Hili la Jonas Mkude kuingia kambini akiwa kapendeza sio poa kabisa

Hakuna cha Common sense hapo ni umbea tu! Kwani bench la ufundi halina watu wake na taratibu zake za kushughulikia mambo haya mpaka wewe mtu uliyeokoteza kijiweni uje kulianika hapa?? Kiherehere ni kitu kibaya sana aisee!
Inaonekana uko mbali sana na watu wa mpira katika nchi yako.

Sasa hebu chukua hii huenda ikakusaidia hapo baadaye. Yafuatayo ni baadhi ya majukumu ya Team Manager wa Taifa Stars(Nadir Haroub):-

1. Overseeing the daily operations of one section within a national team set-up.
2. Supporting a team with training and other eqquipments neccesary for perfomance improvement
3. Identify and communicating with TFF where there is a shortage in requirements needed for improving preparation and training.
4. Develop proper relationships between players and the entire technical bench.
5. Prepare and complete the necessary preparations as the team progresses to the respective matches.
6. Prepare a regular training report and submit it to the relevant department within the football federation (TFF).


Nimekuwasilishia chache tu hizo yakupasa uzifahamu. Ili baadaye unapokuwa una jadiri uweze kujadiri kwa hoja za msingi.
 
Jonas asamehewe mara ngapi? Nenda kamuulize Magoli atakupa jawabu la swali hili.
Kwa hiyo wewe umekuja kulianika hapa ili asisamehewe?? Binadamu wengine tuna roho mbaya sana! Kwaza hilo pombe kwai kaanza kunywa leo?? Mpaka sasa ameshachezea Simba more thana 10yrs, akiwa anapiga hilo pombe, na hata waliomuona kumchagua walimuona akisakata kabumbu akiwa ameshapiga hilo pombe so tuache fitina jamani!
 
Acha kumchafua Mkude wewe.Usitengeneze anguko la mwenzako kwa uzushi na upuuzi kama huu
Kwa hiyo ata Kamati ya nidhani ya simba iliposhauri kuwa Jonas akapatiwe matibabu ya kiutimamu ya muda mfupi walikuwa wanamtengenezea anguko?
 
Kunywa pombe sio kosa. Kosa alilo lifanya ni kuja Kambini akiwa amelewa.

Je, huu utakuwa mfano gani kwa vijana chipukizi walioko Kambini na Taifa Stars?
 
Sasa wewe uliyepost humu ndie Nadir Canavaro??? Acha fitina aisee!
 
Mpaka sasa ameshachezea Simba more thana 10yrs, akiwa anapiga hilo pombe, na hata waliomuona kumchagua walimuona akisakata kabumbu akiwa ameshapiga hilo pombe so tuache fitina jamani!
Ni sawa kama akija Kambini pale Simba SC akiwa amelewa, kwa sababu atakuwa mfano bora kwa wachezaji wengine wa Simba.

Ila Si vyema akaja kambini Taifa Stars akiwa amelewa kwa kuwa kuna mjumuisho wa wachezaji kutoka Vilabu mbalimbali.

Je itakuwa vyema kama wakienda kwenye vilabu vya na tabia waliyoiona kutoka kwa role-model wao?
 
Kunywa pombe sio kosa. Kosa alilo lifanya ni kuja Kambini akiwa amelewa.

Je, huu utakuwa mfano gani kwa vijana chipukizi walioko Kambini na Taifa Stars?
Sasa wewe sio kocha na wala si sehemu ya bench la ufundi! Lakini umekimbilia kuja kuanika hapa JF ili ikusaidie nini?
Mkude na hilo bench la ufundi wakiondolewa stars kwa huu umbea wako wewe unapata faida gani labda???
 
Unajuaje kama na wale anaojumuika nao kuwa si watumiaji wa pombe au wewe ni msemaji wao??
 
Sasa wewe sio kocha na wala si sehemu ya bench la ufundi! Lakini umekimbilia kuja kuanika hapa JF ili ikusaidie nini?
Nimeposti ili isinisaidie demigod bali ikawasaidi kuwaepushia dhahama wale wachezaji vijana walioko Kambini Taifa Stars.

Kwa kuwa ninaamini kama tukiwa na idadi kubwa ya wachezaji pale Taifa Stars wasio walevi basi kuna matumaini Taifa Stars ikafanya vyema.
 
Unajuaje kama na wale anaojumuika nao kuwa si watumiaji wa pombe au wewe ni msemaji wao??
Hata kama wapo basi sio wachezaji wote walioko kambini.

Hata kama wapo basi ni wachache. Hivyo basi ninaamini ulevi wao hauto waathiri wengine, ingekuwa mbaya zaidi kama hao wachache nao waje mazoezini wakiwa wamelewa.
 
Aliposimamishwa na club yake kwa utovu wa nidhamu ambao ni huo media nyingi km sio zote wakaungana na club hasimu zikasimama kila uchao kuhoji afunguliwe na aachiwe na wakaenda mbali mpk kutunga kuwa alikkosea heshima CEO wake ndio maana Boss MO amechukia kuingiliwa na mchezaji maeneo yake

Walienda mbali hadi kumpa kichwa huyu mchezaji akafuta picha za club yake zote kwenye akaunti yake na ikatangazwa kuwa wanataka kumsajili sijui kilitokea nini

Leo ndio hao tena wanakuja na nyimbo hii maana nimeona Kitenge kawa wa Kwanza kuisema hii huku alikuwa wa Kwanza siku zile kupinga adhabu



Sent from my Nokia 3.2 using JamiiForums mobile app
 
Mkude na hilo bench la ufundi wakiondolewa stars kwa huu umbea wako wewe unapata faida gani labda???
Ukisoma vyema utagundua sijashauri bench la ufundi liondolewe, bali nimeshauri Jonas apumzike kuchezea timu ya taifa na aweke jitihada klabuni kwake.

1. Faida Inayopatikana endapo Jonas ataondolewa National Team ni pamoja na kuwa na idadi kubwa ya wachezaji katika timu ya Taifa wasio katika hatari ya kushawishika kutumia Ulevi.

2. Pia, itawasaidia vijana hao hao kufanikisha ndoto za maisha yao kimpira. Sidhani kama kuna timu ulaya inaweza sajili mchezaji mwenye mapafu yaliyo athirika na ulevi.

3. Faida ya mwisho ni furaha ambayo mimi na wewe tutaipata pale Taifa Stars inapo fanya vyema kiwanjani.
 
Hayo ni mawazo yao wakina Kitenge na Media zenu za Tanzania na wala sio Mawazo ya kwangu.
 
Ana msongo wa mawazo, bahati mbaya timu yake hawamsaidii bali wana msimanga kisa alirusha ndoano kwa chombo ya fundi. Kuna tetesi msimu ujao anaachwa.
Mhh!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…