Hili la kifo cha Dkt. Faustine Ndugulile limeniumiza sana, shida ni nini?

Hili la kifo cha Dkt. Faustine Ndugulile limeniumiza sana, shida ni nini?

Hizo hospitali unazosifia hazina maajabu yoyote, tatizo lako umekariri. Ndio maana wadau wengi humu wanakushangaa. Na muda mrefu nilikwambia kuwa viongozi wenyewe wa India hawaendi hizo hospitali wanaenda kutibiwa nje ya India. Kama mwenyeji anafanya hivyo basi ujue kuna shida
Naona unazidi kujivuruga mwenyewe na kuonyesha jinsi usivyo kuwa makini. Hii ni kwa sababu uhitimu wako ni wa chuo cha 'google'!
Mtu mwenye uelewa hawezi kudai kama unavyo fanya hapa kuwa "...viongozi wenyewe wa India hawaendi hizo hospitali, wanaenda kutibiwa nje ya India". Sasa nikueleze kuwa mtu mwenye uelewa wa mambo na elimu ya kutosha hawezi kuweka madai kama hayo unayo yafanya wewe hapa, kwa sababu ukiulizwa ulewte ushahidi unao onyesha hivyo; sehemu pekee unayo kimbilia ni 'google' kwenda kupata mfano mmoja au miwili ya viongozi waliofanya hivyo. Na isitoshe, hutajisumbua kutafuta sababu kwa nini walikwenda kutibiwa kwingine badala ya kwenda kwenye hospitali zao huko India!
Kwa mtu mwenye ufinyu wa uelewa, kama unavyo onyesha wewe hapa toka mwanzo, hiyo inatosha kabisa kujigamba kuwa unajuwa unacho kisemea.
Hali kadhalika, tazama hao wenzako unao waita wewe "...wadau wengi humu wanakushangaa"; wengi wangapi, na wamenishangaa kivipi? Huoni nilipo waita "walevi wenzako" kumbe hukuelewa maana niliyo kuwa nimeilenga? Hao hawana tofauti yoyote na wewe katika ufahamu wa maswala haya.

Unarudia yale yale, eti "hospitali ninazo zisifia hazina maajabu yoyote", kwani nilikwambia popote humu tokea tujibishane kuwa hizo hospitali zina "maajabu"? Hizo hospitali kuwa tofauti na zile za "Public Health Service" ndiyo unataka yawe maajabu? Kwa mara nyingine hii inaonyesha ufinyu wa fikra ulizo nazo kuhusu maswala ya namna hii
Unataka maajabu yawe yapi? Kila mgonjwa anaye kwenda kutibiwa humo atoke akiwa mzima? Hayo wewe uli yaona wapi?

Kiujumla naona sina la ziada kujadili na wewe kuhusu hili la hospitali maalum za India wanako kwenda kutibiwa baadhi ya waTanzania, siyo viongozi pekee; najuwa hata waTanzania wengine huenda huko kutibiwa na wengine hupona na baadhi yao hufariki. Hospitali hizo ni tofauti na zile zinazo toa huduma katika mfumo wa kijamii wa Afya unao tumika India.

Sina la zaidi na wewe.
 
Elimu ya Tanzania ni shida

Kichwa cha habari kinasema kusikitishwa na kifo cha Dr Ndugulile.

A reader expects an eulogy about the person.

The nonsense you read, watanzania hamjui kuandika.

Aargh, to think people dare challenging my writing skills halafu unasoma ujinga kama huu.

Like kabisa WHO hawana employment plans zao, hadi DG wao awapangie; that’s like saying WHO is a nonsensical institutions like the ones we have in Tanzania.

The nonsense
EEEEEeeeeeennnHHhhhEEEeeeeee!
You're in your true elements today, mkuu 'Mayor'!

But I see a lot of sense in there.

BTW: The writer of the piece has identified himself as being a 'researcher' of sorts; and his abode is in Ottawa (you know where that is), so you should blame the education system ya huko; and not yetu hapa Bongo!
 
kama tungekuwa na smart leaders …. No one would go to india…. Kufanya nini
Nakubaliana na sehemu ya kwanza ya sentensi hiyo, hatuna viongozi wenye umakini kwa chochote; siyo maswala ya afya pekee, bali kila eneo.

However, maswala ya kwenda India au kwingineko kupata huduma, siyo ya kiafya pekee, ila hata katika maswala mengineyo, kama ya biashara, hayo ni maswala ya kawaida sana duniani; na yanakuwepo kwa sababu mbalimbali, siyo iwe lazima iwe kwa sababu ya ufinyu wa huduma zinazo tolewa nyumbani

"Medical Tourism" ni jambo la kawaida sana siku hizi. Kuna nchi ambazo zime amua kujipambanua katika eneo hilo na kutoa huduma nzuri kwa njia hiyo.
Thailand ni nchi moja wapo wanao fanya hivi, na wagonjwa toka maeneo mbalimbali duniani huenda kupata huduma hizo (siyo lazima viongozi pekee).
Kwa wananchi wa nchi zilizo endelea, kama Marekani na baadhi ya nchi za Ulaya hutafuta huduma hizi huko, kwa sababu ni nzuri, zinazo kidhi viwango; lakini pia ni nafuu zikilinganishwa na gharama wanazo takiwa kulipia huko makwao.

Nimesoma haraka haraka bandiko lako hapo juu kuhusu mwelekeo wa utoaji wa huduma za afya huko tunako elekea zitakavyo kuwa 'impacted' na maendeleo ya teknolojia, kama ulivyo zitaja. Ni sahihi na kwa kweli mabadiliko hayawezi kuzuiwa; lakini tusikimbie haraka sana. Enzi za 'drive through medical services', zitawadia, lakini bado tujishughulishe na hali ilivyo sasa kwanza.

Huduma za Afya kama ujuavyo zina sehemu nyingi. Kuna upande wa kuzuia watu wasishambuliwe na magonjwa kama malaria tu kwa mfano; au hata 'cholera' pekee (can you imagine?) Cuba is reputed to having a very robust health system; si kwa sababu ya kuwa na very sophisticated equipment (i'm not dicounting them). Kwa hiyo, pamoja na kufanya jitihada za kupata vifaa muhimu, kama hivyo vingi ulivyo vitaja; mfumo wetu wa huduma za afya bado ni mbovu sana.
Ninakubaliana nawe moja kwa moja kwamba viongozi katika mipango ya matumizi ya hicho kidogo tulicho nacho; hawatoi kipa umbele katika mambo muhimu. Na hii siyo katika maswala ya afya pekee!

Can you imagine, tuna kwenda kutafuta wawekezaji wa kutunza mapori yetu na kupanda misitu kwa biashara ya 'Carbon Credits'; eti hakuna waTanzania wanao weza kufanya mambo hayo?

Inaudhi na kukasirisha sana.
 
I am always sensible, you know that.

Anyway nipo likizo; nimejipa time off mpaka January .

Mengine uwa ni uzushi wako tuu.
You make my day, mkuu 'Mayor'!
Asante kwa kunipa hiki kicheko alasiri hii!
 
Naona unazidi kujivuruga mwenyewe na kuonyesha jinsi usivyo kuwa makini. Hii ni kwa sababu uhitimu wako ni wa chuo cha 'google'!
Mtu mwenye uelewa hawezi kudai kama unavyo fanya hapa kuwa "...viongozi wenyewe wa India hawaendi hizo hospitali, wanaenda kutibiwa nje ya India". Sasa nikueleze kuwa mtu mwenye uelewa wa mambo na elimu ya kutosha hawezi kuweka madai kama hayo unayo yafanya wewe hapa, kwa sababu ukiulizwa ulewte ushahidi unao onyesha hivyo; sehemu pekee unayo kimbilia ni 'google' kwenda kupata mfano mmoja au miwili ya viongozi waliofanya hivyo. Na isitoshe, hutajisumbua kutafuta sababu kwa nini walikwenda kutibiwa kwingine badala ya kwenda kwenye hospitali zao huko India!
Kwa mtu mwenye ufinyu wa uelewa, kama unavyo onyesha wewe hapa toka mwanzo, hiyo inatosha kabisa kujigamba kuwa unajuwa unacho kisemea.
Hali kadhalika, tazama hao wenzako unao waita wewe "...wadau wengi humu wanakushangaa"; wengi wangapi, na wamenishangaa kivipi? Huoni nilipo waita "walevi wenzako" kumbe hukuelewa maana niliyo kuwa nimeilenga? Hao hawana tofauti yoyote na wewe katika ufahamu wa maswala haya.

Unarudia yale yale, eti "hospitali ninazo zisifia hazina maajabu yoyote", kwani nilikwambia popote humu tokea tujibishane kuwa hizo hospitali zina "maajabu"? Hizo hospitali kuwa tofauti na zile za "Public Health Service" ndiyo unataka yawe maajabu? Kwa mara nyingine hii inaonyesha ufinyu wa fikra ulizo nazo kuhusu maswala ya namna hii
Unataka maajabu yawe yapi? Kila mgonjwa anaye kwenda kutibiwa humo atoke akiwa mzima? Hayo wewe uli yaona wapi?

Kiujumla naona sina la ziada kujadili na wewe kuhusu hili la hospitali maalum za India wanako kwenda kutibiwa baadhi ya waTanzania, siyo viongozi pekee; najuwa hata waTanzania wengine huenda huko kutibiwa na wengine hupona na baadhi yao hufariki. Hospitali hizo ni tofauti na zile zinazo toa huduma katika mfumo wa kijamii wa Afya unao tumika India.

Sina la zaidi na wewe.
Hizohizo hospitali maalumu Wahindi wenye vibunda wanazikimbia
 
Nataka kusema kitu kila nikiandika najikuta nafuta.
Wacha nitulie alale tuu salama
 
India iko overrated sana na Watanzania

Mtu una hela na mtumishi mkubwa tu serikalini eti unaenda India

Huwezi kusikia kiongozi mkubwa wa mataifa ya Ulaya, Far East Asia, Latin America au Middle East ameenda India

Huu utamaduni wa kwenda India sijui tumeutolea wapi?
Kwani huu utaratibu wa kukatiwa rufaa nje ya nchi yako uko nchi gani na gani?

Hayo mataifa unayoyataja nayo yana huo utaratibu, au yanamaliza matibabu yote ndani ya nchi?
 
Back
Top Bottom