Raimundo
JF-Expert Member
- May 23, 2009
- 13,416
- 12,618
Ishu ya mwalimu bank wala haina nguvu hapa ishu ni serikali kutoa pesa zake kwenye mabank ya biashara NMB ikiwemo na bado wasipokuwa wabunifu watayumba sana,wajipange kwakweli.
Tamko la Serikali kuhamisha account zake ni la January 2016, na kabla ya hapo trend ilikuwa ya kushuka.
Feb 2015, bei 4,300/- wakati Feb 2016 bei ni 2,200/-.
Kwa hiyo hiyo ya kuhamisha acc nayo siyo sababu, na sina uhakika kama kweli hilo zoezi limeshafanyika.
Sababu ninazoweza kuzifikiria ni:-
1. Ushindani wa kibiashara, benki nyingi Multinationals zilizokuwa hazitoi mikopo midogo midogo zimeanza kutoa, kwa hiyo zinakuja kupambana na NMB moja kwa moja
2. Mikopo inayofeli, watu wengi tumeshindwa kulipa mikopo kwa wakati, hivyo kupelekea hasara kwa mabenki husika, ukiangalia kwenye mahesabu yao utakuta impaired loans zinaongezeka kila kukicha
3. Mitandao ya simu kuja kufanya kazi za kibenki imepunguza sana fedha benki ilizokuwa inapata kama vile trensfer charges, withdraw charges, ATM charges etc etc. Ndiyo maana sasa hivi kila benki inajaribu kuwa na mobile banking ili kukimbizana na hizi kitu.
4. Ongezeko la mabenki kama alivyosema The Boss pia siyo la kubeza, na wote wanagombea soko moja
5. NMB imejenga jengo lake hapa karibu na Serena, ile ni investment kubwa sana na lazima kwa namna moja iathiri mzunguko wa fedha, mfano fedha ambazo wangewekeza kwenye Bonds, Bills au kuzikopesha zikaleta interest zimeenda kwenye kujenga, na ukute pia na wao wana mkopo wa hilo jengo (kama ni part financing ambayo ni obvious) watakuwa wanasevu riba pia.
Hayo ni baadhi tu.