Historia kuandikwa leo Tanzania: Yanga na Laliga kusaini mkataba wa mchakato wa mabadiliko wa mfumo wa klabu

Protect

Senior Member
Joined
Apr 4, 2020
Posts
103
Reaction score
362
WanaJF,

Leo kuanzia saa moja usiku nchi itazizima kwa kufanyika tukio kubwa la kihistoria hapa nchini wakati mabingwa kwa kihistoria nchini, Yanga na kampuni ya Laliga ya Spain watakapokuwa wanaingia mkataba wa kuanza kwa mchakato wa mabadiliko ya mfum wa uendeshaji wa timu ya Yanga

Mchakato huo wote utadhaminiwa na kampuni ya Chapa GSM ambao pia ni wadhamini na wafadhili wa klabu ya Yanga. Katika makubaliano hayo wataalamu wa La Liga kwa kushirikiana na Kamati ya Mabadiliko watafanya kazi kupata mfumo sahihi wa uendeshaji wa klabu.

Makubaliano hayo ya leo yatafanyika kwenye hotel ya Serena ya jijini Dar es Salaam na kurushwa live na Azam TV pamoja na youtube channel ya Yanga na kupitia social media zote za Yanga

Rais mstaafu wa awamu ya nne, Mh Jakaya Kikwete ataongoza dozeni ya viongozi watakaokuwepo hapo Serena Hotel kushuhudia historia hiyo ikiwekwa hapa nchini

Yanga sasa inakwenda kuwa klabu kubwa na tishio kabisa Africa

Kama ilivyokuwa ada ya JamiiForums, wanaJF tutakuwa hapa tukifuatilia tukio hilo na kuhabarishana kinachoendelea

Karibuni Sana

Wape Salamu
 
Yaani Mess na Luis watakuja kuichezea yanga au tena kwa mkopo? Simba watajinyonga
 
Yanga wapuuzi sana. Wanapenda vitu cheap ndio mana wamewafata laliga ambao wameshindwa kuifanya ligi yao kuwa maarufu duniani ingawa Wana facilities zote.
 
Yanga wapuuzi sana. Wanapenda vitu cheap ndio mana wamewafata laliga ambao wameshindwa kuifanya ligi yao kuwa maarufu duniani ingawa Wana facilities zote.
Wamejaribu kwa kurudisha nyuma masaa ya mechi zao ndio maana kuna baadhi ya games zao hadi huchezwa saa 7 mchana kwa saa za Tanzania.
.
Tatizo lao ni promotion ya ligi pamoja na lugha hivi vimewashinda. Mechi ya Watford vs Aston villa inamvuto zaidi kuliko mechi ya Athletic Bilbao vs Espanyol!
 
Hivi mnajua maana ya NCHI KUZIZIMA? Nchi izizime Yanga kusaini mkataba ahahaha basi itakuwa nchi ya wendawazimu.

Sick of that word!
Kama taifa linasaini makubaliano ya mabilioni ya dollar na barick and nobody cares ije kuwa mikataba ya La liga ambao wapo hapa Tanzania kwa muda mrefu na wala hata hatujali LMAO!
 
Aiseeeee, mimi huko nyuma nilikuwa shabiki nguli sana wa Dar Young African sports Club, lakini baada ya kugundua ya kwamba kufuatilia soka la bongo ni matumizi mabaya ya akili na muda, siku hizi nimebaki kuwaona tu mnatifuna na kutambiana [emoji38][emoji38][emoji38]
 

Tusiandikie mate mdau, subiri ifike Kuanzia saa 12 jioni uone Kama utaona mtu mtaani, kila mtu atakuwa kwenye TV akifuatilia tukio la kihistoria kwenye nchi yetu
 
Umaarufu wa msimu? Mpaka elclassico ndio dunia ijue Kuna gemu? Ronaldo kaondoka amehama na umaarufu wake sahii watu wanafatilia serie A. Messi akistaafu ataastaafu na umaarufu wake hivyo pia kupunguza mvuto wa laliga.

Kwahiyo Lecce wakiwa wanacheza na Genoa, Tandahimba watu wanakuwa wanajua? au Kakamega Kenya wanakuwa na taarifa hiyo?
 

Rudi nyumbani sasa kumenoga, Yanga inakwenda kuwa katika level nyingine kabisa hapa Africa
 
Yanga wapuuzi sana. Wanapenda vitu cheap ndio mana wamewafata laliga ambao wameshindwa kuifanya ligi yao kuwa maarufu duniani ingawa Wana facilities zote.
Ni kweli Wameshindwa kufanya ligi yao iwe maarufu, lakini wameweza kuifanya ligi yao iwe bora na na kuzifanya timu zao ziwe bora pia. Umaarufu na ubora ni vitu viwili tofauti
 
Umaarufu wa msimu? Mpaka elclassico ndio dunia ijue Kuna gemu? Ronaldo kaondoka amehama na umaarufu wake sahii watu wanafatilia serie A. Messi akistaafu ataastaafu na umaarufu wake hivyo pia kupunguza mvuto wa laliga.
Baada ya Premier League ya England, La LIGA inafuatia kwa mapato (revenue) na ina timu zilizochukua UEFA mara nyngi kuliko timu za ligi nyingine (60 times).
 
Tusiandikie mate mdau, subiri ifike Kuanzia saa 12 jioni uone Kama utaona mtu mtaani, kila mtu atakuwa kwenye TV akifuatilia tukio la kihistoria kwenye nchi yetu
So kila mtu ana Azam tv?
Ahahahaha embu acha kuchekesha watu, Simba na Yanga zenyewe zikicheza watu wanaendelea na shughuli zao sembuse mkataba 😂
.
Hivi unajua La liga wapo Tanzania toka lini?
 
Baada ya Premier League ya England, La LIGA inafuatia kwa mapato (revenue) na ina timu zilizochukua UEFA mara nyngi kuliko timu za ligi nyingine (60 times).
Timu za La liga kuchukua UEFA mara nyingi haimaanishi yenyewe ni maarufu au inapendwa sana.
.
Timu za La liga zina matumizi makubwa ya pesa kuliko zinachoingiza ndio maana ziko radhi hata kununua mchezaji kwa pesa kubwa sana.
.
PSG wanajaribu hili wanakuja kufeli kwenye machaguo wanachagua wachezaji wa daraja la dunia, wana akili sana ila hawana commitment! Hawajitoi kabisa.
 
Baada ya Premier League ya England, La LIGA inafuatia kwa mapato (revenue) na ina timu zilizochukua UEFA mara nyngi kuliko timu za ligi nyingine (60 times).
Spain umaarufu hauletwi na ligi yao isipokuwa vilabu viwili tu. Nasisitiza NI vilabu viwili tu. So watu hawafatilii ligi isipokuwa vilabu hivyo viwili basi. Nahivyo vitafatiliwa kwenye elclassico au eufa championship.
 
La liga ina mapato kuliko ligi nyingine ukiondoa EPL. Mapato ni kitu cha maana zaidi kuliko umaarufu. Umaarufu wakati huingizi hela, unakuwa hauna maana inakuwa kama ligi za singeli.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…