Historia ya Uhuru isimuliwavyo na Mohammed Said yakosolewa


WC,

Inatosha.
Unasema inatosha.

Mbona unatoa mbukwa mapema?
Kwani mnakasha umefikia mwisho?

Yaani sasa basi tupige fatha tufunge darsa?

Mohamed
 
Hapo mwenyewe unajiona ndio umetoa ushahidi kuwa Mkwawa hakuwa Muislam? Go and do your researh and come back with something credible.
UISLAMU au UKRISTO wa Mkwawa unatuhusu nini sisi? Hivi kweli Faiza ni UISLAMU uliokuleta humu JF? Akili yoote hiyo ulionayo ni kwa kuwa ni MUISLAMU? Ukibadili DINI kwa "kuolewa" na mimi kwa mfano basi utakuwa zezeta?
 

Hujaonesha "contradiction" hata moja, unaijuwa maana ya "contradiction" au unazuga tu?
 
WC,

Inatosha.
Unasema inatosha.

Mbona unatoa mbukwa mapema?
Kwani mnakasha umefikia mwisho?

Yaani sasa basi tupige fatha tufunge darsa?

Mohamed
Uzoefu wangu humu na kwingineko mijadala kama hii inayogusa IMANI na DINI huwa haina mwisho na hasa kwa watu kama wewe ambao DINI zimewakolea. Kila utakalolisema, utakalolifanya, utakaloliandika, utakalofikiria ni UISLAMU na WAISLAMU wawepo. Watajwe.
 
Hujaonesha "contradiction" hata moja, unaijuwa maana ya "contradiction" au unazuga tu?

We mi nakuona clown tu huna lolote zaidi ya mizaha ya chumbani. Najadiliana na MS lakini wewe ukidandia mada yangu basi nashuka level ndogo ambayo utaelewa.
 
UISLAMU au UKRISTO wa Mkwawa unatuhusu nini sisi? Hivi kweli Faiza ni UISLAMU uliokuleta humu JF? Akili yoote hiyo ulionayo ni kwa kuwa ni MUISLAMU? Ukibadili DINI kwa "kuolewa" na mimi kwa mfano basi utakuwa zezeta?

Kubaguliwa Waislaam katika historia ya Taifa, kubadilishwa majina ya Waislaam kwa makusudi kabisa, Kutotajwa michango ya Waislaam kama kina Mkwawa na Kimweri na wengine wengi waliofatia baada yao, kupotoshwa kwa historia kwa makusudi kabisa ili Uislaam na Waislaam wasionekane michango yao katika Taifa hili ndio mada yote iliposimamia.

Imeelezwa kwa ufasaha kabisa kuwa si tu kutokuandikwa kwa Waislaam kwenye historia ni kwa bahati mbaya au kwa kuwa hawana mchango wao katika Taifa hili, bali wao ndio waliokuwa mstari wa mbele na ndio walikuwa waasisi wa harakati zote za kudai madaraka, na ikaoneshwa kuwa haikuanzia kwa Waislaam walioanzisha AA, TAA, TANU bali ikabainishwa kuwa hata kina Songea walikuwa Waislaam na walipigania haki ya uzalendo wao na hata wao majina yao kwa makusudi yamefutwa yenye viashirio vya Uislaam, kwanini? Hilo ni swali jepesi sana kwa mtu mwenye fikra fupi, lakini kwa mtu anaeitakia mema hii nchi ni swali zito sana.

Tukatolewa huko tukapelekwa hadi Nyerere alipowageuka hawa wazee wa Kiislaam waliompokea na kufikia hadi kuwatia ndani na kuwafukuza nchi, swali linakuja, anaewatia watu ndani kwa sababu ya dini zao na sababu ya udini wao, huyo ni nani kama sio mdini? mlishasikia kuna askofu au padri amefukuzwa nchi kwa udini wake au kutiwa ndani kwa udini wake? hapana. Kwa hiyo wadini ni masheikh wa Kiislaam tu?

Tumeona mpaka Nyerere amenukuliwa akisema kuwa anaiendesha nchi kwa "[SIZE=-0]In an interview with the Christian Century of March 1, 1972, Mwalimu Nyerere was quoted as saying that his efforts to build African socialism in Tanzania represented his determination to translate in practical terms the teachings contained in The Gospel of Jesus Christ.[/SIZE]"

Bado tu, na vielelezo vingine kibao, halafu unakuja kusema kuwa oooh "udini" udini ni nini? Udini wakati Muislaam anasema kaonewa na mfumo uliojengwa kwa makusudi kabisa? udini ni Muislaam anapouliza ilikuwaje 83% vs 17%? kwanini udini isiwe 83% iwe 17%? Kwanini Nyerere aseme atatekeleza ujamaa wake kwa mafundisho yaliomo kwenye injili ya Yesu kristo? na huo sio udini?

Kuweni wa kweli japo kidogo, Waislaam, tuna kila sababu ya kuandika historia ya nchi hii kama ilivyo na hilo ni kwa kila mtanzania mwenye uwezo wa kuandika. Ambae anaiona hitoria ya Mohamed Said ni ya udini, atuambie historia ya Nyerere na kupewa uwenye "heri"kuelekea "utakatifu" sio udini? au uwenye "heri" ni tuzo ya Serikali ya Tanzania na si ya kanisa?

Iweje kiongozi wa nchi awe mwenye "heri" wakati nchi kaiacha hohehahe? hapo sasa. Hiyo heri ni ipi? hakuna zaidi ya umaskini na ufukara aliouwacha Nyerere kwa wananchi wa Tanzania, walioachwa na utajiri wa Ardhi, mashule, mahospitali ni kanisa katoliki pekee na hilo halina ubishi. kwanini?

Leo Tanzania kanisa katoliki linahodhi ardhi zaidi ya tasisi nyingine yoyote baada ya Serikali, ni kwa bahati nzuri tuu? Leo kanisa katoliki lina shule na vyuo kuliko taasisi yoyote baada ya Serikali, ni kwa bahati nzuri tu? leo kanisa katoliki lina mahospitali kuliko taasisi yoyote baada ya Serikali, ni kwa bahati nzuri tu? leo kanisa katoliki linapokea ruzuku kubwa ya kifedha kutoka serikalini kuliko taasisi yoyote nyingine, ni kwa bahati nzuri tu? la hasha, hizo ndio sababu za Nyerere kupewa uwenye "heri" na si kingine, si kwa kulitumikia Taifa ni kwa kulitumikia kanisa, kwa mgongo wa nani? kwa fedha za nani? kwa rasilmali za nani? za walio wafuasi wa kanisa na wasio wafuasi wa kanisa, na wengi wao ni Waislaam.

Ni mengi, mengi sana madhila yaliofanywa na yanayoendelea kufanywa na ukiuliza unaitwa "mdini" haikuanzia leo na haitokuwa mwisho leo lakini "ngoma ikivuma sana...".

Waislaam wa leo na dunia ya leo si dunia ya kuburuzwa, leo ni dunia ya dot com. Kila kitu kiko wazi, hakuna kuzuia "media" kama wakati wa Nyerere, hakuna kuburuzwa kama wakati wa Nyerere, watu kuswagwa kama ng'ombe kupelekwa maporini kuanzisha vijiji vya ujamaa ambavyo havikuleta tija yoyote zaidi ya kututia kwenye lindi la umaskini. Ukitazama kwa undani utaona alikuwa hajashindwa bali ile ilikuwa ni kisingizio cha kuusambaza mfumo kristo.

Kuna siku tulikuwa tunapita njia za ndani kutokea Manyoni kuelekea Singida, siku hizo barabara kuu ya Manyoni haipitiki ikinyeesha mvua, malori yamekwama yamefunga njia, bahati mume wangu ni mzoefu wa mapori kwani ni "hobby" yake kuwinda, akatuambia tuingie hapa (kulia ukitokea manyoni kabla ya kufika Mkiwa) kuna njia za maporini "nazijuwa" zitatutoa karibu ya Singida, gari tuliokuwa nayo ilikuwa inaruhusu kukatiza porini, tukaingia, huko ndani mbugani niliona kitu cha ajabu sana, tulikuta kanisa, na majengo tofauti ndani ya uzio, na hapo ni mbali na kijiji chochote kile. Nikauliza kwanini wamejenga huku porini kabisa? nikaambiwa walijenga hapa wakati wa vijiji vya ujamaa, watu walihamishiwa huku kutoka vijiji vyao vya asili na Wakatoliki wakaja kujenga hilo kanisa shule na zahanati, elewa kuwa vijiji vya asili huko walipoondolewa watu kuletwa hapo porini vyote vilikuwa Waislaam 90% nani asiyejuwa Wanyaturu wa Mkiwa, Isuna na Puma kwa Uislaam wao? huo ndio ushindi wa Nyerere kwa vijiji vya ujamaa, ni nani ataewacha kupeleka mwanae hapo akasome wakati shule ya karibu na hili kanisa ni kilomita 20 na barabara hazipitiki na kama hiyo shule ya bure ilikuwa na waalim. Ni nani ataacha kupeleka mwanae akatibiwe hapo wakati zahanati ya Serikali ya karibu ni kilomita 20 kutoka hapo na kama ina dawa. Huo ni mfano mmoja tu, na nakumbuka jina la hao waliojenga hilo kanisa na hayo makazi mbugani, na juzi juzi niliona Pinda katolewa picha yake kapiga magoti akiwa huko (Tena alikuwa kanisa lao Mkiwa barababarani si hilo waliloliweka huko mbugani)

Huo ndio ushindi wa Nyerere wa kumpatia tuzo ya uwenye "heri" na "utakatifu", ni udini mtupu hakuna zaidi.
 
We mi nakuona clown tu huna lolote zaidi ya mizaha ya chumbani. Najadiliana na MS lakini wewe ukidandia mada yangu basi nashuka level ndogo ambayo utaelewa.

Huo ni muono wako na siwezi kukupinga, mimi niache kama nilivyo na huna haja ya kujadiliana na mimi, lakini ntapoikuta post iwe yako au ya mwingine yoyote kwenye "open forum" ntaijibu ikibidi.
 
Faiza, una maoni gani juu ya haya:
-Kutaifishwa kwa shule, hospitali za makanisa kulikofanywa na Mwalimu?
-Mwalimu kumkabidhi madaraka Ali Hassan Mwinyi, Muislamu safi kuliko wewe na Mohamed mwaka 1985?
-Mwalimu kumkabidhi uwaziri mkuu Rashid Mfaume Kawawa mwaka 1962?
- Mwalimu kujenga msikiti mzuri tu Butiama ambako Waislamu ni 2%?
- Mwalimu kuwapenda watu kama SAS kwa kiwango kile?
-Mwalimu kukaa na Quran na Biblia pale Ikulu miaka yote ya utawala wake?
 
WC,

Inatosha.
Unasema inatosha.

Mbona unatoa mbukwa mapema?
Kwani mnakasha umefikia mwisho?

Yaani sasa basi tupige fatha tufunge darsa?

Mohamed

Sheikh Mohamed shusha darsa, mnakasha na uendelee, kumbuka hii ni historia nyingine unaiweka humu, hakuna muandishi yoyote Mtanzania wa historia aliyokwisha fanya haya unayoyafanya wewe hapa JF. Washukuriwe JF kwa kuendelea kuuweka huu mjadala, kwani nakumbuka wameshaifunga mingine ghafla kabla ya huu.

Tupeleke kwenye bahari ya historia ya Tanganyika na nnajuwa kuna mengi sana toka na kabla hata ya Vasco Da Gama kuja kwake na kubaki baharini (Vasco Da Gama inasemekana hajagusa ardhi ya nchii hii alibaki jahazini) Iwache hii nyuzi ndio iwe chachu ya kuijuwa nchi yetu, iwache hii nyuzi ndio iwe chachu kuujuwa mchango wa Waislaam na wasio Waislaam katika nchi hii, kila mwenye lake alishushe hapa, lenye maana tutalipokea, lisilo na maana tutaliacha kama lilivyo, kila mmoja wetu akitoka hapa awe anaweza japo kwa uchache kuiongelea historia ya nchi hii.

Ni wengi leo wamemjuwa Abdul Wahid Sykes, Mshume Kiyate, kina Plantan, tumejuwa kuwa chuo kikuu cha kwanza Tanzania uwanja kautoa Rupia, tumejuwa kuwa Kimweri na Mkwawa walikuwa Waislaam (unless proven otherwise), tumemjuwa Sisso ni nani (ni bahati kubwa kuwa nnamuelewa Mzee Rashid Sisso kwani akija kwetu, sikutegemea kuna siku ntamuona kaandikwa kwa sifa njema). Ni mengi mengi sana tunayofaidika nayo, usitukoseshe darsa Sheikh Mohamed, na nimeanza kukopi zile posts nnazoona zina umuhimu kwa upande wangu kwani wengine humu wameshaonyesha mchezo mbaya wa kuzifuta posts, wanapobanwa.
 

1) Utaifishaji wa shule wa Nyerere haukuwa na tija njema yoyote. Umetuongezea ujinga katika hii nchi, leo tazama Uganda na Kenya, jirani zetu wa asili na washirika wetu wa zamani (East African Community) ingawa wao ni wachache kuliko sisi, lakini leo wana wasomi wengi kuliko sisi. Hawa walipopata madaraka hawajataifisha shule.

2) Mwalim kumkabidhi madaraka Ali Hassan Mwinyi ilikuwa kama kudanganya watu, unamkabidhi madaraka halafu unaitisha mkutano na waandishi wa habari unamkemea? huo ndio unafik wa Nyerere. Isitoshe ilikuwa ni kama kumsukumia janga Rais mpya (rejea hotuba ya Mwinyi ya "Mikuki Miwili", alyoitowa Diamond Jubilee kuongea na wazee wa Dar., itakupa picha ya alipokabidhiwa hii nchi ilikuwaje, unamkabidhi nchi mwenzio haina senti tano ya kigeni BOT, haina mafuta, haina mabarabara, unamkabidhi nchi hohehahe hata colgate ni anasa.

Lakini Ali Hassan Mwinyi anastahili kila sifa, katutoa kwenye lindi la umaskini na katufunguwa macho kwa sana tu. Hata TV tulikuwa hatuzijuwi mpaka alipokuja Ali Hassan Mwinyi.

3) Hii ilikuwa ni kupisha tu mambo fulani yafanyike na haina "significance" yoyote.

4) Msikiti hakujenga Mwalim, Msikiti wa Butiama ni fedha ya Gaddafi na umejengwa baada ya kufa Mwalim, yeye alizikalia hizo pesa mpaka anakufa, Maria Nyerere akaona mnhhhh, isije ikawa ndio ule mtetemeko wa ardhi na kaburi kuwaka moto, akaliweka wazi na msikiti ukajengwa.

5) Hata mimi nnakaa na Qur'an na Biblia na huwa nnazisoma zote, licha ya hivyo tu, nnakaa hata na Verda na Upanishads za kihindu na vitabu vingine vingi tu vya imani tofauti hata vya ma Scientologists, ni katika kutafuta ilmu. Nyerere akipenda kusoma, na hili la kukaa na Qur'an na biblia ni kitu cha kawaida kwa msomi yoyote yule, mbaya pale unapovitumia hivi vitabu isivyo na unapozibandika aya zake isivyo kama alivyofanya Mzee Mwanakijiji posts zilizopita, huo unakuwa upotoshaji wa makusudi.
 
Dah! Umejibu kwelikweli. Angalau umeuweka kando UISLAMU katika majibu yako yote. Umemsingizia Mama Maria Nyerere tu.
 
Gospel of Jesus? Ndio gani hiyo? labda ulitaka kusema gospel according to... na hata hivyo hakuna gospel according to jesus. za mbayuwayu unachanganya na zako dadangu!

Nilikuambia nipo kwenye mobile phone, na wala sikutaka kusema "gospel according to..." kama ufikiriavyo wewe, huo ni mnakasha mwingine kabisa. Soma hii halafu uelewe ni nani aliosema hayo maneno:

"[SIZE=-0]In an interview with the Christian Century of March 1, 1972, Mwalimu Nyerere was quoted as saying that his efforts to build African socialism in Tanzania represented his determination to translate in practical terms the teachings contained in The Gospel of Jesus Christ.[/SIZE]"
Surce: Chapter One: Mwembechai Killings and the Political Future of Tanzania
 
Dah! Umejibu kwelikweli. Angalau umeuweka kando UISLAMU katika majibu yako yote. Umemsingizia Mama Maria Nyerere tu.

Sitoweza kuuweka kando Uislaam hata iweje, Na sina sababu za kumsingizia Mama Maria Nyerere kwa wema wa kuujenga msikiti baada ya mumewe kufa. Jee hapo nime"msingizia" au nimemsifia? Unanshangaza!
 

FF,

Mimi nasoma sana kwako we hujui tu.
Mungu akujaze kheri.


Mohamed
 
Endeleen kupiga porojo tu 24 hrs wenzenu KKKT Wameitisha harambee ya kujenga chuo kikuu kingine hapa dar. Wamenunua ekari 100 kule kibaha wanajenga shule kule. Dayosisi ya kagera wanafungua chuo. Waislamu mko busy makongamano ya mfumo kristo ukija kushtuka wenzenu wako km 10000 nyie ndo mnaanza moja.
 
Tofauti na wengi na hasa wale wa Pwani mnaozaliwa na DINI zenu, tunaotoka bara DINI tumezisoma na kubatizwa ukubwani. Hazitusumbui hata kidogo kama ambavyo hazikumsumbua Mwalimu ambaye naye alibatizwa ukubwani.
 
FF,

Mimi nasoma sana kwako we hujui tu.
Mungu akujaze kheri.


Mohamed


Nashkuru kwa Du'a na InshaAllah iwe kwa sote, mimi ndie nijifunzae mengi sana hapa Sheikh wangu, bila ya wewe kuanzisha haya tusingeipata fursa hii, saa hizi tungekuwa jukwaa la porojo za MMU tukimsoma Bujibuji na vituko vyake. Bujibuji usikurupuke hii ni sifa kwako.

Na InshaAllah huu uwe mwanzo mwema watokee wasomi wengi wengi tuu humu na mada tofauti tofauti tuzijadili kama tunavyofanya hapa, ni moja ya faida ya hii mitandao.
 
Sitoweza kuuweka kando Uislaam hata iweje, Na sina sababu za kumsingizia Mama Maria Nyerere kwa wema wa kuujenga msikiti baada ya mumewe kufa. Jee hapo nime"msingizia" au nimemsifia? Unanshangaza!
Soma jibu Na. 4 kwenye ile post yako. Mwalimu alizikalia pesa za Gaddafi kweli? Mama Maria akaona mtetemeko na kaburi kuwaka moto! Porojo na kejeli zingine zinapotolewa na mtu mwenye uwezo mkubwa wa kufikiri kama wewe Faiza haipendezi.
 
Tofauti na wengi na hasa wale wa Pwani mnaozaliwa na DINI zenu, tunaotoka bara DINI tumezisoma na kubatizwa ukubwani. Hazitusumbui hata kidogo kama ambavyo hazikumsumbua Mwalimu ambaye naye alibatizwa ukubwani.

WC,

Waislam hatubatizwi.
Tunazaliwa tayari tu Waislam.

Nyerere akiogopa sana chochote kuhusu Uislam.
Walioishinae khasa baada ya uhuru wakilijua sana hilo.

Walikuwa hawaleti chochote kuhusu Uislam mbele yake.
Siku Abubakar Mwilima alipomuuliza Nyerere kwa nini Waislam bado wako nyuma katika elimu nyuma ilhali wenzao wanaendelea...

Hii katika kamati Kuu.

Nyerere alikuwa kama kapigwa na radi...alikaa kimya bila ya kutoa jibu lolote halafu aliahirisha kikao kwa muda.
Wakati wa chai kila mjumbe hakutaka kuwa karibu na Mwilima wala kuonekana anazungumzanae.

Walijua kuwa Mwilima sasa kachokoza nyuki.

Mohamed
 
Tofauti na wengi na hasa wale wa Pwani mnaozaliwa na DINI zenu, tunaotoka bara DINI tumezisoma na kubatizwa ukubwani. Hazitusumbui hata kidogo kama ambavyo hazikumsumbua Mwalimu ambaye naye alibatizwa ukubwani.

Ngoja nikupe darsa kidogo; Maana ya dini kwa kiarabu (kumbuka dini ni neno lenye asili ya kiarabu) ni mfumo wa maisha, ni namna mtu unavyochaguwa kuishi. Inaweza ikawa dini yako ni kutokuamini kama kuna Mungu, huo ni mfumo wako uliouchaguwa au kuchaguliwa, inaweza kuwa dini yako ni kufata Ukristo, huo ni mfumo wako wa maisha uliouchaguwa au kuchaguliwa, sisi waislaam dini yetu ni Uislaam, ikimaanisha kujiasalimisha kwa Allah, totaly. Hiyo ndio dini "mfumo wa maisha yetu". Kusema sina "dini" kwa mwenye kujuwa maana ya neno "dini" kunamaanisha kusema sina "mfumo wa maisha".

Ni vigumu sana leo kwa Muislaam kumuaminisha kuwa siasa na dini ni vitu tofauti "unless" awe haufaham Uislaam. Hilo neno siasa pia lina asili ya kiarabu, "siasa" ni kumaanisha kufikia malengo fulani bila kutumia nguvu wala ugomvi wala vita. Hiyo ndio siasa, mwana siasa mzuri ni yule anaetumia siasa kufikia malengo ayatakayo na si lazima yawe mema au mabaya kwa wakati ule ili mradi tu ayafikie malengo yake kisiasa.

Kwa hiyo kaa uelewe, hakuna siasa kama itadhalilisha dini "mfumo wa maisha" wa mmoja wapo ikawa hiyo siasa ni ya amani.

Hayo ni kwa mtazamo wa maana halisi ya neno"dini", neno "Uislaam" na neno "siasa", maneno yote hayo yanatokana na Kiarabu na hakuna mbora ataekuja kuyafafanua hayo zaidi ya Muislaam ambae wengi wao ilmu yao ya kwanza ni kufundishwa herufi za kiarabu Alif, Bee, Tee, na hiyo hiyo Alif, Bee, Tee,, ndio leo unalijuwa neno la Kiingereza Alphabet, Alpha-Be-T.

Kama hujanielewa naomba uliza, si rahisi wengine kulielewa darsa, kwa wengine ni rahisi kulielewa darasa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…