Historia ya Uhuru isimuliwavyo na Mohammed Said yakosolewa

Historia ya Uhuru isimuliwavyo na Mohammed Said yakosolewa

Vito...
Umesema kweli nimeandika historia ya wazee wangu hili nitalikataaje wakati mimi mwenyewe katika kitabu rejea yangu kuu ya vuguvugu ya kuasisiwa kwa African Association ni mswada wa kitabu wa Kleist Sykes?

Sikuishia hapo na nikaweka pia rejea mbili DA Sykes Buruku (1968) na John Iliffe (1973) kama ushahidi na rejea zote nikaeleza zinapatikana Chuo Kikuu Cha Dar-es-Salaam.

Hivi karibuni ikaongezeka rejea nyingine Dictionary of African Biography (DAB) hii unaweza ukaipata Library of Congress, Washington DC.

Rejea hizi zote utasoma historia ya Kleist Sykes na watoto zake Abdulwahid, Ally na Abbas kama watu muhimu katika historia ya TAA, TANU na harakati za kupigania uhuru wa Tanganyika.

Hawa wote waliishi Mtaa wa Kipata, Gerezani Dar es Salaam.
Lakini sijalazimisha kuwa hii iwe historia ya taifa.

Historia ya taifa ipo na inaanza na Julius Nyerere 1954.
Historia niliyoandika mimi inaanza nyuma sana mwanzo kabisa wa karne ya 20.

Ni wazi kuwa hizi ni historia mbili tofauti kwa maudhui na nyakati.

Nahitimisha kwa kusema kuwa babu yangu Salum Abdallah alikuwapo toka African Association inaundwa na akashiriki katika kupigania haki za Waafrika akiwa TAA, TANU na akiwa ndani ya Tanganyika Railways African Union (TRAU) chama cha wafanyakazi wa reli.

Historia yake naijua na nimeiandika hapa JF sehemu nyingi.

Ikiwa mtu ataona historia ya wazee wangu haina uhusiano na ukombozi wa Tanganyika hii ni bahati mbaya kwangu.
mimi nimesoma sana historia hii.nashangaa wanakuja watu wanasema historia hii uongo oooh wazee wake!! sasa historia hii kama kweli unaiona sio ya kweli leta zenu na facts tusome tuone nan kasema sio sahihi!! naona kinachouma watu hapa kinajulikana hutuwez kujidanganya nafsi zinajua shida ipo wap hapa wote tunajua."yaliyo nyoyon ni mabaya kushinda wadhihirishayo"
kama historia na facts za Mohamed said unayepinga unaona sio leta facts zako .hivi ni vitu vya kielimu.ukipinga sema wewe sasa ipi ya kweli sio kukaa tu analeta historia ya wazee wake ooh nin ukiulizwa leten bas zenu tuone mnagwaya gwaya.
 
Mr. Mohamed Said kwanza tunashangazwa sana na maneno unayotumia mara kwa mara kwamba:
• Hatufurahiswi
• Tunaumia
• Nyoyo zinatuuma
• Hatupendi kusikia historia ya uislam n.k
Nikuambie tu baadhi ya wachangiaji wanaotoa maoni tofauti na unayoandika hawaamini katika imani hizi kubwa mbili hilo ulielewe vizuri, mtu akipinga mawazo yako haina maana kuwa anapinga imani yako na wala imani yako haimshughulishi kabisa what they need is clarity.

Pia unasema umekuja na historia ambayo tulikuwa hatuijui kabla, ni sawa lakini hilo nalo halituzuii hata kidogo kupima na kuangalia ukweli na uhalisia wa historia yenyewe. Kwa sababu hatukuijua kabla haitupi ithibati kuamini kuwa historia hiyo ina ukweli na uhalisia kwa 100%.

Shida nyingine ya wengi ni wewe kutaka kuuaminisha umma kuwa 'wazee wako' wametoa mchango mkubwa katika kudai uhuru wa nchi hii kisa tu walimpokea Mwalimu Julius Nyerere hivyo ni kama hawapewi coverage ya kutosha kwenye vitabu vya historia.

Lakini kuna mchangiaji mmoja alisema hata hao 'wazee wako' wasingempokea Mwalimu Nyerere au kumpa ushirikiano, uhuru wa nchi hii ungeapatika pasi na shida sababu Nyerere angepata back up kubwa zaidi sehemu nyingine zaidi ya ile ya 'wazee wa gerezani' naamini hili unalitambua la kama hukubaliani nalo unapaswa kufunga huu mjadala.

Pia Mohamed Said unasema na ni mara nyingi unasema watu kama Ally Sykes na Abdul Sykes kuwa wamefutwa kwenye historia hili nalo linatupa shida sana why unataka 'watu wako' wapate special privilege kuliko watu wa sehemu nyingine?

Siku zote historia ina tabia ya kujiimba yenyewe pasipo kuimbiwa. Leo hii katika nchi yetu kuna watu wengi na machifu wengi ambao kwa mchango wao mkubwa sana kwenye hili taifa hadi leo historia inawaimba pasipo kutumika nguvu kubwa kama unayotumia kuwaimba 'wazee wako'

Nakushauri acha kauli ya 'Siwezi kumlazimisha mtu kuamini ninachoandika'

Siku zote tumefunzwa kizuri kin"ajiuza..
Hakuna mahali katumia neno "Uislam", hilo sasa lako wewe unatulisha "tango pori". Rudia kusoma uje na neno sahihi alilotumia Mohamed Said.

Nini kilichoumiza mpaka unabadili maneno?
 
mimi nimesoma sana historia hii.nashangaa wanakuja watu wanasema historia hii uongo oooh wazee wake!! sasa historia hii kama kweli unaiona sio ya kweli leta zenu na facts tusome tuone nan kasema sio sahihi!! naona kinachouma watu hapa kinajulikana hutuwez kujidanganya nafsi zinajua shida ipo wap hapa wote tunajua."yaliyo nyoyon ni mabaya kushinda wadhihirishayo"
kama historia na facts za Mohamed said unayepinga unaona sio leta facts zako .hivi ni vitu vya kielimu.ukipinga sema wewe sasa ipi ya kweli sio kukaa tu analeta historia ya wazee wake ooh nin ukiulizwa leten bas zenu tuone mnagwaya gwaya.
Julai...
Hawawezi kuwa na hstoria nyingne ya African Association.
Hstoria hii ni moja na inatoka mbali sana na hawa wazee waasisi walioko leo ni vitukuu.

Angalia pcha hiyo hapo chini ni mimi na Kleist Abdul Sykes.
Babu zetu wakati wanaasisi African Association 1929 walikuwa na umri wa miaka ya katikati 25.

Mimi na Kleist mwenzangu ametangulia mbele ya haki hapo tunapiga hii picha ya kwanza sote tayari tulikuwa na wajukuu.

Picha ya pili wa kwanza kulia ni mimi na Kleist ni watatu.

Huu ulikuwa mwaka wa 1968 miezi michache baada ya baba yake Kleist, Abdul Sykes kufariki.

Watoto wetu sisi wameijua historia hii kwa kutusikia sisi baba zao tunaihadithia kutoka kwa baba na babu zetu.

Hawa hawawezi kuwa na kumbukumbu hizi.
Wazitoe wapi?

1654188567130.jpeg

1654188621042.jpeg
 
Hakuna mahali katumia neno "Uislam", hilo sasa lako wewe unatulisha "tango pori". Rudia kusoma uje na neno sahihi alilotumia Mohamed Said.

Nini kilichoumiza mpaka unabadili maneno?
Rudia kusoma kwa makini andiko langu la hujalielewa fuatilia tena kwa makini mjadala toka mwazo.

Ahsante.
 
Rudia kusoma kwa makini andiko langu la hujalielewa fuatilia tena kwa makini mjadala toka mwazo.

Ahsante.
Kaangalie wewe uoneshe wapi Mohamed Said kaandika "Uislam"?
Kwanini ubadilishe maneno, ni walewale tu msopenda kusikia au kusoma neno Waislam.

Wewe tuelezee hapa, wazee wako wana historia ipi kudai uhuru wa Tanganyika? Mohamed Said ndiyo kishaandika historia ya wazee wake, sasa wewe weka ya wa kwako, wacha porojo.
 
Kaangalie wewe uoneshe wapi Mohamed Said kaandika "Uislam"?
Kwanini ubadilishe maneno, ni walewale tu msopenda kusikia au kusoma neno Waislam.

Wewe tuelezee hapa, wazee wako wana histori ipi kudai uhuru wa Tanganyika? Mohamed Said ndioyo kishaandika historia ya wazee wake, sasa wewe weka ya wa kwako, wacha porojo.
Maalim Faiza,
Hawakuwako na ndiyo sababu wakaamua kuifuta historia ya wazee wetu.
Sisi tuna kila aina ya ushahidi kuanzia nyaraka hadi picha.

Wala sisi hatawalaumu wao kwa nini hawakuwako.
Tusingeweza sote kufanya jambo lile.

Huyo hapo chini Ali Msham na Mwalimu Nyerere.
Alitoa nyumba yake kuwa ofisi ya TANU kupigania uhuru wa Tanganyika.

Hakupata kujulikana Ali Msham hadi nilipoandika historia yake.

1654205688710.jpeg
 
Kaangalie wewe uoneshe wapi Mohamed Said kaandika "Uislam"?
Kwanini ubadilishe maneno, ni walewale tu msopenda kusikia au kusoma neno Waislam.

Wewe tuelezee hapa, wazee wako wana historia ipi kudai uhuru wa Tanganyika? Mohamed Said ndiyo kishaandika historia ya wazee wake, sasa wewe weka ya wa kwako, wacha porojo.
Dada Foxy naona kama imekupa shida kidogo no need to panic. Tukisema hoja za unayemtetea zina shaka mnalipuka nashangazwa na wewe kuuliza swali kama hilo.

Si mara moja wala mara mbili anatumia neno hilo katika kujibu hoja mbali mbali za wanabodi
20220603_093126.jpg


Kuna kingine labda?
 
Kuna watu kama marehemu Lupembe na Rupia hawa walikuwa wafanyabiashara wakubwa kabla ya Uhuru na walichangia kiasi kikubwa safari ya Nyerere kwenda UN lakini huwa sisikii wakitajwa
 
Kuna watu kama marehemu Lupembe na Rupia hawa walikuwa wafanyabiashara wakubwa kabla ya Uhuru na walichangia kiasi kikubwa safari ya Nyerere kwenda UN lakini huwa sisikii wakitajwa
Rod...
Kitabu cha Historia ya TANU kimeshaandikwa na Chuo Cha CCM Kivukoni na Abdul Sykes hakutajwa.

Haishangazi kuwa Rupia, Lupembe na wazalendo wengine hawamo.
 
Nilipo RED.

Hakika siku zote lazima ujue unaandika katika mazingira gani hususan unapofuata tartibu na kanuun za uandishi.

lazima uelewe pamoja na uliobainisha lakini msingi mkuu wa uandishi unabaki pale pale ni kuelimishana, kupashana habari na kuburudisha jamii.

Siku zote mwandishi anapaswa kuandika kile tu alichokiona pasi na kuegemea upande wowote au kutoa suluhisho la tukio zima kwani kazi hiyo ya kuamua inabaki kwa wasomaji.

Lakini vile vile unatakiwa ujue kuna habari za aina tofauti tofauti. Anachoandika Bw Moh'd katika makala yake ni kuandika historia ya Tanzania. Na amejikita zaidi na kutafiti na kutoa kile anachoamini kuwa ni sahihi kuwajuza historia watanganyika ambao hawakuwepo wakti huo.

Na lazima ufahamu pia kuwa Historia haiwezi fichika na hakuna mwenye uwezo wa kuifuta au kuificha historia kwani hayo ni mambo yaliyofanyika katika jamii. Yawe mabaya au mazuri ni vyema yawekwe hadharani. (Historia ni kama pembe la ng'ombe). Na wajuzi wa mambo ndio maana wanaunda tume za maridhiano ili kuondoa pale penye kasoro na kuhakikisha mambo yanakuwa sawia siku hadi siku.

Usione wajinga South Africa kuunda tume ya maridhiano au Rwanda na mauaji ya kimbari. Hiyo yote ni kuisafisha historia kwani itajiandika kutetea kile kilichokuwepo.
Nawashauri wa Tanganyika ni vizuri kuipokea na kuipinga pale ilipoteleza na kuyafanyia kazi yale ya kweli kwa mustakabali wa nchi yenu. Kwani kuna mengi lakini kubwa kutokana na maandiko yake naona mengi yamejitokeza likiwamo la UDINI ndani ya jamii za wa Tanganyika.

Eleweni kuwa mficha maradhwi siku zote kifo kinamuumbua.

Kila la kheir
Barubaru,
Miaka mingi imepita na mjadala huu haujapata kutokea.

Waliingia watu wengi kuja kunijibu.

Uwanja ulijaa.
Tulifanya mjadala kwa miezi sita mfululizo watu wanokaribia 1m walishiriki.

Hivi sasa uwanja ni mtupu watu wanokuja kukabiliana na mimi ni wachache sana.

Nimebakia peke yangu uwanjani.

Walidhani mimi nafanya maskhara nilipowaambia kuwa historia ya Waislam katika kuuunda AA, TAA, TANU na kupigania uhuru wa Tanganyika ni ya kipekee.

Wengi hawakuniamini lakini jinsi mjadala ulivyokuwa unaendelea na mimi kuwa nakuja na vitu vipya kila ninaponyanyua kalamu akili zao za ndani zikawa sasa zinauliza iweje hapa tunaona picha na maelezo yanoyofanana na picha na kubwa hii historia haikuwa inafahamika?

Leo ukweli umedhihiri kuwa historia iliyokuwa inachukuliwa kuwa ndiyo historia ya TANU na uhuru wa Tanganyika siyo.

Hii ndiyo sababu ya kuandikwa kitabu cha Julius Nyerere, ''Nyerere Biography'' na jopo la waandishi wasomi kutoka Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam wakiongozwa na Prof. Issa Shivji.

Penye ukweli uongo hujitenga.

Mtu akikuonyesha fimbo yake iliyopindika akasema fimbo hiyo imenyooka jibu lake si kupigizana makelele kwa kubishana.

Jibu ni wewe kumwonyesha fimbo yako iliyonyooka.
 
Back
Top Bottom