Historia ya Uhuru isimuliwavyo na Mohammed Said yakosolewa

Mfumo kristo kwa mujibu wa watu fulani fulani wanaojifanya hamnazo ni mfumo unaowapendelea wakristo kwenye nyanja za siasa na elimu. Kwenye kuchambua mfumo kristo mashabiki wake hufanya juhudi zote kuzuia kuvuka mipaka ya "waislamu" kuonewa kwenye siasa na elimu kwani kwa kufanya hivyo nadharia yenyewe ya mfumo kristo itakufa kifo cha mende.

Lakini kundi hili la wapotoshaji wanajifanya hawajui kwamba wakristo si kitu kimoja na wamegawanyika sana kifalsafa, kiitikadi, mapokeo na vitu vingine vingi tuu. Walutheri wanaona wakatoliki ni watu waliozuia injili kupokelwa kama ilivyokuwa toka kwa mitume. wakati huo huo Anglican ni dhehebu la Kiingereza kwa maslahi ya Malikia wa Uingereza na wao na Mashoga ni damudamu. Hayo madhehebu yaliyotangulia kutajwa na yale madhehebu ya kiroho mitizamo yao ni mbingu na Ardhi. Sasa huo mfumo kristo utafanyaje kazi!!

Kwenye kujadili jinsi Mwalimu alivyowafanyia "madhila" "waislamu" hairuhusiwi hata kidogo wakati wa kuonyesha "ubaya" wa Mwalimu kutaifisha shule za "waislamu", kusema pia shule za wakristo wakati Mwalimu anataifisha za "waislamu" zile za wakristo zilikuwa nyingi zaidi na zilikuwa zimetapakaa nchi nzima.

Hata leo wale wanaodai shule za Aga Khan Zilikuwa ni za "waislamu" hawana mahali wanaweza kutuonyesha hati za viwanja vya shule hizo kama zimeandikwa zinamilkiwa na "waislamu" badala yake wakristo wanazo hati za viwanja na kumbukumbu za jinsi walivyozijenga shule zao ambazo zilitaifishwa na Mwalimu.
 

Sweke34,

Mimi sihitaji "credibility" ya mtu yoyote.

Mbona mara nyingi tu nishasema hilo?

Siandiki ili wewe na wengine mfano wako mniamini.

Maandishi yangu yapo kwa kila mwenye akili yake anisome na atoe uamuzi wake ikiwa nisemayo na kweli au mimi ni uzushi.

Ila kama hujui. Miguu yangu imekanyaga nchi nyingi kwa mialiko ya minakasha kutokana na kalamu yangu.

Kote huko sijapata kuitwa mwongo ingawa huwa kuna mengu tu hatukubailiani na huo ndiyo usomi.

Mohamed
 

Umeandika mengi sana, unaonesha ni hodari sana wa kuchambuwa mambo unastahili kila sifa.

Bado hujaonesha ni wapi Mohamed Said hakuwa mkweli na ukweli badala yake hujatuonesha.

Kwa hayo nachukulia kuwa unakubaliana na Mohamed Said aliyoyaandika na hayana shaka. Na wewe kwa upande wako umeleta mtazamo wako wa kisomi. Hongera sana na Ahsante sana kwa kutufundisha mengi.

Tunakuomba na wewe pitia mada na upate darsa kutoka kwa Mohamed Said.
 

Tatizo Mwanakijiji government does not have the trust of Muslims anymore na even they set up a committee it will be just a wastage of our taxes. Sasa unafikiri kuna uwezekano wa kupatikana ukweli? Kwanini serikali isifanye uchunguzi yenyewe kujua kama kuna uongo au tatizo limetokea na je kuna haja kuomba radhi au la.
 

Hawa wazungu si ndiiyo walisema kwamba Iraq kuna silaha za maangamizi? Chanzo cha hiyo habari ni Nyerere, Rweyimamu au nani. Halafu hiyo ya Nyerere kuimarisha Ukatoliki Tanzania kweli kwa miaka 23 aliyokaa Ikulu alifanya jambo lipi la kuimarisha Ukatoliki. Aliimarisha ukatoliki kwa kutaifisha shule zao na Hospitali zao?
 
Pia inaconfirm jinsi Nyerere alivyohangaika kueneza TANU kote nchini Tanganyika. Na kinadhihirisha waanzishi wa TANU hawakuwa akina Sykes peke yao. Walikuwepo wengi. Lakini kwa sababu tumejaa udini tunachagua kuona tu yale tunayotaka kuona. Umeuliza jina la kitabu. Mohamed kishajibu ni "The Making of Tanganyika" by Judith Listowell.
 

Kwa kuhakikisha 83% vs 17% inadumu.
 
Mdondoaji,
Mbona solution rahisi sana? Kama serikali haina trust ya Muslims anymore vote those bastards out. Use your vote, your power to put in place a government you will trust. Serikali kamwe haiwezi kujichunguza. Inarespond kwa shinikizo. Wewe unadhani kweli Kikwete alitaka katiba mpya? Ni baada ya kuona nguvu mpya za CHADEMA.
 

Mohamed Said kisha jibu na ukisoma vizuri post yangu baada ya hiyo unayo i"quote" utaona nimemuambia mleta hilo bandiko ai"disregard" sentensi hiyo na ajibu mengine.

Kuhusu la waanzilishi wa TANU hakuna tatizo ingawa unaoongelewa hapo ni mkutano mmoja tu. Moahamed Said kaelezea kwa kina kwenye kitabu chake. Na hilo ndio nilikuwa nalisema toka mwanzo. Jee, Nyerere anaetajwa pekee kwenye kitabu cha Kigamboni alikuwa "One man Show"? Nikawa sipewi jibu mpaka Saint Ivuga alivyoleta hilo bandiko.

Imekuwa vyema kabisa kujuwa hata hilo jina ni kama alivyotuelezea Mohamed Said. Utata huo umekwisha, inabidi mumpe mji Mohamed Said, kwani hapo imehakikishwa na nyinyi wenyewe kuwa anachoandika ni ukweli.

Mohamed Said, mimi nilikupa Makkah huko nyuma, sasa nakupa Madinah, ukitoka Makkah kafanye ziara kidogo kwenye "Masjid Hadha", alipozikwa bwana Mtume Muhammad.
 
Hicho kitabu cha Kigamboni sijakiona wala kukisoma. Kwa hivyo siwezi kukisemea. Lakini itakuwa ajabu kwamba katajwa Nyerere peke yake maana itakuwa na maana alikuwa akifanya vikao peke yake, akihutubia viti na meza na kujibizana mwenyewe.
 
Hicho kitabu cha Kigamboni sijakiona wala kukisoma. Kwa hivyo siwezi kukisemea. Lakini itakuwa ajabu kwamba katajwa Nyerere peke yake maana itakuwa na maana alikuwa akifanya vikao peke yake, akihutubia viti na meza na kujibizana mwenyewe.

Tupo pamoja, na hilo swali au linafanana na hilo hata mimi nimeliuliza huko nyuma. Cha kushangaza ni pale Muingerea anapoaminiwa kuliko Mtanzania tena kutoka kwenye Ahli ya hao aliowataja Muingereza. Jee, ni kwa jina lake au Utaifa wake?
 
Jasusi,

Ngoja nikupe update ya kitabu cha Kivukoni kilipokuwa kinaandikwa "wataalam" wa historia ya TANU walimwambia nini Hassan Upeka (TANU Inteliigence toka anatoka Tabora School 1956 na kujiunga na TANU):

"Halihii ilijitokeza tena wakati CCM ilipokuwa ikitafiti historia yake. HassanUpeka,[1]mmoja katika wasaidizi wa utafiti ule alipeleka katika jopo lile la utafiti nauandishi wa historia ya TANU, mahojiano aliyofanya na Abdulwahid miaka mingiiliyopita kuhusu historia ya TANU. Hassan Upeka alifahamishwa kuwa historiainayoandikwa haimhusu Abdulwahid Sykes."

Mohamed
 
Halihii ilijitokeza tena wakati CCM ilipokuwa ikitafiti historia yake. HassanUpeka,[1]mmoja katika wasaidizi wa utafiti ule alipeleka katika jopo lile la utafiti nauandishi wa historia ya TANU, mahojiano aliyofanya na Abdulwahid miaka mingiiliyopita kuhusu historia ya TANU. Hassan Upeka alifahamishwa kuwa historiainayoandikwa haimhusu Abdulwahid Sykes.
 

Ngoja nikupe update ya kitabu cha Kivukoni kilipokuwa kinaandikwa "wataalam" wa historia ya TANU walimwambia nini Hassan Upeka (TANU Inteliigence toka anatoka Tabora School 1956 na kujiunga na TANU):

"Halihii ilijitokeza tena wakati CCM ilipokuwa ikitafiti historia yake. HassanUpeka,[1]mmoja katika wasaidizi wa utafiti ule alipeleka katika jopo lile la utafiti nauandishi wa historia ya TANU, mahojiano aliyofanya na Abdulwahid miaka mingiiliyopita kuhusu historia ya TANU. Hassan Upeka alifahamishwa kuwa historiainayoandikwa haimhusu Abdulwahid Sykes."

Mohamed

PS: Jasusi AA ilianzishwa na Kleist Sykes kisha akajenga na hiyo nyumba maarufu "TANU Ilianzishwa hapa 1954" hapo Lumumba Street, Dar es Salaam. Kadi ya Ally Sykes na 2 na 3 kaka yake Abdulwahid. Jasusi acha utani Ally Sykes anaweza kwenda kuwadai pango CCM. MS
 
Mohamed,
Hii ya AA kuanzishwa na Kleist Sykes sidhani kuna yeyote mwenye akili timamu atakayebisha. Hata uanzilishwaji wa TAA. Nyerere kasimulia jinsi alivyoanzisha Tanganyika African Welfare Society alipokuwa Makerere akaandikiwa barua na Mzee Mwangosi kuwa hakuna sababu ya kuanzisha chama kingine kwa sababu tayari kuna TAA. Nyerere akafuta TAWS akaanzisha tawi la TAA pale Makerere. Hiyo ndiyo historia ya wazee wetu. Nakumbuka nilipokuwa najiandaa kwenda Marekani masomoni Kleist alinipeleka ofisini kwa Ally Sykes akanipa dola tano za Kimarekani kama mchango wake kwa kisomo changu. Tumetoka mbali. Tudumishe mshikamano.
 

Jasusi,

Mshikamano ndiyo ule wazee wetu walivyompokea Nyerere Dar es Salaam hadi wakamfikisha walipomfikisha wamekufa wengine hawasemi naye, wengine kawatia kizuizini, Sheikh Hassan bin Amir akamfukuza nchini, Shariff Hussein Badawy na mdogo wake Mwinyibaba akawafukuza nchini vilevile, ikawa hataki kusikia chochote kuhusu Waislam wala Uislam.

Akavunja jumuia za Kiislam akawahujumu vijana wa Kiislam katika elimu akalijenga Kanisa Katoliki sasa ni serikali ndani ya serikali.

Haya ndiyo malipo yetu kwa hisani waliyomfanyia wazee wetu.

Mshikamano utarudi tu kama hii dhulma itatokomezwa na nyie ndugu zetu mna jukumu la kuitanabaisha serikali na Kanisa kuwa wasipuuze kilio cha Waislam.

Mohamed
 
 

Mzee Said..

1. umewahi kumwandikia Katibu Mkuu wa CCM kuhusu malalamiko kuwa Chama cha Mapinduzi hakijaandika historia yake kwa usahihi na kuonesha jinsi gani historia rasmi ya chama (siyo ya Tanzania) haijaandikwa usahihi?

2. Umewahi kuandikia baraza la Maaskofu Katoliki kutaka maelezo juu ya mambo fulani fulani ambayo yanatajwa katika kitabu cha Fr. Sivalon?

3. Je umewahi kuwaandikia BAKWATA kuwaelezea asili yao na kwanini wameugawa umma wa Waislamu? Yaani umejaribu kuwakutanisha watu wa BAKWATA na wa jumuiya nyingine ili kuunda jumuiya moja ya Waislamu wote nchini?
 
Nimesoma mwanzo mwisho na baada ya hapo naona ninawajibu wa kusema neno hapa.. NI hivi, shule hii hapa kuhusu Taifa letu sijawahi kuisoma pengine popote pale, kwanza ina hoja na majibizano murua na utetezi wa hoja, nashukuru sana.
Mimi nimezaliwa miaka 17 baada ya uhuru na nadhan kuna vijana wengine wengi tu wanayasoma haya hapa na kupata funzo la historia cha ajabu ninachokiona hapa ni mjadala kuegemea zaidi ktk udini na kuuacha uhalisia nasema hivyo kwa sababu hizi:
1. Wachangiaji waislam (baadhi) ktk maada hii wanaegemea zaidi ktk kumuunga mkono muislam mwenzao Bw. Said nao wakiacha kuelezea ukweli wanaoujua, pengine hawajui na wanajifunza ila wanaegemea kwenye udin nao, hili sio jema na dhambi kubwa tunalifanyia taifa hili na vijana waliozaliwa badae kama mimi na ambao hawajapata nafasi ya kuifaham historia.
2. Wachangiaji wakristo (baadhi) wameegemea zaidi ktk kuwatetea washiriki wa harakati za uhuru wakristo kama nyerere na wengine na kuiacha historia ikielea pengine ni kutojua na kupotosha au kuona haya kuwataja waislam, hii ni dhambi kubwa kwa taifa letu na hatuwatendei haki vijana na watu wengine ambao hawakupata nafasi ya kuijua historia.
3. Historia inayoelezewa hapa ni nusu nusu maana Bw. Said ameegemea ktk kuelezea historia ya uhuru ktk waislam akiliacha historia ya taifa hili, tunaposema historia ya taifa tunamaanisha taifa zima pengine Bw. Said angeeleka zaidi kama angeipa kichwa cha habari kuwa ni HARAKATI ZA WAISLAMU KTK HISTORIA YA TANGANYIKA nadhan hapo angeeleweka kirahisi.
4. Wale wanompinga pia ingefaa wapinge kwa kutambua watu anaosema walishiriki harakati kama ni kweli walishiriki (km baadhi ya mifano iliyoko ktk mjadala huu) kuliko kukataa tu kila kitu, hapo mnatupoteza ambao hatujui kitu.
5. Nashauri mtu yeyote anaetaka kuelezea historia ya taifa hili aelezee kwa ujumla sio ktk upande ambao yeye anajisikia, kwa kufanya hivyo itamsaidia kila anaepita kusoma mjadala huu kuelewa vinginevyo tunawapotosha watu.
5. Bw. Said usikimbie mjadala kwa kutukanwa, wakati mwingine inakulazimisha kuwa jasiri na kuwakabili wenye maneno makali na matusi ili nao kuweza kuwapatia elimu pengine hawajui na hawajui kuwa hawajui, rudi darasani uelimishe watu ila si kwa kuegemea upande mmoja vinginevyo kweli kama huna historia ya ujumla wa taifa hili basi ni busara ukae kimya.
6. Alichosema Bw. BARUBARU kuwa kila mwenye historia aiandike kwa mtazamo wake na kile anachokijua mimi nasema HAPANA, ni lazima kuwe na historia moja na ya kueleweka najua historia ya taifa hili haijasimuliwa kiasi cha kutoka sasa tunaomba wenye kuijua historia hi wajitokeze kwa pamoja na kuiweka sawa.
7. Naamini kuna watu wazee wetu ambao walishiriki harakati za uhuru, wapo hai baadhi. ni busara sasa wakajitokeza na kuelezea historia hiyo kwa mapana na marefu yake ili nasi vijana tuweze kuifahamu.

Naendelea kujifunza hapa...
 
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…