Hili la Polisi kuruhusiwa 'kuwanyanganya' silaha majambazi na kupandishwa vyeo limekaaje?

Hili la Polisi kuruhusiwa 'kuwanyanganya' silaha majambazi na kupandishwa vyeo limekaaje?

mh, mbona mi naona sawa tu.

just imajin, mtu anakuvamia akiwa na silaha,anakuweka chini ya amri zake, anachukua anachotaka na ukifanya masihara anakutoa maisha mm kwa upande wangu sioni sababu za kuwachekea watu kama hawa.

kuhusu kuongezeka kwa vitendo vya uhalifu, i don't think so, watuwamechishwa na hali ya kutokaa kwa amani.
Hapo hapo jambazi anakimbia njiani polisi wanakutana na ndugu yako wanamfananisha na jambazi waliyemuona bila kuhoji wana mshuuti au sio
 
Katika biblia kuna mwandishi anaitwa Paulo maandiko yake mpk leo inawachanganya wasomi wengi wa biblia na wanazuoni wa elimu Mungu kwakuwa Paulo alikuwa bingwa wa falsafa na aliongea kwa ustadi wa hali yajuu wenye IQ ndogo ni vigumu kumwelewa vivyo ivyo mh Rais wetu ni bingwa wa falsafa watu waropokaji wasiyotakafari kwa kina wanashindwa kumuelewa maneno yake ndiyo maana kila moja anakuja na tafsiri yake. Ni vyema kabla hujaanza kufanya uchambuzi wa maneno ya Dr Magufuli unatakiwa upate tafakuri ya kutosha ili uweze kumuelewa, mh rais aliongelea suala la wanatumia barabara ya mwendokasi watu wakamtafsiri vibaya, juzi kaongelea kuhusu ushirikiano na vyama vya siasa watu wachovu wa fikra wakasema wamezuia vyama siasa kufanya siasa Jana kaongelea mapambano ya polisi na majambazi wamebadilisha kasema majambazi wauwawe. Nadhani sasa tufike wakati tuwe watafakari zaidi kabla ya kufanya uchambuzi. Mungu mbariki shujaa na mzalendo halisi Dr John Pombe Magufuli
Inahitaji ujasiri uliopitiliza kiwango kutetea mambo ambayo yanaliingiza gizani taifa. Unaona sasa hapa unajaribu kupotosha hata ukweli ambao mheshimiwa rais amezungumza kuhusu mikutano ya siasa, na sijui unafanya haya kwa maslahi ya nani. Hivi ulisikia alizungumza nini kuhusu polisi na mikutano ya siasa jana? Eti wenye IQ ndogo hawawezi kumwelewa, kwa hiyo rais anaongea na watu asioelewa uwezo wao wa kuelewa, siyo? Unamaanisha rais ameshushwa kutoka sayari tofauti kabisa na kupewa aongoze watu asiowaelewa? Hivi kwanini mmechagua kutomsaidia rais, au mmetumwa kumpotosha ili ashindwe mapema?
 
Unaandika maandishi meengi na marefu wakati ungeweza kuyafupisha tu, Raisi Magufuli anatumia metaphor anachokisema kina mlengwa na mlengwa siku zote huelewa raisi anamaanisha nini, nitakupa mfano Raisi alivyosema kwamba wanaotumia br. ta DART wakamatwe na magari yao yang'olewe matairi sasa hiyo ni metaphor na wahusika walielewa alichomaanisha kwamba wachukuliwe sheria kali lkn watu mkafanya ikawa ishu kuuubwa wkt ni kitu kidogo tu lkn matokeo yake leo hii wanaovunja hii sheria ni wachache na watu wameanza kustaarabika!

Hivyo raisi Magufuli ni kipimo cha IQ TanZania asiyemuelewa ni kwamba IQ yake haitoshi ni rahisi kihivyo tu ndiyo maana unaona watu wenye uwezo mdogo wa kufikiri kama Mbowe, Msigwa, Sugu &Co. wanapata shida sana kumuelewa raisi anachomaanisha, watu kama ninyi mmezoea mtu awape jibu kwamba 2 +5 =7 lkn akikwambia kinyume na hapo unashindwa kupata jibu na ndiyo maana mnakuja na tafsiri zenu za ajabu ajabu lkn leo hii ukienda kuongea na wahusika wakuu wa Askari wetu watakwambia Raisi alichomaanisha, na kazi itafanyika na matokeo yataonyekana wote tutakuwa mashahidi!
Kwa uelewa wako mdogo unafikiri kazi ya rais ni kutunga mashairi? Rais hapaswi kutumia metaphor! Kwa hiyo Mbowe, Msigwa,... wanauwezo mdogo wakufikiri ila polisi wanauwezo mkubwa wa kufikiri? kila mtanzania anajifanya anajua! Hii ni element za umasikini hasa wa kichwani! Watanzania shidaaaaaaaa!!
 
Katika biblia kuna mwandishi anaitwa Paulo maandiko yake mpk leo inawachanganya wasomi wengi wa biblia na wanazuoni wa elimu Mungu kwakuwa Paulo alikuwa bingwa wa falsafa na aliongea kwa ustadi wa hali yajuu wenye IQ ndogo ni vigumu kumwelewa vivyo ivyo mh Rais wetu ni bingwa wa falsafa watu waropokaji wasiyotakafari kwa kina wanashindwa kumuelewa maneno yake ndiyo maana kila moja anakuja na tafsiri yake. Ni vyema kabla hujaanza kufanya uchambuzi wa maneno ya Dr Magufuli unatakiwa upate tafakuri ya kutosha ili uweze kumuelewa, mh rais aliongelea suala la wanatumia barabara ya mwendokasi watu wakamtafsiri vibaya, juzi kaongelea kuhusu ushirikiano na vyama vya siasa watu wachovu wa fikra wakasema wamezuia vyama siasa kufanya siasa Jana kaongelea mapambano ya polisi na majambazi wamebadilisha kasema majambazi wauwawe. Nadhani sasa tufike wakati tuwe watafakari zaidi kabla ya kufanya uchambuzi. Mungu mbariki shujaa na mzalendo halisi Dr John Pombe Magufuli




Inaonesha tayari umeshamuongeza "mkuu wa kaya" kwenye Ritania za watakatifu kwamba sasa kwenye sala zako unatamka "Mtakatifu Baba J utuombee"........,Ni jambo la kizalendo kuwa na imani kwa kiongozi wako,lakini ni uzalendo uliotukuka kwa mtu kuhoji na kutaka kufahamu mustakabali wa Taifa lake.

Kumlinganisha mwanadamu mwenye " mizuka ya ajabu"na Mitume na Manabii wa Mungu yaweza kuwa dhambi isiyosameheka mbele za Mungu wetu aliye hai.Pole sana.
 
Inahitaji ujasiri uliopitiliza kiwango kutetea mambo ambayo yanaliingiza gizani taifa. Unaona sasa hapa unajaribu kupotosha hata ukweli ambao mheshimiwa rais amezungumza kuhusu mikutano ya siasa, na sijui unafanya haya kwa maslahi ya nani. Hivi ulisikia alizungumza nini kuhusu polisi na mikutano ya siasa jana? Eti wenye IQ ndogo hawawezi kumwelewa, kwa hiyo rais anaongea na watu asioelewa uwezo wao wa kuelewa, siyo? Unamaanisha rais ameshushwa kutoka sayari tofauti kabisa na kupewa aongoze watu asiowaelewa? Hivi kwanini mmechagua kutomsaidia rais, au mmetumwa kumpotosha ili ashindwe mapema?
Ukiwa na IQ ndogo huwezi kumwelewa anachosema Mr President ila wenye IQ pana wanamuelewa vizuri nia yake. Kumbuka IQ huwezi kupata darasani ni kipaji anachoumbwa nacho mwanafamu ni zawadi kutoka kwa Mungu. IQ siyo degree au diploma au cheti
 
Pamoja na kwamba unaonekana Unajua Sana sheria lkn brother kuna mengine umeongeza kutokana na tafsiri zako tu. Rais ameongea kwa umakini mkubwa, majambazi wanyang'anywe silaha kabla hawajazitumia. Hata ikatokea Siku kuna kundi la watu watakaotafsiri kama wewe wakataka kumpeleka boss The Hague atashinda, hajasema polisi waue, wewe ndio umeandika kwamba amemaanisha hivo kitu ambacho not necessarily kwamba uko correct. Kwahiyo brother Acha kupotosha watu.
 

Wanabodi,

Wewe kama mwana JF, unapata an added advantage to be the first to know, ambapo leo katika tukio la maboresho ya jeshi la polisi, Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama, Rais, Dr. John Pombe Magufuli, ametoa kauli kwa kutumia fasihi, ambapo ameliamuru jeshi la polisi, kukabiliana na majambazi wenye silaha kwa "kuwanyang'anya silaha kwa kutumia mbinu za medani, (kivita) (MM) ambazo hutumiwa na majeshi wakati wa vita, ambapo kazi huwa ni moja tuu, kumteketeza adui!.

Amri hiyo kwa Jeshi la Polisi, inamaanisha, Polisi hawahitaji tena kuwakamata majambazi wanaotumia silaha, bali kukabiliana nao kwa kuwaua papo kwa papo, na polisi wataofanya mauaji hayo ya kuwauwa majambazi hayo papo kwa papo bila kuwapeleka mbele ya vyombo vya sheria, hawatafikishwa tena mahakamani, kama zamani, bali sasa watapandishwa vyeo!.

Agizo hilo limepokelewa kwa shangwe na makofi kwa kila aliyekuwe pale.

Rais huku akisema kwa msisitizo kwa kutumia fasihi ya "kuwanyanganya silaha", kwa vile majambazi wanatumia silaha, zenye risasi kufanya ujambazi, na jeshi la polisi nalo wanazo silaha zenye risasi, haoni kwa nini majambazi hayo yasinyang'anywe silaha zao!. Namna pekee ya kunyanganya silaha jambazi mwenye silaha, ni kumalizana nao, papo kwa papo!.

Sina shaka kabisa na nia ya dhati ya rais Magufuli, kutoa amri, hiyo, kufuatia nchi na wananchi kuchoshwa na vitendo vya ujambazi kuongezeka, hivyo majambazi wakijua kuwa wakikamatwa watauwawa right away, then, amri hii badala ya kupunguza ujambazi wa kutumia silaha, ndio kwanza utaongeza impunity kwa majambazi wanaotumia silaha, na wakati huo huo kuligeuza jeshi letu la polisi kugeuka Gestapo!.

Sio majambazi wote wanaotumia silaha, zile silaha zao zina risasi!, wengine huzitumia kutishia tuu, lakini hawana nia ya kufanya mauaji, na kuna wengine hubeba silaha ambazo hazina risasi, na wengine hutumia toy pisto!, lakini kufuatia amri hii, polisi ndio kwanza wamekuwa licenced to kill!.

Tanzania ni nchi ya kidemokasia inayofuata katiba yenye kuzingatia haki na utawala wa sheria!, amri kuu ya kwanza ya haki, ni "no one is condemned unheard", yaani hakuna mtu atakayehukumiwa bila kusikilizwa!. Amri hii ya rais, imewapa mamlaka polisi, sio tena kuchunguza, kukamata na kuwapeleke majambazi wanaotumia silaha, mbele ya sheria, bali sasa polisi hawana tena haja ya kukamata na kufanya uchunguzi, bali kukitokea tuu tukio la uhalifu wa kutumia silaha, polisi wamepewa mamlaka kuwa ni wachunguzi, prosecutors, mahakimu tena kwa kutoa "capital punishment", na hakuna tena haja ya kumsubiri rais kuzisaini hizo hati za capital punishment, bali, wao wenyewe kutumia MM, kuitekeleza adhabu ya kifo, na baada ya hapo kusubirria kupandishwa vyeo!. Just imagine mashindano ya kupanda vyeo miongoni mwa polisi wetu!.

Kama wanasheria wetu, hawatashitushwa na amri hii ya rais, nitaamini sasa Watanzania wameanza kumwelewa rais wetu, na ukiisha elewa, huna haja ya kuhoji!.

Angalizo: Sitetei vitendo vyovyote vya uhalifu wa aina yoyote, bali natetea utoaji wa haki!, hata jambazi anayetumia silaha, anastahili kutendewa haki!. Natolea mfano wa nchi mbili za Maekani na Uingeeza. Miaka ya nyuma nchi zote hizi zilikubwa na vitendo vingi vya mauaji. Uingeeza ikafuta adhabu ya kifo!, vitendo vya mauaji, vikapungua kwa kiasi kikubwa!. Maekani ikaendelea na adhabu ya kifo, vitendo vya mauaji bado vimeongezeka!.

Amri ya kuwaua majambazi papo kwa papo, haitapunguza ujambazi, bali itawafanya hao majambazi ndio kugeua wauwaji wakuu, kwa hoja za "ama zao, ama zetu" na kwenye tukio lolote la ujambazi wa kutumia silaha, polisi wakitokea, sasa sio tena kutuliza amani bali kufanya a blood bath!, hivyo polisi sasa pia watakuwa ni target ya majambazi!.

Kwetu sisi waandishi, ikitokea polisi wakakutana na gun mike, au boom mike, au hata kamera wakaiona ni kama sihaha!, kama ilivyotokea mwa Daudi Mwangosi!, askai mhusika, atapandishwa cheo!. Kama wale vija wa Zombe, sasa watawadiwa vyeo!.

Huko nyuma niliwahi kushauri, kama katiba ni kikwazo, rais Magufuli, aiweke pembeni katiba na badala yake atawale kwa kutumia 'presidential decrees' tuu!. Hivyo kwa amri hii ya polisi kuua majambazi papo kwa papo, kama mahakama ni kikwazo, pia anaweza kuiweka pembeni, na kuwatumia polisi kutoa hukumu za kifo cha papo kwa papo, tena hili litaokoa fedha nyingi sana, maana majaji wa mahakama zetu, wanahudumiwa kwa gharama kubwa sana!.

Wasiwasi wangu kwa amri kama hizi, sio ili kuokoa maisha ya majambazi wanaotumia silaha, au kuwaacha tuu majambazi wanaotumia silaha kuua, lakini wao kuuliwa tuinawatetea!, no!, wasiwasi wangu ni utekelezaji wa amri za aina hii, zisije kuwa kwa majambazi ni mwanzo tuu, baadae amri kama hizi za 'kinyemela' zikaelekezwa kwa makundi mengine, yanayoonekana ni kero!.

Mwaka 1976, kulifanyika mauaji ya wazee waliokuwa wakituhumiwa kuwa ni wachawi. Serikali kupitia waziri wa Mambo ya Ndani kipindi hicho, Ali Hassan Mwinyi Mwinyi, kupitia Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mwanza, chini ya RC Peter Kisumo, RSO, RPC, DSO, na OCD wakadhamiria kwa kauli moja kukomesha vitendo hivyo kwa hizo hizo MM alizoamrisha Magufuli zitumike!.

Katika Mahojiano, yaliyoendeshwa eneo la Kigoto, watuhumiwa wawili, Masanja Makula Mazengenuka, na Isaack Mwanamkoboko, walipoteza maisha!.

Mwalimu Nyerere alikasika sana, Waziri Mwinyi, IGP, Pundugu, Director wa TISS Mzena, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Kisumo, RSO, RPC, DSO na OCD wote wakastaafishwa kwa manufaa, na wengine kupandishwa kizimbani, ambapo wote walifungwa, isipokuwa mshtakiwa Mzee wangu, tena aliokoka kwa vile tuu alikuwa anatetewa na wakili Murtaza Lakha!.

Utendaji wa Jeshi la Polisi unaongozwa na kitu kinachoitwa Police General Ordes ambacho tumekirithi kutoka kwa Waingereza kama tulivyorithi sheria zetu mbalimbali, ambazo zina maelekezo yote ni kwenye mazingira gani polisi anaruhusiwa kutumia silaha kuwadhibiti wahalifu na kuna polisi maalum wa kazi hiyo wanaoitwa snipers au wadunguaji, ambao wana shabaha na uwezo wa kulenga maeneo rasmi ya kulenga ili kumdestabilize mhalifu kwa lengo la kumkamata lakini sio kwa lengo la kumua!. Agizo la jana la Rais Magufuli, ni kuwaelekeza polisi kuua tena kwa haraka bila kuchelewa, na sasa kwa kila mauaji ya polisi, polisi hao badala ya kupandishwa kizimbani, sasa watapandishwa vyeo!.

Japo lengo la agizo hilo la rais, amelitoa kwa dhamira njema,(in good faith), lakini utekelezaji wake, unaweza kuligeuza jeshi letu la polisi kugeuka Gestapo!, na hata Adofu alipoanza, alianza hivi hivi kwa kuwa a populist leader, anayeshangiliwa sana na umati wa watu!, ni baadae sana, ndipo watu wakaja kugundua, by that time, it was too little too late, wakaishia kujuta!, kwa upande wetu, chonde chonde twendeni taratibu jamani, tufungue macho mapema before it is too late, tusije kujuta!.

Jumamosi Njema.

Pasco


Reasonable force inaeleweka tu, wala usiogope kama umebeba silaha haina risasi na umevamia mali za watu subiri tu uone reasonable dhidi ako. Hakuna siasa apa viacheni vyombo vya ulinzi na usalama vifanye kazo zao
 
Unaandika maandishi meengi na marefu wakati ungeweza kuyafupisha tu, Raisi Magufuli anatumia metaphor anachokisema kina mlengwa na mlengwa siku zote huelewa raisi anamaanisha nini, nitakupa mfano Raisi alivyosema kwamba wanaotumia br. ta DART wakamatwe na magari yao yang'olewe matairi sasa hiyo ni metaphor na wahusika walielewa alichomaanisha kwamba wachukuliwe sheria kali lkn watu mkafanya ikawa ishu kuuubwa wkt ni kitu kidogo tu lkn matokeo yake leo hii wanaovunja hii sheria ni wachache na watu wameanza kustaarabika!

Hivyo raisi Magufuli ni kipimo cha IQ TanZania asiyemuelewa ni kwamba IQ yake haitoshi ni rahisi kihivyo tu ndiyo maana unaona watu wenye uwezo mdogo wa kufikiri kama Mbowe, Msigwa, Sugu &Co. wanapata shida sana kumuelewa raisi anachomaanisha, watu kama ninyi mmezoea mtu awape jibu kwamba 2 +5 =7 lkn akikwambia kinyume na hapo unashindwa kupata jibu na ndiyo maana mnakuja na tafsiri zenu za ajabu ajabu lkn leo hii ukienda kuongea na wahusika wakuu wa Askari wetu watakwambia Raisi alichomaanisha, na kazi itafanyika na matokeo yataonyekana wote tutakuwa mashahidi!
Tafsiri ya Pasco ni sahihi na Msemaji hakutumia metaphoric language. Metaphor ni kulinganisha mtu au kitu au jambo na kitu kingine bila kutumia neno la kulinganishia. mfano rais ni Simba. au Pasco ni Jembe. neno lingingine ni "simile" hutamkwa "similii" ambapo hulinganishwa kwa kutumia kilinganishi "kama" mfano rais ana nguvu kama simba.
Tamko la rais is so direct na wala IQ unayosema siui ni ipi!
 
Kwani sifa ya kuwa na uwezo mkubwa mpk uongoze watu wangapi? Au wewe ni moja wao waliyoambiwa wannyang'anywe silaha?
 
Ukiwa na IQ ndogo huwezi kumwelewa anachosema Mr President ila wenye IQ pana wanamuelewa vizuri nia yake. Kumbuka IQ huwezi kupata darasani ni kipaji anachoumbwa nacho mwanafamu ni zawadi kutoka kwa Mungu. IQ siyo degree au diploma au cheti
Swali langu ni kwamba: rais anazungumza na hadhira asiyoielewa? Kwanini mnaanza kumdhalilisha rais kwa kiwango hiki; nani anawatuma?
 
Mkuu kama ni organized crime anawafanya police kuwa target kwa majambazi. Hawa wanaofanya hizo organized crimes they are well trained, wengi ni ex police or para military officers na wao wamemsikia nao watajiandaa kukabiliana kujilinda na mauti. Mimi wasiwasi wangu uko kwa police wetu. Uelewa wao katika hili, Wengi wasivyowaelewa wanaweza kutumia fursa hii kuuwa innocent people kwa kisingizio cha ujambazi ili wapande vyeo.
KATIKA YOTE TUSIBIRI KWANZA MZIGO HUO UANZE NDUGU ZANGU TUKIPATA MAJIBU YA HILO KUWA LINA FAIDA AU HASARA TUTAHAILISHA KAMA VILE ULE MZIGO WA MSOSI MUHIMBILI SIMPLE TU.SERIKALI NI SIKIVU SANA NAAMINI HIVYO NA INAJALI WANANCHI WAKE.PIA MSIMLAUMU SANA MTOA MADA...AMETOA HISIA NA MAWAZO YAKE KAMA VILE MKUU WA KAYA ALIVYOSEMA KWA HISIA.ILA SASA"UKIONA MAJAMBAZI WAMEVAMIA SEHEMU,UKAAMBIWA LALA CHINI..LALA HARAKA SAANA NA USIJE JISHAURI WALA KUJIFANYA MASTER"HIKI NI KIPIMO KIKUBWA SANA,TUTAJUA KUWA USAHIHI UPO WAPI PINDI TU MATUKIO YAKIANZA.NAMALIZIA PIA UKISIKIA TENA KUNA MAJIBIZANO YA RISASI BAINA NA NDUGU HAO NA ASKARI WETU PIA JIFUNGIE HARAKA SANA.SIOMBI NACHOWAZA KITOKEE ILA KILA KINACHOBANWA SAANA SANA KINA NAFASI PIA YA KUJIACHIA."KILA KITU NI SAWA TU"
 
Inahitaji ujasiri uliopitiliza kiwango kutetea mambo ambayo yanaliingiza gizani taifa. Unaona sasa hapa unajaribu kupotosha hata ukweli ambao mheshimiwa rais amezungumza kuhusu mikutano ya siasa, na sijui unafanya haya kwa maslahi ya nani. Hivi ulisikia alizungumza nini kuhusu polisi na mikutano ya siasa jana? Eti wenye IQ ndogo hawawezi kumwelewa, kwa hiyo rais anaongea na watu asioelewa uwezo wao wa kuelewa, siyo? Unamaanisha rais ameshushwa kutoka sayari tofauti kabisa na kupewa aongoze watu asiowaelewa? Hivi kwanini mmechagua kutomsaidia rais, au mmetumwa kumpotosha ili ashindwe mapema?



Mkubwa kujaribu kupambana kihoja na watu waliowekewa mpaka wa ukomo wa fikra zao(rejea tamko toka kwa viongozi wa ngazi za juu wa chama na serikali ya ccm kwa wabunge wa ccm watakaopinga hoja za serikali bungeni)ni kujipotezea muda,hawa watu wameshafungiwa ndani ya box,hawawezi kuwa na fikra huru tena.Ni watu wa kupuuzwa tu kama Mh.Jussa Radhu anavyoendelea kumpuuza Mpanju.
 
Hizo hela za kufanyia maandamano ,nawashauri chagadema wajenge ofisi yenye hadhi ya chama kikuu cha upinzani nchini.

Hii tabia ya kuandamanisha watoto wa wenzenu na kuwashindisha juani ikome Mara moja. @ Nyumbu




Shangata ubongo wako uko sawasawa kweli? Mbona unaleta mada tofauti na iliyomezani? Unatumia ubongo kufikiri au umejaa uji kichwani?
 
UKAWA KUITISHA MAANDAMANO YA KUWATETEA MAJAMBAZI YASIULIWE NA POLISI.

TAARIFA ZINASEMA UKAWA WAKO TAYARI KUUNGANA NA POLISI WAKATI WA MAPAMBANO NA MAJAMBAZI ILI WAWEZE KUWATAMBUA MAJAMBAZI YENYE SILAHA NA KUJARIBU KUWABEMBELEZA WASIVAMIE RAIA.

KATIKA HARAKATI ZAO ..UKAWA WAMEENDA MBALI NA KUANZA KULIFIKISHA MAHAKAMANI JESHI LA POLISI KISA TU LINAPAMBANA NA UHALIFU ULIOKITHIRI...

MASELA HAWA WA UKAWA PIA WANATARAJIA KUBADILI GIA ANGANI NA KUMPA MKUU WA KIKOSI CHA MAJAMBAZI UWANACHAMA WA CHADEMA FASTA FASTA ILI AWEZE KUGOMBEA URAIS WA NCHI HII MNAMO MWAKA 2020 ...

IKIWA UKAWA WATAFANIKIWA KATIKA HILI BASI ILE ADHMA YAO YA NCHI KUTOTAWALIKA ITAKUWA IMETIMIA NA WAO WATAENDA DUBAI NA UJERUMANI KULA BATA.

MAELEKEZO YA KAMATI KUU YAO KWA SASA NI KUSUSIA SHUGHULI ZOTE ZA POLISI IKIWEMO KUTOKUPIGA SIMU POLISU KWA KUTUMIA KITUO KIPYA CHA POLICE CALL CENTER PALE WANAPOVAMIWA MAJUMBANI MWAO WAMEWAASA WANANCHI KUFANYA HIVYI HIVYO ILI KUWALINDA WAPIGA KURA WAO YAANI MAJAMBAZI VIBAKA NA WALA NDUMU.

NIKIRIPOTI KUTOKA UFIPA NI MIMI MWANDISHI WENU NILIYESOMEA SPECIAL DIPLOMA




Ndiyo maana ukaitwa jingalao
 
Back
Top Bottom