Hisia: Kuna idadi kubwa ya Watanzania wanaosumbuliwa na Stockholm Syndrome ikija kwenye kutawaliwa na CCM!

Teuzi hufanyika kulingana na mahitaji ya Nyakati husika
Hilo ni kweli, ila ndio awe Makonda sasa? Hapo ndio utajua Bado ccm kumejaa wajinga wengi na wanaoamini katika kutumia mabavu.
 
Sukuma Gang ni dhana ya uongo, haijapata kuwepo katika uhalisia.
 
Tatizo la siasa za nchi yetu zimejikita katika ubingwa wa kutoa lugha chafu, matusi na kebehi, na kwa hilo Makonda ni bingwa!
Kwa hiyo polisi hawatakamata watu tena??
 
Kwahali ya sasa ya utawala wa bibie hauna lolote jipya,wanachofanya ni kupita mulemule alipopita meko...mpka tufike 2025 utaona maajabu huko ccm,bashiru,polepole watarudishwa na kupewa nafasi kubwa chamani.
Utaweza kusikia mkurugenzi wa NEC ni simon siro
 

Hivi lini watanzania tutaacha chuki?..una uhakika gani that guy has committed those dirty deeds?.
 
Refuu imejaa majungu unafiki, roho mbaya, wivu
 
""Manake haiingii akilini kabisa! Iweje mtu kama Paul Makonda mwenye kashfa nyingi zihusuzo uvunjwaji na ukiukaji wa haki za kibinadamu na makandokando mengine mengi kurudishwa kwake kwenye uongozi wa chama chake kufurahiwe namna hiyo na watu"""



Marekani inaiharibu Dunia kila sehemu ina ujinga usiomithirika ila unamuona Makonda tu

Kumjadili tu ni kumpaisha
 
Watanzania wako zaidi ya milioni 60.

CCM na wanachama wao hawazidi hata milioni 10.

Watanzania zaidi ya milioni 50 tunashindwa nini kuwaondoa CCM?

Uoga tu.
Kuwaondoa ccm halafu uweke chama gani? Chadema iliyojaa ukabila na wahuni? Tatizo hakuna chama mbadala wa ccm
 
Sehemu kubwa ya wachangiaji nadhani wanajaribu kutaka kupata picha ya nini hasa kimetokea mpaka akateuliwa ?!

Je upo mpasuko Chamani ?
Watu wanaunganisha dots kwanza ule uhamisho wa Chalamila kuletwa Dar na huu wa Mwenezi wa Chama kuteuliwa hivi sasa !
Watu wanajiuliza na wanataka kujua je remote imeisha betri ??!
😅😅😅🙏🙏
Speculations kama kawaida ya wabongo ndio inayosumbua !!
 
Mkuu umesema kweli. Tuna taifa lenye watu wapumbavu wengi sana. Kuna wengine wanadiriki kuandika kuwa eti ndiye Rais wa Tanzania mwaka 2030.

Nimeshangaa sana mawazo kama haya. Wengine wanasema eti kaI ya Mwenezi wa CCM ni sawa kuwafuatilia mawaziri na ma RCs.

Kama kweli Rais kamteua ili atumike kuwabwatukia Mawaziri wazembe, basi ni bora Rais akubali kuwa ameshindwa kuwasimamia watu aliowateua mwenyewe. Tujue tunatafuta Rais mwingine
 
Angalau alijaribu kupambana na wauza ngada.
 
Hukuwa na haja ya kutumia Stockholm syndrome pasipo kueleza bayana hicho ni kitu gani, na kashafa nyingi za Makonda ni uzushi na wivu, Enzi za Magufuli Makonda alisaidia wenye shida ikiwemo wajane na waliodhulumiwa Mali zao
 
 
Ukweli uwekwe wazi !! Kwa hali ilipo fikia CCM imeharibu pakubwa uwezo wa watu kufikiri sawasawa na kupambania mambo yakinifu Kwa utimamu wake.

Hata kama Mimi siijui vyema ccm lakini Kwa Yale tuliyo yaona na kusikia Makonda akiwa RC Dar hafai kuwa na nafasi kama aliyo pewa sasa.


Otherwise mabosi wake Wana sababu za kutunza masilahi ya wachache au Binafsi. Ni si Kwa faida ya taifa.
 
Hii ilikua bonge moja ya content km kichwa kingesomeka hivi:

Hisia: Kuna idadi kubwa ya Watanzania wanaosumbuliwa na Stockholm Syndrome.

Full stop.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…