Historia ya Abbas Kleist Sykes na Julius Kambarage Nyerere (1952 – 1999)

Historia ya Abbas Kleist Sykes na Julius Kambarage Nyerere (1952 – 1999)

Sheikh Mohammed Said hawa wanaokataa hii historia unayokuja nayo hapa, kama wanaona si kweli wangekuja na yao ingependeza kwelikweli, ila nafkiri wasifanye chuki na maandiko yako bali wanachopaswa ni kujiuliza kwanini unachokijiua wewe hakifanani na walichonacho vichwani mwao.
 
Sheikh Mohammed Said hawa wanaokataa hii hustoria unayokuja nayo hapa, kama wanaona si kweli wangekuja na yao ingependeza kwelikweli, ila nafkiri wasifanye chuki na maandiko yako bali wanachopaswa ni kujiuliza kwanini unachokijiua wewe hakifanani na walichonacho vichwani mwao.
AVRAM,
Ni bahati mbaya sana kuwa historia hii imetia hofu na kusababisha taharuki kubwa.
Hii ndiyo historia ya TANU hakuna nyingine nje ya hii na hili linajulikana.
 
Mzee Said, Abbas Ni mtoto wa nani? Nipe mtiririko vizuri kuanzia baba yao hadi hawa akina Abass na Kaka zake
 
Mzee Said, Abbas Ni mtoto wa nani? Nipe mtiririko vizuri kuanzia baba yao hadi hawa akina Abass na Kaka zake
Nemo,

1574248347696.png

Kushoto waliokaa: Kleist Sykes (1894 -1949), Abbas Sykes (1929 - ),
Nyuma kushoto Ally Sykes (1926 - 2013), Abdulwahid Sykes (1924 - 1968)
Picha hii ilipigwa 1942 Abdul Sykes aliporudi Dar es Salaam kuaga kutoka Lower Kabete
Kenya kabla ya kwenda Burma Vita Vya Pili Vya Dunia (1939 - 1945) akiwa katika
King's African Rifles (KAR)

1574249185458.png

Bi. Mruguru bint Mussa (1909 - 1974) mke wa Kleist Sykes
na mama wa watoto wake wote watatu

 
Nemo,

View attachment 1267416
Kushoto waliokaa: Kleist Sykes (1994 -1949), Abbas Sykes (1929 - ),
Nyuma kushoto Ally Sykes (1926 - 2013), Abdulwahid Sykes (1924 - 1968)
Picha hii ilipigwa 1942 Abdul Sykes aliporudi Dar es Salaam kuaga kutoka Lower Kabete
Kenya kabla ya kwenda Burma Vita Vya Pili Vya Dunia (1939 - 1945) akiwa katika
King's African Rifles (KAR) kabla ya kwenda Burma

View attachment 1267431
Bi. Mruguru bint Mussa (1909 - 1974) mke wa Kleist Sykes
na mama wa watoto wake wote watatu


Asante kwa picha nzuri Mzee Said,

Aliyewahi kuja kuwa Meya wa Jiji ni nani?
 
Ambaye ni Mtoto wa Abdulwahid, Asante sana
Nemo...,
Watu wanasema dunia inazunguka na historia inajirudia.

Picha ya Kleist Abdulwahid Sykes ambae alizoeleka kwa jina la Kleist Sykes akiwa na Karim Aga Khan mimi imenirudisha nyuma karibu sasa miaka 90.

Babu yake Karim Aga Khan, Sultan Mohamed Shah alikuja Tanganyika mwaka wa 1936 na katika sehemu alizotembelea Dar es Salaam ilikuwa shule ya Al Jamiatul Islamiyya mtaa wa New Street na Stanley Street.

Hii Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika iliasisiwa na wale wale wazee wa Dar es Salaam walioasisi African Association - Kleist Sykes, Mzee bin Sudi, Ibrahim Hamis, Zibe Kidasi, Ali Said Mpima na Suleiman Majisu.

Waasisi wa African Association ukiwatoa Cecil Matola, Raikes Kusi na Rawson Watts waliobakia walikuwa Waislam.

Tatizo lililojitokeza ilikuwa hata matatizo ya Waislam yakawa yanapitishwa kupitia African Association ambayo kilikuwa chama ambacho hakikutakiwa kufangamana na dini yoyote.

Kwa ajili hii basi wazee wetu wakaona itakuwa bora waunde Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika (Umoja wa Waislam wa Tanganyika) ili ishughulike na yote yanayohusu Waislam.

Ndipo Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika ikaundwa mwaka wa 1933 Rais akiwa Mzee Bin Sudi na Katibu Kleist Sykes nafasi ambaz ndizo walizokuwa wameshika katika African Association.

Alipokuja Aga Khan Tanganyika ana kutembelea Al Jamiatula Islamiyya akakuta pana shule inajeagwa lakini haijakamilika.

Abdul Sykes akiwa mwanafunzi wa shule hii ndiyo aliyesoma risala ya kumkaribisha Aga Khan.

Aga Khan alivutiwa sana na juhudi hizi za Waislam na katika kujibu risala ile akajitolea kukamilisha ujenzi wa shule pamoja na ofisi za Al Jamiatul Islamiyya.

Kleist Sykes alikuwa na uhusiano mzuri na jamii ya Ismailia kwani yeye alikuwanao katika Dar es Salaam Chamber of Commerce na inaaminika ndiye alikuwa Mwafrika wa kwanza kujiunga na taasisi hii ya wafanyabiashara.

Sasa nikiangalia picha hiyo nikawa nakumbuka historia ya familia hizi mbili kuwa kijana Abdul akiwa na umri wa miaka 12 alikutana na babu yake Karim Aga Khan na ikasadif takriban miongo tisa baadae mjukuu wa Sultan Mohamed Aga Khan, Karim Aga Khan anakutana na mtoto wa Abdul Sykes akiwa Mayor wa Dar es Salaam na huyu Mayor Kleist kama alivyokuwa baba yake, Abdul Sykes alianza darasa la kwanza kwenye shule aliyosaidia kujenga babu yake Karim Aga Khan mwaka wa 1936.

Mwaka wa 1959 jamii ya Kiismailia Tanganyika ilitaka kuuza Mercedes Benz 280 SE ambayo waliinunua kwa matumizi ya Karim Aga Khan alipokuja Tanganyika mwaka wa 1956.

Muki yaani kiongozi wa Ismailia wakati ule alikuwa baba yake Anoor Kassam na wakaamua kuwa gari hiyo isiuzwe katika jamii yao bali auziwe mtu maarufu katika jamii ya Waafrika.

Gari hii ya aliyopanda Aga Khan katika safari yake Tanganyika mwaka wa 1956 Mercedes Benz 280 SE Jamii ya Aga Khan Tanganyika walimuuzia Abdul Sykes mwaka wa 1959.

Kuna mengine ambayo jamii ya Waasia walikuwa wakifanya chinichini na Abdul Sykes wakati wa kupigania uhuru wa Tanganyika ili Waingereza wasijue, iko siku ikitokea fursa kama hii In Shaa Alah nitaeleza.
 
Nemo...,
Watu wanasema dunia inazunguka na historia inajirudia.

Picha ya Kleist Abdulwahid Sykes ambae alizoeleka kwa jina la Kleist Sykes akiwa na Karim Aga Khan mimi imenirudisha nyuma karibu sasa miaka 90.

Babu yake Karim Aga Khan, Sultan Mohamed Shah alikuja Tanganyika mwaka wa 1936 na katika sehemu alizotembelea Dar es Salaam ilikuwa shule ya Al Jamiatul Islamiyya mtaa wa New Street na Stanley Street.

Hii Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika iliasisiwa na wale wale wazee wa Dar es Salaam walioasisi African Association.

Waasisi wa African Association wengi wao walikuwa Waislam wakiongozwa na Kleist Sykes.
Tatizo lililojitokeza ilikuwa hata matatizo ya Waislam yakawa yanapitishwa kupitia African Association ambayo kilikuwa chama ambacho hakikutakiwa kufangamana na dini yoyote.

Kwa ajili hii basi wazee wetu wakaona itakuwa bora waunde Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika (Umoja wa Waislam wa Tanganyika).

Ndipo Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika ikaundwa mwaka wa 1933.

Alipokuja Aga Khan Tanganyika ana kutembelea Al Jamiatula Islamiyya akakuta pana shule inajemgwa lakini haijamilika.

Abdul Sykes akiwa mwanafunzi wa shule hii ndiyo aliyosoma risala ya kumkaribisha Aga Khan.

Aga Khan alivutiwa sana na juhudi hizi za Waislam na katika kujibu risala ile akajitolea kukamilisha ujenzi wa shule pamoja na ofisi za Al Jamiatul Islamiyya.

Kleist Sykes alikuwa na uhusiano mzuri na jamii ya Ismailia kwani yeye alikuwanao katika Dar es Salaam Chamber of Commerce na inaaminika ndiye alikuwa Mwafrika wa kwanza kujiunga na taasisi hii ya wafanyabiashara.

Sasa nikiangalia picha hiyo nikawa nakumbuka historia ya familia hizi mbili kuwa kijana Abdul akiwa na umri wa miaka 12 alikutana na babu yake Karim Aga Khan na ikasadif mi

Jitihada za Kleist Sykes kuanzisha shule, au Umoja huo kuanzisha shule ziliishia wapi, je walikwamishwa na nini? au ipo taasisi madhubuti iliyoanzishwa na wazee hao ingali Mpaka sasa?
 
Jitihada za Kleist Sykes kuanzisha shule, au Umoja huo kuanzisha shule ziliishia wapi, je walikwamishwa na nini? au ipo taasisi madhubuti iliyoanzishwa na wazee hao ingali Mpaka sasa?
Nemo...
Shule ilijengwa na ndiyo shule aliyosoma baba yangu na watoto rika lake kama Abdul na Ally Sykes, Mwalimu Sakina na nduguye Mwalimu Fatna na hawa akaina mama wakajakuwa waalimu shuleni hapo katika miaka ya 1950 na kuendelea.

Shule hii ilikuwa ikisomesha Qur'an, Lugha ya Kiarabu na masomo mengine ya kisekula.
Kiarabu ambacho wazee wetu walipokuwa wakifurahi wakikimwaga walikipata hapo.

Mchanganyiko huu wa lugha hizi mbili Kiarabu na Kiingereza ndiyo iliwafanya wazee wetu wakizungumza Kiingereza utaburudika na ile ''accent,'' yao.

Naambiwa Julius Nyerere akipenda sana kumsemesha Abdul Kiingereza labda alikuwa akifurahishwa na ile ''accent,'' yake.

Mzee Abdallah aliyekuwa muhudumu ofisini kwa Abdul Sykes alipata kunihadithia siku Mzungu Town Clerk alipomvamia Abdul Sykes ofisini kwake Kariakoo Market akamkuta anauza kadi za TANU.

Mzee Abdallah anasema yeye alikuwapo pale siku ile na ingawa hajui Kiingereza lakini alikuwa akistarehe kusikiliza jinsi Abdul Sykes na Mzungu walivyopambana kwa Kiingereza.

Mzee Abdallah anasifia ananambia, ''Abdul alikuwa anasema Kizungu kama maji.''

Kuhofia Abdul kufukuzwa kazi ndiyo wazee wa Dar es Salaam wakaamua kumfanyia Abdul dua kama ile waliyomfanyia Mwalimu Nyerere baadae ambayo imekuwa maarufu watu wengi wanapenda kuihadithia pale wazee walipomwambia Nyerere baada ya kuruka damu, ''Twining amekwisha.''

Historia ya TANU ilikuwa na mikasa.

Dua nyingine aliyofanyiwa Nyerere ilikuwa Lindi dua iliyofanywa na Sheikh Yusuf Badi na dua ya mwisho ni dua ya Uchaguzi wa Kura Tatu Tanga, Mnyanjani mwaka wa 1958, dua ya akina Sheikh Rashid Sembe, Mmaka Omari na Hamisi Heri.

Naona hii ndiyo ilikuwa dua ya kuleta uhuru.

Baada ya hapo uhuru mwaka wa 1961

Serikali imetaifisha Al Jamiatil Islamiyya School na Waislam wameomba warejeshewe shule yao lakini hadi leo zaidi ya miaka 20 wanazungushwa ilhali St. Joseph'Convent ilipoombwa tu ikarejeshwa kwa wenyewe,

1574261797603.png
 
Tatizo ni ulivyojaa hila za makusudi!!

Kusoma kutabu kuhusu Mwalimu ndii kumfahamu kuliko wanavyomfahamu wanae na mkewe?

Nataka siku moja useme hapa, kuwa ulienda kwa mama Maria akakuambia hivi kuhusu hiki! Au unangoja nae afe ili uanze kuandika kwa kupotosha?

Uache kuandika huku unachomeka hila, na upotovu....la sivyo wengine tutaendelea kukudharau kama tinavyovidharau vitabu vingi tu vilivyojaa hila na upotoshaji!
tatizo una miemko... relax
 
Serikali imetaifisha Al Jamiatil Islamiyya School na Waislam wameomba warejeshewe shule yao lakini hadi leo zaidi ya miaka 20 wanazungushwa ilhali St. Joseph'Convent ilipoombwa tu ikarejeshwa kwa wenyewe,

Kulikoni kila mara unaishia ku compare na ku contrast kati ya Waislamu na Wakatoliki? Nauliza, Singasinga, Baniani, Ahmadiyya, Ismailia hata Walutheri, Mabudha na Wapentekoste nao vipi vis-a-vis Uislamu wako?
 
Nemo...
Shule ilijengwa na ndiyo shule aliyosoma baba yangu na watoto rika lake kama Abdul na Ally Sykes, Mwalimu Sakina na nduguye Mwalimu Fatna na hawa akaina mama wakajakuwa waalimu shuleni hapo katika miaka ya 1950 na kuendelea.

Shule hii ilikuwa ikisomesha Qur'an, Lugha ya Kiarabu na masomo mengine ya kisekula.
Kiarabu ambacho wazee wetu walipokuwa wakifurahi wakikimwaga walikipata hapo.

Mchanganyiko huu wa lugha hizi mbili Kiarabu na Kiingereza ndiyo iliwafanya wazee wetu wakizungumza Kiingereza utaburudika na ile ''accent,'' yao.

Naambiwa Julius Nyerere akipenda sana kumsemesha Abdul Kiingereza labda alikuwa akifurahishwa na ile ''accent,'' yake.

Mzee Abdallah aliyekuwa muhudumu ofisini kwa Abdul Sykes alipata kunihadithia siku Mzungu Town Clerk alipomvamia Abdul Sykes ofisini kwake Kariakoo Market akamkuta anauza kadi za TANU.

Mzee Abdallah anasema yeye alikuwapo pale siku ile na ingawa hajui Kiingereza lakini alikuwa akistarehe kusikiliza jinsi Abdul Sykes na Mzungu walivyopambana kwa Kiingereza.

Mzee Abdallah anasifia ananambia, ''Abdul alikuwa anasema Kizungu kama maji.''

Kuhofia Abdul kufukuzwa kazi ndiyo wazee wa Dar es Salaam wakaamua kumfanyia Abdul dua kama ile waliyomfanyia Mwalimu Nyerere baadae ambayo imekuwa maarufu watu wengi wanapenda kuihadithia pale wazee walipomwambia Nyerere baada ya kuruka damu, ''Twining amekwisha.''

Historia ya TANU ilikuwa na mikasa.

Dua nyingine aliyofanyiwa Nyerere ilikuwa Lindi dua iliyofanywa na Sheikh Yusuf Badi na dua ya mwisho ni dua ya Uchaguzi wa Kura Tatu Tanga, Mnyanjani mwaka wa 1958, dua ya akina Sheikh Rashid Sembe, Mmaka Omari na Hamisi Heri.

Naona hii ndiyo ilikuwa dua ya kuleta uhuru.

Baada ya hapo uhuru mwaka wa 1961

Serikali imetaifisha Al Jamiatil Islamiyya School na Waislam wameomba warejeshewe shule yao lakini hadi leo zaidi ya miaka 20 wanazungushwa ilhali St. Joseph'Convent ilipoombwa tu ikarejeshwa kwa wenyewe,


Shukrani Kwa Historia nzuri Mzee Said, na jitihada zako na Wazee wako simulizi adimu sana hizi kuzipata
 
Kulikoni kila mara unaishia ku compare na ku contrast kati ya Waislamu na Wakatoliki? Nauliza, Singasinga, Baniani, Ahmadiyya, Ismailia hata Walutheri, Mabudha na Wapentekoste nao vipi vis-a-vis Uislamu wako?

Mkuu usiwe na jazba, tupo imani tofauti humu ila tusichukulie kwa mitazamo mibaya, je si haki kwa wao kutodai haki hiyo? Je sababu za kuporwa ni zipi?
 
Kulikoni kila mara unaishia ku compare na ku contrast kati ya Waislamu na Wakatoliki? Nauliza, Singasinga, Baniani, Ahmadiyya, Ismailia hata Walutheri, Mabudha na Wapentekoste nao vipi vis-a-vis Uislamu wako?
Ndjabu,
Hizi ndizo dini kubwa mbili Tanzania na hawa ndiyo waliokuwa na maslahi katika hali ya baadae ya Tanganyika.

Historia ya uhuru inazunguka kati yao.
Umenikumbusha kitu.

Katika historia ya TANU kulikuwa na Kadiani wawili - Kaluta Amri Abeid na Jumanne Abdallah na wote hawa wameacha kumbukumbu kubwa.

Siku ikitokea fursa nitakueleza mchango wa Jumanne Abdallah katika mapinduzi ya Zanzibar mwaka wa 1964.
 
Nemo,

View attachment 1267416
Kushoto waliokaa: Kleist Sykes (1994 -1949), Abbas Sykes (1929 - ),
Nyuma kushoto Ally Sykes (1926 - 2013), Abdulwahid Sykes (1924 - 1968)
Picha hii ilipigwa 1942 Abdul Sykes aliporudi Dar es Salaam kuaga kutoka Lower Kabete
Kenya kabla ya kwenda Burma Vita Vya Pili Vya Dunia (1939 - 1945) akiwa katika
King's African Rifles (KAR)

View attachment 1267431
Bi. Mruguru bint Mussa (1909 - 1974) mke wa Kleist Sykes
na mama wa watoto wake wote watatu


Sahihisho Mzee Kleist alizaliwa mwaka 1894
 
Mkuu usiwe na jazba, tupo imani tofauti humu ila tusichukulie kwa mitazamo mibaya, je si haki kwa wao kutodai haki hiyo? Je sababu za kuporwa ni zipi?
Wao ni kina nani hao? Muddy et al? Kama ni ndiyo, Muddy et al ni nani? Nipo Mbweni hapa nimepita local mosque asubuhi hii, nashangaa msikiti mpya lakini umezungukwa na vichaka ndani na nje, kuta za msikiti zishajenga nyufa halafu kuna bango barabarani lenye picha za bendera za TZ na Oman, na kwamba fence imejengwa kwa msaada wa Waislamu wa Uarabuni.
 
Back
Top Bottom