Hili la Polisi kuruhusiwa 'kuwanyanganya' silaha majambazi na kupandishwa vyeo limekaaje?

Kwakuwa hauna ndugu au jamaa yako wa karibu alieuawa na majambazi utaona kama JPM anakosea,
Na kwa kuwa huna ndugu au jamaa wako wa karibu aliyeuawa na polisi kwa kisingizio cha kupambana na majambazi (kumbe ni njia ya kuchukua fedha au mali zake), utaona kama JPM anapatia
 
Mwengeso, hivi kwanini Magufuli anaongea kwa kiswahili na nyie mnamsaidia kutafsiri kwa kiswahili, huoni kuna shida hapo?
Sawa, kiingereza hapo tumekubali ni bilabila, atafsiriwe!
Na Kiswahili je?
 
Ni kweli anakuja kwa kutaka ulicho nacho na anajua kweli unacho habatishi ila ikifikia swala la polisi hapo wanakula pamoja na haki yako hauipati. Ukweli polisi na hao jamaa ni sawa na paka na samaki kila mmoja anapenda. kinacho tula sisi ni polisi wetu.
 
Inaonekana JPM hakufuatilia kesi ya kina Zombe & co. na hawajui sawa sawa polisi wetu!!! Napata woga sana!!!!
ukikopi uzi mrefu namna hii na kukomenti maneno mawili, unatuumiza sisi tunaotumia visimu vya mchina.
Samahani kwa usumbufu.
 
kwa nn atumie mafumbo ambayo anajua wengi hawatomuelewa lengo lakuzungumza na wanachi ni nn sasa?
 
Something pigs kila kitu ni kupinga tu!! Unawatetea majambazi?? Hapa mwanza walikuwa wanaua na kupora maduka ya mpesa unamteteaje mtu kama huyo,,subiri waje wakuinamishe siku moja ndo utajua majambazi sio wenzako
 
Yule trafic alipe pewa order ya Rais apandishwe cheo hadi leo hajapandishwa. Hapa kazi tuu
 
Ukiona anaongea,alafu kuanzia waziri wa wizara husika hadi IGP wanatabasamu..we jua kuwa alikuwa anagmfurahisha jukwaa!!

Ila katika hali ya kawaida majambazi wanakera Sana,kama mwizi wa kuku mtaani anakamatwa na kutwangwa hadi kufa..iweje kwa jambazi anaekuja na kunijerui kisha kuchukua Mali yangu???
Police watekeleze huo utani waliotaniwa bila kubambikia watu makesi ya kijinga kisa kutaka vyeo..maana hawachelewi kuja na kukupa gobore kisha wakakutandika risasi za kifua na kukuburuza kwenda kupandishwa cheo!!

Kama walengwa ni majambazi wa kweli basi utani huo na ukaanze kufanya kazi..
Tumechoka kutafuta kwa jasho then yanakuja majitu yanakupora kama uliyafanyia kazi!!

Na hawa Wa huku mitaani wanaopora simu zetu tutajitahidi TUWANYANG'ANYE HARAKA HARAKA kabla hawajakimbia nazo..
 
Ha ha ha ha ha, mkuu nayaona maumivu nafsini kwako, mtaani kwetu kuna Mzee mmoja alishawahi kuibiwa baiskeli miaka ya nyuma, yeye akisikia kelele za mwizi cha kwanza anatafta lungu lake, pili lazima aje na kiberiti na tatu lazima aje na nyasi zilizokauka za kutosha!
 
Wewe hujaelewa anachomaanisha pasco watanzania ni wavivu wa kusoma na kutafsili hebu ludia kusoma uzi ukishindwa kuelewa anachomaanisha njoo jamvini useme tukueleweshe
 
Akina zombe &co waliua majambazi? Sio kila kauli ni ya kushabikia siku akiuawa ndg yako kisa katembea na demu wa askari utashelehekea?
 
Tunashukuru kwa ufafanuzi ila mwandiko wako kama wa Jesykah
 
Mkuu,wezi ni wato wabaya Sana na hawafai kabisa kujumuika na jamii..hebu fikiri huyo mzee alitumia muda gani kupata usafiri mwingine???

Nilipata kuwa katika kijiji flani kuna mzee kidogo yuko na uwezo pale,walivamia kwake wakamtaka awape hela za walijua anazo maana alitoka kukusanya kodi zake huko..mzee alikuwa ameshaweka bank..hawakuelewa walimtandika risasi za kichwa na kufuani akafa pale pale..

Sasa katika hali kama hiyo naanzia wapi kuwatetea watu kama hao???

Watu tumewahi kukoswakoswa kuuliwa na haya majitu..Leo nitoe wapi ujasiri Wa kuyatetea!!

Watu WAOVU kama hawa ni WAKUPOKONYWA SILAHA HARAKA HARAKA!!

Wakati mwingine wanapora na kuuwa watu..hata hawafungwi!!

Dawa ni KUWAPORA SILAHA HARAKA HARAKA!!

Angalizo ni kwamba,hii iwahusu MAJAMBAZI TU!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…