Historia ya Uhuru isimuliwavyo na Mohammed Said yakosolewa

Historia ya Uhuru isimuliwavyo na Mohammed Said yakosolewa

WC,

Waislam hatubatizwi.
Tunazaliwa tayari tu Waislam.

Nyerere akiogopa sana chochote kuhusu Uislam.
Walioishinae khasa baada ya uhuru wakilijua sana hilo.

Walikuwa hawaleti chochote kuhusu Uislam mbele yake.
Siku Abubakar Mwilima alipomuuliza Nyerere kwa nini Waislam bado wako nyuma katika elimu nyuma ilhali wenzao wanaendelea...

Hii katika kamati Kuu.

Nyerere alikuwa kama kapigwa na radi...alikaa kimya bila ya kutoa jibu lolote halafu aliahirisha kikao kwa muda.
Wakati wa chai kila mjumbe hakutaka kuwa karibu na Mwilima wala kuonekana anazungumzanae.

Walijua kuwa Mwilima sasa kachokoza nyuki.

Mohamed
Mohamed,
Unaongopa hadi basi. Mwalimu kafanyakazi na WAISLAMU na UISLAMU tangu TAA. Ipo siku alifunga na WAISLAMU akiombea kitu fulani. Kichwa kikamuuma. Hiyo hadithi aliisimulia katika moja ya hotuba zake akimtaja Mzee wako mmoja wa Bagamoyo. Amefanya kazi na Waislamu wengi wa Zanzibar. Amehudhuria mabaraza ya IDD. Majibu ya Mwalimu kwa Mwilima mngeyavumilia? Mwalimu alikuwa mkweli sana. Asingemjibu Mwilima halafu akaeleweka misikitini.
 
Soma jibu Na. 4 kwenye ile post yako. Mwalimu alizikalia pesa za Gaddafi kweli? Mama Maria akaona mtetemeko na kaburi kuwaka moto! Porojo na kejeli zingine zinapotolewa na mtu mwenye uwezo mkubwa wa kufikiri kama wewe Faiza haipendezi.

Hakuna porojo hapo soma:
quote_icon.png
By Field Marshall ES
.MWILI WA NYERERE WAPOKEWA KWA MVUA NA RADI KALI BUTIAMA

Mwili wa Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere, umewasili hapa na kupokelewa kwa taratibu za kijadi huku kukiwa na mvua kubwa na ngurumo kali za radi. Mwili huo uliwasili majira ya saa 1.45 usiku, ukitokea Musoma ambako ulipokelewa kwa taratibu za kijeshi.


Pia habari zaidi kutoka Butiama zinasema kuwa jana usiku kulikuwa na tetemeko kubwa la ardhi kijijini hapo, hali ambayo wanakijiji wa hapo wanaihusisha na kifo cha Chifu wao Mwalimu Nyerere. Wakati mwili huo ukipitishwa wananchi wengi kwa malefu walikuwa kwenye miti na mapaa ya nyumba wakijaribu angalau kuliona jeneza hilo.
 
WC,

Wanaomfahamu Nyerere wanasema alikuwa anakwepa sana ile ya uso kwa uso yaani nipe nikupe. Nadhani umenifahamu.

Ninazozifahamu mimi za nipe nikupe uso kwa uso ni nne na zote kapambana na Waislam:
  1. Schneider Plantan baada ya kuachiwa kutoka kizuizini alimfata Nyerere nyumbani kwale kukawa na mnakasha wa aina yake.
  2. Bilali Rehani Waikela, katika mkutano wa EAMWS Ukumbi wa Shule ya Wasichana Agakhan, Dar es Salaam1963, ilikuwa hotuba ya kuonyeshana vidole
  3. IGP Hamza Aziz baada ya kukataa kutii amri kumkamata Mufti Sheikh Hassan bin Amir, ndani ya katika Kamati Kuu
  4. Mwilima, ndani ya Kamati Kuu
Mohamed
 
Hongera sana Mwakajila kwa mchango wako wa kuelimisha jamaa zetu hapo juu, japo nadhani hawakuelewa kulingana na sisis watanzania tulivo wavivu wa kusoma takwimu, na vitabu mbalimbali
 
Mohamed,
Unaongopa hadi basi. Mwalimu kafanyakazi na WAISLAMU na UISLAMU tangu TAA. Ipo siku alifunga na WAISLAMU akiombea kitu fulani. Kichwa kikamuuma. Hiyo hadithi aliisimulia katika moja ya hotuba zake akimtaja Mzee wako mmoja wa Bagamoyo. Amefanya kazi na Waislamu wengi wa Zanzibar. Amehudhuria mabaraza ya IDD. Majibu ya Mwalimu kwa Mwilima mngeyavumilia? Mwalimu alikuwa mkweli sana. Asingemjibu Mwilima halafu akaeleweka misikitini.

Mwalimu hakuwa mkweli alikuwa mnafiki, mchoyo na mbaguzi

Alifanya upendeleo kwa kanisa akifikiri kupata dhawabu kwa Mungu wake (udini)

Ila hakuwa mwizi tu
 
Ngoja nikupe darsa kidogo; Maana ya dini kwa kiarabu (kumbuka dini ni neno lenye asili ya kiarabu) ni mfumo wa maisha, ni namna mtu unavyochaguwa kuishi. Inaweza ikawa dini yako ni kutokuamini kama kuna Mungu, huo ni mfumo wako uliouchaguwa au kuchaguliwa, inaweza kuwa dini yako ni kufata Ukristo, huo ni mfumo wako wa maisha uliouchaguwa au kuchaguliwa, sisi waislaam dini yetu ni Uislaam, ikimaanisha kujiasalimisha kwa Allah, totaly. Hiyo ndio dini "mfumo wa maisha yetu". Kusema sina "dini" kwa mwenye kujuwa maana ya neno "dini" kunamaanisha kusema sina "mfumo wa maisha".

Ni vigumu sana leo kwa Muislaam kumuaminisha kuwa siasa na dini ni vitu tofauti "unless" awe haufaham Uislaam. Hilo neno siasa pia lina asili ya kiarabu, "siasa" ni kumaanisha kufikia malengo fulani bila kutumia nguvu wala ugomvi wala vita. Hiyo ndio siasa, mwana siasa mzuri ni yule anaetumia siasa kufikia malengo ayatakayo na si lazima yawe mema au mabaya kwa wakati ule ili mradi tu ayafikie malengo yake kisiasa.

Kwa hiyo kaa uelewe, hakuna siasa kama itadhalilisha dini "mfumo wa maisha" wa mmoja wapo ikawa hiyo siasa ni ya amani.

Hayo ni kwa mtazamo wa maana halisi ya neno"dini", neno "Uislaam" na neno "siasa", maneno yote hayo yanatokana na Kiarabu na hakuna mbora ataekuja kuyafafanua hayo zaidi ya Muislaam ambae wengi wao ilmu yao ya kwanza ni kufundishwa herufi za kiarabu Alif, Bee, Tee, na hiyo hiyo Alif, Bee, Tee,, ndio leo unalijuwa neno la Kiingereza Alphabet, Alpha-Be-T.

Kama hujanielewa naomba uliza, si rahisi wengine kulielewa darsa, kwa wengine ni rahisi kulielewa darasa.
Nipe darsa jingine. Ilikuwaje huko Nchi za Kiarabu ambako ndiko chimbuko halisi la Uislamu wakakubali kutawaliwa namna ile ya Tunisia, Libya, Misri, SaudArabia, Syria,.....Halafu wanazinduka sasa na kuanza kuchinjana?
 
Nipe darsa jingine. Ilikuwaje huko Nchi za Kiarabu ambako ndiko chimbuko halisi la Uislamu wakakubali kutawaliwa namna ile ya Tunisia, Libya, Misri, SaudArabia, Syria,.....Halafu wanazinduka sasa na kuanza kuchinjana?

Hatupo katika mjadala huu kuizungumzia Tunisia, Libya, Misri, Saudi Arabia wala Syria. Soma Kichwa cha mjadala hapo juu kisha njoo na maswali na majibu yanayohusu.

Ukipenda kujadili hayo mengine yafungulie nyuzi na wenye interest nayo watakuja kujibu.
 
Soma jibu Na. 4 kwenye ile post yako. Mwalimu alizikalia pesa za Gaddafi kweli? Mama Maria akaona mtetemeko na kaburi kuwaka moto! Porojo na kejeli zingine zinapotolewa na mtu mwenye uwezo mkubwa wa kufikiri kama wewe Faiza haipendezi.

Kama ile haijakutosha hii hapa nyingine, hakuna porojo hapa:

Field Marshall ES
...Matetemeko mawili mfululizo, yalitokea tena jana katika maeneo hayo ya mazishi huko Butiama...
 
WC,

Wanaomfahamu Nyerere wanasema alikuwa anakwepa sana ile ya uso kwa uso yaani nipe nikupe. Nadhani umenifahamu.

Ninazozifahamu mimi za nipe nikupe uso kwa uso ni nne na zote kapambana na Waislam:
  1. Schneider Plantan baada ya kuachiwa kutoka kizuizini alimfata Nyerere nyumbani kwale kukawa na mnakasha wa aina yake.
  2. Bilali Rehani Waikela, katika mkutano wa EAMWS Ukumbi wa Shule ya Wasichana Agakhan, Dar es Salaam1963, ilikuwa hotuba ya kuonyeshana vidole
  3. IGP Hamza Aziz baada ya kukataa kutii amri kumkamata Mufti Sheikh Hassan bin Amir, ndani ya katika Kamati Kuu
  4. Mwilima, ndani ya Kamati Kuu
Mohamed
Sio Mwalimu tunayemfahamu! Akataliwe hata na aloowateua akina IGP Hamza Aziz wa Mtoni kwa Aziz Ali? Mwalimu alikuwa mvumilivu na msikivu pia. Ukumbuke pia kwamba kuijenga nchi isiyo na DINI kutoka TANU ya WAISLAMU wa misimamo mikali kama masheikh unaowataja hapo haikuwa kazi ndogo.
 
Ngoja nikupe darsa kidogo; Maana ya dini kwa kiarabu (kumbuka dini ni neno lenye asili ya kiarabu) ni mfumo wa maisha, ni namna mtu unavyochaguwa kuishi.

Maana ya neno dini na maana ya dini inaweza kuwa ni vitu viwili tofauti ndugu yangu. Ukiuulizwa neno kiti lina maana gani na ukiulizwa kiti ni nini ni maswali mawili yanayohusu kitu kimoja kwa muktadha tofauti. Dini kwa maana ya matendo ya mtu na dini kwa maana ya jina ni vitu viwili tofauti. Mtu anaweza kuitwa muislamu lakini asiishi maisha ya kiislamu kwani uislamu una vitu vingi mno hata kiasi kwamba kimoja kikipungua huwezi kuutoa uislamu wa mtu.
kutukana ni kinyume cha uislamu lakini si kama anayetukana unauvua uislamu waka papo papo. Dini kama mfumo ni kitu cha kujadili. Na tafsiri ya neno huwa haina uhusiano na kitu chenyewe, Hebu angalia hii. Kiti, kichumbi, Ichumbi,Kigoda, chitengo au chair. haya maneno yanazungumzia dhana tofauti?

Inaweza ikawa dini yako ni kutokuamini kama kuna Mungu, huo ni mfumo wako uliouchaguwa au kuchaguliwa, inaweza kuwa dini yako ni kufata Ukristo, huo ni mfumo wako wa maisha uliouchaguwa au kuchaguliwa, sisi waislaam dini yetu ni Uislaam, ikimaanisha kujiasalimisha kwa Allah, totaly. Hiyo ndio dini "mfumo wa maisha yetu". Kusema sina "dini" kwa mwenye kujuwa maana ya neno "dini" kunamaanisha kusema sina "mfumo wa maisha".

Mbona Mohamed Said kasema nyie waislamu huwa mnazaliwa mkiwa waislamu?

Ni vigumu sana leo kwa Muislaam kumuaminisha kuwa siasa na dini ni vitu tofauti "unless" awe haufaham Uislaam. Hilo neno siasa pia lina asili ya kiarabu, "siasa" ni kumaanisha kufikia malengo fulani bila kutumia nguvu wala ugomvi wala vita. Hiyo ndio siasa, mwana siasa mzuri ni yule anaetumia siasa kufikia malengo ayatakayo na si lazima yawe mema au mabaya kwa wakati ule ili mradi tu ayafikie malengo yake kisiasa.

Neno siasa na siasa ni vitu viwili tofauti kwa sasa. Neno Demokrasia lilikotoka na jinsi demokrasia yenyewe inavyotafsiriwa sasa ni tofauti kabisa. Kwa asili neno Jambazi lilimaanisha jitu lenye miraba minne, haya majambazi yetu ya sasa hivi yana miraba minne?

Kwa hiyo kaa uelewe, hakuna siasa kama itadhalilisha dini "mfumo wa maisha" wa mmoja wapo ikawa hiyo siasa ni ya amani.

Siyo dini tu,siasa yoyote inayodhalilisha utu wa mtu ni siasa mbaya.

Hayo ni kwa mtazamo wa maana halisi ya neno"dini", neno "Uislaam" na neno "siasa", maneno yote hayo yanatokana na Kiarabu na hakuna mbora ataekuja kuyafafanua hayo zaidi ya Muislaam ambae wengi wao ilmu yao ya kwanza ni kufundishwa herufi za kiarabu Alif, Bee, Tee, na hiyo hiyo Alif, Bee, Tee,, ndio leo unalijuwa neno la Kiingereza Alphabet, Alpha-Be-T.

The word "alphabet" came into Middle English from the Late Latin word Alphabetum, which in turn originated in the Ancient Greek ἀλφάβητος (alphabētos), from alpha and beta, the first two letters of the Greek alphabet. Alpha and beta in turn came from the first two letters of the Phoenician alphabet, and meant ox and house respectively. There are dozens of alphabets in use today, the most common being Latin, deriving from the first true alphabet, Greek. Most of them are composed of lines (linear writing); notable exceptions are Braille, finger spelling, and Morse code.



Kama hujanielewa naomba uliza, si rahisi wengine kulielewa darsa, kwa wengine ni rahisi kulielewa darasa.
Darsa au darasa?
 
Jasusi,

Ndugu yangu ni shida sana kupambana na yote niliyosema hapa jamvini kwani hii yako ni ndogo sana tena sana. Mimi nakuomba wewe na wanaukumbi wenzetu watafakari na haya hapa chini:

Geofrey Sawaya alipewa ruksa na nani kuzunguka Tanzania Bara yote na mifuko ya fedha kuhonga vibaraka kuunga mkono BAKWATA? Mzee Bilal Rehani Waikela mmoja wa viongozi wa EAMWS yu hai yuko Tabora atakae kujua mengi na akamuulize yeye alikataa hongo hiyo. Soma hapa chini:
"Sikuchache baada ya tukio hili Waikela aliitwa na Mkurugenzi wa Upelelezi wa Jinaikusailiwa kwa nini anaipinga BAKWATA. Wakiwa ndani ya chumba cha Tabora Hotel,Geoffrey Sawaya, Mkrugenzi wa C.I.D, alimpiga maswali Waikela na kutaka kujuakwa nini yeye hayuko tayari kushirikiana na serikali kuipa nguvu na kuienezaBAKWATA. Sawaya akatoa hongo ya shilingi elfu arobaini kwa Waikela ili asaidiekuimarisha BAKWATA. Waikela kama istizai alimuuliza Sawaya kama fedha zilezilikuwa zimetoka "bait mal." Waikela alikataa kupokea hongo ile. Sawayaakamtisha lakini Waikela hakutishika. Waikela aliwekwa ndani ya chumba kileakiulizwa maswali kwa kiasi cha saa nne na kisha akaamrishwa kuweka sahihi yakekatika makaratasi fulani. Hili alilifanya. Waikela hakufuatwa tena na serikali.Ingawa kulikuwepo na juhudi za chinichini za kuipinga BAKWATA, juhudi hizihazikushinda kwa kuwa BAKWATA iliweza kufungua matawi yake nchi nzima pamoja naTabora. Wapo baadhi ya viongozi ambao hawakuweza kuhimili vishawishi vyakupokea ile hongo ya serikali na kwa ajili hii walishirikiana na serikali hivyokuwezesha ofisi za BAKWATA kufunguliwa, hata kama zipo pale kwa jina tu."

Marehemu Rashid Kayugwa wa Usalama wa Taifa alipewa ruksa na nani kuwa mshauri wa kundi lililokuwa linashirikiana na Nyerere katika kuvunja EAMWS:

"RashidKayugwa Afisa wa Usalama Taifa, Dar es Salaam ndiye aliyepewa kazi ya kudumishamawasiliano kati ya kundi la Adam Nasibu serikali. Kayugwa ndiye aliyekuwaakielekeza kundi la Adam Nasibu mbinu za propaganda na nini kifanyike na kwawakati gani ili kuvunja umoja wa Waislam. Kayugwa alikuwa amepata mafunzo yakeya ukachero Israel, Checkoslovakia na Marekani. Katika kuhakikisha mafanikio yamkutano wa Iringa, Kayugwa ambae ni mzaliwa wa Iringa alipendekeza mkutano waWaislam wa Taifa ufanyike Iringa kwa kuhofu vurugu na upinzani kutoka kwaWaislam wa Dar es Salaam. Baada ya kusoma kitabu cha Padri John Sivalonkilichoeleza kuwa Kanisa baada ya uhuru liliendesha hujuma dhidi ya Uislam naWaislam kwa kupitia serikali, ndipo ilipomdhihirikia ukweli na kuona kuwaalipokuwa akitumiwa kuhujumu EAMWS hakuwa akitumikia serikali kama alivyokuwaanadhani bali alikuwa akilitumikia Kanisa, kama kuomba maghufira kwa MwenyeziMungu, aliamua kueleza mchango wake katika kuwahujumu Waislam na Uislam ili iwefundisho na onyo kwa Waislam watakao kuwa katika utumishi wa vyombo kama hivyosiku za usoni. Kabla ya kufa kwake alieleza masikitiko yake kwa kukandamizwakwa Waislam na akatoa mfano wake mwenyewe wa kutopandishwa cheo katika Usalamawa Taifa kwa sababu tu yeye alikuwa Muislam."

Mohamed



Mohamed,
Yote hayo nilishayasoma kwenye kitabu chako. Hakuna haja ya kuyarudiarudia hapa. Nimesema Nyerere hakuwa mdini, alikuwa nationalist. Na hilo huwezi kulisuta. Ulichotaka wewe ni kile kilichotokea Kenya ambako Kenyatta na ukoo wake na kabila lake walijiona wao ndio wana haki ya kuwa na lion's share ya national power. Lakini matokeo yake tuliyaona 2007. Wewe ulitaka Waislamu wa Gerezani ndio wawe akina Buhari, Tafawa Balewa (yaani Wahausa) wa Tanzania. Mwalimu alituepusha na hilo na leo kuna level playing field. Hilo huwezi kusuta. Haya mengine yote ni hadidu za rejea tu. Wenye udini ni ninyi mnaojiona kuwa mlinyang'anywa entitlements zenu.
 
Mwalimu hakuwa mkweli alikuwa mnafiki, mchoyo na mbaguzi

Alifanya upendeleo kwa kanisa akifikiri kupata dhawabu kwa Mungu wake (udini)

Ila hakuwa mwizi tu
Hauwezi kuwa mnafiki halafu ukaacha kuwa mwizi. Hizi ni sifa kama pacha wale wa yai moja.
 
Wenzako wanaiona hiyo ndio baadhi ya miujiza ya kumfanya Mwalimu awe MTAKATIFU wewe unadhani ni fedha za msikiti wa Gaddaffi?

Hao "wenzako" wanaoona huo ndio utakatifu sijui kigezo chao. Mimi siamini tetemeko la ardhi liwe ni "utakatifu".
 
1) Utaifishaji wa shule wa Nyerere haukuwa na tija njema yoyote. Umetuongezea ujinga katika hii nchi, leo tazama Uganda na Kenya, jirani zetu wa asili na washirika wetu wa zamani (East African Community) ingawa wao ni wachache kuliko sisi, lakini leo wana wasomi wengi kuliko sisi. Hawa walipopata madaraka hawajataifisha shule.

2) Mwalim kumkabidhi madaraka Ali Hassan Mwinyi ilikuwa kama kudanganya watu, unamkabidhi madaraka halafu unaitisha mkutano na waandishi wa habari unamkemea? huo ndio unafik wa Nyerere. Isitoshe ilikuwa ni kama kumsukumia janga Rais mpya (rejea hotuba ya Mwinyi ya "Mikuki Miwili", alyoitowa Diamond Jubilee kuongea na wazee wa Dar., itakupa picha ya alipokabidhiwa hii nchi ilikuwaje, unamkabidhi nchi mwenzio haina senti tano ya kigeni BOT, haina mafuta, haina mabarabara, unamkabidhi nchi hohehahe hata colgate ni anasa.

Lakini Ali Hassan Mwinyi anastahili kila sifa, katutoa kwenye lindi la umaskini na katufunguwa macho kwa sana tu. Hata TV tulikuwa hatuzijuwi mpaka alipokuja Ali Hassan Mwinyi.

3) Hii ilikuwa ni kupisha tu mambo fulani yafanyike na haina "significance" yoyote.

4) Msikiti hakujenga Mwalim, Msikiti wa Butiama ni fedha ya Gaddafi na umejengwa baada ya kufa Mwalim, yeye alizikalia hizo pesa mpaka anakufa, Maria Nyerere akaona mnhhhh, isije ikawa ndio ule mtetemeko wa ardhi na kaburi kuwaka moto, akaliweka wazi na msikiti ukajengwa.

5) Hata mimi nnakaa na Qur'an na Biblia na huwa nnazisoma zote, licha ya hivyo tu, nnakaa hata na Verda na Upanishads za kihindu na vitabu vingine vingi tu vya imani tofauti hata vya ma Scientologists, ni katika kutafuta ilmu. Nyerere akipenda kusoma, na hili la kukaa na Qur'an na biblia ni kitu cha kawaida kwa msomi yoyote yule, mbaya pale unapovitumia hivi vitabu isivyo na unapozibandika aya zake isivyo kama alivyofanya Mzee Mwanakijiji posts zilizopita, huo unakuwa upotoshaji wa makusudi.
Bi Faiza,
Acha uwongo. Nina hakika dini yako inakataza uwongo. Nilikuwepo Butiama wakati wa mazishi ya Mwalimu, na msikiti ule niliuona ukiwa umeshamalizika kujengwa. Leo unathubutu kuja hapa kuuambia kadamnasi kwamba msikiti ulijengwa na Mama Maria? Staflulaaah! Na hii ndiyo mindset yenu?
 
Mohamed,
Yote hayo nilishayasoma kwenye kitabu chako. Hakuna haja ya kuyarudiarudia hapa. Nimesema Nyerere hakuwa mdini, alikuwa nationalist. Na hilo huwezi kulisuta. Ulichotaka wewe ni kile kilichotokea Kenya ambako Kenyatta na ukoo wake na kabila lake walijiona wao ndio wana haki ya kuwa na lion's share ya national power. Lakini matokeo yake tuliyaona 2007. Wewe ulitaka Waislamu wa Gerezani ndio wawe akina Buhari, Tafawa Balewa (yaani Wahausa) wa Tanzania. Mwalimu alituepusha na hilo na leo kuna level playing field. Hilo huwezi kusuta. Haya mengine yote ni hadidu za rejea tu. Wenye udini ni ninyi mnaojiona kuwa mlinyang'anywa entitlements zenu.

Nyerere hakutuepuesha chochote...

Yeye aliifaidisha kanisa na dini yake above national interest of course intention yake apate dhawabu kwa mungu wake (udini)
 
Bi Faiza,
Acha uwongo. Nina hakika dini yako inakataza uwongo. Nilikuwepo Butiama wakati wa mazishi ya Mwalimu, na msikiti ule niliuona ukiwa umeshamalizika kujengwa. Leo unathubutu kuja hapa kuuambia kadamnasi kwamba msikiti ulijengwa na Mama Maria? Staflulaaah! Na hii ndiyo mindset yenu?

Kama ulikuwepo msikiti basi ni kabla ya kujengwa upya kwa fedha za Gaddafi alizozikalia Nyerere mpaka anakufa. Mama Maria mwenyewe alitangaza kuwa kuna fedha Nyerere alipewa na Gaddafi za kujengea msikiti na utajengwa huko. Kama ni huo umejengwa upya au kuna mwingine umejengwa kwa hizo fedha baada ya kufa Nyerere hilo pia linawezekana. Si sifa yangu kusema uongo na nnauhakika na niyasemayo.
 
Hao "wenzako" wanaoona huo ndio utakatifu sijui kigezo chao. Mimi siamini kuetetemeka kwa ardhi kuwe ni "utakatifu".
Sio "utakatifu" bali muujiza! Mwalimu hakuwa wa kawaida kama mimi na wewe tukibahatika kupewa nafasi alookuwa nayo. Mmekosa cha maana cha kumkosoa mmekimbilia UDINI.
 
Mohamed,
Yote hayo nilishayasoma kwenye kitabu chako. Hakuna haja ya kuyarudiarudia hapa. Nimesema Nyerere hakuwa mdini, alikuwa nationalist. Na hilo huwezi kulisuta. Ulichotaka wewe ni kile kilichotokea Kenya ambako Kenyatta na ukoo wake na kabila lake walijiona wao ndio wana haki ya kuwa na lion's share ya national power. Lakini matokeo yake tuliyaona 2007. Wewe ulitaka Waislamu wa Gerezani ndio wawe akina Buhari, Tafawa Balewa (yaani Wahausa) wa Tanzania. Mwalimu alituepusha na hilo na leo kuna level playing field. Hilo huwezi kusuta. Haya mengine yote ni hadidu za rejea tu. Wenye udini ni ninyi mnaojiona kuwa mlinyang'anywa entitlements zenu.

Jasusi,

Tutakuwa tunarudia humo kwa humo.

Waislam baada ya kuzunguka nchi nzima wakiuelimisha umma kuhusu mfumokristo wametoa kijitabu kinachoonyesha viwango vya mambo mengi kati ya Waislam na Wakristo.

Bahati mbaya mimi sijakipata lakini katika ugawanajiwa madaraka Wakristo wamehodhi 83% na Waislam wamabakiziwa 17%.

Serikali imeombwa itoe maelezo hali hii imekujaje.

Tusubiri majibu.

Mohamed
 
Back
Top Bottom