Historia ya uhuru kama ilivyoandikwa na Ramadhani Makero

Historia ya uhuru kama ilivyoandikwa na Ramadhani Makero

Wanalazimisha tuwatambue wehu wengine waliokuwa wanashinda kwenye bao wakati mwalimu yupo busy kuweka mikakati ya kuikomboa Nchi

Hawa wazee ni kuwaacha tu wanamatatizo mengi
Tatitzo kubwa ni udini umeathiri fahamu zao
Mkuu lazima tukubali kuwa kazi ya kuipigania uhuru hakufanya mwalimu pekee yake kama mdau mmoja alivyoandika japo Mwl alifunga goli la ushindi si vibaya kuwafahamu wachezaji wenzake walioshirikana kutafuta goli/ushindi.
 
Zamani nilikuwa nikizisoma makala za huyu Mzee Mohamed Said ki-ushabiki na nikaona anawatukuza zaidi waislamu wenzake!

Baadae nilipoanza kumuelewa nikaja kufahamu kuwa he knows a lot about our past!

Kuignore mchango wa "wenye majina ya kiislamu" katika ukombozi wa nchi yetu ni kujitia upofu usio na faida.

Ligi za sijui huyu ni Bora kuliko huyu hata hazitujengi zaidi ya kutuvuruga.

Kikubwa wenzetu walipambana, nasi tukapata Uhuru!

Tanzania ni yetu sote wenye dini na wasio na dini, let truth be revealed as nothing poison here.

Binafsi nikushukuru Mzee wetu Mtoi Kwa historia nzuri ya nchi yetu as tunapata Mengi ambayo hatukuyasoma shuleni.

Naupenda Sana na kujifunza kupitia uungwana na unyeyekevu wako!

Ubarikiwe
 
Wanaosoma kitabu chako Ni tayari wana nadharia km zako kichwani

Mimi nimesoma vitabu vingi vya Uhuru lkn siwezi kusoma kitabu chako kwa sababu vimejaa bias
Na kumbuka vitabu vyako sio reference vitabu vyako ni vihadithi vya kuunga unga tu

No one take it for serious
Mikocheni,
Hajalazimishwa mtu chochote.

Nimeandika kitabu cha historia ya TANU watu wamekipenda na sasa tunakwenda toleo la nne.

Wengi mmeguswa na kitabu hiki mnakuja hapa Majlis kukipinga na ndiyo huu mjadala.

Kutokana na hii mijadala kitabu kimepata umaarufu mkubwa na mauzo yameongezeka sana.
 
Mzee Mohamed Said anaweza kuwa alijua , mengi juu ya machache au machache juu ya mengi.. Shida ilipokuja ni pale mtu anapoegemea kwenye angle ya uislam au watu wa pwani zaidi, bila kuonyesha mchango wa watu wa maeneo mengine kwenye uhuru wa Tanganyika. Pengine, watafiti wengine wanaweza wakafanya hayo. Kwa sababu Tanganyika ilikuwa kubwa, lazima kuna watu wana michango ya aina mbalimbali.. Ni kama sasa hivi kufikiri maendeleo ya Tanzania yanatokana na mikoa fulani au watu fulani pekee. Safari ya ufahamu bado ndefu.
 
Ngongo,
Si kama watu wanaandika historia hizi ambazo hazikuwako kwa nia ya kumshusha Mwalimu Nyerere na sijui kwa nini uhisi hivyo, historia hizi zinaandikwa kwa kumamilisha historia ya Mwalimu mwenyewe.

Hakuna atakaeweza kubisha kuwa mchango wa Nyerere ulikuwa mkubwa na ikiwa yeyote awaye yule ataandika historia ya TANU na uhuru wa Tanganyika kwa nia ya kumdogosha kalamu yake haitafika popote pale.

Badala ya kuchukia kwa nini zinaandikwa historia za wazalendo wengine kama hii ya Ally Sykes iliyoandikwa na ndugu yetu Ramadhani ni wajibu wetu sisi kutia hima kila mwenye uwezo wa kutafiti na kuandika historia kama hizi akafanya hivyo.
Mwalimu ndo' mzalendo no 1 wa Taifa hili.Hakuna mwengine wa kuchukua hiyo no,baada ya yeye ndo wanafuata wengine.
 
Pascal,
Hili la ufadhili mkuu si rahisi kulieleza kwa uhakika na kusema kuwa fulani alimzidi mwenzake katika kuchangia.

Wafadhili wa TANU pale New New Street walikuwa John Rupia, Dossa Aziz Abdul na Ally Sykes na kila mtu alitoa kwa nafasi yake na kwa njia nyingi tofauti.

Kutajwa katika ufadhili kunategemea na kile kilichotolewa kwa wakati gani na kilikuwaje cha kuonekana au cha faragha.

Dossa Aziz alitoa gari nzima kuipa TANU kwa matumizi ya Mwalimu Nyerere.

Abdul Sykes nyumba yake ndiyo ilikuwa kama ofisi ya pili ya TANU kwa shughuli nyingi za chama na kwa ajili hii saa 24 watu wakiingia na wageni wakifikia kwake kutoka sehemu tofauti za Tanganyika kuanzia machifu hadi watu wa kawaida na wengine ilibidi wakae kwake.

Nyumbani kwa Abdul Sykes, Mzee Abdallah aliyekuwa mhudumu wa ofisi ya Abdul Kariakoo Market anasema kuna nyakati alikuwa anachinja hadi kuku 20 kwa siku kupeleka nyumbani kwa Abdul kwa ajili ya kitoweo.

Dossa Aziz yeye alikuwa akitoa matumizi ya siku kwa siku ya ofisi ya TANU na yeye na Mzee Rupia, Abdul na Ally ndiye pia wakilipa bili zote za chakula na vinywaji katika kila shughuli ya TANU kwa siku za mwanzo hadi walipokuja kusaidiwa na Baraza la Wazee wa TANU mfadhili mkubwa akiwa Mshume Kiyate.

Si rahisi kusema fulani yeye alitoa zaidi ya fulani kwa kuwa wafadhili wa TANU wote walisaidiana.

Iko siku In Shaa Allah nitaeleza kisa cha ''sanduku la fedha la Bwana Abdul'' kama nilivyoelezwa na mkewe mama yetu Bi. Mwamvua.

Historia ya TANU ina mengi sana.
Pindisha maneno,refusha...Mfadhili mkuu wa TANU ni John Rupia,huo ni ukweli utasimama mpaka kiama unaochoma nyoyo yako kwasababu ya jina lake na dini yake.
 
Niliposoma tu hili bandiko nikawa namwona mzee wangu Mohamed Said, na nilijua tu atatokea sio muda.... shukrani pia mtangulizi Sky Eclat heshima kwenu mzidi kutufunza na kutukumbusha.
 
Sasa maandishi ya soga hutaki kupingwa?huo umekuwa 'msahafu'?
Mikocheni,
Hajalazimishwa mtu chochote.

Nimeandika kitabu cha historia ya TANU watu wamekipenda na sasa tunakwenda toleo la nne.

Wengi mmeguswa na kitabu hiki mnakuja hapa Majlis kukipinga na ndiyo huu mjadala.

Kutokana na hii mijadala kitabu kimepata umaarufu mkubwa na mauzo yameongezeka sana.
 
Nafurahi sana ninaposoma historia halisi kuliko hizi tunazolazimishiwa.
 
Zamani nilikuwa nikizisoma makala za huyu Mzee Mohamed Said ki-ushabiki na nikaona anawatukuza zaidi waislamu wenzake!

Baadae nilipoanza kumuelewa nikaja kufahamu kuwa he knows a lot about our past!

Kuignore mchango wa "wenye majina ya kiislamu" katika ukombozi wa nchi yetu ni kujitia upofu usio na faida.

Ligi za sijui huyu ni Bora kuliko huyu hata hazitujengi zaidi ya kutuvuruga.

Kikubwa wenzetu walipambana, nasi tukapata Uhuru!

Tanzania ni yetu sote wenye dini na wasio na dini, let truth be revealed as nothing poison here.

Binafsi nikushukuru Mzee wetu Mtoi Kwa historia nzuri ya nchi yetu as tunapata Mengi ambayo hatukuyasoma shuleni.

Naupenda Sana na kujifunza kupitia uungwana na unyeyekevu wako!

Ubarikiwe
nilitaka sema nami mda si mrefu huu uzi watu watauchafua...
 
Pindisha maneno,refusha...Mfadhili mkuu wa TANU ni John Rupia,huo ni ukweli utasimama mpaka kiama unaochoma nyoyo yako kwasababu ya jina lake na dini yake.
Lukubuzo,
Mimi nimechangia tu kwa kile nikijuacho una uhuru na haki ya kuamini utakavyo.
 
Mzee Mohamed Said anaweza kuwa alijua , mengi juu ya machache au machache juu ya mengi.. Shida ilipokuja ni pale mtu anapoegemea kwenye angle ya uislam au watu wa pwani zaidi, bila kuonyesha mchango wa watu wa maeneo mengine kwenye uhuru wa Tanganyika. Pengine, watafiti wengine wanaweza wakafanya hayo. Kwa sababu Tanganyika ilikuwa kubwa, lazima kuna watu wana michango ya aina mbalimbali.. Ni kama sasa hivi kufikiri maendeleo ya Tanzania yanatokana na mikoa fulani au watu fulani pekee. Safari ya ufahamu bado ndefu.
Japokua ni kweli ila kama Mzee Mohamed Said asingekua na uthubutu wa kusema hayo michango ya hawa watu ingekua imefutika kabisa katika historia.
 
Mzee Mohamed Said anaweza kuwa alijua , mengi juu ya machache au machache juu ya mengi.. Shida ilipokuja ni pale mtu anapoegemea kwenye angle ya uislam au watu wa pwani zaidi, bila kuonyesha mchango wa watu wa maeneo mengine kwenye uhuru wa Tanganyika. Pengine, watafiti wengine wanaweza wakafanya hayo. Kwa sababu Tanganyika ilikuwa kubwa, lazima kuna watu wana michango ya aina mbalimbali.. Ni kama sasa hivi kufikiri maendeleo ya Tanzania yanatokana na mikoa fulani au watu fulani pekee. Safari ya ufahamu bado ndefu.
Newazz,
Hayo usemayo yote yamo kwenye kitabu cha Abdul Sykes.

Mtafute kitabu umsome Mama bint Maalim, Bi. Halima Selengia, Yusuf Olotu hawa kutoka Moshi.

Umsome Yusuf Chembela, Salum Mpunga, Bi.Sharifa bint Mzee na Sheikh Yusuf Badi wa Lindi.

Umsome Haruna Taratibu na Omari Suleiman kutoka Dodoma.

Usiingie katika mjadala bila kuwa na uelewa wa kinachojadiliwa.
 
Back
Top Bottom