Historia ya Qur'an

Historia ya Qur'an

Wakatoliki ndio walioanzisha Uislamu Ili kuwaweka waarabu ndani ya utawala mmoja wa kiimani, kabla waarabu walikuwa wakiabudu miungu yao mbalimbali kupitia masanamu Ili iwe rahisi kuwatawala, Majasusi wa Shirika la Jesuit vatican wakaanzisha dini mpya itwayo islam,itakayowaunganisha waarabu wote kiimani mwaka 600 AD. Mapadre watano wa kikatoliki ndio walioandika kitabu cha Quran na kumtafuta mwanamke mfanyabiashara aitwae Bi Hadija na kumpa utajiri. Bi khadija ndie alimtafuta kijana aitwae Muhammad akamkabidhi kwa mapadre wa kikatoliki ndio waliomfunza Quran mapangoni.Ndipo Uislamu ukaenea kwa kasi Sana Katika nchi za kiarabu ambazo zamani zilikuwa ni nchi za Kikristo ukavuka mpaka na kutaka kuingia nchi za Ulaya mashariki kutokea Uturuki Ili kwenda kuiteka Vatican, Majasusi wa Jesuit wakaingia tena vitani wakarudisha nyuma kupitia vita vya msalaba waarabu wakala Sana panga toka vatican wakarudi nyuma, rejea vita vya msalaba na ottoman empire. Majuzi magaidi wa ISIS tokea iraq wakataka kuendeleza mpango ulioshindwa wa ottoman empire kuupenyesha utawala wa kiislamu Ulaya. Wakasambaratishwa na USA na NATO na kumuua Al baghad kiongozi wa ISIS. Huku kundi la ISIL tawi la ISIS Syria likipelekwa kuzimu na ndege za Putin.
Dini zote uzionazo duniani ni tawi la ukatoliki, maprostetant wote ni watoto wa katoliki.
Hii habari inaweza kuwa kweli maana niiona mahali, hatar sana
 
Sikiliza vizuri au una lengo lako jengine hapo hapajasemwa njia ya kuwashinda Juja wa maajuja ni kupitia Issa bin mariam au kiengereza huelewi vizuri nikuwekee ya kiswahili ??
Nimesikiliza vizuri sana, na kiinglish nakipata vizuri sana.

Nikuulize, Humo Issa bin Mariamu ametajwa. Ametajwa kwamba ana jukumu gani?
 
Naona mtunzi alipoona Musa alishushiwa zile amri kumi nae akasema imeshushwa ila kihistoria zilikua nyingi kabla ya utawala mmoja uarabuni kuzikusanya na kuchambua kuiweka kuwa moja na kuzipiga marufuku kuran nyingine kutumika.
Hii Ndio ukweli, zingine walichoma.

Leo wanazuoni wa kiisalam wanabishana kuhusu hii kauli kuwa Quran ilishushwa
 
NYIE mnaosema muhammad alikuwa anaabudu nini before mulishawahi swali hilo hilo kwa yesu,musa na wengineo?
Yesu alikuwa Myahudi.

Musa hakuna ushahidi wa Kihistoria kama alikuwa ni historical figure au legendary figure
 
Unataka kuniambia wayahudi wakimjua Mungu kwa jina la Yesu ?
Wakati wa Yesu kulikuwa na makundi kadhaa ya Wayahudi.
1. Wafarisayo
2. Sedukayo
3. Essenes
4. Zealots
5. wakristo (Wafuasi wa Yesu)
 
Kama hakukuwa na uislamu Mona inasemekana watangulizi wake mtume walikuwa waislamu yaani akina Ibrahim Musa na Adam, hapo imekaaje?
Propaganda hizo mkuu. Waislam hujipa moyo
 
Umeandika

Kuhusu Mohamad kushushiwa Quran. Kwa kifupi Mohammad alikuwa ni mtu mwenye akili nyingi sana, ni mtu alieisoma Biblia au alikariri kwa umakini na akaja na idea ya kupinga utatu mtakatifu. Ukweli ni kwamba Mohammad alitunga Quran na kuanzisha dini, na msingi wake mkubwa ulikuwa ni kupinga utatu mtakatifu, ukuu wa Yesu na ufufuko wa Yesu, hizo ndio hoja zake kubwa.

Swali

Lete ushahidi wa haya maneno yako kwamba Mtume alijua kusoma
Nimesema, uenda Mohammed alikuwa anajua kusoma au alikariri Bible. Ukisoma Quran utaona

Mfano hapa hii Aya ya Surah Al Mahidah 116, ukitafakari vizuri hii ni akili ya Mwanadamu ikitunga majungu

Na pale Mwenyezi Mungu atakapo sema: Ewe Isa bin Maryamu! Ati wewe uliwaambia watu: Nifanyeni mimi na mama yangu kuwa ni miungu badala ya Mwenyezi Mungu? (Na Isa) atasema: Subhanaka, Wewe umetakasika! Hainifalii mimi kusema ambayo si haki yangu. Ikiwa nilisema basi bila ya shaka umekwisha yajua. Wewe unayajua yaliyo ndani ya nafsi yangu, lakini mimi siyajui yaliyo katika nafsi yako. Hakika Wewe ndiye Mjuzi mkubwa wa yaliyo fichikana.​

 
Quran imeshushwaje mwezi wa ramadhani wakati uislam ulianza baada ya kushushwa kwa Quran na Muhammad ndiye aliyekuwa muislam wa kwanza

Kama una aya inaosema kuwa manabii kabla ya Muhammad walikuwa na mwezi wa ramadhani onyesha hapo au reference yoyote kama ipo

Pia kwanini Allah ashushe hadithi ambazo zilikuwa tayar zipo kwenye biblia?
Mwezi wa ramadhani ulikuwepo kabla ya mtume ni jumla ya miezi katika mwaka wa kalenda ya kiislamu lakini kabla ya mtume hakukuna na swaumu za mwezi mzima Kama ilivyo Sasa Ila swaumu ilikuwepo kabla ya mtume mwezi huu una fadhila nyingi mno kwa waumini wa kiislamu na mtume ametusihi tufunge ndani ya mwezi huu ili kujiongezea thamani ya fadhila zinazopatikana kwenye mwezi huu na kusherehekea kushuka kwa Quran pia na hitisho lake ni siku ya iddy'l fitr ambayo tunasherehekea kukamilika kwa ibada yetu
 
FADHILA NA SIFA ZA KIPEKEE ZA RAMADHAAN

Utangulizi
Mwezi wa Ramadhan uliobarikiwa umetufikia, mwezi ambao ni msimu wa kuchuma thawabu kwa Muislamu na kufaidika na fadhila zake nyingi. Mwezi huu Mtukufu Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) ameutukuza na kuuchagua kuliko miezi mingine ilobaki.

Fadhila za Mwezi wa Ramadhaan
1. Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) amefanya funga yake ni faradhi na nguzo katika nguzo tano za Uislamu.

Imethibiti kwa Bukhari na Muslim kupitia kwa 'Abdullah bin 'Umar (Radhiya Allaahu 'anhumaa) aliyesimulia kwamba Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa sallam) amesema:

"Uislamu umejengwa juu mambo Matano: Kushuhudia ya kwamba hapana Mungu anayepasa kuabudiwa wa haki isipokuwa Allaah na kwamba Muhammad ni Mtume wake; Kusimamisha sala; Kutoa zaka, Kufunga mwezi wa Ramadhani; na kuhiji Nyumba tukufu ya Allaah iliyopo Makka."

2. Allaah (Ta'ala) amejaaliya kufunga Ramadhani ni miongoni mwa sababu za kusamehewa madhambi na kupandishwa daraja.

Amesema Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa sallam) katika Hadiyth Swahiyh:
"Mwenye kufunga Ramadhaan kwa imani (kwamba kufunga ni lazima) na kwa ikhlasi na matarajio (kwamba atalipwa kwa funga yake) basi atasamehewa madhambi yake yaliyotangulia."

Ni vyema ikaeleweka kuwa mwenye kufunga Ramadhaan kwa imani na matarajio kama iliyoelezwa hapo juu basi atapata malipo makubwa. Ama kwa yule ambaye anafunga kwa sababu ya kutaka kuonekana au kufunga bila ya kuwa na elimu sahihi ya funga huyo atakuwa kala hasara.

3. Allaah (Ta'ala) ameweka katika Shari'ah kupitia Mtume Wake kuwa kusimama usiku na kusali ni miongoni mwa sababu za kusamehewa madhambi:

Amesema Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa sallam):
"Mwenye kusimama [usiku wa] Ramadhaan kwa imani na matarajio basi atasamehewa madhambi yake yaliyotangulia."

Vile vile amesema (Swalla Allaahu 'alayhi wa sallam):
"Mwenye kusali pamoja na imamu (mpaka mwisho wa sala yaani) imamu akaondoka, basi anaandikiwa kama amesali usiku mzima."

4. Miongoni mwa sifa za kipekee za Ramadhaan ni kuwepo usiku mtukufu unaopatikana katika masiku kumi ya mwisho. Kuna fadhila kubwa katika usiku huo mtukufu wenye cheo ambapo ibada yoyote inayofanywa (ikiwa sala au dhikri) ni bora kuliko ibada ilofanywa katika miezi elfu ya kawaida.

5. Matendo yanalipwa maradufu katika mwezi huu kama vile kisomo cha Qur-aan, kuleta Adhkaar za asubuhi na jioni, kutoa sadaqa, kuwazuru jamaa na kadhalika.

6. Allaah (Ta'ala) amefanya Ramadhaan njia ya kufikia uchamungu.

Allaah Anasema:
"Enyi mlioamini! Mmelazimishwa kufunga (Saumu) kama walivyolazimishwa waliokuwa kabla yenu ili mpate kumcha Allaah."[2:183]

Hitimisho
Tujitahidi kufaidika na Ramadhaan kwa kutumia muda wetu vizuri. Kujiepusha kupoteza muda na kufanya mambo ya upuuzi.

Ee Allaah Tupe Tawfiiq ya kufaidika na Ramadhaan
 
TAFSIRI YA QUR'AN; SURA AL-GHASHIYAH (88) AYA YA 1-10

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ هَلْ أَتَاكَ حَدِيثُ الْغَاشِيَةِ
1
"Ewe Muhammad ﷺ" Je! Imekufikia khabari ya msiba wa kufunika? ( Yaani: kwa Yakini Imekufikia, Ewe muhammad Habari ya tukio la lifunikalo, ambalo ni Qiyaama. Qiyaama kimeeitwa KIFUNIKACHO kwa sababu Kitawafunika Viumbe Kwa matukio yake ya Kutisha.

وُجُوهٌ يَوْمَئِذٍ خَاشِعَةٌ
2
Siku hiyo nyuso zitakuwa Dhalili. ( kwa Yakini Siku ya Qiyaama Nyuso zitakuwa Dhalili na Zenye Unyonge. Watu siku ya Qiyaama watakuwa makundi mawili. La Kwanza, ni la Waovu. Na La Pili ni wale watu Wema.

عَامِلَةٌ نَاصِبَةٌ
3
Zikifanya kazi, nazo taabani.(yaani Ni wale Waliokuwa Wakifanya Ibada alafu hawana Amali njema, Hao Watakuwa Taabani.

تَصْلَىٰ نَارًا حَامِيَةً
4
Ziingie katika Moto unao waka -( Yaani Wale Madhalili Madhalimu, walio Kufa bila Amali Njema, Basi Mungu anatoa amri Hao Waingie kwenye moto mkali sana,

تُسْقَىٰ مِنْ عَيْنٍ آنِيَةٍ
5
Zikinyweshwa kutoka chemchem inayo chemka.(
na Wanyweshwe Maji yenye kuchemka sana. AL-AANIY ni Maji yenye Ukali wa Kutokota.

لَيْسَ لَهُمْ طَعَامٌ إِلَّا مِنْ ضَرِيعٍ
6
Hawatakuwa na chakula isipo kuwa kichungu chenye miba. (ADH-DHARII: Katika Lugha ya Waquraysh Ni aina ya Miba ambayo inapokuwa mibichi inaitwa Al-Shabraq.. Ikikauka inaitwa Adh-dharii: hiyo ndio chakula cha Madhalili.

لَا يُسْمِنُ وَلَا يُغْنِي مِنْ جُوعٍ
7
Hakinenepeshi wala hakiondoi njaa.( Yaani Miba Hiyo hainenepeshi wala Haiondoi njaa aliyo nayo huyo anae kula.)

AYA YA 8- Inakusudia yule mwenye matendo mema, basi huyo uso wake utakuwa na Nuru na Wenye Kung'aa.

وُجُوهٌ يَوْمَئِذٍ نَاعِمَةٌ
8
Siku hiyo nyuso nyengine zitakuwa kunjufu. (Yaani, Nyuso zitakuwa na Neema na Furaha. Nyuso hizi ni za Watu wa kundi la Pili (Watu Wema) Watakuwa hivyo kwa sababu ya Mwisho wao Mwema.

لِسَعْيِهَا رَاضِيَةٌ
9
Zitakuwa radhi kwa juhudi yao( juhudi ya mema waliyo fanya Wameridhika )

فِي جَنَّةٍ عَالِيَةٍ
10
Katika Bustani ya juu.( Yaani Wale watu wema, watakuwa katika Jannah Ya Juu zaid) Neno jannah Ni Peponi Kwa kingereza ni Paradise.

Allah atujalie Mwisho Mwema, Siku ya Qiyaamah akatuweke kwenye VITI vya Mbele Ili tuwaone manabii wake Kisha atuingize Jannat

WABILLAH TAUFIYQ 💕

KARIBU KATIKA UISLAMU
 
HII NDO TOFAUTI KUBWA KATIKA YA QUR'AN NA BIBLIA(Historia ya Waisrael)

Biblia... 👇

Mwanzo 1:1 "Hapo mwanzo Mungu aliziumba mbingu na nchi."

Qur'an 👇

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَـٰنِ الرَّحِيمِ

(AL-FAATIH'A - 1)
KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU.
 
UISLAM UMESIMAMA IMARA👌

WAISLAM TEMBEENI VIFUA MBELE KWA KUWA MPO KWENYE NJIA ILIYO NYOKA SAWASAWA👌

QURANI KUFANANA BAADHI YA AYA ZA BIBILIA SI HOJA KUWA QURAN IMECOPY HUKO NI KUKOSA ILIMU NA NI DALILI TOSHA KUWA HUYU MTU NI MJINGA HAJUI KITU👈

JE ni KWELI DAI la MAKAFIRI VIBUBUSA kwamba MTUME MUHAMMAD [ s.a.w ] ALIANDIKA QUR'AN kwa MSAADA wa MAYAHUDI na WAKRISTO ?

KAMA DAI LA MAKAFIRI LINA UKWELI WOWOTE kwamba MTUME MUHAMMAD [ s.a.w ] AMENAKILI BIBLIA KUANDIKA QUR'AN ,

JE kuna UZITO GANI kwa MAKAFIRI hao PAMOJA na MAJINI WAKICHANGANYIKA KULETA MFANO wa ANGALAU SURA MOJA ya QUR'AN ?

QUR'AN IMETOA CHANGAMOTO hiyo TANGU kuanza KUSHUKA kwake:

"SEMA " Hata WAKIJIKUSANYA #WATU [ WOTE ] na #MAJINI kuleta MFANO wa hii QUR'AN basi #HAWANGALIWEZA kuleta MFANO wake, hata kama WATASAIDIANA [ VIPI ] WAO kwa WAO."
[ QUR'AN SURA 17:88 ]

JE ,ni IPI HUKUMU YA BIBLIA ENDAPO MTUME / NABII wa MWENYEZI MUNGU ATAINGIZA UWONGO WAKE KATIKA KAZI ALIYOTUMWA na MWENYEZI MUNGU ?

................................................................
MAKAFIRI wa KARNE hii SIO tu WALIOANZISHA MADAI haya #BALI MADAI HAYA ni MAKONGWE kuanzia KARNE hizo za KUSHUSHWA QUR'AN kwa MTUME MUHAMMAD [ s.a.w ] mpaka hivi LEO.

Aidha , MAKAFIRI wengine WANASEMA MTUME MUHAMMAD [ s a.w ] ALINAKILI MAFUNDISHO ya BIBLIA na halafu AKADAI kuwa YANATOKA kwa MWENYEZI MUNGU .

ILA MAKAFIRI HAO HAO WANADAI kuwa MTUME MUHAMMAD [ s.a.w ] #HAKUNAKILI kila kitu BALI ALICHAGUWA SEHEMU FULANI FULANI ALIZOZIONA NZURI .

USHAHIDI wa KIBUBUSA WANAOUTOA MAKAFIRI HAO ni kwamba ZIPO SEHEMU katika QUR'AN ambazo ZINAFANANA na zile ZILIZOMO katika BIBLIA.

Hivyo, MAKAFIRI hao VIBUBUSA #huthubutu KUSEMA , KWA kuwa ILITANGULIA BIBLIA kabla ya QUR'AN ni WAZI kuwa QUR'AN ndiyo ILIYOCHOTA KUTOKA katika BIBLIA.

.............................................................
MADAI haya ni DHAIFU kwa SABABU zifuatazo:

(i) MTUME MUHAMMAD [s.a.w ] alisema na KUSISITIZA kuwa QUR'AN IMETOKA kwa MWENYEZI MUNGU.

(ii) MTUME MUHAMMAD [ s.a.w ] HAKUJUA KUSOMA wala KUANDIKA .

(iii) NAKALA ya KWANZA ya AGANO la KALE [ Old Testament ] #KUFASIRIWA kwa #LUGHA_ya_KIARABU ILIPATIKANA mwaka 900 A.D , WAKATI huo ILIKUWA IMEKWISHAPITA MIAKA 200 TANGU MTUME MUHAMMAD [ s.a.w ] KUTAWAFU .

Ama,
AGANO JIPYA [ New Testament ] lilitolewa kwa MARA ya KWANZA MWAKA 1616, MIAKA ELFU [ 1000 ] BAADA ya MTUME MUHAMMAD [ s.a.w ] KUFARIKI DUNIA!

(iv) QUR'AN SURA 4:82 , imesema kuwa lau kama hii QUR'AN ingetoka kwa ASIYE kuwa MWENYEZI MUNGU ingekuwa na KHITILAFU nyingi.

Hivyo,
MTU mwenye SHAKA na AITUMIE FURSA hiyo KUTAFUTA KHITILAFU katika QUR'AN .

(v)Isitoshe , IKIWA kuna TUNGO MBILI au VITABU VIWILI VIMEFANANA, KUFANANA huko PEKE YAKE #si USHAHIDI wa KUTOSHA kuwa KITABU KIMOJA #KIMENAKILI kutoka KATIKA KITABU cha KWANZA KUANDIKWA .

Hii ni kwa SABABU yawezekana pia kuwa VITABU vyote VIWILI vikawa vimetegemea au KUNAKILI kutoka katika KITABU cha TATU ambacho sisi HATUKIJUI.

ILIVYO kuwa TORATI, INJILI na QUR'AN ni VITABU vya MWENYEZI MUNGU.

Hivyo ni WAZI kuwa kama BIBLIA #IMENUKUU AYA halisi za TORATI na INJILI lazima AYA hizo ZITAFANANA na AYA za QUR'AN ,kwa vile ZOTE ZINATOKANA na MWENYEZI MUNGU .

Isitoshe UTAFITI uliofanywa na BAADHI ya WANAZUONI umeonesha kuwa AMRI KUMI za MUNGU zilizomo katika AGANO la KALE kwa MFANO, ZIMEKUWEMO katika VITABU vya WAHINDU KABLA ya KUJA kwa AGANO hilo la KALE.

Je, TUSEME BIBLIA #ilinakili AMRI hizo kutoka kwa WAHINDU ?
SI LAZIMA iwe HIVYO.

PAMOJA na KUFANANA huko katika BAADHI ya SEHEMU bado KIMSINGI BIBLIA na QUR'AN #ZIMETOFAUTIANA KIASI kikubwa.

TOFAUTI ZA KIMSINGI KATI YA QUR -AN NA BIBLIA.

QUR-AN pia ilikuja #KUYABAINISHA yale YOTE yaliyokuwa YAKIFICHWA na MAYAHUDI HAO MIONGONI MWA MAAGIZO YA MWENYEZI MUNGU KWA MAYAHUDI HAO KATIKA kipindi cha MTUME MUHAMMAD [ S.A.W ]

1.BIBLIA #SI KITABU KIMOJA bali ni #MKUSANYIKO wa VITABU #73 kwa MUJIBU wa MADHEHEBU ya WAKATOLIKI au vitabu VITABU #66 kwa MUJIBU wa MADHEHEBU ya WAPROTESTANTI.

VITABU hivyo VYA BIBLIA VILIANDIKWA na WAANDISHI WASIOJULIKANA WASIOPUNGUA 40.

QUR'AN ni KITABU KIMOJA kilichotoka kwa MWENYEZI MUNGU na AYA zake ZOTE ziliandikwa MARA tu BAADA ya KUSHUKA.

2.BIBLIA ni KITABU chenye #MCHANGANYIKO wa MANENO ya MWENYEZI MUNGU, MITUME na #MAONI_ya_WANAHISTORIA.

QUR'AN ni NENO la MWENYEZI MUNGU tu PEKE YAKE .
Hata MANENO ya MTUME MUHAMMAD [ s.a.w ] #hayamo katika QUR'AN.

3.Katika AGANO la KALE na AGANO JIPYA yapo MAELEZO juu ya HISTORIA ya MAISHA ya MITUME.
KUMBUKUMBU la TORATI SIYO tu UJUMBE wa MWENYEZI MUNGU kwa WATU bali pia HISTORIA ya MAISHA ya NABII MUSA [a.s].

INJILI ya MATHAYO, LUKA , MARKO na YOHANA zinaelezea HISTORIA ya YESU kama ILIVYOSIMULIWA na WANAFUNZI wake.

QUR'AN inataja HABARI za MITUME waliopita ili kutoa MAFUNDISHO kwa WATU lakini #SIO kama SIRA [ BIOGRAPHY ] za MITUME hao.

4.BIBLIA inavyo VITABU KDHAA ambavyo VILIANDIKWA MIAKA MINGI SANA BAADA ya KUTAWAFU MITUME hao.
Ndio MAANA wanazuoni WAKIKRISTO HUPATA MATATIZO SANA katika UCHAMBUZI wa MAANDIKO hayo kwani HUSHINDWA KUMJUA NANI MWANDISHI na ALIANDIKA LINI.

Kwa MFANO katika BIBLIA iliyotolewa na COLLINS iitwayo:
REVISED STANDARD VERSION ya 1971;
KATIKA uk. 12 -17 IMEANDIKWA kuwa MWANDISHI wa 1 SAMWELI #HAJULIKANI ,

Pia HAJULIKANI MWANDISHI wa KITABU cha
2 #SAMWELI,
1 #WAFALME ,
1 #MAMBO_ya_NYAKATI ,
#ESTA ,
#AYUBU ,
#YONA na
#HABAKUKI.

Hali KADHALIKA MPAKA LEO HII kuna WASIWASI kama KITABU cha #WAEBRANIA KILIANDIKWA na #PAULO au na MTU MWENGINE.

Na ENCYCLOPAEDIA BRITANNICA #INAKIRI kuwa MPAKA hivi #HATUNA_UHAKIKA JINSI au #WAPI VITABU VINNE [ 4 ] vya INJILI #VILIZUKA.

KINYUME chake , QUR'AN YOTE ILIANDIKWA wakati wa UHAI wa MTUME MUHAMMAD [s.a.w] BAADA ya KUSHUSHWA na MALAIKA JIBRIL na IKAHIFADHIWA VIFUANI na MAMIA ya WATU.

5.INJILI NNE [ 4 ] zilizomo katika AGANO JIPYA siyo INJILI zote ZILIZOANDIKWA , Zilikuwapo INJILI nyingine NYINGI.

ILIFANYIKA SINODI [ MKUTANO wa WAWAKILISHI wa MAKANISA ] MWAKA 325 ili KUAMUA INJILI ZIPI ZICHUKULIWE na ZIPI ZIKATALIWE .

INJILI ya BARNABAS ILIKATALIWA.
Na katika HISTORIA ya KANISA viko VITABU VILIKUBALIWA na BAADAYE KUKATALIWA na KINYUME chake.

Ni BINAADAMU waliokuja BAADAYE NDIO waliokuwa na UWEZO wa KUAMUA LIPI liwe NENO la MUNGU na LIPI lisiwe NENO la MUNGU.

KATIKA UISLAMU HAKUKUWA na IJITIMAI YOYOTE iliyokaa KUAMUA SURA IPI iwe QUR'AN ama SURA IPI isiwe QUR'AN .

.................................................................
WAISLAMU WANAAMINI pasi na TONE la SHAKA kuwa QUR'AN ni KITABU cha MWENYEZI MUNGU NENO kwa NENO kama MWENYEWE MWENYEZI MUNGU anavyothibitisha:

"Hiki ni KITABU KISICHOKUWA na SHAKA ndani yake, ni UONGOZI kwa WAMCHAO MWENYEZI MUNGU ."
[ QUR'AN SURA 2:2 ]

PAMOJA na UTHIBITISHO huu, MAKAFIRI wa ZAMA za KALE na ZAMA za SASA WAMEIBUKA na UPINZANI wa KIBUBUSA dhidi ya QUR'AN na KUDAI kuwa KITABU hiki AMEKITUNGA MWENYEWE MTUME MUHAMMAD [s.a.w ]

"Au ndio WANASEMA kuwa hii QUR'AN AMEITUNGA (Muhammad) ?
Bali wao HAWAAMINI lolote."
[ QUR'AN SURA 52:33 ]

Basi walete hadithi [ QUR'AN ] kama hii ikiwa [ MAKAFIRI ] wanasema KWELI.
[ QUR'AN SURA 52:34 ]

UFAFANUZI :
BASI WALETE HADITHI kama HII :
Ndiyo MASHINDANO WANAYOPEWA MAKAFIRI ENZI na ENZI , na DAIMA WAMESHINDWA KULETA MFANO wa QUR'AN.

MAKAFIRI WANAAMBIWA na MWENYEZI MUNGU , kama MTUME MUHAMMAD [s.a.w ] AMEYATUNGA MWENYEWE MANENO haya YA QUR'AN , basi walete MANENO ya NAMNA hii TOKA kwa #M'GANGA wao au #MWEHU wao au #MTUNGAJI MWENGINE ikiwa MAKAFIRI hao #WANASEMA_KWELI.

DAI hili la kumpa MTUME MUHAMMAD [ s.a.w ] UTUNZI wa QUR'AN LIMEWAKILISHWA katika NAMNA mbali mbali na MAKAFIRI wa ZAMA mbali mbali.

...........................................................
JICHO LA CAMERA LA BIBILIA LINATUFAHAMISHA UTARATIBU WA ADHABU KAMA ALIYOTANGAZIWA MTUME MUHAMMAD [ s.a.w ] ENDAPO MANABII wa KWELI wa MWENYEZI MUNGU WANGELITHUBUTU KUWEKA MANENO YA UWONGO.

HIYO ndiyo #KANUNI_ILIYOELEZWA katika CHUO cha NABII MUSA.
[Kumbukumbu la Torati 18:20; 13:5 ]

#MWENYE_KUMZULIA_MUNGU_UWONGO_HUANGAMIZWA_na_UPANGA_na_NJAA,
[Jer. 14:15].

MVUA KALI ya HASIRA na #GHADHABU ya MWENYEZI MUNGU #HUMKOMESHA.
[Ezekiel 13:13].

HIYO ni DESTURI ya MWENYEZI MUNGU tangu AWALI mpaka SASA , IJULIKANAYO katika KILA NCHI na KILA KARNE , KUMUANGAMIZA MUONGO na KUMNUSURU MKWELI.

MTUME MUHAMMAD [s.a.w] angekuwa MTUNGA UWONGO , jinsi WADHANIVYO WATU WALALAMISHI na VIBUBUSA , ASINGEFAULU.

ADUI zake MTUME MUHAMMAD [s.a.w ] ndio WALIOTEKETEZWA na UPANGA na NJAA na ADHABU nyingine KALI.

KWA SABABU kwa KUMKADHIBISHA mwenye HAKI huyo WALIONEKANA kuwa WANAPIGANA na MUNGU.
[ MATENDO 5:34 -39 ].

HII NI SAFARI TUMETOKA KWA ALLAH NA TUNARUDI KWAKE
 
Mara Nyingi Wakristo Ukiwabana Kwa Hoja, Wanakimbilia Kusema👉Nyie Waislamu Ni Ndugu Wa MAJINI.. SASA Leo JICHO LA CAMERA 📸 La BIBLIA linatuonyesha kuwa Wakristo ndio Ndugu wa MASHETANI NA MAJINI ⬇️⬇️

Katika Historia Ya BIBLIA, Waandishi Wa BIBLIA Wanatueleza Kuwa, MAJINI Yalikuwa Yanamuita Yesu Ni Mwana Wa Mungu ⬇️

LUKA 4-41 Wale MAPEPO WACHAFU (MAJINI) Yakumuita Yesu Ni Mwana Wa Mungu, Yesu Akawakemea..

NAAM SWADAKTA, HAPA 👆Tunapata Somo Kuwa, MAJINI Ambao Ndio MAPEPO WACHAFU, Walikuwa Wanamtambua Yesu Ni Mwana Wa Mungu. Ila Yesu Akawakemea Akasema Yeye Ni Mwana Wa Adamu

Hapa Tuanapata funzo kumbe Wakristo wanaishi na MAPEPO MAKANISANI kwakuwa Wanamuita Yesu ni Mwana Wa Mungu.

WAKRISTO NI NDUGU WA MAJINI ⬇️

UFUNUO 2-12+13 KANISANI ni Katika Kiti CHA Enzi Cha SHETANI.

1TIMOTHEO 1-20 Nawapeleka Kwa Shetani Ili Awafundishe.

PAULO ANASEMA KATIKA WAKORINTHO WA PILI, YEYE ANAONGOZWA NA MAJINI KIFUANI.

SWALI 👉 JE WAKRISTO WANALO ANDIKO LOLOTE KUWA WAISLAMU NI NDUGU WA MAJINI ??

SOMA TAFSIRI YA QURAN ⬇️⬇️

Sura Al Mulk -5 ( Moto Wa Jahannam Kwa Ajili ya Mashetani )

Surah _Al-Baqarat_Ayah _208

يَٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ ٱدۡخُلُواْ فِي ٱلسِّلۡمِ كَآفَّةٗ وَلَا تَتَّبِعُواْ خُطُوَٰتِ ٱلشَّيۡطَٰنِۚ إِنَّهُۥ لَكُمۡ عَدُوّٞ مُّبِينٞ

Enyi mlio amini! Ingieni katika Uislamu kwa ukamilifu, wala msifuate nyayo za She'tani; hakika yeye kwenu ni adui aliye wazi.

NAAM, NI QURAN INATUAMBIA SISI WAISLAMU, MAJINI NA MASHETANI NI ADUI YETU.

ILA KATIKA BIBLIA, SHETANI MAKAO YAKE NI KITI CHA KANISA.

SHETANI NDIO ALIKUWA ANAMUITA YESU MWANA WA MUNGU

IVYO, Ukimuita Yesu ni Mwana Wa Mungu,Basi Wewe unae MAJINI.

Kwanza Unatakiwa Kujua Utofauti WA Jini Na Shetani.....👇

YOHANA 6-70 Je Sikuwachagueni Ninyi Thenashara? Na mmoja wenu ni Shetani ?

Katika Aya Hiyo Yesu anamuita Petro ni Shetani yaani ni Jini.

Mathayo 12-26 Na Shetani akimtoa Shetani, Amefitinika juu ya nafsi yake, basi ufalme wake utasimamaje?
 
FAHAMU FAIDA KUMI ZA KUSOMA
QUR'AN KILA SIKU
☆☆☆☆☆☆☆☆☆☆

Mtu Mwenye Kusoma Qur'an Kila Siku Ni Sawa Na Mtu Huyo Kuwa Ni Mwenye Nuru Kubwa Katika Maisha Yake

Ewe Ndugu Yangu Katika Imani Tambua Kwamba Mtu Mwenye Kukisoma Kitabu Cha ALLAH SUBHANA WA TA'ALA Na Akakizingatia Maneno Hayo Ipasavyo Hakika Mtu Huyo Hatopata Tabu Katika Ulimwengu

#FAIDA
1》Qur'an Ni Kinga Katika Majumba Yetu Na Viwiliwili Vyetu

2》Qur'an Ni Msaada Mkubwa Na Huondosha Huzuni Katika Matatizo

3》Qur'an Huleta Furaha Katika Nyoyo Za Wenye Kuisoma

4》Qur'an Ni Shufaa Kubwa Kwa Wenye Maradhi

5》Qur'an Huleta Rizki Za Mali Na Watoto

6》Qur'an Huleta UchaMungu Kwa Wenye Kuisoma

7》Qur'an Huleta Ulinzi Mkubwa Katika Mali

8》Qur'an Huongeza Ufahamu Mkubwa Wa Akili Hasa Kwa Watoto Wanao Soma Elimu Na Wakawa Hawana Ufahamu

9》Qur'an Ni Tiba Halisi Ya Hasidi Anapo Taka Kukuhusudu

10》Qur'an Huleta Ushindi Na Mafanikio Kwa Mwenye Kuisoma
☆☆☆☆☆☆☆☆☆

Tambua Mwenye Kuisoma Qur'an ALLAH SUBHANA WA TA'ALA Humpa Dhamana Mja Huyo Kwa Rizki Zake Zote Za Siku Nzima

#TIBA
Kama Una Matatizo Yako Binafsi Kwanza Hakikisha Swala Tano Unatimiza Kisha Hakikisha Kwa Siku Hukosi Juzuu Moja Hakikisha Una Hitimisha Msaafu

PENDELEA SANA KUSOMA
Sutatul Nass ×3

Suratul Falaq ×3

Suratul Ikhlas ×3

Kila Siku Hakika ALLAH SUBHANA WA TA'ALA Atakupa Nuru Kubwa Ya Maisha Yako Bila Kutegemea

Hii Ndio Sadaka Yangu Kwako Hakikisha Unampa Na Mwenzio Mkono Kwa Mkono Hadi Peponi...

NAMUOMBA ALLAH SUBHANA WA
TA'ALA ATUJALIE MAZINGATIO
TUNAPOISOMA QUR'AN
#Allahummah_Aamiin
Kwa Leo naishia hapa kwenye nakala hizi mpaka wakati ujao wako katika Imani KatetiMQ
 
HISTORIA YA QUR'AN.

Sehemu ya Pili (3).

Naam, Kama tulivyopata kuona mwanzo wa DARASA hili juu ya kuteremshwa kwa Qur'an, lakini pia Qur'an imeshushwa kwa lengo la kuwaongoza wanaadamu katika kila kipengele cha maisha ya kila siku ya kibinafsi na kijamii. Lengo la Qur-an linabainishwa katika aya ifuatayo:

👉“Ni mwezi wa Ramadhani ambamo imeshushwa Qur-an ili iwe mwongozo kwa watu na hoja zilizo wazi na upambanuzi (baina ya haki na batili) " (2:185)
Katika kuendea lengo lake hili, Qur-an humuongoza mwanaadamu kukiendea kila kipengele cha maisha yake ya kibinafsi na kijamii na hutoa hoja zenye mashiko dhidi ya wapinzani wake.

Katika kuonesha uwezo wake katika kumuongoza mwanaadamu katika kila kipengele cha maisha yake, Qur-an imeitwa (imesifiwa) kwa majina yafuatayo:

1. Al-Qur-an
Maana yake ni "Chenye kuunganishwa pamoja" au "chenye kusomwa. "Yaani Qur-an ni kitabu kilichofumwa na herufi, silabi, maneno, aya na sura, kinachosomwa mara kwa mara. Kitabu hiki kimeitwa kwa jina hili la "Al-Qur-an" kwa sababu ni mkusanyiko wa mafunzo ya msingi ya maisha ambayo mtu hanabudi kuyarejea mara kwa mara. Qur-an ndio Mwongozo sahihi pekee wa maisha ya mwanadamu hivi sasa.

2. Kalamullah:
Maneno ya Allah (s.w). Qur-an yote ni maneno ya Allah (s.w) yenye kutoa mwongozo kwa walimwengu wote kupitia kwa Mtume Muhammad (s.a.w) kwa njia ya Wahy kupitia kwa Malaika Jibril (a.s).

3. Al-Mus-haf:
Mkusanyiko wa kurasa. Hili ni jina mashuhuri lililotumiwa na maswahaba wa Mtume (s.a.w) baada ya Qur-an kukamilika kushuka na kuwekwa katika sura ya kitabu kikubwa.

4. Al-Kitaab:
Kitabu pekee (Unique book). Qur-an ni kitabu kikamilifu kisicho na upogo wala dosari yoyote wala hakina mfano wa kitabu chochote kimuundo, maudhui na uwasilishaji wa maudhui hayo. Qur-an yenyewe imeliweka hili wazi katika aya ifuatayo:

👉"Hiki ni kitabu pekee (Al-Kitaab) kisicho na shaka ndani yake na ni mwongozo kwa wamchao Mwenyezi Mungu." (2:2)

5. Al-Furqaan:
Kipambanuzi cha Haki na Batili au ukweli na uwongo. Yaani Qur-an ndio kipimo cha Haki na Batili au Zuri na Baya au Jema na Ovu, Tawhiid na Shiriki, Uislamu na Ukafiri

6. Adh-Dhikru:
Mawaidha au ukumbusho. Qur-an ni mawaidha yenye kumkumbusha kila mwenye kusoma na kuzingatia.

7. At-Tanziil:
Mshuko au wahy kutoka kwa aliye juu. Jina hili linasisitiza kuwa Qur-an ni kitabu cha Allah (s.w) kilichoshushwa kwa njia ya wahy kwa Mtume Muhammad(s.a.w) kupitia kwa malaika Jibril(a.s) ili awaongoze walimwengu kwacho.

8. Al-Hukmu:
Kitabu pekee kinachostahiki kumuhukumu mwanaadamu. Hukumu yoyote kinyume na Hukumu ya Qur-an ni upinzani na uasi dhidi ya Allah (s.w) na ni dhulma dhidi ya wanaadamu kama inavyosisitiza Qur-an yenyewe:

👉“…Na wasiohukumu kwa yale aliyoteremsha Mwenyezi Mungu, basi hao ndio makafiri." (5:44)

👉“….Na wasiohukumu kwa yale aliyoteremsha Mwenyezi Mungu, basi hao ndio madhalimu." (5:45)

👉“…. Na wasiohukumu kwa yale alioteremsha Mwenyezi Mungu, basi hao ndio waasi (mafasiki)." (5:47)
Neno “wasiohukumu” hapa limetumika kwa maana ya wanaoendesha maisha yao kinyume na yale aliyoteremsha Allah au wale wasioendesha maisha yao kwa mujibu wa Qur-an

9. Al-Hikma:
Kitabu pekee chenye Hikima isiyo kikomo. Ni kitabu cha Allah (s.w) ambaye ndiye chimbuko (source) la Elimu na Hekima. Hekima ni jambo la sawa sawa lililofanywa kwa namna ya sawa sawa katika mazingira na wakati wasa wasa ili kufukia lengo tarajiwa. Qur’an ni Hikma na humuuongoza binaadamu aishi maisha ya Hikma.

10. Ash-Shifau:
Ponyo au dawa pekee. Qur-an imeitwa kwa jina hili la "Ponyo pekee" kwa sababu Qur-an ndio dawa pekee ya kuponya maradhi ya "nafsi". Maradhi makubwa ya nafsi ni Ukafiri, Ushirikina, Unafiki na Uasi wa kila aina. Qur-an imejizatiti katika kuyaelezea magonjwa haya ili kila mtu mwenye akili timamu ayafahamu bayana na imeelekeza kwa ufasaha namna ya kuyatibu.

11. Ar-Rahmat:
Rehema kwa watu. Vipawa vinavyomfanya binaadamu atofautiane na wanyama ni akili na elimu. Vipawa hivi vikitumika bila ya kufuata mwongozo kutoka kwa Allah (s.w) humpelekea binaadamu kufanya uharibifu katika ardhi kuliko mnyama yoyote yule. Binaadamu akitumia akili yake na elimu aliyotunukiwa kwa kufuata mwongozo wa Qur-an huwa juu na bora kuliko viumbe vyote.

12. Al-Khayr:
Qur-an ni kheri pekee. Yaani Qur-an ndio chanzo cha kheri zote. Kheri hupatikana kwa kufuata Qur-an vilivyo.
13.Ar-Ruuhu:
Qur-an ni roho ya maisha. Yaani mtu asiyeishi kwa kufuata Qur-an ni kama maiti japo anaishi. Allah (s.w) anawaasa waumini wasiwakumbatie wapinzani wa Qur-an (makafiri) kwani wao ni kama maiti walio makaburini.

👉"Enyi mlioamini! Msifanye urafiki wa ndani na watu ambao Mwenyezi Mungu amewakasirikia na wamekata tamaa ya akhera kama walivyokwisha kata tamaa makafiri waliozikwa makaburini." (60:13)

14. Al-Bayaana:
Qur-an ni kitabu pekee chenye maelezo ya wazi na kinachofafanua aya zake kwa uwazi kwa kutumia mifano iliyozoeleka katika mazingira ya watu kwa nyakati zote za historia. Hivyo, kila mwenye akili timamu anao uwezo wa kuielewa Qur-an na ikamuongoza.

15. An-Nuur:
Qur-an ni nuru pekee. Qur-an ni mwanga unaomuonesha binaadamu njia sahihi ya maisha itakayomfikisha kwenye lengo la kuumbwa kwake. Kuishi bila ya kufuata Qur-an ni sawa na mtu anayetembea katika giza nene na matokeo ya kutembea kwenye giza nene yanafahamika kwa kila mwenye akili timamu. Qur-an inatukumbusha:

👉"Allah ni kiongozi wa walioamini. Huwatoa kwenye giza na kuwaingiza katika nuru (mwanga). Lakini waliokufuru viongozi wao ni Matwaghuti huwatoa katika nuru na kuwaingiza katika giza. Hao ndio watu wa motoni, humo watakaa milele." (2:257)

16. Al-Burhan:
Hoja pekee iliyowazi. Qur-an ni kitabu kinachotoa hoja zilizo wazi kwa wasomaji wake. Kwa mfano Qur-an inatoa hoja zilizo wazi, kuwa lazima pawe na Muumba mmoja wa ulimwengu na vyote vilivyomo mwenye ujuzi na Hekima. Pia Qur-an pamoja na kutoa hoja maridhawa juu ya kumuamini Allah (s.w) na nguzo nyinginezo za imani , huonesha lengo la kumuabudu Allah (s.w) na umuhimu na hekima ya kufuata Qur-an na Sunnah kama mwongozo pekee wa njia sahihi ya maisha ya binaadamu.

17. Al-Haqq:
Qur-an ni Haki. Qur-an ni haki kwa sababu ni maneno ya Allah (s.w) ambaye ni mjuzi wa kweli aliyeepukana na upungufu wa aina yeyote. Qur-an humuongoza binaadamu kwenye njia ya haki na huhukumu kwa waki.

18. Ahsan-ul-Hadith:
Maneno mazuri au maelezo mazuri kuliko yote kwa kuwa yanatoka kwa Allah (s.w), Mjuzi, mwenye hekima.
Kitabu hiki cha Allah (s.w), kilichosifiwa kwa majina haya, kina aya 6,236 zilizogawanywa katika sura 114 (Rejea jedwali 1). Pia kitabu cha Qur-an (Al-Mas-haf) kimegawanywa kwenye juzuu au mafungu (30) yaliyo sawa sawa.

Inaendelea InshaaAllah...

Allah Ni Mjuzi Zaidi.
nzuri
 
FAHAMU FAIDA KUMI ZA KUSOMA
QUR'AN KILA SIKU
☆☆☆☆☆☆☆☆☆☆

Mtu Mwenye Kusoma Qur'an Kila Siku Ni Sawa Na Mtu Huyo Kuwa Ni Mwenye Nuru Kubwa Katika Maisha Yake

Ewe Ndugu Yangu Katika Imani Tambua Kwamba Mtu Mwenye Kukisoma Kitabu Cha ALLAH SUBHANA WA TA'ALA Na Akakizingatia Maneno Hayo Ipasavyo Hakika Mtu Huyo Hatopata Tabu Katika Ulimwengu

#FAIDA
1》Qur'an Ni Kinga Katika Majumba Yetu Na Viwiliwili Vyetu

2》Qur'an Ni Msaada Mkubwa Na Huondosha Huzuni Katika Matatizo

3》Qur'an Huleta Furaha Katika Nyoyo Za Wenye Kuisoma

4》Qur'an Ni Shufaa Kubwa Kwa Wenye Maradhi

5》Qur'an Huleta Rizki Za Mali Na Watoto

6》Qur'an Huleta UchaMungu Kwa Wenye Kuisoma

7》Qur'an Huleta Ulinzi Mkubwa Katika Mali

8》Qur'an Huongeza Ufahamu Mkubwa Wa Akili Hasa Kwa Watoto Wanao Soma Elimu Na Wakawa Hawana Ufahamu

9》Qur'an Ni Tiba Halisi Ya Hasidi Anapo Taka Kukuhusudu

10》Qur'an Huleta Ushindi Na Mafanikio Kwa Mwenye Kuisoma
☆☆☆☆☆☆☆☆☆

Tambua Mwenye Kuisoma Qur'an ALLAH SUBHANA WA TA'ALA Humpa Dhamana Mja Huyo Kwa Rizki Zake Zote Za Siku Nzima

#TIBA
Kama Una Matatizo Yako Binafsi Kwanza Hakikisha Swala Tano Unatimiza Kisha Hakikisha Kwa Siku Hukosi Juzuu Moja Hakikisha Una Hitimisha Msaafu

PENDELEA SANA KUSOMA
Sutatul Nass ×3

Suratul Falaq ×3

Suratul Ikhlas ×3

Kila Siku Hakika ALLAH SUBHANA WA TA'ALA Atakupa Nuru Kubwa Ya Maisha Yako Bila Kutegemea

Hii Ndio Sadaka Yangu Kwako Hakikisha Unampa Na Mwenzio Mkono Kwa Mkono Hadi Peponi...

NAMUOMBA ALLAH SUBHANA WA
TA'ALA ATUJALIE MAZINGATIO
TUNAPOISOMA QUR'AN
#Allahummah_Aamiin
Kwa Leo naishia hapa kwenye nakala hizi mpaka wakati ujao wako katika Imani KatetiMQ
Allah akulipe kheri
 
Nimesema, uenda Mohammed alikuwa anajua kusoma au alikariri Bible. Ukisoma Quran utaona

Mfano hapa hii Aya ya Surah Al Mahidah 116, ukitafakari vizuri hii ni akili ya Mwanadamu ikitunga majungu

Na pale Mwenyezi Mungu atakapo sema: Ewe Isa bin Maryamu! Ati wewe uliwaambia watu: Nifanyeni mimi na mama yangu kuwa ni miungu badala ya Mwenyezi Mungu? (Na Isa) atasema: Subhanaka, Wewe umetakasika! Hainifalii mimi kusema ambayo si haki yangu. Ikiwa nilisema basi bila ya shaka umekwisha yajua. Wewe unayajua yaliyo ndani ya nafsi yangu, lakini mimi siyajui yaliyo katika nafsi yako. Hakika Wewe ndiye Mjuzi mkubwa wa yaliyo fichikana.​


Aya ipi kwenye biblia imeandikwa hivyo?? ambayo Mtume aliikariri ??
 
Back
Top Bottom