bongo dili
JF-Expert Member
- Feb 13, 2015
- 12,350
- 25,180
Kakuambia nani kutengeneza basi kunahitaji vyeti zaidi.elimu ni kitu cha muhimu ndugu, unasema uchumi wa nchi umeshikwa kuanzia mabasi, madaladala, hivi unajua hayo mabasi na madaladala yametengenezwana watu waliosoma? wote tungekuwa waislam tusiosoma hayo mabasi ungetengeneza kwa elimu ya kuran? mbona unakuwa lijinga sana ndugu yangu.
tuambie ni basi gani bokoharam, au mwarabu yeyote aliwahi kutengeneza. taja moja tu. ila usitaje Ngamia, hilo sio basi ni mnyama na hatengenezwi.Kakuambia nani kutengeneza basi kunahitaji vyeti zaidi.
Ulisomea ujinga
Google unadhani Wana import mabus kama sisituambie ni basi gani bokoharam, au mwarabu yeyote aliwahi kutengeneza. taja moja tu. ila usitaje Ngamia, hilo sio basi ni mnyama na hatengenezwi.
umeshindwa kutaja. mwarabu alichotengeneza ni mkojo wa ngamia na tende tu. isingekuwa mafuta wangekuwa wanakula mchanga wa jangwani wale.Google unadhani Wana import mabus kama sisi
Mfalme...umeshindwa kutaja. mwarabu alichotengeneza ni mkojo wa ngamia na tende tu. isingekuwa mafuta wangekuwa wanakula mchanga wa jangwani wale.
Mfalme...
Ndugu zanguni.
Mambo haya yanahitaji mtu kusoma vizuri ili ayajue.
Yako mengi lakini tunaweza kuanza na huu ubishi wa Waarabu
Tuutumieni huu ukumbi kujielinisha siyo mahali pa kuzozana na kufanya kejeli.
Ingieni Google: Arab Scientists and Their Inventions.
Mkata...ADUI YA WAISLAMU WA TANZANIA NI UTAMADUNI MBOVU WA MWARABU
Waarabu walipokuja kwenye karne ya 13 walileta vitu kadhaa vikuu vikiwa ni viwili: dini nzuri ya Kiislamu na utamaduni wao wa kishenzi. Ndiyo, sijateleza ulimi wala mkono, Waarabu walileta utamaduni wa kishenzi. Utamaduni wa Kiarabu siyo dini ya Kiislamu na dini ya Kiislamu siyo utamaduni wa Kiarabu.
Watanzania wengi wanachanganya haya mawili kwa kutokuwa na upeo. Tuulizeni tuliosafiri duniani, kuna Wazungu na Wachina Waislamu na kuna Waarabu Wakristo kama Wakoptiki wa Misri. Uislamu siyo Uarabu na Uarabu siyo Uislamu na kwa hakika Uislamu ndio uliopunguza ushenzi wa Waarabu (ujahiliya) na kuwapa utu na ustaarabu.
Tukumbuke pia, Uislamu ndiyo ulioongoza elimu duniani kwenye karne ya sita, saba na nane na hata vyuo vikuu vya kwanza duniani vilikuwa vya waislamu, na haya majoho ya mahafali za leo yalianzishwa na Waislamu, siyo wazungu.
Nirejee kwenye rekodi. Taasisi ya kwanza ya kielimu kwa Waarabu duniani ilikuwa Ez-Zitouna ya
Tunisia iliyoanzishwa mwaka 737, lakini kinachokubalika kama chuo kikuu cha kwanza duniani ni
Al-Karaouine cha Moroko cha mwaka 859. Chuo kikuu cha pili duniani kilikuwa Al-Azhar cha Misri
mwaka 970 na cha tatu kilikuwa Nizamiyya cha Iraki mwaka 1065. Wazungu pamoja na kelele zao zote, chuo kikuu chao kwa kwanza ni Bologna cha Italia mwaka 1088 na baadaye mwaka 1096 kile cha Paris. Hakuna, ubishi, Waislamu ndio waanzilishi wa vyuo vikuu duniani.
Saba, lakini si waislamu wote hupenda elimu, kama ilivyo kwa dini nyingine pia. Ukienda kwenye
nchi za Maghrebu (Afrika Kaskazini) kama Moroko, Algeria, Tunisia, na Misri na zile za Mashariki
ya Kati kuanzia na Uturuki, Siria, Iraki, Lebanoni, na Yodani kidogo, hadi Irani, kuna waislamu
wengi wenye elimu kubwa.
Hapa Marekani Waislamu wa mataifa haya wanaheshimika, mathalani, wahandisi na wataalamu mahiri wa teknohama hutoka Uturuki, Pakistani na India wakati madaktari mahiri hutoka Irani. Mataifa ya Pakistani na Irani ndiyo pekee yaliyomudu kuwa na wataalamu wake wenyewe wa nyuklia bila kusaidiwa na mataifa ya Ulaya na Marekani na wote walikuwa Waislamu, akiwemo Abdul Qadeer Khan wa Pakistani.
Aidha, mwanasayansi aliyesimamia urushaji wa satelaiti ya India ya kwanza mwaka 1980, ni mwislamu Avul Abdul Kalam ambaye baadaye alikuwa Rais wa India mwaka 2002 hadi 2007. Ninachotaka kusema ni kwamba ukiondoa Waislamu walioko kwenye
Ghuba ya Uarabuni, wengine wote ni wasomi wa uhakika. Sababu ni moja tu: UTAMADUNI.
Nane, hali ni tofauti sana kule Ghuba kwenye nchi za Saudia Arabia, Yemeni, Kuwaiti, Omani,
Katari, Imarata (Falme za Kiarabu) na Bahareni. Huko Ghuba watu hawataki shule. Tusiwasitiri sana na kuficha ukweli: Ghuba hawataki shule. Hawa watu wa Ghuba ndiyo waliotuletea utamaduni wao huu Afrika Mashariki kuanzia kule Somalia, shuka hadi Lamu, Malindi na Mombasa Kenya, njoo kwetu Tanzania anzia na Pangani hadi Kilwa na Mafia, teremka mpaka Pemba iliyoko kaskazini mwa Msumbiji - kote huku kuna watu wenye utamaduni wa Ghuba wa kukataa shule.
Tusifichane ukweli, maeneo haya watu hawataki shule. Hili liko wazi. Kwa kuwa Waarabu wa Ghuba ndiyo walioleta pia Uislamu, basi watu hujumuisha kwa pamoja tatizo la kukosa elimu na hii dini nzuri ya Uislamu. Narudia tena, utamaduni wa kukataa shule ni wa Waarabu wa Ghuba, siyo Waislamu hapa duniani. Tatizo letu Tanzania ni kwamba Waislamu wengi (siyo wote) wamechukua utamaduni wa kimwinyimwinyi wa Ghuba wa kuzikimbia shule kana kwamba ndio ujanja. Hiki ndiyo chanzo cha malalamiko yote haya; hakuna cha uonevu wala nini!
Saudia watu ni vilaza watupu kiasi kwamba kuna Wamisri milioni moja na zaidi wanaofanya kazi za kitaalamu. Kila taifa la Ghuba isipokuwa Yemeni na Omani, lina wageni wengi zaidi nchini mwake kuliko wenyeji kwa sababu wananchi wao ni vilaza; hawataki shule. Yemeni na Omani hawana mafuta wala gesi asilia, yaani ni maskini na ndio maana hakuna wageni wengi. Hata hivyo, ukienda Omani kuna Watanzania wengi sana (hasa wenyeji wa Zanzibar), laki sita na ushee na wao pia shule hamna kitu; wanaiga uvivu wa wenyeji wao.
Tisa, hivyo basi, Waislamu wa pwani ya Tanzania, kama wenzao wote wa Somalia, Lamu, Malindi, Mombasa, Pemba, Unguja, Mafia, Kilwa, Lindi na Pemba ya Msumbiji, wana utamaduni wa Waarabu wa Ghuba wa kugomea shule. Tofauti na Waislamu wa Tanzania walioko Machame na Usangi mkoani Kilimanjaro, au Usukumani, au kule Bukoba, na hata wale wa Uganda (kabila la Baganda), wao wanapenda shule.
Maeneo yote waliyokaa Waarabu, kuanzia Bagamoyo, halafu fuata ile barabara ya watumwa hadi Kondoa, nenda hadi Tabora, fika mpaka Ujiji, ingia mpaka Kongo Mashariki, kote huku shule si mali kitu. TATIZO SI UISLAMU BALI NI UTAMADUNI WA UARABU WA GHUBA. Anayebisha hongera zake.
Kumi, tafiti tatu ninazozijua, moja ya Ilana Kessler wa Chuo Kikuu cha Georgetown cha Marekani
ya mwaka 2005, na ile ya Erasmus Kaijage wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ya mwaka 1999,
zinaonesha kwamba wanafunzi wa shahada ya kwanza wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam waliokuwa Waislamu ni kati ya asilimia 14 15 tu ya wanafunzi wote.
Aidha, Baraza la Udhamini la Waislamu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (DUMT), liliwahi kutoa taarifa yake kwamba kati ya mwaka 1986 hadi 1990, kwa wanafunzi walioingia chuoni hapo kusoma shahada ya kwanza Waislamu walikuwa asilimia 13 tu. Hiki ni kiasi kidogo mno, lakini ni kidogo cha kiasi gani cha Waislamu nchini? Lazima tujue hili nalo pia, hata kwa makadirio tu.
Kumi na Moja, sasa turudi kwenye jingine. Nyerere aliamua tuachane na sensa ya kupekua dini za watu kwa sababu nzuri kabisa - alitaka Watanzania tusitambuane kwa dini zetu (na makabila pia). Hivyo, ili kuweka usawa tukaanzisha msemo huu: Tanzania sisi nusu ni Waislamu na nusu ni Wakristo. Huu ni msemo tu na hauna usahihi. Aidha, hata kama sensa ya zamani ilionesha kwamba waislamu, ama wakristo, au wapagani ndiyo wengi, haina maana yoyote leo wakati taifa letu lina watu milioni 45 hivi. Tulipata uhuru tukiwa milioni 12 na baadaye Zanzibar ikaongeza laki tatu. Watanzania hatukuwa na kelele za asilimia ngapi ni dini hii na ile. Leo zimerudi. Inakera sana!
Kwa mujibu wa taarifa kadhaa za kitafiti (siyo mimi), Waislamu nchini Tanzania ni theluthi moja ya wananchi wote. Aidha, kwa bahati ama kwa mpangilio, rais wetu wa sasa, Mheshimiwa Kikwete, alipoteua mawaziri Novemba 2010 aliweka theluthi moja waislamu, na hivyo hivyo kwa manaibu. Wote tunajua. Hali kadhalika, alipoteua mawaziri na manaibu wao hii juzi, aliweka theluthi moja waislamu kwenye uwaaziri na pia kwenye unaibu.
Alipoteua Tume ya Kupitia Katiba, kwa wajumbe wa Bara aliweka pia theluthi moja yake waislamu. Iko wazi. Rais Kikwete, nijuavyo mimi, anajaribu kwa kila hali kuliangalia hili suala la kelele za udini ili asiiharibu nchi yetu. Hatopenda kukumbwa na malalamiko akishaondoka kwani na yeye ni binadamu kama sisi. Anakuwa mwangalifu sana hata kama kuna wakati anateleza kibinadamu. Je, hesabu zake zina maana gani? Nina hakika anajua anachokifanya na kamwe hawezi kuwaonea waislamu ambao ni Watanzania kama sisi wote. Hawezi kufanya uonevu.
| Year | Total Selected | Muslims | Percentage of Muslims Selected |
| 1978 | 956 | 216 | 23 |
| 1979 | 903 | 194 | 22 |
| 1980 | 1071 | 247 | 23 |
| Year | Muslim % | Non-Muslim % | Total |
|
| 17 | 83 | 100 |
| *1970/71 | - | - | - |
| 1971/72 | 13 | 87 | 100 |
| 1972/73 | 14 | 86 | 100 |
| 1973/74 | 13 | 87 | 100 |
| *1974/75 | - | - | - |
| 1975/76 | 15 | 85 | 100 |
| *1976/77 | - | - | 1. - |
| *1977/78 | - | - | - |
| 1978/79 | 14 | 86 | 100 |
| **1979/80 | 14 | 86 | 100 |
| **1980/81 | 11 | 89 | 100 |
| **1981/82 | 16 | 84 | 100 |
| Year | % Muslim | % Christians | Others | % TotTotal |
| 1971/72 | 13 | 86 | 1 | 100 |
| 1972/73 | 14 | 84 | 2 | 100 |
| 1973/74 | 13 | 79 | 8 | 100 |
| No. | School | Level | Region |
1. 2. 3. 4. 5. 6. 7. 8. 9. 10. 11. 12. 13. 14. 15. 16. 17. 18. 19. | Mafinga Ujiji Kilema Maua Uru Nanupa Makoko Kasita Lutheran Junior Saint Peter’s Nyegezi Kaengesa Likonde Mwadui Dungunyi Itaga Soni Katoke Rubiya | “O” “ “A” “O” “ “ “ “ “ “ “ “ “A” “O” “ “A” “O” “ “ | Iringa Kigoma Kilimanjaro Kilimanjaro Kilimanjaro Lindi Mara Morogoro Morogoro Morogoro Mwanza Rukwa Ruvuma Shinyanga Singida Tabora Tanga Kagera Kagera |
Mkata...
Haya hapo chini yanaweza kusaidia kuelewa matatizo haya tunayojadili hapa:
Warsha kikundi cha vijana wasomi wa Kiislam waliweza kujipenyeza BAKWATA na uongozi wa BAKWATA uliwakubali na kuwaamini.
Hapo ndipo walipofanya utafiti huo hapo chini ambao baada ya kukamilika ulitolewa kama waraka kwa kila Muislam wa Tanzainia.
Table 1
Selection of Std.VII Pupils to Form I in Dar es Salaam Region 1978-1981
Source: Dar es Salaam City Council, Department of Education.
Year Total Selected Muslims Percentage of
Muslims Selected1978 956 216 23 1979 903 194 22 1980 1071 247 23
NB: In 1967 census Muslims in Dar es Salaam Region were 67%; therefore the number of Muslim students in Dar es Salaam Primary Schools is greater than that of Christians. This should have reflected in the selection.
Table 2
Religious Distribution University of Dar es Salaam 1971/72-1973/74
* Official Statistics not available
Year Muslim % Non-Muslim % Total 1969/70 17 83 100 *1970/71 - - - 1971/72 13 87 100 1972/73 14 86 100 1973/74 13 87 100 *1974/75 - - - 1975/76 15 85 100 *1976/77 - - 1. - *1977/78 - - - 1978/79 14 86 100 **1979/80 14 86 100 **1980/81 11 89 100 **1981/82 16 84 100
** Students selected for Faculty of Agriculture, Forestry and Veterinary Science and medicine not included.
Source: 1969/70-1978/79 University of Dar es Salaam Students Directory.
1979/80-1981/82 Daily News June 1979/1981.
Table 3
Religious Distribution of University Admission 1971/72-1973/74
Source: University of Dar es Salaam Student Directory
Year % Muslim % Christians Others % TotTotal 1971/72 13 86 1 100 1972/73 14 84 2 100 1973/74 13 79 8 100
Table 4
Christian Seminary Secondary Schools 1980
Source: Ministry of National Education, Dar es Salaam.
No. School Level Region
1.
2.
3.
4.
5.
6.
7.
8.
9.
10.
11.
12.
13.
14.
15.
16.
17.
18.
19.Mafinga
Ujiji
Kilema
Maua
Uru
Nanupa
Makoko
Kasita
Lutheran Junior
Saint Peter’s
Nyegezi
Kaengesa
Likonde
Mwadui
Dungunyi
Itaga
Soni
Katoke
Rubiya“O”
“
“A”
“O”
“
“
“
“
“
“
“
“
“A”
“O”
“
“A”
“O”
“
“Iringa
Kigoma
Kilimanjaro
Kilimanjaro
Kilimanjaro
Lindi
Mara
Morogoro
Morogoro
Morogoro
Mwanza
Rukwa
Ruvuma
Shinyanga
Singida
Tabora
Tanga
Kagera
Kagera
Mohamed Said Historia, Siasa na Maendeleo Tanzania February 14, 2014 0
Reinveting BAKWATA, 1981 Part One
Reinventing BAKWATA, 1981 Part One Strangely the BAKWATA leadership at the headquarters decided to turn the organisation into a profi...mohamedsaidsalum.blogspot.com
Reinventing BAKWATA, 1981
Part One
USHAHIDI WA PICHA KWA HAYO NILIYOANDIKA HAPO JUUNyongeza:
ANASEMA MSEMAJI KUWA WAISLAM TANZANIA NI THELUTHI MOJA
Msomaji kamsoma huyu msemaji sasa kaniuliza anasema kuwa mimi nimeandika kitabu, "The Life and Times of Abdulwahid Sykes (1924 - 1968) The Untold Story of the Muslim Struggle Against British Colonialism in Tanganyika," (London 1998) je, hii struggle ya Waislam kupigania uhuru wa Tanganyika ilikuwa ya hawa Waislam theluthi moja?
Hili swali lake la kwanza.
Swali la pili anauliza hii theluthi mbili ilikuwa wapi haikushiriki katika kupigania uhuru kiasi kupigania uhuru wa Tanganyika kubebwe na Waislam wachache theluthi moja peke yao?
Jibu langu ni kuwa kama kweli Waislam wangekuwa theluthi moja na kama historia ya kupigania uhuru inavyoonyesha kuwa Waislam ndiyo waliokuwa mstari wa mbele kupambana kwanza na Wajerumani kwa silaha katika Vita Vya Maji Maji (1905 - 1907) kisha Muingereza kwa siasa kitendo hiki kingeweka historia ya pekee ulimwenguni.
Hapa ieleweke kuwa hakuna nchi duniani ambayo jamii yake ya watu wachache ndiyo iliyojitokeza kuihami nchi yao kwa silaha dhidi ya wakoloni wakati walio wengi wamejitenga pembeni.
Uko ushahidi wa kutosha kuthibitisha ukweli huu.
Ukichukua mfano huu jibu lisilo na shaka ni kuwa Waislam hawajapata kuwa theluthi moja Tanganyika.
Wangekuwa theluthi moja historia ya uhuru isingekuwa kama historia niliyoandika katika kitabu changu hicho nilichokitaja hapo juu.
Kwa ukweli huu basi yote ambayo mwandishi kaandika kuhusu Waislam si sawa kwa kukosa ushahidi unaosimama kwenye ukweli wa utafiti.
Nyongeza:
ANASEMA MSEMAJI KUWA WAISLAM TANZANIA NI THELUTHI MOJA
Msomaji kamsoma huyu msemaji sasa kaniuliza anasema kuwa mimi nimeandika kitabu, "The Life and Times of Abdulwahid Sykes (1924 - 1968) The Untold Story of the Muslim Struggle Against British Colonialism in Tanganyika," (London 1998) je, hii struggle ya Waislam kupigania uhuru wa Tanganyika ilikuwa ya hawa Waislam theluthi moja?
Hili swali lake la kwanza.
Swali la pili anauliza hii theluthi mbili ilikuwa wapi haikushiriki katika kupigania uhuru kiasi kupigania uhuru wa Tanganyika kubebwe na Waislam wachache theluthi moja peke yao?
Jibu langu ni kuwa kama kweli Waislam wangekuwa theluthi moja na kama historia ya kupigania uhuru inavyoonyesha kuwa Waislam ndiyo waliokuwa mstari wa mbele kupambana kwanza na Wajerumani kwa silaha katika Vita Vya Maji Maji (1905 - 1907) kisha Muingereza kwa siasa kitendo hiki kingeweka historia ya pekee ulimwenguni.
Hapa ieleweke kuwa hakuna nchi duniani ambayo jamii yake ya watu wachache ndiyo iliyojitokeza kuihami nchi yao kwa silaha dhidi ya wakoloni wakati walio wengi wamejitenga pembeni.
Uko ushahidi wa kutosha kuthibitisha ukweli huu.
Ukichukua mfano huu jibu lisilo na shaka ni kuwa Waislam hawajapata kuwa theluthi moja Tanganyika.
Wangekuwa theluthi moja historia ya uhuru isingekuwa kama historia niliyoandika katika kitabu changu hicho nilichokitaja hapo juu.
Kwa ukweli huu basi yote ambayo mwandishi kaandika kuhusu Waislam si sawa kwa kukosa ushahidi unaosimama kwenye ukweli wa utafiti.
Fresh...Mzee Mohammed, kwenye hoja ya waislamu wengi kushiriki kupigania uhuru , sababu kuu ni advantage ya location. yaani hayo ni makabila yaliyopokea uislam. na ardhi yao ipo kwenye miji iliyotumika kupiganiwa uhuru.
mfano Dar es salaam, harakati nyingi za kupigania uhuru zimefanyikia Dar es salaam, na Wote tunajua Dar es salaam ni mji wa wazaramo na wandengereko ambapo hayo makabila yameupokea uislam. wazaramo na wandengereko ni waislamu. imagine uhuru umepiganiwa kwao. lazima wengi washiriki kupigania uhuru. Binafsi sijawai kuona mzaramo mkristo na wala mndengereko mkristo.
sababu kuu ya waislam wengi kuwa kwenye harakati za kupigania uhuru ni kwamba harakati hizo zilifanyikia kwenye ardhi ya nyumbani kwao walipokuwa wanaishi.
kama harakati za uhuru zingefanyikia Mbeya maana yake wanyakyusa ambao wengi ni wakristo ndio wangejaa kwenye kupigania uhuru huo.
kama harakati za uhuru zingefanyikia Kilimanjaro Moshi maana yake wachaga ambao wengi ni wakristo ndio wangekuwa wengi
JokaKuu Mohamed Said Pascal Mayalla zitto juniorhabari wadau.
naonaga lawama nyingi za waislamu wakimlaumu Rais wa awamu ya kwanza Nyerere aliwabania kuwapa madaraka na fursa nzuri serikalini baada ya uhuru.
Mzee wetu kipenzi Mohamed Said huwa analiongelea swala hili la nyerere na waislamu mara kwa mara.
nimeshangaa kukuta maneno ya marehemu Bibi Titi Mohammed kwenye historia yake kueleza hali halisi ambayo waislamu walikuwa wanapitia kutoka kwa wazazi wao linapokuja swala la kwenda kusoma elimu dunia. ukisoma kipengele 2 . 1 kwenye historia iliyokwekwa hapo chini utajionea mwenyewe
waislamu wachache waliokubali kwenda shule enzi hizo ndio hao walipewa fursa. waliogoma kusoma nyerere aliwabeba waliobebeka kwa kujiendeleza kama Bibi Titi Mohammed
BIBI TITI MOHAMED: MWANAMAMA SHUPAVU NA MPIGANIA UHURU HODARI ALIYETINGISHA NA KUHESHIMIKA AFRIKA MASHARIKI NZIMA!!!
MICHUZI BLOGatSunday, February 17, 2019MAJAMBO,MAKTABA YA GLOBU YA JAMII,
1. Usuli:
1.1 TITI Kuzaliwa:
TITI MOHAMED SALUM MANDWAGA alizaliwa mwezi Juni 1926 jijini Dsm.
1.2 Wazazi Wa TITI: Baba yake aliitwa Bw. MOHAMED BIN SALIM na mama yake aliitwa Bi. HADIJA BINTI SALIM. Wazazi hawa walitokea Rufiji.
Baba yake alikuwa mfanyabiashara ya mbuzi na ng'ombe na mama yake alikuwa mkulima.
2. Elimu:
2.1 Baba Agoma TITI Asisome:
Baba yake alikataa katukatu kwamba TITI asisome shule kwa hofu angekuwa kafiri.
2.2 Mama Ampeleka TITI Shule:
Baba yake alifariki TITI akiwa na miaka 9 tu. Mamaye akatumia fursa hiyo kumpeleka TITI Shule ya Wasichana Uhuru ambako alisoma hadi darasa la 4.
3. TITI Aolewa na MHENGA akiwa na miaka 14 tu:
TITI aliolewa na mwanaume mzee ambaye angeweza hata kuwa baba yake wakati yeye akiwa binti wa miaka 14 tu.
4. TITI Ajifungua Mtoto wa Kike:
TITI alijifungua mtoto wa kike aitwae HALIambaye alikuja kuolewa na MZEE IDD HAMIS, Mshambuliaji hatari wa Cosmopolitans, klabu ya kwanza kutwaa ubingwa TZ ambapo walikuwa wakiishi mtaa wa Skukuu na Udowe na kubahatika kupata watoto 3 wa kiume.
4. TITI Aachana na mumewe:
TITI aliachana na mume huyo kijeba ambaye alikuwa ni baba wa HALIMA , mume ambaye hakuwa chaguo lake.
5. TITI Awa Maarufu kwa ngoma za Maulid:
TITI alianza kuwa maarufu angali mdogo alipokuwa kiongozi wa ngoma za maulid ambazo zilimjenga uwezo wa kujiamini na hivyo akawa maarufu sana.
6. TITI Aolewa na BOI SELEMAN:
TITI aliolewa na dreva wa teksi aitwae Boi Selemani, baada ya ndoa yake ya kwanza kusambaratika.
6. TITI Ajiunga na TANU:
TANU ilizaliwa tarehe 7.7.1954. Wanachama wa mwanzo kupata kadi za TANU walikuwa NYERERE(Kadi na.1), A. SYKES Na.2, A. SYSKES No.3 D. AZZIZ No.4, DENIS PHOMBEAH No.5, DOME OKOCH Na.6, J. RUPIA Na.7.
Bw. BOI, mme wa TITI, alikuwa ni rafiki wa Bw. SCHNEIDER PLANTAN aliyekuwa mmoja wa viongozi wa TAA. Siku moja, Bw. PLANTAN alienda nyumbani kwa BOI na kumweleza kuwa ametumwa kumweleza TITI ajiunge na TANU.
BOI alikubali na akajinunulia kadi na.15 ya TANU na pia akamnunulia TITI kadi na.16. Jumla alitoa TZS 12/= kwani kila kadi iliuzwa TZS 6/=.Ndivyo walivyojiunga TANU. BOI pia alichangia TSH 10/= kwa ajili ya nauli ya Mwalimu NYERERE kwenda UNO (TSH 5/= kila mmoja).
7. TITI Asomba wamama Lukuki Kujiunga TANU!!!
Tarehe 8.7.1955, TITI akiwa Mwenyekiti wa Tawi la Wanawake wa TANU, alifanya mkutano mkubwa na kuvuna wanachama 400 na ndani ya miezi 3 tu akawa amepata wanachama 5,000:
"Nilizungumza na mama Swalehe Kubunju, Kiongozi wa "Tongakusema" na akawaita wakinamama wote wa Tongakusema. Nikakutana nao Livingstone street alikokuwa akiishi mama Kubunju ambaye alihimiza: -"Ewe mwanamke, TITI anakuita, TITI yuko hapa". Hivyo wamama wakawa wanakuja kirahisi. Wakija nikawa nawaambia tunataka uhuru lakini hatuwezi kuupata kabla ya kujiunga TANU. Wanawake ndio nguvu ya dunia, hawa wanaume wote tumewazaa. Nilizunguka Tanganyika nzima. Safari ya kwanza mikoani tulienda Tanga tarehe 1.1.1956 mimi, Bwana mkubwa na RAJAB DIWANI na tukazunguka Tanga nzima kwa siku 21. Tuliporudi Kamati Kuu ikanipa ruhusa ya kusafiri peke yangu. Pia nilifanya safari nyingi na OSCAR KAMBONA. Tukiwa na KAMBONA tulikuwa tukipita nyumba hadi nyumba, usiku na mchana".
8. TITI Atia Fora Mikutano ya NYERERE:
TITI ndiye aliyekuwa akiimbisha na kuhutubia kwanza kabla ya NYERERE kupanda jukwaani "kushusha" nondo. Kwa hakika, TITI alikuwa akikonga nyoyo kwa kiswahili chake cha pwani na nyimbo zake: (Hongera mwanangu eeh na mi nihongere eeh hongera X 2) na (Mama Usungu, Mama Usungu X 2).
9. KENYA Wamuomba TITI "Awapige Tafu" Kudai Uhuru"
Uwezo mkubwa wa kushawishi na kujiamini kulifanya jina la TITI livuke mipaka ya Tanganyika. Wapigania uhuru wa Kenya TOM MBOYA, JARAMOGI OGINGA ODINGA nk walipopata sifa za TITI walituma ujumbe kumuomba aende Kenya kusaidia kuishawishi serikali ya mkoloni kumwachia huru JOMO KENYATTA.
TITI alienda Kenya na alitia fora sana maeneo ya Nairobi, Machakos, Kisumu na Mombasa.
Miaka michache baada ya KENYATTA kuachiwa, mara moja alikuja TZ. KENYATTA alihutubia mkutano mkubwa Jangwani akiwa na suaruali ya kodrai ya udongo na koti kubwa la kijivu huku akipeperusha usinga mweusi alimshukuru sana TITI kwa jitihada zake mujarab alipokuwa nchini Kenya.
Ni katika mkutano huu ndipo Mwalimu NYERERE alisema yuko tayari kuona Tanganyika inachelewa kupata uhuru ili Kenya ipate uhuru wake na ziweze kuungana.
10. TITI Amsindikiza NYERERE Airport kwenda UNO:
Tarehe 17.2.1955, TITI alikuwa mmoja wa wanaTANU waliomsindikiza NYERERE Airport kwenda UNO kuwaeleza kuwa "Tanganyika lazma kieleweke".
11. TITI Akumbana na changamoto kedekede:
Katika harakati zake za kuwashawishi wanawake na wanaume kujiunga na TANU, TITI alikumbana na changamoto lukuki. Kwanza aliambiwa ni mwizi wa waume za watu na pia akaambiwa anatafuna michango ya TANU:
"Kulikuwa na changamoto nyingi sana. Siku moja nilienda nyumba moja kuarifu mkutano wa TANU. Nikakuta wanawake wamekusanyika na kudai eti nimeenda kuiba waume wa watu. Lakini mmoja wao akawaambia huyu mama ndiye anaetangaza chama cha NYERERE nilimuona pia nyumba ya mbele, hana lengo baya".
12. BOI Alalamika kwa PLANTAN kuwa Amegeuka Housegirl:
Mmewe TITI, BOI alilalamika vikali kwa PLANTAN kuwa TITI hatulii nyumbani kutokana na harakati za TANU hadi yeye kugeuka yaya wa kujipikia na kujifulia nguo na hakuona tena faida ya ndoa. BOI akamshutumu PLANTAN kwa kumuingiza TITI kwenye chama cha TANU.
BOI pia wivu ulikuwa umerindima kwenye "medula oblangata yake" hadi akabwabwaja'- "TITI ni mwanamke wa kiislam, kasoma madrasa, kapanda jukwaani bila baibui. Hii si sawa kabisa".
13. Ndoa ya TITI Yaparaganyika Sababu ya Harakati za Kudai Uhuru:
Kutokana na mishemishe na safari zisizoisha za TITI, ndoa ya TITI ikaparanganyika kama alivyoelezea mwenyewe:
"BOI mwenyewe ndie aliyeniruhusu kujiunga na TANU na tena ndiye aliyeninunulia kadi ya uanachama. TANU pia ilimwandikia barua anisaidue mambo ya TANU.Lakini mwisho hizi safari zilimshinda. Nilikuwa nakaa nje ya Dsm hata kwa miezi 3 na nikirudi sikai hata siku 10, nasafiri tena. BOI akaniambia anataka kuoa mke mwingine. Nikamwambia sawa, niache na kazi yangu kwani nimeizoea. Kwahiyo BOI akamuoa Bi. KHADIJA lakini wakashindwana wakaachana. Nilifunga mizigo yangu nikaondoka kwa BOI".
TITI akaja kuolewa tena.
14. NYERERE na TITI "Waangusha" rhumba "La kufa mtu" siku ya uhuru".
Tarehe 9.12.1961, ilikuwa siku ya kipekee kwa Mwalimu NYERERE na TITI ambao kwa miaka kadhaa hapo nyuma walizunguka kila kona ya Tanganyika kuhimiza wananchi kujiunga na TANU na kudai uhuru.
Siku hiyo, Mwalimu NYERERE na TITI walikaa "High Table" na usiku wakiwa nadhifu walifungua muziki wa kuukaribisha uhuru kwa kusakata rhumba kwa bashasha kubwa!.
15. TITI Ashinda Ubunge Rufiji:
TITI alishinda ubunge Rufiji na kuteuliwa kuwa Waziri mdogo wa wizara ya Utamaduni na Maendeleo. Pia alishika wadhifa wa Waziri mdogo wa Afya na pia Uwaziri mdogo wizara ya Maendeleo ya Jamii. Aidha, tarehe 2.11.1962, Rais NYERERE aliagiza vyama vyote vya wanawake vivunjwe na iundwe UWT na TITI akawa ndiye Mwenyekiti.
Mwaka 1965, TITI alishindwa ubunge huko Rufiji.
16. TITI Apelekea KISWAHILI Kutumika Bungeni:
TITI alikuwa ameishia darasa la 4 tu hivyo alikuwa hawezi "kutema yai" kwa ufasaha. Siku moja mwanzoni mwa 1960s akiwa bungeni akatoa hoja kwamba wananchi wa magomeni wanataka nao wawe na taa za barabarani ambapo alisema -: "We want fire in Magomeni.... We want fire in small bottles".
Wabunge wengi walicheka pamoja na NYERERE akiwa PM ambapo aliamuru KISWAHILI kianze kutumika bungeni.
17. TITI Alitolea nje Azimio la Arusha:
Mwaka 1967, TITI, bila kupepesa macho wala kutikisa pua, akabwaga manyanga na kujiuzulu ujumbe wa Kamati Kuu ya TANU kwani alikuwa hakubaliani na Kipengele cha 5(a) cha Azimio la Arusha kuhusu maadili kwamba ni marufuku kiongozi wa serikali au TANU kuwa na nyumba ya kupangisha.
TITI alikuwa na nyumba 2 ambapo moja aliijenga kwa kuuza vito vyake vya dhahabu na nyingine ni ya mkopo. Nyumba moja ipo Upanga mkabala na Makao Makuu, JWTZ na nyingine ipo Temeke.
Uhusiano wa NYERERE na TITI ukawa umelegalega.
18. TITI Akamatwa na Kushtakiwa kwa Uhaini:
TITI alikamatwa mwezi Octoba 1969 na kudaiwa kuwa alikula njama pamoja na OSCAR KAMBONA, GREY MATTAKA, JOHN CHIPAKA, MICHAEL KAMALIZA, WILLIAM CHACHA na ALFRED MILLINGA, kuipindua serikali. TITI alikuwa ni mwanamke pekee katika kesi hiyo.Walidaiwa kupanga kutekeleza azma hiyo wakati Rais NYERERE atakapokuwa nje ya nchi. Kesi ilianza kurindima 6.6.1970 chini ya Jaji Mkuu, Georges, CJ na upande wa mashtaka ukiongozwa na MARK BOMANI.
Kesi ilinguruma kwa siku 127. TITI ns wenzake kasoro Bw. MILLINGS walitiwa hatiani kutokana na ushahidi madhubuti na kupewa kifungo cha maisha. TITI akaenda kutumikia kifungo gereza la Isanga, Dodoma.
19. Mume wa TITI Amwacha solemba!
Baada ya TITI kukumbwa na dhahama ya kesi ya uhaini, mmewe akaamua kumuacha kwani aliona hiyo ni fedheha kubwa isiyovumilika!.
20. Nyumba 2 za Bibi TITI Zataifishwa:
Wakati akiwa anatumikia kifungo chake cha maisha, serikali ikataifisha nyumba zake mbili zilizotajwa hapo juu.
21. MWANAMAMA Mkenya Amuomba Mwalimu Amsamehe TITI:
Mwanamama mmoja mwanasiasa machachali wa Kenya baada ya kupata habari za TITI kufungwa maisha alikuja Butiama na akaomba aonane na Mwalimu na mama yake. Alipoonana nao akasema:
"Utakuwa ni wizi wa fadhila kama wewe NYERERE utaendelea kumfunga TITI licha ya yote aliyokufanyia wewe, TZ na sehemu hii ya dunia. Tafadhali sana nimetumwa na wanawake wa Kenya nikuombe umwachie huru kama yeye alivyopigania kuachiwa huru kwa JOMO KENYATTA".
Mwalimu NYERERE alimjibu mama huyo kuwa maombi hayo ameyapokea na atayafanyia kazi.
22. TITI Achiwa kwa Msamaha wa Rais, 1972:
Rais NYERERE, akitumia mamlaka yake chini ya ibara ya 45 ya Katiba, alimsamehe TITI mwezi April 1972.
23. TITI Akwea "gogo" kuja Dsm:
Baada ya kusikia msamaha huo, TITI hakuamini maskio yake kwani aliishaamua kupambana na hali yake na alijua angefia gerezani. Hivyo, alipanda garimoshi na kuja Dsm akiwa na furaha tele na meno yote 32 nje.
Ndugu zake walimlaki kwa bashasha na akaenda kuishi kwenye nyumba kuukuu ya mama yake iliyoko Temeke. Mama yake, aliyekuwa mtu mzima sana, almanusra azimie kwa mshtuko wa kumuona mwanae!.
24. MH. MALECELA Atumwa Kenya kuekeza TITI Yuko Huru:
Rais NYERERE alimtuma Mh. JOHN SAMWELI CIYEGWEYAMIS MALECELA , Waziri wa Mambo ya Nje, kwenda Kenya kumweleza yule mama Mwanasiasa machachali kuwa TITI ameachiwa. Baada ya kupata ujumbe huo, Mwanamama huyo aliyejawa na furaha akasema: "Naomba kamwambie Mwalimu NYERERE kwa niaba ya wanawake wote wa Kenya na wananchi wa Afrika Mashariki, nasema asante sana kwa uungwana wake".
25. TITI Aishi Maisha ya Kifukara:
Baada ya kuachiwa toka Lupango, TITI alienda kuishi Temeke. Maisha yake yalikuwa ya kipweke sana kwani ndugu na marafiki walimnyanyapaa: "Mtu angeweza kufikiri kwamba nina ugonjwa wa kuambukiza". TITI akawa muda mwingi anakaa kibarazani kwao akiuza mafuta ya taa ya rejareja ili kuweza kumudu maisha!.
26. BIBI TITI Arudishiwa nyumba zake:
Rais ALI HASSAN MWINYI alimrudishia BIBI TITI nyumba zake zote 2. Hivyo, Bibi TITI akahamia nyumba ya Upanga.
27. BIBI TITI Afariki:
BIBI TITI alifariki tarehe 5.11.2000 katika hospitali ya Net care, Afrika Kusini alikokwenda kwa matibabu.
28. BIBI TITI Apewa Mtaa, Dsm:
Kama kumbukizi ya kuheshimu mchango mkubwa wa mwanamama huyu wa kipekee, mtaa mmoja maarufu jijini Dsm umepewa jina lake "Barabara ya Bibi TITI".
MWISHO:
Huyu ndiye BIBI TITI MOHEMED, Mwanamama shupavu aliyetoa mchango mkubwa katika kupatikana kwa uhuru wa Tanganyika aliyekuwa si mnafiki na hapindishi maneno kwa kile alichokiamini wala hamwogopi binadamu yeyote zaidi ya Mungu!!
historia hii nimeitoa kwenye blog ya michuzi.
BIBI TITI MOHAMED: MWANAMAMA SHUPAVU NA MPIGANIA UHURU HODARI ALIYETINGISHA NA KUHESHIMIKA AFRIKA MASHARIKI NZIMA!!!
1. Usuli: 1.1 TITI Kuzaliwa: TITI MOHAMED SALUM MANDWAGA alizaliwa mwezi Juni 1926 jijini Dsm. 1.2 Wazazi Wa TITI: Baba yake al...www.michuzi.co.tz
Utasoma vip elimu mkoloni ili uwe kibaraka ,enzi hizo waliokuwa wanakataa elimu ni wale wanaotaka uhuru ...Waliokubali elimu ndio walitunga mashairi ya kupinga ukombozi..msubiri yule mzee mwenye profile la soda mixa udini aje kujaza maelezo kwa nini baba yake kakosa kuwa serikalini
Ni zaidi ya nyumba ndogo. Ni moja ya waasisi wa Kisutu womenNyumba ndogo ya mwalimu