Historia ya Qur'an

Historia ya Qur'an

Huyu jamaa nakumbuka siku waliyomfukuza Uislamu..

Aliita Jopo la Ulaamaa Na Masheikh wa Madhehebu yote/Wawakilishi halafu akawaambia eti yeye Hamza amekuja kwenye Mwili Yeye ni Nabii Ilyassa (Nabii Elisha)..

Alipigwa Spana Na kufukuzwa kwenye uislamu Juu...

Akaanzisha Dini yake Yenye mchanganyiko wa Uislamu na Ukristo 🤣🤣

PART 2 : ANAENDELEA KUTOWA DARSA


View: https://m.youtube.com/watch?v=MZAn-s-3Wzs
 
Wakatoliki ndio walioanzisha Uislamu Ili kuwaweka waarabu ndani ya utawala mmoja wa kiimani, kabla waarabu walikuwa wakiabudu miungu yao mbalimbali kupitia masanamu Ili iwe rahisi kuwatawala, Majasusi wa Shirika la Jesuit vatican wakaanzisha dini mpya itwayo islam,itakayowaunganisha waarabu wote kiimani mwaka 600 AD. Mapadre watano wa kikatoliki ndio walioandika kitabu cha Quran na kumtafuta mwanamke mfanyabiashara aitwae Bi Hadija na kumpa utajiri. Bi khadija ndie alimtafuta kijana aitwae Muhammad akamkabidhi kwa mapadre wa kikatoliki ndio waliomfunza Quran mapangoni.Ndipo Uislamu ukaenea kwa kasi Sana Katika nchi za kiarabu ambazo zamani zilikuwa ni nchi za Kikristo ukavuka mpaka na kutaka kuingia nchi za Ulaya mashariki kutokea Uturuki Ili kwenda kuiteka Vatican, Majasusi wa Jesuit wakaingia tena vitani wakarudisha nyuma kupitia vita vya msalaba waarabu wakala Sana panga toka vatican wakarudi nyuma, rejea vita vya msalaba na ottoman empire. Majuzi magaidi wa ISIS tokea iraq wakataka kuendeleza mpango ulioshindwa wa ottoman empire kuupenyesha utawala wa kiislamu Ulaya. Wakasambaratishwa na USA na NATO na kumuua Al baghad kiongozi wa ISIS. Huku kundi la ISIL tawi la ISIS Syria likipelekwa kuzimu na ndege za Putin.
Dini zote uzionazo duniani ni tawi la ukatoliki, maprostetant wote ni watoto wa katoliki.
Leta nyaraka hatununui maelezo matupu shekh
 
Mbona wewe hujakaa kimya wakati hujui lolote? Jibu joja zangu kama wewe siyo boya tu

.
Kuna mtu unaweza kujadiliana nae kwakuwa anamwelekeo lkn siyo wewe,,,,, Kile kitendo tu cha kusema Quran imetungwa na wakatoliki inatosha kujua jinsi ulivyo mweupe ktk bahari hii ya elimu

Kwa taarifa yako Quran ililetwa kidogo Kidogo kutokana na matukio kwa mda wa miaka 23

Haya je inawezekanaje kwa binadamu kuweza kutabiri matukio yajayo miaka 23 na kuleta maandiko yanayo sadifu hali halisi ya wakati huo?

Lengo si kujadiliana na wewe kwakuwa najua utanipotezea muda wangu bure

Acha porojo za mitaani katufute elimu sahihi ndo uje kwenye meza ya majadiliano

Asante
 
Kuna msemo unasema kila zama na kitabu chake ikiwa na maana manabii/mitume waliopita walikuwa na vitabu vyao mfano wa torati, injili, zaburi na quran.

Kwa mujibu wa uislaam kila nabii alipewa kitabu chake kulingana na zama alizonazo lakini maudhui yakiwa ni kumtangaza Mungu mmoja.

Nmejibu kile nnachofaham mkuu mtoa maada atakujibu zaid kwa anachofaham na yeye
Hivyo vitabu vya Alah vya Torati, Zaburi na Injili Umewahi kuviona? Mohamad amewahi kuviona?

Nitajie mtu mmoja tu aliyewahi kuviona.
 
Hivyo vitabu vya Alah vya Torati, Zaburi na Injili Umewahi kuviona? Mohamad amewahi kuviona?

Nitajie mtu mmoja tu aliyewahi kuviona.
Kila dini ina doubt nyingi ila uislamu muhammad ali fabricated vitu vingi sana
Ugumu wanaopata wanaotetea uislamu kabla muhammad hajazaliwa civilization tayari ilishakuwepo kwa hiyo kudanganya

Ndo maana wayahudi na wakristo walimkataa muhamad waziwazi sababu alitaka kuweletea story ambazo wao wanazo miaka nenda rudi kabla hata hajazaliwa alafu anawaambia kashushiwa

Katika watu ambao nitawapa tuzo za uongo ni muhammad jamaa ni genius kwenye uongo (master of fabrication) hakuna kama yeye
 
Nimesumbuka kupitia uzi mpaka mwisho nipate majibu ya hizi hoja lakini hakuna kitu. Njooni mjibu hizi hoja angalao na sisi tupate elimu ya bure.
Wkt mwingine hoja muhimu hazijibiwi kutokana na upuuzi kutamalaki,,,, ila zitajibiwa usijali
 
Mtume alikuwa Muislam kwa miaka 23 (kuanzia miaka 40 hadi 53)..Mimi naomba kujibiwa maswali yafuatayo:

1. Tangu kuzaliwa kwake Mtume hadi alipofika umri wa miaka 40 alikuwa anaabudu wapi?
2. Mungu wake alikuwa nani?
3. Kibla chake kilikuwa wapi?
4. Msikiti wake ulikuwa wapi?
5. Utaratibu wake wa kuswali ulikuaje?
6. Alikuwa akifunga Ramadhan? (Ilikuwa na maana gani kwake?
7. Alikuwa akienda kuzunguruka Kabah? Je Kabah Ilikuwa na midoli au haikuwa nayo?

mgen
Che mittoga
HISTORIA FUPI YA MTUME (Swalla Allahu Aleyhi Wa Salam)

JINA LAKE NA NASABA YAKE.
Jina lake ni Mohammad bin Abdallah bin Abdul Mutwalib bin Hashim bin Abdul Manaf bin Quswai bin Kilaab. Na ukoo wake mtukufu unamalizikia kwa mtume Ibrahiim (Aleyhi Salam)

MAMA YAKE.
Mama yake ni Amina binti Wahab bin Abdul Manafi bin Zuhra bin Kilaab.

JINA LAKE MASHUHURI.
1- Mustafa, na anayo majina mengine mengi yaliyo pokelewa ndani ya Qur’ ani tukufu kama:
2- Khaatamun nabiyyiin.
3- Al ummiyyi.
4- Al muzammil.
5- Al mudathir.
6- Al mubiin.
7-Al kariim.
8- An nuur.
9- An niima.
10- Ar rahmaan.
11- Ash shaahid.
12- Al mubashir.
13- An nadhiir.
14- Abdur rauuf.
15- Ar rahiim.
16- Ad daai na mengine mengi.

TAREHE YA KUZALIWA KWAKE.
Alizaliwa tarehe 12 mwezi wa Rabiiul awwal, mwaka wa tembo sawa na mwaka 571 A.D.kutokana na kauli iliyo mashuhuri kwa wanahistoria.

SEHEMU ALIPO ZALIWA.
Alizaliwa katika mji wa Makkatul Mukarramah ulioko katika nchi ya Saudi Arabia.

KUPEWA KWAKE UTUME.
Ali pewa rasmi utume tarehe 27 mwezi wa Rajab katika mji wa Makka baada ya kutimiza miaka 40 ya umri wake mtukufu.

MAFUNDISHO YAKE.
Mtume (Swalla Allahu Aleyhi Wa Salam) alikuja na wito wa usawa kwa viumbe wote, na alikuwa akilingania undugu, na msamaha kwa kila mwenye kuingia kwenye Dini ya ki islaam. kisha aliweka sheria iliyo nyepesi, na kanuni za uadilifu alizo zipokea kutoka kwa Allah Subhana Wa Ta'ala alie takasika, kisha waislaam wakazipokea kutoka kwa Mtume (Swalla Allahu Aleyhi Wa Salam).

MIUJIZA YAKE.
Muujiza wake pekee wa milele na milele ni Qur’ ani tukufu; ama miujiza yake iliyo dhihiri mwanzoni mwa uislaam ni mingi
sana kwani hai hesabiki.

WITO WAKE.
Mtume (Swalla Allahu Aleyhi wa Salam) ali walingania watu kwenye upweke wa Allah katika mji wa Makka na kwa njia ya siri kwa muda wa miaka mitatu, na baada ya kipindi cha siri ali waita watu kwa njia ya wazi kwa muda wa miaka kumi.

KUHAMA KWAKE.
Alihama kutoka katika mji wa Makkah kwenda Madina mwanzoni mwa mwezi wa rabiul awwal baada ya kupita miaka 13 tangu kupewa utume, na kuhama huko kulitokana na maudhi mengi ya makuraishi, mushrikina na makafiri kumuelekea yeye na maswahaba wake.

VITA VYAKE.
Allah Subhana Wa Ta'ala Alie takasika Alimpa idhini ya kuwapiga vita mushrikina na makafiri na wanafiki, na baada ya idhini hiyo aliweza kuingia kwenye mapambano na watu hao kwenye vita vingi sana, na kati ya hivyo vilivyo kuwa mashuhuri ni Badri, Uhudi, Khandaq (Al ahzaab) Khaibar, na Hunain.

WAKEZE MTUME (Swalla Allahu Aleyhi Wa Salam).
Mtume alikuwa na wake Kama ifuatavyo : Wakwanza ni :


1 Khadijah bint Khuwailid.
2 Sauda bint Zam'ah. 3 'Aishah bint Abi-Bakr. 4 Zainab bint Khuzaymah.
5 Umm Salamah. 6 Hafsah bint 'Umar. 7 Zainub bint Jahsh. 8 Juwayriyah bint al-Haarith.
9 Umm Habibah bint Abi Sufyaan.
10 Safiyya bint Huyayy. 11 Maymuna bint al-Haarith.
12 Mariya Bint Sham'un - Mqibti (Mamake Ibrahim)

WATOTO WAKE MTUME (Swalla Allahu Aleyhi Wa Salam).
Watoto wake ni kama wafuatao:

1- Abdallah.
2- Qaasim.
3- Ibrahiim
4- Fatima
5- Zainab
6- Ruqayya
7- ummu kulthum

BABA ZAKE WADOGO.
Mtume (Swalla Allahu Aleyhi Wa Salam) ana baba wadogo tisa (9), nao ni watoto wa Abdul Mutwalib kama wafuatao:
1- Al haarith.
2- Zubair.
3- Abu Twalib.
4- Hamza.
5- Al ghidaaq
6- Dharaar Al Muqawwim,
7- Abu Lahab.
8- Al Abbas.

SHANGAZI ZAKE MTUME (Swalla Allahu Aleyhi Wa Salam).
Mtume (s.a.w) alikuwa na shangazi sita kutokana na akina mama tofauti nao ni kama wafuatao:
1- Umaimah.
2- Ummu hakiimah.
3- Burrah.
4- Aatikah.
5- Swafiyyah.
6- Arwy.

MLINZI WAKE.
Mlinzi wake alikuwa ni Anas.

WAADHINI WA MTUME (Swalla Allahu Aleyhi Wa Salam).
1- Bilal Al –habashi
2- Ibnu Ummu Makhtuum.
3- Saad Al-qurt.

NEMBO YA PETE YA MTUME (Swalla Allahu Aleyhi Wa Salam).
Nembo ya pete yake ilikuwa ni (( Mohmmad rasuulu llah)).

UMRI WAKE (Swalla Allahu Aleyhi Wa Salam).
Aliishi kwa muda wa miaka 63.

MUDA WA UTUME WAKE (Swalla Allahu Aleyhi Wa Salam).
Utume wake ulidumu kwa muda wa miaka 23.

TAREHE YA KUFARIKI KWAKE (Swalla Allahu Aleyhi Wa Salam).
Alifariki dunia tarehe 28 mwezi wa safar mwaka wa 11 hijiria.

SEHEMU ALIYO FIA (Swalla Allahu Aleyhi Wa Salam).
Mtume alifia katika mji wa Madinatul Munawwarah.

SEHEMU ALIYO ZIKIWA (Swalla Allahu Aleyhi Wa Salam).
Alizikiwa katika mji wa Madina ndani ya Chumba cha mkewe Bi Aisha bint Abubakar.

SEHEMU ALIOZALIWA MTUME MUHAMMAD (Swalla Allahu Aleyhi Wa Salam).

Hii nisehemu ya makumbusho kwa vizazi vyetu kwa sasa ambayo alizaliwa kiumbe bora kuliko viumbe vyote hapa Duniani. Na sehemu hii ni moja ya sehemu yenye kuheshimiwa Sana ktk mji wa makka.

Watu wa serikali ya kifalme ya mji wa makkah walipata taabu sana kuienzi sehemu kwa kuweka nini ili sehemu hii iweze kutambulika vyema.

Wapo waliosema ujengwe mnara mkubwa Sana ili ulitambulishe eneo hili, wapo waliosema eneo hili lisawazishwe tu kisha lizungushiwe wigo na liandikwe kuwa ndio sehemu Alipozaliwa Mtume Mohammad.

Baada ya mbishano mkubwa ikabidi serikali ya Saudia iwasikilize wataalam wa dini na wasomi wa dini wanahukumu vipi kuhusu eneo hili ndipo wasomi wadini hii tukufu wakatoa wazo kuwa sehemu hii tukufu alipozaliwa mtume wa Allah na kiumbe bora.

Pajengwe Maktaba ya kiislamu Na pawekwe vitabu vyoote vya kidini ili waislam wapate faida kupitia maktaba hiyo, ndipo lilipojengwa jengo hili la maktaba hapo na watu huingia bure kabisa kujisomea vitabu mbalimbali vya dini yetu tukufu ya kiislam hapa.
 
HISTORIA YA QUR'AN.

Sehemu ya Pili (3).

Naam, Kama tulivyopata kuona mwanzo wa DARASA hili juu ya kuteremshwa kwa Qur'an, lakini pia Qur'an imeshushwa kwa lengo la kuwaongoza wanaadamu katika kila kipengele cha maisha ya kila siku ya kibinafsi na kijamii. Lengo la Qur-an linabainishwa katika aya ifuatayo:

👉“Ni mwezi wa Ramadhani ambamo imeshushwa Qur-an ili iwe mwongozo kwa watu na hoja zilizo wazi na upambanuzi (baina ya haki na batili) " (2:185)
Katika kuendea lengo lake hili, Qur-an humuongoza mwanaadamu kukiendea kila kipengele cha maisha yake ya kibinafsi na kijamii na hutoa hoja zenye mashiko dhidi ya wapinzani wake.

Katika kuonesha uwezo wake katika kumuongoza mwanaadamu katika kila kipengele cha maisha yake, Qur-an imeitwa (imesifiwa) kwa majina yafuatayo:

1. Al-Qur-an
Maana yake ni "Chenye kuunganishwa pamoja" au "chenye kusomwa. "Yaani Qur-an ni kitabu kilichofumwa na herufi, silabi, maneno, aya na sura, kinachosomwa mara kwa mara. Kitabu hiki kimeitwa kwa jina hili la "Al-Qur-an" kwa sababu ni mkusanyiko wa mafunzo ya msingi ya maisha ambayo mtu hanabudi kuyarejea mara kwa mara. Qur-an ndio Mwongozo sahihi pekee wa maisha ya mwanadamu hivi sasa.

2. Kalamullah:
Maneno ya Allah (s.w). Qur-an yote ni maneno ya Allah (s.w) yenye kutoa mwongozo kwa walimwengu wote kupitia kwa Mtume Muhammad (s.a.w) kwa njia ya Wahy kupitia kwa Malaika Jibril (a.s).

3. Al-Mus-haf:
Mkusanyiko wa kurasa. Hili ni jina mashuhuri lililotumiwa na maswahaba wa Mtume (s.a.w) baada ya Qur-an kukamilika kushuka na kuwekwa katika sura ya kitabu kikubwa.

4. Al-Kitaab:
Kitabu pekee (Unique book). Qur-an ni kitabu kikamilifu kisicho na upogo wala dosari yoyote wala hakina mfano wa kitabu chochote kimuundo, maudhui na uwasilishaji wa maudhui hayo. Qur-an yenyewe imeliweka hili wazi katika aya ifuatayo:

👉"Hiki ni kitabu pekee (Al-Kitaab) kisicho na shaka ndani yake na ni mwongozo kwa wamchao Mwenyezi Mungu." (2:2)

5. Al-Furqaan:
Kipambanuzi cha Haki na Batili au ukweli na uwongo. Yaani Qur-an ndio kipimo cha Haki na Batili au Zuri na Baya au Jema na Ovu, Tawhiid na Shiriki, Uislamu na Ukafiri

6. Adh-Dhikru:
Mawaidha au ukumbusho. Qur-an ni mawaidha yenye kumkumbusha kila mwenye kusoma na kuzingatia.

7. At-Tanziil:
Mshuko au wahy kutoka kwa aliye juu. Jina hili linasisitiza kuwa Qur-an ni kitabu cha Allah (s.w) kilichoshushwa kwa njia ya wahy kwa Mtume Muhammad(s.a.w) kupitia kwa malaika Jibril(a.s) ili awaongoze walimwengu kwacho.

8. Al-Hukmu:
Kitabu pekee kinachostahiki kumuhukumu mwanaadamu. Hukumu yoyote kinyume na Hukumu ya Qur-an ni upinzani na uasi dhidi ya Allah (s.w) na ni dhulma dhidi ya wanaadamu kama inavyosisitiza Qur-an yenyewe:

👉“…Na wasiohukumu kwa yale aliyoteremsha Mwenyezi Mungu, basi hao ndio makafiri." (5:44)

👉“….Na wasiohukumu kwa yale aliyoteremsha Mwenyezi Mungu, basi hao ndio madhalimu." (5:45)

👉“…. Na wasiohukumu kwa yale alioteremsha Mwenyezi Mungu, basi hao ndio waasi (mafasiki)." (5:47)
Neno “wasiohukumu” hapa limetumika kwa maana ya wanaoendesha maisha yao kinyume na yale aliyoteremsha Allah au wale wasioendesha maisha yao kwa mujibu wa Qur-an

9. Al-Hikma:
Kitabu pekee chenye Hikima isiyo kikomo. Ni kitabu cha Allah (s.w) ambaye ndiye chimbuko (source) la Elimu na Hekima. Hekima ni jambo la sawa sawa lililofanywa kwa namna ya sawa sawa katika mazingira na wakati wasa wasa ili kufukia lengo tarajiwa. Qur’an ni Hikma na humuuongoza binaadamu aishi maisha ya Hikma.

10. Ash-Shifau:
Ponyo au dawa pekee. Qur-an imeitwa kwa jina hili la "Ponyo pekee" kwa sababu Qur-an ndio dawa pekee ya kuponya maradhi ya "nafsi". Maradhi makubwa ya nafsi ni Ukafiri, Ushirikina, Unafiki na Uasi wa kila aina. Qur-an imejizatiti katika kuyaelezea magonjwa haya ili kila mtu mwenye akili timamu ayafahamu bayana na imeelekeza kwa ufasaha namna ya kuyatibu.

11. Ar-Rahmat:
Rehema kwa watu. Vipawa vinavyomfanya binaadamu atofautiane na wanyama ni akili na elimu. Vipawa hivi vikitumika bila ya kufuata mwongozo kutoka kwa Allah (s.w) humpelekea binaadamu kufanya uharibifu katika ardhi kuliko mnyama yoyote yule. Binaadamu akitumia akili yake na elimu aliyotunukiwa kwa kufuata mwongozo wa Qur-an huwa juu na bora kuliko viumbe vyote.

12. Al-Khayr:
Qur-an ni kheri pekee. Yaani Qur-an ndio chanzo cha kheri zote. Kheri hupatikana kwa kufuata Qur-an vilivyo.
13.Ar-Ruuhu:
Qur-an ni roho ya maisha. Yaani mtu asiyeishi kwa kufuata Qur-an ni kama maiti japo anaishi. Allah (s.w) anawaasa waumini wasiwakumbatie wapinzani wa Qur-an (makafiri) kwani wao ni kama maiti walio makaburini.

👉"Enyi mlioamini! Msifanye urafiki wa ndani na watu ambao Mwenyezi Mungu amewakasirikia na wamekata tamaa ya akhera kama walivyokwisha kata tamaa makafiri waliozikwa makaburini." (60:13)

14. Al-Bayaana:
Qur-an ni kitabu pekee chenye maelezo ya wazi na kinachofafanua aya zake kwa uwazi kwa kutumia mifano iliyozoeleka katika mazingira ya watu kwa nyakati zote za historia. Hivyo, kila mwenye akili timamu anao uwezo wa kuielewa Qur-an na ikamuongoza.

15. An-Nuur:
Qur-an ni nuru pekee. Qur-an ni mwanga unaomuonesha binaadamu njia sahihi ya maisha itakayomfikisha kwenye lengo la kuumbwa kwake. Kuishi bila ya kufuata Qur-an ni sawa na mtu anayetembea katika giza nene na matokeo ya kutembea kwenye giza nene yanafahamika kwa kila mwenye akili timamu. Qur-an inatukumbusha:

👉"Allah ni kiongozi wa walioamini. Huwatoa kwenye giza na kuwaingiza katika nuru (mwanga). Lakini waliokufuru viongozi wao ni Matwaghuti huwatoa katika nuru na kuwaingiza katika giza. Hao ndio watu wa motoni, humo watakaa milele." (2:257)

16. Al-Burhan:
Hoja pekee iliyowazi. Qur-an ni kitabu kinachotoa hoja zilizo wazi kwa wasomaji wake. Kwa mfano Qur-an inatoa hoja zilizo wazi, kuwa lazima pawe na Muumba mmoja wa ulimwengu na vyote vilivyomo mwenye ujuzi na Hekima. Pia Qur-an pamoja na kutoa hoja maridhawa juu ya kumuamini Allah (s.w) na nguzo nyinginezo za imani , huonesha lengo la kumuabudu Allah (s.w) na umuhimu na hekima ya kufuata Qur-an na Sunnah kama mwongozo pekee wa njia sahihi ya maisha ya binaadamu.

17. Al-Haqq:
Qur-an ni Haki. Qur-an ni haki kwa sababu ni maneno ya Allah (s.w) ambaye ni mjuzi wa kweli aliyeepukana na upungufu wa aina yeyote. Qur-an humuongoza binaadamu kwenye njia ya haki na huhukumu kwa waki.

18. Ahsan-ul-Hadith:
Maneno mazuri au maelezo mazuri kuliko yote kwa kuwa yanatoka kwa Allah (s.w), Mjuzi, mwenye hekima.
Kitabu hiki cha Allah (s.w), kilichosifiwa kwa majina haya, kina aya 6,236 zilizogawanywa katika sura 114 (Rejea jedwali 1). Pia kitabu cha Qur-an (Al-Mas-haf) kimegawanywa kwenye juzuu au mafungu (30) yaliyo sawa sawa.

Inaendelea InshaaAllah...

Allah Ni Mjuzi Zaidi.
 
Qur'an haina faida yeyote kwa Mtanzania kujuwa, ni haibu kwako mleta mada kuwaletea Watanzania wenzako vitu visivyo na tija katika maisha yao. Hivi hata wewe mwenyewe huoni haibu kweli, hiki kitabu ni cha Waarab, wewe kama Mtanzania kinakuhusu nini? Tuachane na ujinga wa kujitakia.
Kwanza kajifunze kuandika "haibu" = aibu.
 
Hapana Ila nitakupa maele



036.Je, Uislamu ulikuwepo kabla Mtume Muhammad s.a.w?

Naam, ulikuwepo kabla,Uislamu ndiyo Msingi ambao kila mteule wa Mungu Mwenyezi alikuwa akiwahubiria watu wake,kila Zama ilikuwa Ni juu ya watu kutakiwa wasilimu,
Ukisoma hapa utaona Quran.com/4/163 quran.com/42/13

Sasa Soma hapa

127. Na kumbukeni Ibrahim na Ismail walipo inyanyua misingi ya ile Nyumba wakaomba: Ewe Mola Mlezi wetu! Tutakabalie! Hakika Wewe ndiye Msikizi Mjuzi.



128. Ewe Mola Mlezi wetu! Tujaalie tuwe ni wenye kusilimu kwako, na pia miongoni mwa vizazi vyetu wawe umma ulio silimu kwako. Na utuonyeshe njia za ibada yetu na utusamehe. Bila shaka Wewe ndiye Mwenye kusamehe Mwenye kurehemu.



129. Ewe Mola Mlezi wetu! Waletee Mtume anaye tokana na wao, awasomee Aya zako, na awafundishe Kitabu na hikima na awatakase. Hakika Wewe ndiye Mwenye nguvu, Mwenye hikima.



130. Na nani atajitenga na mila ya Ibrahim isipo kuwa anayeitia nafsi yake katika upumbavu? Na kwa yakini Sisi tulimteuwa yeye katika dunia; na hakika yeye katika Akhera atakuwa miongoni mwa watu wema.



131. Na Mola wake Mlezi alipo mwambia: Silimu, Nyenyekea! Alinena: Nimesilimu, nimenyenyekea kwa Mola wa walimwengu wote.



132. Na Ibrahim akawausia wanawe, na pia Yaaqub: Enyi wanangu! Hakika Mwenyezi Mungu amekuteulieni Dini hii; basi msife ila nanyi mmekuwa Waislamu, wanyenyekevu.



133. Je! Mlikuwapo yalipo mfikia Yaaqub mauti, akawaambia wanawe: Mtamuabudu nani baada yangu? Wakasema: Tutamuabudu Mungu wako na Mungu wa baba zako, Ibrahim na Ismail na Is- hak, Mungu Mmoja tu, na sisi tunasilimu kwake.



134. Hao ni watu walio kwisha pita. Watapata waliyo yachuma, nanyi mtapata mtakayo yachuma; wala hamtaulizwa nyinyi waliyo kuwa wakiyafanya wao.



135. Na wakasema: Kuweni Mayahudi au Wakristo ndio mtaongoka. Sema: Bali tunashika mila ya Ibrahim mwongofu, wala hakuwa katika washirikina.



136. Semeni nyinyi: Tumemuamini Mwenyezi Mungu na yale tuliyo teremshiwa sisi, na yaliyo teremshwa kwa Ibrahim na Ismail na Is-hak na Yaakub na wajukuu zake, na waliyo pewa Musa na Isa, na pia waliyo pewa Manabii wengine kutoka kwa Mola wao Mlezi; hatutafautishi baina ya yeyote katika hao, na sisi tumesilimu kwake.



137. Basi wakiamini kama mnavyo amini nyinyi, itakuwa kweli wameongoka. Na wakikengeuka basi wao wamo katika upinzani tu. Na Mwenyezi Mungu atakutosheni kukukingeni na shari yao, na Yeye ndiye Msikizi, Mjuzi.



138. Huko ndiko kupaka rangi kwa Mwenyezi Mungu, na nani aliye mbora wa kupaka rangi kuliko Mwenyezi Mungu? Na sisi ni wenye kumuabudu Yeye tu.



139. Sema: Mnahojiana nasi juu ya Mwenyezi Mungu, naye ni Mola wetu Mlezi na Mola wenu Mlezi, na sisi tuna vitendo vyetu na nyinyi mna vitendo vyenu? Nasi tunamsafia Yeye tu.



140. Au mnasema kuwa Ibrahim na Ismail na Is-hak na Yaakub na wajukuu zao walikuwa Mayahudi au Wakristo? Sema: Je, nyinyi mnajua zaidi au Mwenyezi Mungu? Na ni nani mwenye kudhulumu zaidi kuliko yule aliye ficha ushahidi alio nao utokao kwa Mwenyezi Mungu? Na Mwenyezi Mungu si mwenye kughafilika na hayo myafanyayo.



141. Hao ni watu walio kwisha pita. Wao watapata waliyo yachuma, na nyinyi mt apata mliyo yachuma, wala hamtaulizwa nyinyi yale waliyo kuwa wakifanya wao.

Quran 2
Unatumia vyanzo vya kiislam kuutetea uislam.Nje ya Quran na bible ni wapi tutapata ushahidi wa existance za uislam kabla ya Muhammad?
 
HISTORIA FUPI YA MTUME (Swalla Allahu Aleyhi Wa Salam)

JINA LAKE NA NASABA YAKE.
Jina lake ni Mohammad bin Abdallah bin Abdul Mutwalib bin Hashim bin Abdul Manaf bin Quswai bin Kilaab. Na ukoo wake mtukufu unamalizikia kwa mtume Ibrahiim (Aleyhi Salam)

MAMA YAKE.
Mama yake ni Amina binti Wahab bin Abdul Manafi bin Zuhra bin Kilaab.

JINA LAKE MASHUHURI.
1- Mustafa, na anayo majina mengine mengi yaliyo pokelewa ndani ya Qur’ ani tukufu kama:
2- Khaatamun nabiyyiin.
3- Al ummiyyi.
4- Al muzammil.
5- Al mudathir.
6- Al mubiin.
7-Al kariim.
8- An nuur.
9- An niima.
10- Ar rahmaan.
11- Ash shaahid.
12- Al mubashir.
13- An nadhiir.
14- Abdur rauuf.
15- Ar rahiim.
16- Ad daai na mengine mengi.

TAREHE YA KUZALIWA KWAKE.
Alizaliwa tarehe 12 mwezi wa Rabiiul awwal, mwaka wa tembo sawa na mwaka 571 A.D.kutokana na kauli iliyo mashuhuri kwa wanahistoria.

SEHEMU ALIPO ZALIWA.
Alizaliwa katika mji wa Makkatul Mukarramah ulioko katika nchi ya Saudi Arabia.

KUPEWA KWAKE UTUME.
Ali pewa rasmi utume tarehe 27 mwezi wa Rajab katika mji wa Makka baada ya kutimiza miaka 40 ya umri wake mtukufu.

MAFUNDISHO YAKE.
Mtume (Swalla Allahu Aleyhi Wa Salam) alikuja na wito wa usawa kwa viumbe wote, na alikuwa akilingania undugu, na msamaha kwa kila mwenye kuingia kwenye Dini ya ki islaam. kisha aliweka sheria iliyo nyepesi, na kanuni za uadilifu alizo zipokea kutoka kwa Allah Subhana Wa Ta'ala alie takasika, kisha waislaam wakazipokea kutoka kwa Mtume (Swalla Allahu Aleyhi Wa Salam).

MIUJIZA YAKE.
Muujiza wake pekee wa milele na milele ni Qur’ ani tukufu; ama miujiza yake iliyo dhihiri mwanzoni mwa uislaam ni mingi
sana kwani hai hesabiki.

WITO WAKE.
Mtume (Swalla Allahu Aleyhi wa Salam) ali walingania watu kwenye upweke wa Allah katika mji wa Makka na kwa njia ya siri kwa muda wa miaka mitatu, na baada ya kipindi cha siri ali waita watu kwa njia ya wazi kwa muda wa miaka kumi.

KUHAMA KWAKE.
Alihama kutoka katika mji wa Makkah kwenda Madina mwanzoni mwa mwezi wa rabiul awwal baada ya kupita miaka 13 tangu kupewa utume, na kuhama huko kulitokana na maudhi mengi ya makuraishi, mushrikina na makafiri kumuelekea yeye na maswahaba wake.

VITA VYAKE.
Allah Subhana Wa Ta'ala Alie takasika Alimpa idhini ya kuwapiga vita mushrikina na makafiri na wanafiki, na baada ya idhini hiyo aliweza kuingia kwenye mapambano na watu hao kwenye vita vingi sana, na kati ya hivyo vilivyo kuwa mashuhuri ni Badri, Uhudi, Khandaq (Al ahzaab) Khaibar, na Hunain.

WAKEZE MTUME (Swalla Allahu Aleyhi Wa Salam).
Mtume alikuwa na wake Kama ifuatavyo : Wakwanza ni :


1 Khadijah bint Khuwailid.
2 Sauda bint Zam'ah. 3 'Aishah bint Abi-Bakr. 4 Zainab bint Khuzaymah.
5 Umm Salamah. 6 Hafsah bint 'Umar. 7 Zainub bint Jahsh. 8 Juwayriyah bint al-Haarith.
9 Umm Habibah bint Abi Sufyaan.
10 Safiyya bint Huyayy. 11 Maymuna bint al-Haarith.
12 Mariya Bint Sham'un - Mqibti (Mamake Ibrahim)

WATOTO WAKE MTUME (Swalla Allahu Aleyhi Wa Salam).
Watoto wake ni kama wafuatao:

1- Abdallah.
2- Qaasim.
3- Ibrahiim
4- Fatima
5- Zainab
6- Ruqayya
7- ummu kulthum

BABA ZAKE WADOGO.
Mtume (Swalla Allahu Aleyhi Wa Salam) ana baba wadogo tisa (9), nao ni watoto wa Abdul Mutwalib kama wafuatao:
1- Al haarith.
2- Zubair.
3- Abu Twalib.
4- Hamza.
5- Al ghidaaq
6- Dharaar Al Muqawwim,
7- Abu Lahab.
8- Al Abbas.

SHANGAZI ZAKE MTUME (Swalla Allahu Aleyhi Wa Salam).
Mtume (s.a.w) alikuwa na shangazi sita kutokana na akina mama tofauti nao ni kama wafuatao:
1- Umaimah.
2- Ummu hakiimah.
3- Burrah.
4- Aatikah.
5- Swafiyyah.
6- Arwy.

MLINZI WAKE.
Mlinzi wake alikuwa ni Anas.

WAADHINI WA MTUME (Swalla Allahu Aleyhi Wa Salam).
1- Bilal Al –habashi
2- Ibnu Ummu Makhtuum.
3- Saad Al-qurt.

NEMBO YA PETE YA MTUME (Swalla Allahu Aleyhi Wa Salam).
Nembo ya pete yake ilikuwa ni (( Mohmmad rasuulu llah)).

UMRI WAKE (Swalla Allahu Aleyhi Wa Salam).
Aliishi kwa muda wa miaka 63.

MUDA WA UTUME WAKE (Swalla Allahu Aleyhi Wa Salam).
Utume wake ulidumu kwa muda wa miaka 23.

TAREHE YA KUFARIKI KWAKE (Swalla Allahu Aleyhi Wa Salam).
Alifariki dunia tarehe 28 mwezi wa safar mwaka wa 11 hijiria.

SEHEMU ALIYO FIA (Swalla Allahu Aleyhi Wa Salam).
Mtume alifia katika mji wa Madinatul Munawwarah.

SEHEMU ALIYO ZIKIWA (Swalla Allahu Aleyhi Wa Salam).
Alizikiwa katika mji wa Madina ndani ya Chumba cha mkewe Bi Aisha bint Abubakar.

SEHEMU ALIOZALIWA MTUME MUHAMMAD (Swalla Allahu Aleyhi Wa Salam).
Mkuu mbona nilisikia Mtume wenu alipaa mbinguni !
 
Unatumia vyanzo vya kiislam kuutetea uislam.Nje ya Quran na bible ni wapi tutapata ushahidi wa existance za uislam kabla ya Muhammad?
Chief

Bahati mbaya sana wengi wenu mnaulewa mbaya kuhusu nini ni Uislamu?

Mnadhani uislamu ni kuswali swala tano, kufunga ramadhani, kuvaa kanzu na kofia na kadhalika.

Maana halisi ya Uislamu ni kujisalimisha au kunyenyekea chini ya Mwenyezi Mungu.

Yeye ndio muumbaji wa huu ulimwengu na vyote viliomo ndani yake na ana mamlaka yote juu ya kila kitu,,,, hivyo viumbe vyote vinamtegemea yeye, na vinapaswa kunyenyekea na kujisalimisha kwake na huo ndio Uislamu

Sasa kuanzia binadamu wa kwanza Baba yetu Adamu alikuwa mnyenyekevu na alijisalimisha kwa Allah,,,,, kwahiyo Uislamu ndio umbile halisi la wanadamu wote mbele ya Mola wao.

Asante
 
KatetiMQ nakupa ushauri mmoja, jikite zaidi kwenye mada yako,,, na jibu hoja tu ambazo unaona zina hekima na Busara kwasababu kwa uzoefu wa mambo haya ya dini ubishani wa kipuuzi ni mwingi mno.

Pili jifunze kuwapuuza baadhi ya watu kwani ni wapuuzi mno wanajifanya wanajua kumbe hawana wanachojua

Asante
Hii ni sawa na kumshauri akimbie maswali magumu, kwa kisingizio kwamba ni ya kipuuzi.
 
ARV kama ulivyosema ktk comment yako kuna hoja ulitaka zijibiwe,,,, basi twende pamoja taratibu

Hoja ya kwanza tangu kuzaliwa kwake Mtume swalla aallahu alayhi wasallam mpaka anafikia miaka 40 aliabudu wapi?

Kwanza mitume wa Allah sio kama wanasiasa kwamba ameibuka ghafla na kuamua kuingia ktk siasa,,,, Mitume wa Allah huwa wameandaliwa na Allah vizazi na vizazi ni swala la muda tu ukifika hutambulishwa katika jamii yake,na huwa tayar ujio wake unajulikana toka katika vitabu vya Allah toka huko zamani, sasa je huenda kwanini labda maandiko kumuhusu Muhammad hayaonekani katika vitabu vyenu ni kutokana na watu kuchezea vitabu vya Mungu na kubadilisha maneno yake.

Wale watu wa mwanzo waliobahatika kupata nakala halisi wanajua ujio wa Mtume Muhammad swalla aallahu alahyi wa sallamu.

Mfano bibi Khadija baada ya Mtume kukutana na Malaika Jibril /Gabriel kwa mara ya kwanza,,, alimpeleka Mtume Kwa mwanazuoni mmoja alikuwa mkristo, akasema kumwambia Mtume kuwa "natamani ningekuwa kijana na kuwa na mda mrefu wa kuishi nije kuona jinsi watu wako watakavyokuja kukukataa na kukufukuza katika mji wako" na hili lilikuja kutokea kweli,,, Kwa kufupisha mambo tunapata kujua ujio wa Muhammad ulijulikana.

Mfano wa pili siku moja Mtume alikuwa Katika msafara wa kibiashara walipofika katika mji mmoja ,kulikuwa na mtawa wa kiyahudi, alishangazwa na kumuona Mtume kila anapoenda kuna kivuli juu kinamfuata, baadae akaongea na mtu aliyeongozana na Mtume na kumwambia huyu kijana si wa kawaida, akamsogelea na kutaka kumuangalia shingoni kwani alisema hakika mitume huwa wana mihuri ya asili shingoni mwao, kuangalia kweli upo, akamwambia yule mtu aliyeambatana na Mtume kuwa awe makini na yule kijana wasije watu wabaya wakamgundua na kumdhuru.

Nilianza na hoja hizo ili kwanza uone Mitume huwa na asili gani.

Sasa kwakuwa Mitume hutayarishwa na Allah basi huepushwa na kila aina shiriki,Muhammad hakuwahi kuabudu sanamu wala kushiriki mambo ya shughuli za kipuuzi toka ujana wake, na alikuwa anajulikana na Makka yote kama kijana mwaminifu, yeye ndio alikuwa anatunza amana za watu wa Makka kwa uaminifu wake.

Na ndio maana alilopanda juu ya jabari kwa mara ya kwanza kuwatangazia watu kwamba yeye ni Mtume wa Allah, alianza kwa kusema je nikiwaambia nyuma ya mlima huu Kuna jeshi la adui linakuja kuwavamia je mtaniamini? Umati mzima wakajibu tutakuamini kwakuwa hukuwahi kusema UWONGO.

Hapo unaona ni jinsi kiumbe huyu mtukufu alipambwa na tabia njema zote unazo zijua wewe.

Kwahiyo hakushiriki katika ibada haramu na alikuwa anatatizwa sana na jamii yake kuabudu masanamu na miungu mingine, ndio maana alikuwa akienda huko mbali katika jabali na kutafakari juu ya Mungu wa kweli.

Nitarejea tena kujibu hoja nyingine,,, kuwa na subira ,ukiwa na hekima na busara tutaenda sawa.

Asante
 
NYIE mnaosema muhammad alikuwa anaabudu nini before mulishawahi swali hilo hilo kwa yesu,musa na wengineo?
 
Najua hata mwenyewe unajua kuwa kuna mambo ya kipuuzi
Inaonekana wewe ni muoga wa maswali magumu.

Mara kwa mara unamsihi mleta mada apuuze maswali.

Kimsingi hakuna swali la kuignore, kila swali linahitaji jibu.
 
Back
Top Bottom