Historia ya Uhuru isimuliwavyo na Mohammed Said yakosolewa

Historia ya Uhuru isimuliwavyo na Mohammed Said yakosolewa

Huyu Mohamed Said analo tatizo kubwa, Tuliosoma zamani wakati wa mkoloni tulisoma kitabu cha zamani cha historia kilichoitwa Watanganyika.

Ndani ya hicho kitabu makabila yote yaliyojulikana kama Watanganyika wazawa yaliorodheshwa,

Tanganyika haikuwa na Wazulu, Wamanyema, Wanubi wala wengi wa hao wanaodaiwa na mohamed Saidi kwamba eti ndio walipigania uhuru wa Tanganyika.

Shame on you Mohamed Said, uongo wako hakika umebuma na umebakia kutapatapa tu kama mfa maji. Kwa lugha ya FaizaFoxy, nasema unanchekesha.
Mimi nakuhisi wewe ndiye unaetapatapa. Hukuipenda historia iliyoandikwa na Mohamed Said?

Sasa wewe huoni kuwa walioandika hicho kitabu ulichokitaja walikuwa wanakgawa ili wakutawale bila kujijuwa. Hata hii mipaka uionayo leo huelewi kuwa ni kukugawa tu? Ukianza kutazama makabila basi ukienda nyuma zaidi kwenye historia hata Mbantu ardhi hii kuna wakati alikuwa mgeni pia. Mmasai ukisoma historia ni mhamiaji tu ardhi hii.

Wewe ni kabila gani katika hayo makabila ili nawe tukupe historia yako. Au wewe ni mwiko kwako kutaja asili yako?

Kwa jinsi unavyoandika ni wazi hata wewe ni wakuja tu. Tena wewe inaonesha ni wakuja na mwenge tu.

Kila binaadam ana historia ya kuwepo kwake hapo alipo. Wewe je?
 
Nipo safarini nikajikuta nimezama kwenye huu mjadala mpaka safari naiona fupi, hii elimu hapa ni ziadi ya elimu yenyewe, ila huyu mzee Saidi inaonekana muongo balaa.
 
Nipo safarini nikajikuta nimezama kwenye huu mjadala mpaka safari naiona fupi, hii elimu hapa ni ziadi ya elimu yenyewe, ila huyu mzee Saidi inaonekana muongo balaa.
Roy...
Katika hayo uliyosoma kipi unachoona kuwa ni uongo balaa?
 
Naipo safarini nikajikuta nimezama kwenye huu mjadala mpaka safari naiona fupi, hii elimu hapa ni ziadi ya elimu yenyewe, ila huyu mzee Saidi inaonekana muongo balaa.
Mohamed Said ameandika historia ya ndugu zake wa kariakoo na magomeni...halafu analazimisha iwe historia ya taifa.
 
Mohamed Said ameandika historia ya ndugu zake wa kariakoo na magomeni...halafu analazimisha iwe historia ya taifa.
Vito...
Umesema kweli nimeandika historia ya wazee wangu hili nitalikataaje wakati mimi mwenyewe katika kitabu rejea yangu kuu ya vuguvugu ya kuasisiwa kwa African Association ni mswada wa kitabu wa Kleist Sykes?

Sikuishia hapo na nikaweka pia rejea mbili DA Sykes Buruku (1968) na John Iliffe (1973) kama ushahidi na rejea zote nikaeleza zinapatikana Chuo Kikuu Cha Dar-es-Salaam.

Hivi karibuni ikaongezeka rejea nyingine Dictionary of African Biography (DAB) hii unaweza ukaipata Library of Congress, Washington DC.

Rejea hizi zote utasoma historia ya Kleist Sykes na watoto zake Abdulwahid, Ally na Abbas kama watu muhimu katika historia ya TAA, TANU na harakati za kupigania uhuru wa Tanganyika.

Hawa wote waliishi Mtaa wa Kipata, Gerezani Dar es Salaam.
Lakini sijalazimisha kuwa hii iwe historia ya taifa.

Historia ya taifa ipo na inaanza na Julius Nyerere 1954.
Historia niliyoandika mimi inaanza nyuma sana mwanzo kabisa wa karne ya 20.

Ni wazi kuwa hizi ni historia mbili tofauti kwa maudhui na nyakati.

Nahitimisha kwa kusema kuwa babu yangu Salum Abdallah alikuwapo toka African Association inaundwa na akashiriki katika kupigania haki za Waafrika akiwa TAA, TANU na akiwa ndani ya Tanganyika Railways African Union (TRAU) chama cha wafanyakazi wa reli.

Historia yake naijua na nimeiandika hapa JF sehemu nyingi.

Ikiwa mtu ataona historia ya wazee wangu haina uhusiano na ukombozi wa Tanganyika hii ni bahati mbaya kwangu.
 
Kumbe mzee alichezea za Uso huku, alitandikwa na vitu vizito akawa kama piritoni
Masta...
Si kweli kuwa walinishinda.

Hawawezi kunishinda katika kuihadithia historia ya wazee wangu na kizazi hiki nilichozaliwa mimi.

Kitabu nilichoandika kimefanyiwa book review tatu na mabingwa wa African History (John Iliffe, James Brennan na Jonatho Glassman) na zote zimechapwa kwa nyakati tofauti katika Cambridge Journal of African History.

Mambo hayakuishia hapo.

Nikaalikwa Northwestern University Evanston, Chicago kuzungumza katika Ukumbi wa Eduardo Mondlane.

Ikiwa unawajua hao wanahistoria, ukiwa unawajua Cambridge na ukiwa unawajua Northwestern bila wasiwasi wowote utaelewa ninachokueleza.

Mimi si piritoni.
Piritoni huenda ikawa wewe mwandishi na wao.

Na waliochezea za uso si Mohamed Said Salum Abdallah.
 
Masta...
Si kweli kuwa walinishinda.

Hawawezi kunishinda katika kuihadithia historia ya wazee wangu na kizazi hiki nilichozaliwa mimi.
Ni kweli historia ya Wazee wako unaifahamu vizuri, lakini katika historia ya Harakati za Uhuru wa Tanganyika wazee wako unawavika vyeo wasivyokua navyo.
 
Vito...
Umesema kweli nimeandika historia ya wazee wangu hili nitalikataaje wakati mimi mwenyewe katika kitabu rejea yangu kuu ya vuguvugu ya kuasisiwa kwa African Association ni mswada wa kitabu wa Kleist Sykes?

Sikuishia hapo na nikaweka pia rejea mbili DA Sykes Buruku (1968) na John Iliffe (1973) kama ushahidi na rejea zote nikaeleza zinapatikana Chuo Kikuu Cha Dar-es-Salaam.

Hivi karibuni ikaongezeka rejea nyingine Dictionary of African Biography (DAB) hii unaweza ukaipata Library of Congress, Washington DC.

Rejea hizi zote utasoma historia ya Kleist Sykes na watoto zake Abdulwahid, Ally na Abbas kama watu muhimu katika historia ya TAA, TANU na harakati za kupigania uhuru wa Tanganyika.

Hawa wote waliishi Mtaa wa Kipata, Gerezani Dar es Salaam.

Lakini sijalazimisha kuwa hii iwe historia ya taifa.

Historia ya taifa ipo na inaanza na Julius Nyerere 1954.

Historia niliyoandika mimi inaanza nyuma sana mwanzo kabisa wa karne ya 20.

Ni wazi kuwa hizi ni historia mbili tofauti kwa maudhui na nyakati.

Nahitimisha kwa kusema kuwa babu yangu Salum Abdallah alikuwapo toka African Association inaundwa na akashiriki katika kupigania haki za Waafrika akiwa TAA, TANU na akiwa ndani ya Tanganyika Railways African Union (TRAU) chama cha wafanyakazi wa reli.

Historia yake naijua na nimeiandika hapa JF sehemu nyingi.

Ikiwa mtu ataona historia ya wazee wangu haina uhusiano na ukombozi wa Tanganyika hii ni bahati mbaya kwangu.
Hii historia unayoielezea ni sehemu ndogo sana ya historia ya TANU na TAA ... Historia yako imejikita Dar Es Salaam tu... Wakati harakati za kudai uhuru zilisambaa Tanganyika yote.
 
Hii historia unayoielezea ni sehemu ndogo sana ya historia ya TANU na TAA ... Historia yako imejikita Dar Es Salaam tu... Wakati harakati za kudai uhuru zilisambaa Tanganyika yote.
Vito...
Hapana nilifika kwingi katika utafiti wangu.
Angalia hapo chini:

Part One​

Abdulwahid Sykes 1924-1968​

Chapter 1. The Sykes: Origins 1894-1929
The Old Town of Dar es Salaam and its Elites
Kleist Sykes, Pioneer and Man of Ideas: 1894-1949
World War One 1914-1918
The Founding of the African Association and Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika (Muslim Association of Tanganyika), 1929-1933

Chapter 2.The Second World War and Tanganyika’s Political Foundation, 1938-1945

The Burma Infantry, 1942
Chapter 3. Dar es SalaamDockworkers Movement 1947-1950
Dar es Salaam Port, 1947
Erika Fiah
The Dockworkers’ Union, 1948

Chapter 4. The Genesis of Open Politics in Tanganyika 1950 -1954
The Tanganyika African Association, 1950
TAA Political Subcommittee, 1951
Tanganyika as a Mandate Territory
Kenyan Nationalists in the Struggle of Tanganyika,1950
TAA and KAU: Attempts at Linkage and Solidarity, 1950
The Meru Land Evictions, 1950
Chapter 5. Julius Kambarage Nyerere
The Story of Julius Nyerere, 1952
Tanganyika African National Union (TANU)-The Party of Independence, 1954
Chapter 6. The Pan African Congress of Northern Rhodesia, 1953
Ally Kleist Sykes

Part Two​

Mass Mobilisation and Independence 1954-1961​

Chapter 7. Mass Mobilisation 1954
The Elders’ Council and Nyerere’s Visit to the United Nations, New York, 1954
Idd Faiz Mafongo
The African Press-Ramadhani Mashado Plantan, 1950
Ahmed Rashad Ali-Radio Free Africa (Radio ya Afrika Huru), 1952
Propagandists-The Bantu Group,1955
Incorporation of Swahili Women’s Societies into the Struggle, 1955
Football As a Political Weapon
Chapter 8. The Formation of the Party in the Provinces
Central Province, 1955
Southern Province, 1955
Western Province, 1955
Tanga Province, 1956
TANU in Mombasa, Kenya, 1957
Chapter 9. The Tabora Conference-The Road to Independence, 1958
The Tanga Strategy, 1958
The Debate for Tripartite Voting
Pan-African Movement of East and Central Africa (PAFMECA), 1958
Independence, 1961

Part Three​

Conspiracy Against Islam 1961-1970​

Chapter 10. The Muslim Factor in Post-Independence Tanzania 1961-1970
Islam: The Ideology of Colonial Resistance
The First Muslim Congress, 1962
Resistance to Change
The Second Muslim Congress, 1963
Proposal for an Islamic University, 1964
The Politics of Islam, Church, State and the African Christian
Chapter 11. The East African Muslim Welfare Society (EAMWS) ‘Crisis’
Fomentation of the BAKWATA ‘Crisis’
Nyerere, Tewa, Bibi Titi Encounter, 1968
The Islamic National Conference, 1968
Omissions Analysed
Betrayal of Ideals
Conspiracy Theory
Epilogue
Bibliography
 
Nimegundua huyu mzee wetu kuna watu inawachoma moyo kwa Yale aandikayo, mzee Allah akupe umri mrefu, najuta kumsoma historia chekelesha na safisha ya wafia teuzi toka enzi za 1954.
 
Nimegundua huyu mzee wetu kuna watu inawachoma moyo kwa Yale aandikayo, mzee Allah akupe umri mrefu, najuta kumsoma historia chekelesha na safisha ya wafia teuzi toka enzi za 1954.
Mbogo...
Ahsante.

Yaliyotokea baada ya kitabu hiki kuchapwa Uingereza na kuingia nchini mimi yalinistaajabisha.

Watu wengi walishangaa na yale waliyosoma.

Walikuwapo waliofurahi sana.
Walikuwapo pia na walioghadhibika.

Lakini hakuna aliyesema nimeandika uongo.
 
Hii historia unayoielezea ni sehemu ndogo sana ya historia ya TANU na TAA ... Historia yako imejikita Dar Es Salaam tu... Wakati harakati za kudai uhuru zilisambaa Tanganyika yote.
Andika basi hapa unalolijuwa wewe kuhusu huko kwengine, maana naona Mohamed Said si mikoani tu, kavuka mpaka mipaka ya Tanganyika kwenye maandiko yake.

Unasubiri nini kuleta ulijuwalo?
 
Tumesoma vitabu vingi na kwa kina sana juu ya historia ya Tanzania, tumepitia na vitabu vya mzee wetu Mohamed Said. Itoshe kusema sikubaliani hata kidogo na anachokitetea na Kukisimamia Mohamed Said.

Huhitaji PhD kuona bias na ukakasi wa hali ya juu katika alichoandika na anakichosema mzee huyu. Kama alichoandika/kusema Mohamed Said kingekuwa hakina ukakasi pasingetokea mivutano isiyo ya lazima wala tija hapa jukwaani (Hii ni dalili kuna shida mahali)

Kitu kingine cha kusikitisha anatetea historia anayodai ni ya kweli huku akiwa amevaa koti la 'kidini' na 'ukanda' (refer previous posts) hakuna mtu anayepima mambo kwa kina anaweza kukubaliana na hili labda watu ambao pia wapo kwenye mrengo huo wa kidini au ukanda.

Na kitu kingine ambacho naweza sema ni weakness kubwa kwa Mohamed Said ni kutoa majibu irrelevant na kile anachoulizwa au kutakiwa kujibu hili nimeliona mara nyingi sana labda hii inakuja kutokana na hoja nyingi zinazotolewa hivyo anashindwa kuzimili kwa wingi wake.

Kama huu ndio utaendelea kuwa misimamo wa Mohamed Said ni wazi hata miaka 100 ijayo historia hii itaendelea kupigwa kama inavyopingwa leo.
 
Tumesoma vitabu vingi na kwa kina sana juu ya historia ya Tanzania, tumepitia na vitabu vya mzee wetu Mohamed Said. Itoshe kusema sikubaliani hata kidogo na anachokitetea na Kukisimamia Mohamed Said.

Huhitaji PhD kuona bias na ukakasi wa hali ya juu katika alichoandika na anakichosema mzee huyu. Kama alichoandika/kusema Mohamed Said kingekuwa hakina ukakasi pasingetokea mivutano isiyo ya lazima wala tija hapa jukwaani (Hii ni dalili kuna shida mahali)

Kitu kingine cha kusikitisha anatetea historia anayodai ni ya kweli huku akiwa amevaa koti la 'kidini' na 'ukanda' (refer previous posts) hakuna mtu anayepima mambo kwa kina anaweza kukubaliana na hili labda watu ambao pia wapo kwenye mrengo huo wa kidini au ukanda.

Na kitu kingine ambacho naweza sema ni weakness kubwa kwa Mohamed Said ni kutoa majibu irrelevant na kile anachoulizwa au kutakiwa kujibu hili nimeliona mara nyingi sana labda hii inakuja kutokana na hoja nyingi zinazotolewa hivyo anashindwa kuzimili kwa wingi wake.

Kama huu ndio utaendelea kuwa misimamo wa Mohamed Said ni wazi hata miaka 100 ijayo historia hii itaendelea kupigwa kama inavyopingwa leo.
Jones...
Nimekusoma na kwa hakika huna tofauti na wale wote wasiofurahishwa na historia hii.
Lakini nakuuliza swal moja tu.

Ulikuwa unaijua historia hii niiyoandika kabla hujaisoma kutoka kwangu?
Hukuwa unaijua hili nina yakini isiyoshaka.

Ushajiuiza kwa nini historia hii ikafutwa na ikawekwa nyingine hiyo unayoijua wewe?
Umejihangaisha kutaka kujua kwa nini?

Hili la kuwa mimi ni mdini kwa kuandika historia ya wazee wangu mimi halinishughulishi kamwe.

Hili la ''irrelevancy,'' ya majibu yangu si kweli wengi kinachokuumizeni ni kuwa katika majibu yangu mnasoma mengi mapya ambayo yanaunguza nyoyo zenu.

hampendi kusikia lolote zuri kutoka kwa Waislam.

Mathalan mtu atantambia kwa kusema, ''Julius Nyerere alikuwa Rais wa kwanza wa TANU.''
Mimi nitamjibu kwa kumweleza kuwa anajua alifikaje hadi akawa rais wa TANU?

Anajua kuwa hyo kadi No. 1 ya Territorial President aliandikiwa na Ally Sykes na kadi No. 2 ni ya Ally Sykes na No. 3 ni Abdul Sykes?

Hii imekuwaje?
Hakuna maelezo?

Mbona hawa wamefutwa katika historia ya TANU?

Hapo nitakwenda nyuma katika kuasisiwa kwa African Association 1929 na nitaeleza kuwa hcho chama mmoja wa waasisi wake ni Kleist Sykes na nitamweleza na chama kingine alichoasisi ambacho kilikuwa kinakwenda pamoja na AA ni Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika (Umoja wa Waislam wa Tanganyka).

Kisha nitamweleza kuwa hiyo nafasi ya Rais wa TANU mtu wa kwanza kupendekezwa alikuwa Chief David Kidaha Makwaia na alipendekezwa na Abdul Sykes nk. nk.

Hamza Mwapachu akamtaka nafasi hiyo apewe Julius Nyerere.

Haya yanawachoma roho kwa kuwa ni historia ambayo inamweka Mwalimu katika nafasi yake anayostahili na inawaweka wazalendo wengine pale pia wanapostahili katika historia ya uhuru wa Tanganyika.

Mimi sina tatizo na kupingwa histora hii ya wazee wangu.
Siwezi kumlazimisha mtu kuniamini niliyoandika.

Lakini ninachotaka kusema hapa ni kuwa nimeirejesha historia ya jamii yangu ya kizazi kizima miaka zaidi ya mia moja ambayo ilkuwa imepotea.

Iwe iwavyo historia hii sasa ipo na inasomwa.

1654172586873.png

Kulia Abdulwahid Kleist Sykes (1924 - 1968), Hamza Kbwana Mwapachu (1913 - 1962)​
 
Jones...
Nimekusoma na kwa hakika huna tofauti na wale wote wasiofurahishwa na historia hii.
Lakini nakuuliza swal moja tu.

Ulikuwa unaijua historia hii niiyoandika kabla hujaisoma kutoka kwangu?
Hukuwa unaijua hili nina yakini isiyoshaka.

Ushajiuiza kwa nini historia hii ikafutwa na ikawekwa nyingine hiyo unayoijua wewe?
Umejihangaisha kutaka kujua kwa nini?

Hili la kuwa mimi ni mdini kwa kuandika historia ya wazee wangu mimi halinishughulishi kamwe.

Hili la ''irrelevancy,'' ya majibu yangu si kweli wengi kinachokuumizeni ni kuwa katika majibu yangu mnasoma mengi mapya ambayo yanaunguza nyoyo zenu.

hampendi kusikia lolote zuri kutoka kwa Waislam.

Mathalan mtu atantambia kwa kusema, ''Julius Nyerere alikuwa Rais wa kwanza wa TANU.''
Mimi nitamjibu kwa kumweleza kuwa anajua alifikaje hadi akawa rais wa TANU?

Anajua kuwa hyo kadi No. 1 ya Territorial President aliandikiwa na Ally Sykes na kadi No. 2 ni ya Ally Sykes na No. 3 ni Abdul Sykes?

Hii imekuwaje?
Hakuna maelezo?

Mbona hawa wamefutwa katika historia ya TANU?

Hapo nitakwenda nyuma katika kuasisiwa kwa African Association 1929 na nitaeleza kuwa hcho chama mmoja wa waasisi wake ni Kleist Sykes na nitamweleza na chama kingine alichoasisi ambacho kilikuwa kinakwenda pamoja na AA ni Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika (Umoja wa Waislam wa Tanganyka).

Kisha nitamweleza kuwa hiyo nafasi ya Rais wa TANU mtu wa kwanza kupendekezwa alikuwa Chief David Kidaha Makwaia na alipendekezwa na Abdul Sykes nk. nk.

Hamza Mwapachu akamtaka nafasi hiyo apewe Julius Nyerere.

Haya yanawachoma roho kwa kuwa ni historia ambayo inamweka Mwalimu katika nafasi yake anayostahili na inawaweka wazalendo wengine pale pia wanapostahili katika historia ya uhuru wa Tanganyika.

Mimi sina tatizo na kupingwa histora hii ya wazee wangu.
Siwezi kumlazimisha mtu kuniamini niliyoandika.

Lakini ninachotaka kusema hapa ni kuwa nimeirejesha historia ya jamii yangu ya kizazi kizima miaka zaidi ya mia moja ambayo ilkuwa imepotea.

Iwe iwavyo historia hii sasa ipo na inasomwa.

View attachment 2248148
Kulia Abdulwahid Kleist Sykes (1924 - 1968), Hamza Kbwana Mwapachu (1913 - 1962)​
Mr. Mohamed Said kwanza tunashangazwa sana na maneno unayotumia mara kwa mara kwamba:
• Hatufurahiswi
• Tunaumia
• Nyoyo zinatuuma
• Hatupendi kusikia historia ya uislam n.k
Nikuambie tu baadhi ya wachangiaji wanaotoa maoni tofauti na unayoandika hawaamini katika imani hizi kubwa mbili hilo ulielewe vizuri, mtu akipinga mawazo yako haina maana kuwa anapinga imani yako na wala imani yako haimshughulishi kabisa what they need is clarity.

Pia unasema umekuja na historia ambayo tulikuwa hatuijui kabla, ni sawa lakini hilo nalo halituzuii hata kidogo kupima na kuangalia ukweli na uhalisia wa historia yenyewe. Kwa sababu hatukuijua kabla haitupi ithibati kuamini kuwa historia hiyo ina ukweli na uhalisia kwa 100%.

Shida nyingine ya wengi ni wewe kutaka kuuaminisha umma kuwa 'wazee wako' wametoa mchango mkubwa katika kudai uhuru wa nchi hii kisa tu walimpokea Mwalimu Julius Nyerere hivyo ni kama hawapewi coverage ya kutosha kwenye vitabu vya historia.

Lakini kuna mchangiaji mmoja alisema hata hao 'wazee wako' wasingempokea Mwalimu Nyerere au kumpa ushirikiano, uhuru wa nchi hii ungeapatika pasi na shida sababu Nyerere angepata back up kubwa zaidi sehemu nyingine zaidi ya ile ya 'wazee wa gerezani' naamini hili unalitambua la kama hukubaliani nalo unapaswa kufunga huu mjadala.

Pia Mohamed Said unasema na ni mara nyingi unasema watu kama Ally Sykes na Abdul Sykes kuwa wamefutwa kwenye historia hili nalo linatupa shida sana why unataka 'watu wako' wapate special privilege kuliko watu wa sehemu nyingine?

Siku zote historia ina tabia ya kujiimba yenyewe pasipo kuimbiwa. Leo hii katika nchi yetu kuna watu wengi na machifu wengi ambao kwa mchango wao mkubwa sana kwenye hili taifa hadi leo historia inawaimba pasipo kutumika nguvu kubwa kama unayotumia kuwaimba 'wazee wako'

Nakushauri acha kauli ya 'Siwezi kumlazimisha mtu kuamini ninachoandika'

Siku zote tumefunzwa kizuri kinajiuza..
 
Ila mzee inabidi uamie Afghanistan wewe na Taliban mna itikadi zinazofanana.
 
Mr. Mohamed Said kwanza tunashangazwa sana na maneno unayotumia mara kwa mara kwamba:
• Hatufurahiswi
• Tunaumia
• Nyoyo zinatuuma
• Hatupendi kusikia historia ya uislam n.k
Nikuambie tu baadhi ya wachangiaji wanaotoa maoni tofauti na unayoandika hawaamini katika imani hizi kubwa mbili hilo ulielewe vizuri, mtu akipinga mawazo yako haina maana kuwa anapinga imani yako na wala imani yako haimshughulishi kabisa what they need is clarity.

Pia unasema umekuja na historia ambayo tulikuwa hatuijui kabla, ni sawa lakini hilo nalo halituzuii hata kidogo kupima na kuangalia ukweli na uhalisia wa historia yenyewe. Kwa sababu hatukuijua kabla haitupi ithibati kuamini kuwa historia hiyo ina ukweli na uhalisia kwa 100%.

Shida nyingine ya wengi ni wewe kutaka kuuaminisha umma kuwa 'wazee wako' wametoa mchango mkubwa katika kudai uhuru wa nchi hii kisa tu walimpokea Mwalimu Julius Nyerere hivyo ni kama hawapewi coverage ya kutosha kwenye vitabu vya historia.

Lakini kuna mchangiaji mmoja alisema hata hao 'wazee wako' wasingempokea Mwalimu Nyerere au kumpa ushirikiano, uhuru wa nchi hii ungeapatika pasi na shida sababu Nyerere angepata back up kubwa zaidi sehemu nyingine zaidi ya ile ya 'wazee wa gerezani' naamini hili unalitambua la kama hukubaliani nalo unapaswa kufunga huu mjadala.

Pia Mohamed Said unasema na ni mara nyingi unasema watu kama Ally Sykes na Abdul Sykes kuwa wamefutwa kwenye historia hili nalo linatupa shida sana why unataka 'watu wako' wapate special privilege kuliko watu wa sehemu nyingine?

Siku zote historia ina tabia ya kujiimba yenyewe pasipo kuimbiwa. Leo hii katika nchi yetu kuna watu wengi na machifu wengi ambao kwa mchango wao mkubwa sana kwenye hili taifa hadi leo historia inawaimba pasipo kutumika nguvu kubwa kama unayotumia kuwaimba 'wazee wako'

Nakushauri acha kauli ya 'Siwezi kumlazimisha mtu kuamini ninachoandika'

Siku zote tumefunzwa kizuri kinajiuza..
Jones...
Mwaka wa 1968 Abdul Sykes alipofariki magazeti ya TANU Uhuru na The Nationalist walitoa taarifa ya kifo cha Abdul Sykes kama taarifa tu ya Julius Nyerere kuhudhuria maziko yake.

Hapakuwa na jingine.
Si taaza wala kueleza Abdul Sykes ni nani katika historia ya kupigania uhuru wa Tangayika.

Mhariri wa magazeti haya alikuwa Benjamin William Mkapa.

Mwaka wa 1981 wakati CCM imeunda jopo chini ya Dr. Mayanja Kiwanka kuandika historia ya TANU kupitia Chuo Cha CCM Kivukoni, mwanajopo moja jina lake Hassan Upeka (TANU Intelligence toka 1956) aliwasilisha ''notes,'' za Abdul Sykes alizoandika kuhusu hstoria ya TANU baada ya kufanya mahojiano na Abdul Sykes kabla hajafariki.

Jibu alilopewa na kiongozi wa jopo ni kuwa historia ya TANU haa uhusiano wowote na Abdul Sykes.
Haya hadi hapa yanatosha kueleza kuhusu kutofurahishwa na hayo mengine ya nyoyo kuuma.

Kitabu kilipotoka jina la Abdul Sykes na wengi walokuwa mstari wa mbele katika kuunda TANU hayakuwamo: Sheikh Hassan bin Ameir, Sheikh Suleiman Takadir, Mshume Kiyate kwa kuwataja wachache wa pale TANU HQ, Dar es Salaam.

Mwaka wa 1988 Africa Events ilichapa makala yangu, ''In Praise of Ancestors,'' ndani yake ilikuwapo historia ya Abdul Sykes na Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika.

Toleo lote lilikusanywa na kutolewa kwenye mzunguko lisisomwe.
Mimi sibabaishi kauli zangu nasema kweli hata kama itamuudhi mtu.

Hakuna Muislam aliyekichukia kitabu cha Abdul Sykes kilipotoka kwa mara ya kwanza mwaka wa 1998 khasa wale waliokuwa wanajua kuwa historia ya TANU ya Kivukoni haiko sawa.

Kizazi hiki cha sasa cha Waislam wa leo hiki ni kitabu chao na ndiyo waliosababisha kitabu leo kufikia toleo la nne.
Hawa wachangiaji wa mada hii wanaotaabishwa na historia hii wengi ni watu wa aina yako.

Hili nalo jibu ndlo hilo.

Ukweli gani utakaokuwanao wewe kwenye maisha ya wazee wangu unishinde mimi ninaotokana na wao wengine kwa nasaba na wengine kwa ujamaa?

Utayajuaje wewe yale yaliyofanywa na wazee wangu?
Au unahusika nini na yale ninayoeleza katika maisha ya wazee wangu kiasi uingie ndani ya maelezo yangu kunisahihisha?

Unaijua historia ya babu yangu Salum Abdallah au Mzee bin Sudi na Ali Jumbe Kiro katika African Association, Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyka hadi TANU?

Nimekuwekea majina haya matatu kwa kuwa hawa waliishi toka vuguvugu la African Association linaanza hadi wakaunda TANU na wakauona uhuru wa Tanganyika 1961.

Hawa kwangu mimi ni babu zangu na baadhi yao nimewaona na nazijua historia zao.

Sijamlazimisha mtu yeyote kuamini historia ya wazee wangu katika kuunda vyama hivyo vyote na kuvitumia katika kupambana na ukoloni.

Tatizo liko wapi?

Kuhusu mchango mkubwa wa wazee wangu.
Wewe amini kuwa hata hawakufanya lolote wala hiyo AA na TANU hawakuasisi wao

Tatizo liko wapi?
Historia hii ilifutwa.

Nani kameguka kashtakiwa kwa kuwa kuwa historia ya babu zake Mohamed Said imefutwa?
Ngoja nikuambie.

Hata kama Nyerere asingefika Dar es Salaam uhuru ungepatikana.
Hata pia kama wazee wangu wasingeunda AA na TANU tusingetawaliwa na Waingereza daima.

Nadhani hapa tumeelewana.

Abdul na Ally Sykes.
Unadhani unaweza kuandika historia ya TANU bila ya kuwataja hawa?

Wala sijasema popote kuwa wao ni wazalendo makhsusi ila huwataja pale inapobidi kusahihisha historia ya uhuru.

Nakuuliza tu unaweza kuandika hstoria ya Mwalimu Nyerere na harakati za kupigania uhuru wa Tanganyika ukamtaja Nyerere peke yake?

Chuo Cha Kivukon wamelifanya hili katika kitabu chao, ''Historia ya TANU,'' na si unaona balaa lake?
Leo mnakuja kwangu kusoma historia mpya ya TANU na historia mpya ya Julius Nyerere.

Hii ndiyo sababu leo wewe uko hapa unajadili na mimi kuhusu historia hii.
Kwa nini hujadili na CCM?

Unasema kuna machifu walipigania uhuru wa Tanganyka.
Hawa machfu walipigania uhuru wa Tanganyika wakiwa wanachama wa chama kipi TANU?

Mimi namjua mmoja Mwami Theresa Ntare tena alinihadithia mwenyewe vipi aliingiza TANU Buha.
Ukipenda kumsoma nifahamishe nikuwekee historia yake hapa.

Hakuna nguvu kubwa yoyote ninayotumia katika kuisomesha historia hii.
Waliotumia nguvu kubwa kuifuta histora ya wazee wangu wapo na ipo historia yao.

Ikiwa unapenda kuisoma nifahamishe nitakuweka hapa.
Nakufahamisha kwa mara nyingine kuwa sikulazimishi kuamini historia ya wazee wangu.

Uko huru kuamini upendacho iwe historia ya TANU ya Temu na Kimambo (1969) au ya Chuo Cha CCM Kivukoni (1981).
Hii ni nchi huru.

1654180158863.png

1654180081200.jpeg

1654179967540.png
 
Back
Top Bottom