Uchaguzi 2020 Hili la Sheikh Ponda liacheni. Hatua ya Ponda ni kwa maslahi ya Waislam na Watanzania

 
Nasubiri tamko kutoka kwa Maaskofu wangu wa Katoliki kuhusu kumtenga na kutomchagua yule mgombea mkatoliki aliyeahidi hadharani kuoa mke wa pili kinyume kabisa na utaratibu wa Kanisa letu linalo amini uwepo wa ndoa ya mke mmoja tu!
Ni yule aliye ahidi kumwoza mama yake mzazi kwa mtu aliyempa jogoo?
 
Vipi kuhusu anayebagua wananchi wake kwa kutopeleka miradi yamaendeleo kwenye majimbo ya wapinzani?
 

Tukusikilize wewe ,tumpigie kura Magufuli tuendelee kuyapata haya mateso au tumsikilize Sheikh Ponda tumchaguwe Lisu aliyeahidi kuyaondosha madhila haya?
 

Attachments

  • VID-20201021-WA0000.mp4
    18 MB

Kutokupiga kura ndio unawarahisishia kazi hao unaojifanya kusema ni madhalimu
 

Attachments

  • VID-20201021-WA0014.mp4
    5.2 MB
Siasa ipi unayotaka kutuambia , au ya kuwaweka hawa aliotudhulumu muda mrefu ??? Ndugu zetu wako majela kwa makosa ya kubambikiziwa na Majambazi hawa , unataka tujikalie kimya ??
Ushawahi kuwa na ushahidi halisi wa hayo unayoyasema, mbali na kusikiliza mtandaoni?

Aina hii ya siasa ya kuzuliana majukwaani, kupakaziana uzushi Uislamu hairuhusu kwani inapiga vita uongo na uzandiki wa mambo hayo. Kufungamana na siasa hiyo ni makosa, hivyo Sheikh Ponda hayupo sahihi na amekiuka mifumo ua kiislamu.

Siasa halali kwenye Uislamu ni ile ya mfumo wa uongozi wa serikali ya kiislamu pekee. Na si hii ya kuongea uongo na uzandiki, kuzushia mtu na akija upande wa pili basi mnamsifia.... Kiyfupi dini haiendani na siasa za namna hiyo
 
s munaleta udini bas nchi hii hataweza kuongoza mwislam hata siku moja, sie wakrist ni weng kinyama nchi hii!! all in all acheni ujinga wa kuleta udin wa kiislam hapa ponda kakosea anashili adhabu yake kutoka kwa masheh.
 


Ponda ameunga mkono upinzani kwa sababu upinzani umeonyesha dhamira ya dhati ya kuwaachilia huru masheikh wetu na hilo ni jambo zuri na la kuigwa na kila muislamu nchini.

Kuiunga mkono CCM kwenye uchaguzi huu maana yake ni kuisaidia katika uonevu na udhalimu wake dhidi ya masheikh na maulamaa wetu!

Sheikh Ponda hajakiuka mfumo wowote wa kiislamu la sivyo wewe unataka kutuma meseji kuwa waislamu wasipige kura, wasigombee wadhifa wowote wa kisiasa nchini. Yaani unamaanisha mzee Mwinyi na Kikwete walitenda dhambi kugombea uraisi na kuwa maraisi!!!. Ajabu hii!!!

Yaani ukija na mawazo hayo unamaanisha masheikh wote waliomsaidia Nyerere kumng'oa mkoloni wote walikiuka uislamu n.k

Unao mfano wa nchi yeyote duniani inayoongozwa kwa mfumo unaouita wa kiislamu?, au elezea mfumo wa kiutawala wa kiislamu ni upi na mfano wake ni upi?

Mawazo yako siyo sahihi!
 
Ninaweza kukubaliana na post yako.

Ila kwa hili huwa siamini Sana.

Kweli ingekua mbaya Kama teuzi zote zingekua za Dini moja.

Ila hatuwezi kulazimisha lazima uwiano uwe 50:50.

Maana mteuzi huangalia mtu ambaye atamfaa kwa kazi anayohitaji ifanyike. Sasa Kama katika uteuzi wake ikatokea umelalia upande Fulani tusiamini Kama alidhamiria kulalia huko.

Tuangalie Je Kuna ubaguzi wa dhahiri wa sera , ama Sheria au utendaji wa kupendelea upande mmoja au kukandamiza upande mmoja.?

Hapo lazima wananchi wote tukemee na kushinikiza vitendo hivyo vikome.

Ila swala la Nani kateuliwa, Kama anafuata taratibu za Kisheria na katiba( katiba yetu Haina upendeleo wa Kidini).

Basi hiyo sio hoja.
 

Hatuzungumzi kubalance, kusema kweli mimi mwenyewe siyo shabiki wa kubalance ila kuna fairness fulani ikikosa unaiona wazi kuwa sonething is wrong!

Hebu fikiria, hivi kwa nini haijawahi kuwa kinyume, yaani all the time kila teuzi zinazoinvolve watu wengi unakuta watu wa imani moja ni wengi kuliko wa imani nyingine? .

Usiniambie kuwa hakuna waislamu wa kutosha wenye elimu na vigezo vya kushika nafasi maana waislamu wenye ekimu na sifa wapo kutosheleza kila aina ya nafasi, maana nafasi na teuzi zote hazizidi watu 2000, na kuna maelfu na maelfu ya waislamu wenye madigrii, uzalendo, ujuzi, nidhamu na kila aina ya sifa.

Hivi una habari kuwa rais akiamua anayo mamlaka ya kuteua 80% ya hizo teuzi kuwa ni wasukuma kushika nafasi za wakuu wa mikoa, wa wilaya, wakurugenzi n. k. kisha akajitetea kuwa kwani hawa niliowateua hawana sifa?. Na kweli kila ukiangalia vigezo wanavyo!. Lakini akifanya hivyo siyo sahihi ni Ukabila wa wazi. Hivyo hivyo kuteua 80% watu wa dini moja wakati hata watu wa dini nyingine wapo wenye vigezo ni udini wa wazi!

Ngoja nikupe challenge tu, itokee raisi Muislamu nchini halafu kia teuzi anagonga 80% waislamu, 20% Wakiristo halafu uje uone kelele za udini zitakavyomuandama kila kona!

Jiwe hana aibu ananuka udini ajabu!
 

Kwa hivyo ndugu yangu aendelee kusota gerezani kwa kosa la kwenda kuposa mtoto wa mtu aliyebambikiziwa kesi ya ugaidi. Viongozi wa CCM waendelee kutuibia pesa tunazokatwa kodi huku wengine wakijijengea majumba zaidi ya 30 . Unataka Tuusubiri huo uongozi wa mfumo wa kiislamu?
 
Nitoe mimi, asinihusishe kabisa na sichaguliwi wa kumchagua

Ndugu yangu naomba kura yako umpigie Lissu ili akawatoe maulamaa na masheikh wetu wanaosota Jela kwa sababu ya udhalimu wa serikali ya CCM

Kura yako ni msaada kwa wake, watoto, ndugu na familia za masheikh wetu zinazoangamia na kuteketea kwa ukosefu wa kiongozi wa familia ndani ya nyumba.

Kama wewe siyo muislamu basi wanusuru ndugu zako binadamu wenzio wako jela kwa sababu ya uonevu wa serikali ya CCM

Kama wewe ni muislamu basi jua ndugu zako hao katika imani wana hali ngumu sababu ya dhulma. Na wewe una dhima ya kuwasaidia. Sasa wasaidie hawa kwa kuweka mtu madarakani atakayekwenda kuwaachia huru.
 
BORA LISSU IKIWA UTAMUONA KAFIRI KULIKO MUISILAMU MNAFIKI IKIWA UTAMUONA NA JEI KEI..
BORA KAFIRI KULIKO MUISLAM MNAFIKI
 
BORA LISSU IKIWA UTAMUONA KAFIRI KULIKO MUISILAMU MNAFIKI IKIWA UTAMUONA NA JEI KEI..
BORA KAFIRI KULIKO MUISLAM MNAFIKI
Lissu asingekuwa mnafki asingempigia kampeni Lowassa 2015 ambaye alituambia ni fisadi,ila alivyo mnafki akala matapishi yake kisha akatuambia et kama Lowassa ni fisadi mbona hashtakiwi?

Lakini kama haitoshi Lissu alituambia kuwa ACT si chama cha upinzani na hakijawahi kuwa chama cha upinzani bali kipo hapo kuuwa upinzani kinatumika na serikali,na akamtaja hadi Zitto kabwe kuwa sio mpizani anatumika na serikali. Sasa alivyo mnafki et sasa hivi anashirikiana na chama kisicho cha upinzani(ACT), Lissu atuambie ni lini ACT kimekuwa chama cha upinzani hadi yeye amekubali kushirikiana nacho?

Huyu ni namfki na maneno yake ya kisiasa kama walivyo wanasiasa wengine,sasa kama waislamu wameingia kwenye 18 za huyu mwanasiasa basi ni uamuzi wao ila hakuna kitu hapo.
 
Mkuu Lisu hakutumwa na Amsterdam kuja kuwaokoa au kuwasaidia waislam usijidanganye kabisa, Lisu ana maslahi yake binafsi si Kwa waislam wala watanzania, wewe mchague Mimi nitachagua nitakaye, pia hakuna kiongozi upande wa pili atamsaidia Islam kama tumeshindwa kusaidiana wenyewe
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…