ni wakati sasa Jonas Mkude asitishe kuichezea Taifa Stars na awape nafasi Vijawa wengine chipukizi.
Nimescroll ili nione picha ila nimeambulia patupu
 
kwani ni wachezaji wengine hawanywi pombe mkuu? Au hujawahi kutana nao! Nachojua asilimia kubwa Wachezaji wanavuta sigara na kunywa pombe
Kuna wachezaji ambao ni walevi na wamekubali kuwa walevi na pia wana Ustaarabu wao katika kufanya ulevi.

Uwezi Kunywa pombe saa 6 mcha ili hali ukijua kuwa saa 10 jioni unatakuwa mazoezini. (Hata hao wachezaji walevi wengine sio wajinga kiasi hiki).
 
Wamsamehe bure, Mkude alifiwa na mtoto hivi kariui hueda anajariu kujisahaulisha na tukio ndo kisa anaamua kupiga pombe!
Hata hivyo mtoa mada wewe i mnazi sana! Kwanza umemtaja Canavaro tu kuwa ndiye aliyejaribu kumsaidia Mkude kishkaji, l;akini mwishoni unawaingiza wa bench la ufundi na hata kuanza kuwatabiria mabaya, Hebu acha umbea aisee!
 
Wakati mkude akiwa katika kiwango cha maridadi kijana mmoja anaitwa feisal alikuwa ndio Kwanza anauzoea mpira anaruka ruka tu uwanjani Wana wakmwambia

"Dogo kaza kama mkude usiwe rojo rojo"

Dogo alikaza kweli Hadi kuwa mhimili wa timu yake

Baada ya dogo kuanza sasa kuonekana yuko katika kiwango maridadi

Mkude graph ikaporomoka vibaya

Akaanza kiburi,ulevi ,utovu wa nidhamu nk.

Kjjana fei mchukulie mkude Kama anti-model wako sio role model he is finished "amekwisha"

So sad!!! Aisee
 
Wakati mkude akiwa katika kiwango cha maridadi kijana mmoja anaitwa feisal alikuwa ndio Kwanza anauzoea mpira anaruka ruka tu uwanjani Wana wakmwambia

"Dogo kaza kama mkude usiwe rojo rojo"

Dogo alikaza kweli Hadi kuwa mhimili wa timu yake

Baada ya dogo kuanza sasa kuonekana yuko katika kiwango maridadi

Mkude graph ikaporomoka vibaya

Akaanza kiburi,ulevi ,utovu wa nidhamu nk.

Kjjana fei mchukulie mkude Kama anti-model wako sio role model he is finished "amekwisha"

So sad!!! Aisee
Feisal ana mengi ya kujifunza kwa Jonas ila ni machache ya kuyaacha.
 
Wamsamehe bure, Mkude alifiwa na mtoto hivi kariui hueda anajariu kujisahaulisha na tukio ndo kisa anaamua kupiga pombe!
Jonas asamehewe mara ngapi? Nenda kamuulize Magoli atakupa jawabu la swali hili.
 
Usimba & Uyanga usikufanye ushindwe kutumia common sense.
Hakuna cha Common sense hapo ni umbea tu! Kwani bench la ufundi halina watu wake na taratibu zake za kushughulikia mambo haya mpaka wewe mtu uliyeokoteza kijiweni uje kulianika hapa?? Kiherehere ni kitu kibaya sana aisee!
 
Hata hivyo mtoa mada wewe ni mnazi sana! Kwanza umemtaja Canavaro tu kuwa ndiye aliyejaribu kumsaidia Mkude kishkaji,
Inaonekana kwenye jukwaa hili wewe ni mgeni. Kila mtu anafahamu kuwa mimi ni Mwanachi. Je nikiwa shabikin sipaswi kutoa maoni Yangu?

Cannavaro ndio Team Manager wa Taifa Stars, Je unafahamu mojawapo kati ya majukumu ya Team Manager?
 
Ana msongo wa mawazo, bahati mbaya timu yake hawamsaidii bali wana msimanga kisa alirusha ndoano kwa chombo ya fundi. Kuna tetesi msimu ujao anaachwa.
 
Acha kumchafua Mkude wewe.Usitengeneze anguko la mwenzako kwa uzushi na upuuzi kama huu
 
Back
Top Bottom