Historia ya uhuru kama ilivyoandikwa na Ramadhani Makero

Historia ya uhuru kama ilivyoandikwa na Ramadhani Makero

Wanaosoma kitabu chako Ni tayari wana nadharia km zako kichwani

Mimi nimesoma vitabu vingi vya Uhuru lkn siwezi kusoma kitabu chako kwa sababu vimejaa bias
Na kumbuka vitabu vyako sio reference vitabu vyako ni vihadithi vya kuunga unga tu

No one take it for serious

NIMEELEWA KWA NINI UMELALAMIKA KILA UKIANZISHA UZI WAKO MOD WANAUUNGANISHA COZ INAONEKANA YOUR PATHETIC
 
Pascal,
Hili la ufadhili mkuu si rahisi kulieleza kwa uhakika na kusema kuwa fulani alimzidi mwenzake katika kuchangia.

Wafadhili wa TANU pale New New Street walikuwa John Rupia, Dossa Aziz Abdul na Ally Sykes na kila mtu alitoa kwa nafasi yake na kwa njia nyingi tofauti.

Kutajwa katika ufadhili kunategemea na kile kilichotolewa kwa wakati gani na kilikuwaje cha kuonekana au cha faragha.

Dossa Aziz alitoa gari nzima kuipa TANU kwa matumizi ya Mwalimu Nyerere.

Abdul Sykes nyumba yake ndiyo ilikuwa kama ofisi ya pili ya TANU kwa shughuli nyingi za chama na kwa ajili hii saa 24 watu wakiingia na wageni wakifikia kwake kutoka sehemu tofauti za Tanganyika kuanzia machifu hadi watu wa kawaida na wengine ilibidi wakae kwake.

Nyumbani kwa Abdul Sykes, Mzee Abdallah aliyekuwa mhudumu wa ofisi ya Abdul Kariakoo Market anasema kuna nyakati alikuwa anachinja hadi kuku 20 kwa siku kupeleka nyumbani kwa Abdul kwa ajili ya kitoweo.

Dossa Aziz yeye alikuwa akitoa matumizi ya siku kwa siku ya ofisi ya TANU na yeye na Mzee Rupia, Abdul na Ally ndiye pia wakilipa bili zote za chakula na vinywaji katika kila shughuli ya TANU kwa siku za mwanzo hadi walipokuja kusaidiwa na Baraza la Wazee wa TANU mfadhili mkubwa akiwa Mshume Kiyate.

Si rahisi kusema fulani yeye alitoa zaidi ya fulani kwa kuwa wafadhili wa TANU wote walisaidiana.

Iko siku In Shaa Allah nitaeleza kisa cha ''sanduku la fedha la Bwana Abdul'' kama nilivyoelezwa na mkewe mama yetu Bi. Mwamvua.

Historia ya TANU ina mengi sana.
shukrani kwa historia hii nzuri
 
Pascal,
Hili la ufadhili mkuu si rahisi kulieleza kwa uhakika na kusema kuwa fulani alimzidi mwenzake katika kuchangia.

Wafadhili wa TANU pale New New Street walikuwa John Rupia, Dossa Aziz Abdul na Ally Sykes na kila mtu alitoa kwa nafasi yake na kwa njia nyingi tofauti.

Kutajwa katika ufadhili kunategemea na kile kilichotolewa kwa wakati gani na kilikuwaje cha kuonekana au cha faragha.

Dossa Aziz alitoa gari nzima kuipa TANU kwa matumizi ya Mwalimu Nyerere.

Abdul Sykes nyumba yake ndiyo ilikuwa kama ofisi ya pili ya TANU kwa shughuli nyingi za chama na kwa ajili hii saa 24 watu wakiingia na wageni wakifikia kwake kutoka sehemu tofauti za Tanganyika kuanzia machifu hadi watu wa kawaida na wengine ilibidi wakae kwake.

Nyumbani kwa Abdul Sykes, Mzee Abdallah aliyekuwa mhudumu wa ofisi ya Abdul Kariakoo Market anasema kuna nyakati alikuwa anachinja hadi kuku 20 kwa siku kupeleka nyumbani kwa Abdul kwa ajili ya kitoweo.

Dossa Aziz yeye alikuwa akitoa matumizi ya siku kwa siku ya ofisi ya TANU na yeye na Mzee Rupia, Abdul na Ally ndiye pia wakilipa bili zote za chakula na vinywaji katika kila shughuli ya TANU kwa siku za mwanzo hadi walipokuja kusaidiwa na Baraza la Wazee wa TANU mfadhili mkubwa akiwa Mshume Kiyate.

Si rahisi kusema fulani yeye alitoa zaidi ya fulani kwa kuwa wafadhili wa TANU wote walisaidiana.

Iko siku In Shaa Allah nitaeleza kisa cha ''sanduku la fedha la Bwana Abdul'' kama nilivyoelezwa na mkewe mama yetu Bi. Mwamvua.

Historia ya TANU ina mengi sana.
naomba anipe habari kidogo kuhusu Aziz Ally,hasa utajiri wake
 
Ngongo,
Si kama watu wanaandika historia hizi ambazo hazikuwako kwa nia ya kumshusha Mwalimu Nyerere na sijui kwa nini uhisi hivyo, historia hizi zinaandikwa kwa kumamilisha historia ya Mwalimu mwenyewe.

Hakuna atakaeweza kubisha kuwa mchango wa Nyerere ulikuwa mkubwa na ikiwa yeyote awaye yule ataandika historia ya TANU na uhuru wa Tanganyika kwa nia ya kumdogosha kalamu yake haitafika popote pale.

Badala ya kuchukia kwa nini zinaandikwa historia za wazalendo wengine kama hii ya Ally Sykes iliyoandikwa na ndugu yetu Ramadhani ni wajibu wetu sisi kutia hima kila mwenye uwezo wa kutafiti na kuandika historia kama hizi akafanya hivyo.
kwenye Siku hizi huoni! kama FaizaFoxy husema shuleni mmesomea nini vile!?
 
Historia hiyo ni (taboo) kwa watu wa aina ya paschal mayalla inawauma sana kwani hawana cha kuhadithia cha wazee wao katika harakati za uhuru.

Hao wamekuta watu wamexhagua mchele wakaengua chuya wakatayarisha nyama wakasafisha viungo wakaandaa kuni, shaba na karamu ikaandaliwa. Wakatandikiwa wakala sasa wameshiba badala ya kusifia wapishi wanajisifia wao kuwa, aah pilau tumeikomesha. Hawana kheri hao ni kama punda tu ambao fadhila yao ni mateke.

Sifahamu kinachowauma ni nini? Kutajwa hao wazee waliokuwa mstari wa mbele kwenye harakati za Uhuru au Uislam wao?

Huyo paschal mayalla mwenyewe bila ukarimu wa Waislam wa Dar. Asingekuwa hapo alipo.

Labda awe amewasahau kina Abdallah Jabir na Shariff Mehboub Al Haddad na kina Alioki waliomtoa tongotongo za ushamba.
Faiza naomba maelezo kidogo kuhusu yule sheikh binamiri,sijajua jina lake spelling zake
 
Mikocheni,
Hajalazimishwa mtu chochote.

Nimeandika kitabu cha historia ya TANU watu wamekipenda na sasa tunakwenda toleo la nne.

Wengi mmeguswa na kitabu hiki mnakuja hapa Majlis kukipinga na ndiyo huu mjadala.

Kutokana na hii mijadala kitabu kimepata umaarufu mkubwa na mauzo yameongezeka sana.
Kwahiyo unapata pesa kwa upotoshaji?
 
Newazz,
Ndiyo historia ya TANU ilivyokuwa si kama mimi nimeitengeneza iwe hivyo.

La unadhani kuwa mimi nimeandika uongo fanya utafiti hata mdogo katika mikoa na uje na majibu.

Najua inawachoma wengi historia hii maana naona jinsi Majlis ilivyogeuka na watu sasa wananitukana.

Ukweli ni kuwa baada ya kuchapwa kitabu changu London (1998) publisher akakitangaza kwingi katika vyuo Ulaya na Marekani na hakika kitabu kimebadili historia nzima ya uhuru wa Tanganyika.

Kitabu hiki kikasababisha mimi kutiwa kwenye miradi miwili ya kuandika historia.

Mradi wa kwanza ulikuwa wa Oxford University Press, Nairobi na wa pili wa Harvard na Oxford University Press, New York.

Miradi yote hii imekamilika na vitabu vimechapwa na vinasomeshwa.

Nakumbuka katika mhadhara niliofanya Northwestern University, Chicago kuhusu Abdul Sykes na wazalendo wengine ambao historia zao zilikuwa zimefutika Mkuu wa Idara ya Historia ya Afrika Jonathon Glassman ambae ndiye aliyenialika, katika kutoa neno la shukurani mwisho wa mhadhara alisema kuwa hawakujua kuwa uhuru wa Tanganyika na Nyerere kuwa kiongozi kulichangiwa sana na wazalendo kama Hamza Mwapachu, Abdul Sykes, Sheikh Hassan bin Ameir na kuungwa mkono na Waislam.

Kwa kuwa ghadhabu ziko juu na siwezi kujibu matusi nimeacha kufanya majadiliano na hawa walioghadhibika kama njia ya kuepusha shari nitaendelea na wale ambao wana hamu ya kujifunza historia hii ambayo haikuwapo kabla.

View attachment 1197667
Northwestern University, Evanston Chicago
nice
 
Kwahiyo unapata pesa kwa upotoshaji?
Duduwasha,
Hapana ingekuwa nimeandika kitabu chenye makosa nisingeweza kutiwa katika miradi hiyo ya Oxford na Harvard na kitabu kingekufa zamani sana.

Ikiwa wewe unaona kuna upotoshaji nifahamishe kile nilichopotosha.
 
Hawa wazee kumbe walikuwa wakizungukana pia wao kwa wao? Ila unaposema baada ya uhuru hawa wasaliti waliachwa kufanya kazi na wale waliokuwa wanawahujumu inashangaza pia.
Proved,
Nilikuwa kila ninapozungumza na Ally Sykes alikuwa heshi kumlaumu Mwalimu Nyerere kwa kutowafukuza kazi.

Nadhani Mwalimu aliwabakisha hawa kazini kwa ajili ya ujuzi ambao waliokuwanao katika kazi za kikachero.

Ally Sykes adui yake mkubwa alikuwa Amiri Kweyamba, kijana wa Kihaya ambae alimwandama sana.

Soma mkasa huu:

Nitaeleza yale ninayoyajua na kutokana na kauli ya mwenyewe Ally Sykes
kuhusu makachero wa wakoloni ambao waliwahangaisha sana wapigania
uhuru.

Jina Amiri Kweyamba lilikuwa sana katika ulimi wa Ally Sykes na kuna kisa
alinihadithia akiwa pamoja na mkewe mama yetu Bi. Zainab.

Miezi michache kabla ya kuundwa kwa TANU Ally Sykes alikuwa akichapa
makaratasi ya uchochezi ambayo hayakuwa na nembo ya TAA yaliyokuwa
yameandikwa kwa kuanza na ujumbe huu: ''Kwa Waafrika Wote.''

Ally Sykes alikuwa na ''cyclostyle machine,'' ambayo alikuwa ameificha
nyumbani kwake Mtaa wa Kipata.

Ally Sykes alikuwa akishayachapa alikuwa anawapa wafanyakazi maalum
wa treni na hawa walikuwa wakiyagawa kwa watu maalum katika stesheni
za treni katika Reli ya Kati na ka njia hii makaratasi yake yaliweza kufika hadi
Kigoma na Mwanza.

Makaratasi haya yalifika mikononi mwa Special Branch na yakawa wanayatafuta
na hapo ndipo siku moja wakaingiliwa nyumbani na Amir Kweyamba kuja
kufanyiwa upekuzi.

Mlango ulipogongwa Ally Sykes alikuwa mitamboni anachapa na Bi. Zainab
alipomfahamsiha kuwa Kweyamba yuko mlangoni ikawa heka heka na Ally Sykes
anasema aliweza kwa haraka sana kuyachukua makaratasi na kuyatumbukiza
chooni na mashine ikarushwa ua kwa ua na Kweyamba na askari wake walipoingia
ndani hapakuwa na kitu.

Nyumba za Dar es Salaam zamani zilikuwa na ua na mtu alikuwa anaweza kupita ua
kwa ua hata nyumba kumi bila kutoka barabarani.

Huyu Kweyamba aliwahangaisha sana wanasiasa lakini kwa ninayoyajua mimi ni
kuwa ingawa Kitwana Kondo alikuwa katika Special Branch lakini yeye hakushiriki
katika operesheni kama hizi za kuvamia majumba ya wapigania uhuru.
 
Wanalazimisha tuwatambue wehu wengine waliokuwa wanashinda kwenye bao wakati mwalimu yupo busy kuweka mikakati ya kuikomboa Nchi

Hawa wazee ni kuwaacha tu wanamatatizo mengi
Tatitzo kubwa ni udini umeathiri fahamu zao


Kauli hii ni ya kishetani kabisa,

Mwalimu nyerere katika moja ya hutuba zake za kung'atuka alipata kusema juu ya mchango wa Waislamu juu harakati za kupigania uhuru, na specifically--- alitaja siku alipoitwa na wazee kwenda usiku kwa mzee Jumbe Tambaza kwa ajili ya kumfanyia "Kafara", akielezea , Nyerere alisema kwamba alipofika akakuta Beberu la mbuzi na Shimo limechimbwa, yule beberu alichinjwa huku damu yake kumiminiwa mle shimoni kisha Nyerere akaambiwa atambuke lile shimo, alipotambuka wale wazee wakasema Twinning amekwisha, sasa nenda zako hakuwezi tena.

Kabla ya nyerere kufanyiwa kafara alifanyiwa dua na baadaye ikaja hiyo kafara.

Baadaye akaelezea jinsi alivyokwenda Bagamoyo kwa Shk Ramia, ambapo walikuwa wakishinda makaburini wakifanya matambiko kwa ajili ya kudai uhuru, na akaeleza kisa kimoja juu ya vita vya maumau, kwamba Shk Ramia akasema inawapasa wafunge saumu kwa ajili ya kuwaombea mashujaa wa Maumau waliofungwa, Nyerere anasema ilipofika muda mchana wa saumu alisikia kichwa kinauma sana na akamuomba shk Aspro (dawa ya zamani ya maumivu), Shk Ramia akamjibu; asubiri, ilipofika muda wa kufuturu, wakafuturu baada ya muda kidogo, shk Ramia akamuuliza Nyerere ; je kichwa bado kinauma??---- Nyerere akajibu hapana, na, anasimulia; kumbe kile kichwa kilikuwa ni sababu ya njaa (saumu).

Nyerere akasema; yeye na wale wazee wake wa kiislamu walitoka mbali sana na walielewana vizuri sana, yeye MKRISTO peke yake na wao waislamu na safari fulani John Rupia aliambatana na nyerere.

🖕🏻Maneno hayo yamo katika moja ya hotuba za Nyerere muda mfupi baada ya kung'atuka alipokuwa akiwaaga wazee wa Dar.

Sasa Nyerere anathamii mchango wa Waislamu katika harakati za uhuru, anatokea mtu na chuki za kidini na wala asiyejua historia na anaanza kukashifu.🤔🤔
 
Faiza naomba maelezo kidogo kuhusu yule sheikh binamiri,sijajua jina lake spelling zake

Hilo la Sheikh Hassan Bin Amir nnamwachia kaka yangu Allama Mohamed Said maana anamfahamu vizuri sana.

Allama nnaomba nisaidie kujibu hilo swali.

Mimi nnakuwekea clip utampata humo akielezewa...

 
Faiza naomba maelezo kidogo kuhusu yule sheikh binamiri,sijajua jina lake spelling zake
Pablo,
Sheikh Hassan bin Ameir.


Ukitaka kumjua zaidi Maalim Faiza kaweka video clip.
Nami nakuongezea hapo chini:

1567625007388.png

Mwisho kulia ni Tewa Said Tewa

 
Pablo,
Sheikh Hassan bin Ameir.


Ukitaka kumjua zaidi Maalim Faiza kaweka video clip.
Nami nakuongezea hapo chini:

View attachment 1198160
Mwisho kulia ni Tewa Said Tewa



Ni historia nzuri ya kisiasa na kidini "iliyofichwa" kuhusu Marhum Shk, Hassan bi Ameir.
Mungu amlaze peponi.

Nimefurahi sana kuona Lugha safi sana ya kiingereza imetumika kuelezea historia hiyo, dunia itajua japo sisi tumefunga macho na masikio. 🤝🏻
 
Ni historia nzuri ya kisiasa na kidini "iliyofichwa" kuhusu Marhum Shk, Hassan bi Ameir.
Mungu amlaze peponi.

Nimefurahi sana kuona Lugha safi sana ya kiingereza imetumika kuelezea historia hiyo, dunia itajua japo sisi tumefunga macho na masikio. 🤝🏻
Mokaze,
Amin.
 
History nzuri tu.kwa watu wa Dar hasa,mitaa ya kariakoo haya majina ni yalikuwa yanasikika sana mpaka miaka ya themanin,wengi walikuwa bado wanaishi nakumbuka kumuona mzee mtemvu kariakoo mtaa wa Narung'ombe,nilipoambiwa huyu ndio alikuwa mwanasiasa TAA nilishangaa alikuwa kachoka kidogo na mkononi kabeba kikapu cha ukindu.Wengi tunakuelewa mkuu.
 
Mohamed Said , unafahamika unajadili kutokea wapi.... Angle moja waislam , hata hao uliowaandika ni mule mule waislam.. Kwani wasio waislam hawakufanya mchango..Hata kma utaweka majina machache bado mwisho wa siku miwani yako ni waislam. Hicho ndio hoja kuu.. Vua miwani hiyo..
Hili haliepukukiki, maana wapiginai na Uhuru wengi walikuwa waislam ,mfano akina mkwawa,kinjekitile, millambo nk
 
Kwa hili la ufadhili nakubaliana na wewe hatuwezi ku quotify kwa kupitia viwango nani alitoa nini, lakini ndani ya wafadhili hao, kulikuwa na mfadhili mkubwa kabisa aliyetoa kitu kikubwa kuliko wote, bila hata kujitaja ni nani, huyu ni Mzee John Rupia, huyu ndie alitoa guarantee kwa Mwalimu kuacha kazi ya mshahara serikalini because he had a guarantee na the guarantor ni Mzee John Rupia.

Kitu ambacho nakubaliana na wewe ni thamani ya huo ufadhili, mfano kwa vile Mzee John Rupia ndio alikuwa tajiri kupita wote (hapa naomba msilete ubishi), thamani ya mchango wake hata akichangia shilingi milioni mia moja kati ya Bilioni moja na yule mama muuza maandazi aliyechangia thumuni kati Shilingi moja yake, yule mama ndio ametoa zaidi.

Kuna wachingiaji wa kuonekanika na invisible donors waliochagia pakubwa in kind kuliko hata nominal values, mfano aliyemfundisha Mama Maria kupika chapati na kuokoa fedha za kitafunio, ametoa mchango mkubwa kuliko yule anayemnunulia mkate.
P
mkuu wewe umesimuliwa na kusoma historia.

huyu mzee kaishi katika hiyo historia.

bila shaka ungerega sikio uzuri mzee akufunze maisha yao waati huo vipi yalikuwa.

tuliza akili hapo akupe habari uzidi kuujaz ubongo zaidi ya hapo.
 
Historia hiyo ni (taboo) kwa watu wa aina ya paschal mayalla inawauma sana kwani hawana cha kuhadithia cha wazee wao katika harakati za uhuru.

Hao wamekuta watu wamechagua mchele wakaengua chuya wakatayarisha nyama wakasafisha viungo wakaandaa kuni, shaba na karamu ikaandaliwa. Wakatandikiwa wakala sasa wameshiba badala ya kusifia wapishi wanajisifia wao kuwa, aah pilau tumeikomesha.

Hawana kheri hao, ni kama punda tu ambao fadhila yao ni mateke.

Sifahamu kinachowauma ni nini? Kutajwa hao wazee waliokuwa mstari wa mbele kwenye harakati za Uhuru au Uislam wao?

Huyo paschal mayalla mwenyewe bila ukarimu wa Waislam wa Dar. Asingekuwa hapo alipo.

Labda awe amewasahau kina Abdallah Jabir na Shariff Mehboub Al Haddad na kina Alioki waliomtoa tongotongo za ushamba.
aisee pascal mayalla hata nikimuangalia namuona kabisa ni mtupu katika mambo ya historia zetu kwani anaonekana ni mtu msomi wa historia kuliko uhalisia.
 
Back
Top Bottom