Historia ya Daraja la Selander la Jijini Dar es Salaam

Historia ya Daraja la Selander la Jijini Dar es Salaam

Naomba kujua kuhusu daraja la Salender ambalo liko jijini Dar es Salaam

1. Lilijengwa mwaka gani.

2. Mkandarasi / engineer aliyelijenga daraja hilo.

3. Na ni nani aliyesimama ujenzi kipindi hicho.

4. Na kwa nini eneo hilo la barabara na daraja hilo linaonekana liko imara sana.

5. Na je hatuwezi kuwapata walioshiriki kujenga daraja hilo wakatusaidia mawazo nini kilipelekea kujenga daraja imara kiasi hicho.

6. Pia naomba kujua kiasi cha fedha zilizotumika kukamilisha ujenzi wa daraja hilo.

7. Na ni kwa nini maji ya mito yote hayajazi eneo hilo la daraja.

Natanguliza shukrani kwa yoyote atakusaidia kwa namna moja au nyingine...


"My take: kwangu mimi DARAJA HILI LINGEWEKWA KWENYE MAAJABU YA DUNIA, kwa kuweza kupitisha maji ya mvua zinazoendelea kunyesha jijini Dar es Salaam bila wasiwasi!
Daraja la Selander ni daraja kwenye Barabara ya Ali Hassan Mwinyi (Bagamoyo Road) ambalo linavuka mto Msimbazi jijini Dar es Salaam, Tanzania.

Daraja hili lilitengenezwa mwaka 1929 likapewa jina kwa kumbukumbu ya John Einar Selander aliyekuwa mkurugenzi wa kwanza wa ujenzi katika eneo la Tanganyika chini ya utawala wa Waingereza.[1]

Daraja hili lilipanuliwa na Japan International Cooperation Agency mnamo 1980[2] kuwa na njia 4 za magari.

Tangu mwaka 2019 daraja la pili limeanza kujengwa takriban mita 300 kando yake upande wa Oyster Bay.

Chanzo: Daraja la Selander - Wikipedia, kamusi elezo huru
 
Treni ya Odds 60+.. 🔥 🔥
1630851469747.png
 
Huwa napita nikiwa kwenye gari sikujua kama kuna madaraja mawili pale.
Hata ukipita kwa gari unaliona la pili. Ukiwa unatoka Mjini kuja Traffic Light za pale Stanbic lenyewe liko kushoto (Upande wa Mikoko, sio Upande wa Bahari).
 
Hata ukipita kwa gari unaliona la pili. Ukiwa unatoka Mjini kuja Traffic Light za pale Stanbic lenyewe liko kushoto (Upande wa Mikoko, sio Upande wa Bahari).
Hilo daraja bado linaendelea kujizolea mahistoria
 
Hata ukipita kwa gari unaliona la pili. Ukiwa unatoka Mjini kuja Traffic Light za pale Stanbic lenyewe liko kushoto (Upande wa Mikoko, sio Upande wa Bahari).
Kaka unavuta nini wakati unapoendesha gari??? Daraja jipya liko upande wa bahari!!! Haidhuru unapoelekea.
 
Kaka unavuta nini wakati unapoendesha gari??? Daraja jipya liko upande wa bahari!!! Haidhuru unapoelekea.
Wewe huelewi kinachojadiliwa hapa, yaani umekurupuka kujadili bila kujua chochote.

Ukiacha lile Daraja linalojengwa sasa kule baharini kutolea Coco mpaka Agha Khan, pale Selander tunapopita kuna madaraja mawili, moja jembamba lililojengwa na mkoloni lililoko upande wa mikoko, na jingine upande wa bahari ndo linalopitisha magari lililojengwa na Kajima miaka ya 1980s.

Sasa wapi Mimi nimesema daraja jipya ndio liko upande wa mikoko?
 
Wewe huelewi kinachojadiliwa hapa, yaani umekurupuka kujadili bila kujua chochote.

Ukiacha lile Daraja linalojengwa sasa kule baharini kutolea Coco mpaka Agha Khan, pale Selander tunapopita kuna madaraja mawili, moja jembamba lililojengwa na mkoloni lililoko upande wa mikoko, na jingine upande wa bahari ndo linalopitisha magari lililojengwa na Kajima miaka ya 1980s.

Sasa wapi Mimi nimesema daraja jipya ndio liko upande wa mikoko?
Unasema kweli (labda) kumbe lile daraja la baisikeli na waenda kwa miguu ni lile la Selander mwenyewe? Sawasawa, nitaiangalia sasa kwa macho mapya!
Asante!
 
Unasema kweli (labda) kumbe lile daraja la baisikeli na waenda kwa miguu ni lile la Selander mwenyewe? Sawasawa, nitaiangalia sasa kwa macho mapya!
Asante!
Hapo Sasa tuko pamoja Mkuu
 
Kaka unavuta nini wakati unapoendesha gari??? Daraja jipya liko upande wa bahari!!! Haidhuru unapoelekea.
Nadhani hujamwelewa Shark

Siku nyingine jaribu kumwelewa mtu kabla hujamshambulia kwa kejeli/dharau.

Ni ushauri tu
 
JE WAJUA? JE UNAJUA Kituo cha Polisi cha Selander Bridge zamani ilikuwa ni hoteli moja maarufu sana?

Jengo hili zamani ilikuwa ni hoteli maarufu iliyokuwa inaitwa “Sun and Sands Hotel”
iliyokuwa inamilikiwa na familia ya Punja waliokuwa mabepari wakubwa wa kihindi miaka ya 1920- 50. Hotel ilijengwa mwaka 1949.

Hii hoteli ilikuja kutaifishwa na kuchukuliwa na serikali baada ya makomando wa kikaburu kulipua daraja la Selander, Nyumba ya Balozi wa Uingereza pale Toure Drive na Oil Depot Kurasini mwaka 1972. Makomando hawa (South African Special Forces Brigade-RECCE) waliitumia fukwe mbele ya hili jengo kujitayarisha na mission yao. Baada ya huu mkasa ndo serikali ikaamua kuongeza ulinzi na ikajenga Kituo cha Polisi cha Selander Bridge na hili jengo likataifishwa.
 
Baada ya kujengwa kwa daraja jipya na Kajima, haikuwa na haja kuendelea kuliita Selander
Lingepewa jina la kitanzania au angalau jina la mjapani mhandisi mkuu aliyechora na kusimamia ujenzi wa hilo daraja....
 
JE WAJUA? JE UNAJUA Kituo cha Polisi cha Selander Bridge zamani ilikuwa ni hoteli moja maarufu sana?

Jengo hili zamani ilikuwa ni hoteli maarufu iliyokuwa inaitwa “Sun and Sands Hotel”
iliyokuwa inamilikiwa na familia ya Punja waliokuwa mabepari wakubwa wa kihindi miaka ya 1920- 50. Hotel ilijengwa mwaka 1949.

Hii hoteli ilikuja kutaifishwa na kuchukuliwa na serikali baada ya makomando wa kikaburu kulipua daraja la Selander, Nyumba ya Balozi wa Uingereza pale Toure Drive na Oil Depot Kurasini mwaka 1972. Makomando hawa (South African Special Forces Brigade-RECCE) waliitumia fukwe mbele ya hili jengo kujitayarisha na mission yao. Baada ya huu mkasa ndo serikali ikaamua kuongeza ulinzi na ikajenga Kituo cha Polisi cha Selander Bridge na hili jengo likataifishwa.
1695583732633.png
 
Urejee mkuu, nna hamu ya kujua kuhusu hilo.
FROM SUN & SAND HOTEL TO SELANDER BRIDGE POLICE STATION.
Watu wengi wanalifahamu hili jengo sasa hivi kama kituo cha polisi cha Selander Bridge lakini hawajui kuwa hili jengo zamani ilikuwa ni hotel maarufu sana iliyokuwa inatumiwa na matajiri iliyokuwa inaitwa Sun and Sand Hotel. Hii hotel ilikuwa ikimilikiwa na familia ya Panju na ilijengwa mwaka 1949. Hili jengo lilitaifishwa na kugeuzwa kituo cha polisi baada ya Makaburu kulipua daraja la Selander mwaka 1972.
Baada ya serikali yetu kuficha huu mkasa kwa miaka mingi nilikuja kuusoma huu mkasa kwenye kitabu kilichoandikwa na Kaburu anayeitwa Peter Stiff kinachoitwa “The Silent War: South African Recce Operations 1969-1994.”
Baadae nilimsikia Raisi Kikwete akiisema hii stori kwenye sherehe za maadhimisho ya miaka 40 toka kuanzishwa kwa SADCC mwaka 2020 (nanukuu in English toka kwenye nakala iliyoandikwa na Hilda Muhagama wa Tanzania Standard:
“The facility had to hurriedly but meticulously be turned into a police station, thanks to the liberation movement, with Tanzania leading from the front.The Boers were very upset with countries that led the liberation struggles during that time, it was actually here where South African commandos pitched camp at Kigamboni before proceeding to set a bomb at the Selander Bridge,” revealed former President Jakaya Kikwete at a symposium to mark the 40th anniversary since the establishment of the Southern African Development Community (SADC), which was organised by the University for Dar es Salaam (UDSM).
Dr Kikwete, who served the country between 2005 and 2015, further revealed how the 92-year-old bridge was too strong for the explosive to detonate. Adding the commandos involved in the incident was writing a book that will delve into the details of the liberation struggles and Selander bridge survival.
“The threat raised an alarm and called for beefing up of security in the area, hence the police station we see to date,” he disclosed.
The bridge was named after John Einar Selander, Tanganyika’s first Director of Public Works.
So volatile was the situation back then, that people living around the bridge weren’t allowed to switch on their lights.
“There was a time where people living in the surrounding Selander Bridge were not allowed to switch on their lights, lest they get exposed to any potential threat.
He added: Some of the front liners, including Tanzania grappled with difficult moments but they still soldiered on and accomplished the mission.”
Kama unataka kusoma mkasa wote ulivyoenda kama movie stori iko hapa toka kwenye kitabu cha Kaburu: https://www.facebook.com/photo/?fbid=10158264615939498&set=pb.673909497.-2207520000..
Picha nimeitoa kwenye kitabu cha “Street Level by Sarah Parkes” kiko pale Tanzania Publishing House (Mkuki na Nyota).
 
kinazungumzia tukio la 1980 hapo selander bridge?
Ndio, ni mkusanyo wa operation zao zote ikiwemo Tanzani na Angola, Namibia, Zambia, Lesotho, Mozambique and Botswana.
Na pia ya Tanzania, inaongelewa kuanzia mipango ilivyopangwa na mafunzo waliyokuwa wafanya, kwa kutumia submarine na tug boats kuja Tanzania na siku ya tukio lilivyotokea.
 
Back
Top Bottom