Bilionea Asigwa
JF-Expert Member
- Sep 21, 2011
- 16,515
- 28,506
- Thread starter
-
- #21
Inaendelea
JUMA NATURE NDANI YA WANAUME HALISI
Baada ya kuvunjika kwa kundi maarufu la Wanaume TMK, alitoa albamu akiwa peke yake aliyoipa jina la ‘Ubinadamu Kazi’, iliyosheheni nyimbo mbalimbali zikiwamo ‘Mtoto Idi’, ‘Dance With Me’, na ‘Salio Lovers’, aliipa albamu hiyo jina hilo kutokana na misukosuko aliyopitia hadi kufika hapo na kundi lililovunjika, ambapo licha ya kutamani liwepo aliumia kwa kutokuwapo Wanaume TMK.
“Ni kundi lililokuwa na nia njema, lilianza kama utani lakini mafanikio yalikuwa makubwa. Kuvunjika kwake kulinikera sana, hasa nikiamini kwa asilimia 100 kuwa ni binadamu wachache wasiokuwa na uelewa wala kujitambua wanatakiwa kufanya nini katika dunia, ndiyo waliochangia kulivunja. Nikaamua kuja na ‘Ubinadamu kazi’, ninasisitiza ni kazi kweli kweli, “anasema Nature.
Nature hakupenda kuwa peke yake katika muziki kwa kuwa aliamini wapo vijana wengi wanaopenda kazi hiyo na kwamba kuwa nao pamoja kimuziki ni kupigana na tatizo la ajira linaloongezeka nchini, hivyo akafikiria kuanzisha kundi lingine.
Wakati akiwaza hayo hakukaa na yeyote, bali aliwasiliana na baadhi ya vijana alikuwa nao katika kundi la mwanzo(TMK), ambao aliwaona wana uelewa na kuwaeleza azma yake hiyo, wazo hilo halikupingwa kutokana na uaminifu aliojijengea kwa vijana hao kipindi chote alichokuwa nao katika Kundi la Wanaume TMK, ndipo wakaanzisha kundi jipya na kuliita, Wanaume Halisi.
Wasanii alioanzisha nao kundi hilo kuwa ni pamoaj na Mzimu, Luteni Kalama, Dollo, BK ambaye kwa sasa ni marehemu, Kakaman, Bob Q , D. Chief, Abdu Malipo, Inspector Haroun na baadaye KR Mulla akajiunga nao kuongeza nguvu na kulifanya liwe na mwonekano tofauti na bora zaidi .
“Nakwenda nao pamoja kwa kuwa natambua mchango wa kila mmoja katika kundi. Nafahamu na kusisitiza hakuna aliye bora kuliko mwingine bali tunategemeana kwa namna moja au nyingine. Kwangu mimi, huo ndiyo uongozi,”anasema Nature maarufu pia kwa jina la msitu wa vina.
Kuanzishwa kwa kundi la Wanaume Halisi kulimpa wazo la kutoa albamu mpya aliyoipa jina la ‘History’ likieleza maisha yake tangu alipoanza muziki, katika albamu hiyo kulikuwa na nyimbo iliyojulikana kwa jina la ‘Mgambo’ ambayo ilibamba vilivyo kila kona ya Jiji la dar es Salaam na kujenga historia mpya kuwa kila anapotoka na kitu lazima aache gumzo.
Kila alichopata katika muziki, fedha na heshima kilimfanya awe karibu na jamii aliyoamini imemfikisha alipo akifafanua kuwa anawaheshimu ‘masela’, ambao kwa namna moja au nyingine wamekuwa wakifuatilia kazi zake hata kuwa ni sehemu ya maisha yao.
“Kuna vijana nawafahamu, wanatamani hata wabadili majina yao na kujiita Nature, wapo pia waliothubutu kufanya hivyo kwa kuthamini kazi yangu nawaheshimu sana, popote walipo napenda kuwaambia kwamba nafahamu kama wapo kwa ajili yangu na muziki wa nchi hii, “anasema Nature kwa hisia.
Tuzo alizowania na kushinda
Mwanzoni mwa mwaka 2006 alichaguliwa kuwania Tuzo za Msanii Bora wa Afrika zilizoandaliwa na M.T. V nchini Denmark, lakini alishindwa kuhudhuria kutokana na kutosa msaada wa Serikali.
“Uongozi wangu haukuwa makini kama nilivyosema awali, nilijitahidi kwenda wizarani mara kadhaa ili waniwezeshe kwenda safari hiyo, lakini ilishindikana. Hivyo, sikuhudhuria, niliumia sikuwa na jinsi zaidi ya kutokwenda,” anasema Nature anayejulikana pia kwa jina la Kibla.
Oktoba 11 mwaka 2007 alichaguliwa kuwania Tuzo Video Bora kutoka Afrika Mashariki kutokana na wimbo wake ‘Mgambo’
Kuchaguliwa kwake ilikuwa ni furaha na uthibitisho kuwa muziki wake unakua na kwamba alihakikisha hapotezi nafasi hiyo kwa kutokwenda kama ilivyokuwa kwa uteuzi wa awalinchini Denmark.
Tuzo hizo zilitolewa Johanesburg City Hall nchini Afrika Kusini ambapo aliibuka kidedea kutokana na video ya wimbo ‘Mgambo’.
Akiwa nchini humo baada ya kupata tuzo hiyo, vyombo vya habari vilikuwa vikimuuliza anazungumziaje ushindi huo, jibu lilikuwa moja tu ni kwa ajili ya Watanzania na kuitangaza nchi yake.
Studio iliyorekodi wimbo huo kuwa ni Bongo Records chini P- Funk, huku video ikitengenezwa na Visual Lab iliyokuwa chini ya uongozi wa Adam Juma.
INAENDELEA
JUMA NATURE NDANI YA WANAUME HALISI
Baada ya kuvunjika kwa kundi maarufu la Wanaume TMK, alitoa albamu akiwa peke yake aliyoipa jina la ‘Ubinadamu Kazi’, iliyosheheni nyimbo mbalimbali zikiwamo ‘Mtoto Idi’, ‘Dance With Me’, na ‘Salio Lovers’, aliipa albamu hiyo jina hilo kutokana na misukosuko aliyopitia hadi kufika hapo na kundi lililovunjika, ambapo licha ya kutamani liwepo aliumia kwa kutokuwapo Wanaume TMK.
“Ni kundi lililokuwa na nia njema, lilianza kama utani lakini mafanikio yalikuwa makubwa. Kuvunjika kwake kulinikera sana, hasa nikiamini kwa asilimia 100 kuwa ni binadamu wachache wasiokuwa na uelewa wala kujitambua wanatakiwa kufanya nini katika dunia, ndiyo waliochangia kulivunja. Nikaamua kuja na ‘Ubinadamu kazi’, ninasisitiza ni kazi kweli kweli, “anasema Nature.
Nature hakupenda kuwa peke yake katika muziki kwa kuwa aliamini wapo vijana wengi wanaopenda kazi hiyo na kwamba kuwa nao pamoja kimuziki ni kupigana na tatizo la ajira linaloongezeka nchini, hivyo akafikiria kuanzisha kundi lingine.
Wakati akiwaza hayo hakukaa na yeyote, bali aliwasiliana na baadhi ya vijana alikuwa nao katika kundi la mwanzo(TMK), ambao aliwaona wana uelewa na kuwaeleza azma yake hiyo, wazo hilo halikupingwa kutokana na uaminifu aliojijengea kwa vijana hao kipindi chote alichokuwa nao katika Kundi la Wanaume TMK, ndipo wakaanzisha kundi jipya na kuliita, Wanaume Halisi.
Wasanii alioanzisha nao kundi hilo kuwa ni pamoaj na Mzimu, Luteni Kalama, Dollo, BK ambaye kwa sasa ni marehemu, Kakaman, Bob Q , D. Chief, Abdu Malipo, Inspector Haroun na baadaye KR Mulla akajiunga nao kuongeza nguvu na kulifanya liwe na mwonekano tofauti na bora zaidi .
“Nakwenda nao pamoja kwa kuwa natambua mchango wa kila mmoja katika kundi. Nafahamu na kusisitiza hakuna aliye bora kuliko mwingine bali tunategemeana kwa namna moja au nyingine. Kwangu mimi, huo ndiyo uongozi,”anasema Nature maarufu pia kwa jina la msitu wa vina.
Kuanzishwa kwa kundi la Wanaume Halisi kulimpa wazo la kutoa albamu mpya aliyoipa jina la ‘History’ likieleza maisha yake tangu alipoanza muziki, katika albamu hiyo kulikuwa na nyimbo iliyojulikana kwa jina la ‘Mgambo’ ambayo ilibamba vilivyo kila kona ya Jiji la dar es Salaam na kujenga historia mpya kuwa kila anapotoka na kitu lazima aache gumzo.
Kila alichopata katika muziki, fedha na heshima kilimfanya awe karibu na jamii aliyoamini imemfikisha alipo akifafanua kuwa anawaheshimu ‘masela’, ambao kwa namna moja au nyingine wamekuwa wakifuatilia kazi zake hata kuwa ni sehemu ya maisha yao.
“Kuna vijana nawafahamu, wanatamani hata wabadili majina yao na kujiita Nature, wapo pia waliothubutu kufanya hivyo kwa kuthamini kazi yangu nawaheshimu sana, popote walipo napenda kuwaambia kwamba nafahamu kama wapo kwa ajili yangu na muziki wa nchi hii, “anasema Nature kwa hisia.
Tuzo alizowania na kushinda
Mwanzoni mwa mwaka 2006 alichaguliwa kuwania Tuzo za Msanii Bora wa Afrika zilizoandaliwa na M.T. V nchini Denmark, lakini alishindwa kuhudhuria kutokana na kutosa msaada wa Serikali.
“Uongozi wangu haukuwa makini kama nilivyosema awali, nilijitahidi kwenda wizarani mara kadhaa ili waniwezeshe kwenda safari hiyo, lakini ilishindikana. Hivyo, sikuhudhuria, niliumia sikuwa na jinsi zaidi ya kutokwenda,” anasema Nature anayejulikana pia kwa jina la Kibla.
Oktoba 11 mwaka 2007 alichaguliwa kuwania Tuzo Video Bora kutoka Afrika Mashariki kutokana na wimbo wake ‘Mgambo’
Kuchaguliwa kwake ilikuwa ni furaha na uthibitisho kuwa muziki wake unakua na kwamba alihakikisha hapotezi nafasi hiyo kwa kutokwenda kama ilivyokuwa kwa uteuzi wa awalinchini Denmark.
Tuzo hizo zilitolewa Johanesburg City Hall nchini Afrika Kusini ambapo aliibuka kidedea kutokana na video ya wimbo ‘Mgambo’.
Akiwa nchini humo baada ya kupata tuzo hiyo, vyombo vya habari vilikuwa vikimuuliza anazungumziaje ushindi huo, jibu lilikuwa moja tu ni kwa ajili ya Watanzania na kuitangaza nchi yake.
Studio iliyorekodi wimbo huo kuwa ni Bongo Records chini P- Funk, huku video ikitengenezwa na Visual Lab iliyokuwa chini ya uongozi wa Adam Juma.
INAENDELEA