Fedor von Bock
JF-Expert Member
- Apr 16, 2015
- 2,321
- 2,157
Wanaosoma kitabu chako Ni tayari wana nadharia km zako kichwani
Mimi nimesoma vitabu vingi vya Uhuru lkn siwezi kusoma kitabu chako kwa sababu vimejaa bias
Na kumbuka vitabu vyako sio reference vitabu vyako ni vihadithi vya kuunga unga tu
No one take it for serious
shukrani kwa historia hii nzuriPascal,
Hili la ufadhili mkuu si rahisi kulieleza kwa uhakika na kusema kuwa fulani alimzidi mwenzake katika kuchangia.
Wafadhili wa TANU pale New New Street walikuwa John Rupia, Dossa Aziz Abdul na Ally Sykes na kila mtu alitoa kwa nafasi yake na kwa njia nyingi tofauti.
Kutajwa katika ufadhili kunategemea na kile kilichotolewa kwa wakati gani na kilikuwaje cha kuonekana au cha faragha.
Dossa Aziz alitoa gari nzima kuipa TANU kwa matumizi ya Mwalimu Nyerere.
Abdul Sykes nyumba yake ndiyo ilikuwa kama ofisi ya pili ya TANU kwa shughuli nyingi za chama na kwa ajili hii saa 24 watu wakiingia na wageni wakifikia kwake kutoka sehemu tofauti za Tanganyika kuanzia machifu hadi watu wa kawaida na wengine ilibidi wakae kwake.
Nyumbani kwa Abdul Sykes, Mzee Abdallah aliyekuwa mhudumu wa ofisi ya Abdul Kariakoo Market anasema kuna nyakati alikuwa anachinja hadi kuku 20 kwa siku kupeleka nyumbani kwa Abdul kwa ajili ya kitoweo.
Dossa Aziz yeye alikuwa akitoa matumizi ya siku kwa siku ya ofisi ya TANU na yeye na Mzee Rupia, Abdul na Ally ndiye pia wakilipa bili zote za chakula na vinywaji katika kila shughuli ya TANU kwa siku za mwanzo hadi walipokuja kusaidiwa na Baraza la Wazee wa TANU mfadhili mkubwa akiwa Mshume Kiyate.
Si rahisi kusema fulani yeye alitoa zaidi ya fulani kwa kuwa wafadhili wa TANU wote walisaidiana.
Iko siku In Shaa Allah nitaeleza kisa cha ''sanduku la fedha la Bwana Abdul'' kama nilivyoelezwa na mkewe mama yetu Bi. Mwamvua.
Historia ya TANU ina mengi sana.
naomba anipe habari kidogo kuhusu Aziz Ally,hasa utajiri wakePascal,
Hili la ufadhili mkuu si rahisi kulieleza kwa uhakika na kusema kuwa fulani alimzidi mwenzake katika kuchangia.
Wafadhili wa TANU pale New New Street walikuwa John Rupia, Dossa Aziz Abdul na Ally Sykes na kila mtu alitoa kwa nafasi yake na kwa njia nyingi tofauti.
Kutajwa katika ufadhili kunategemea na kile kilichotolewa kwa wakati gani na kilikuwaje cha kuonekana au cha faragha.
Dossa Aziz alitoa gari nzima kuipa TANU kwa matumizi ya Mwalimu Nyerere.
Abdul Sykes nyumba yake ndiyo ilikuwa kama ofisi ya pili ya TANU kwa shughuli nyingi za chama na kwa ajili hii saa 24 watu wakiingia na wageni wakifikia kwake kutoka sehemu tofauti za Tanganyika kuanzia machifu hadi watu wa kawaida na wengine ilibidi wakae kwake.
Nyumbani kwa Abdul Sykes, Mzee Abdallah aliyekuwa mhudumu wa ofisi ya Abdul Kariakoo Market anasema kuna nyakati alikuwa anachinja hadi kuku 20 kwa siku kupeleka nyumbani kwa Abdul kwa ajili ya kitoweo.
Dossa Aziz yeye alikuwa akitoa matumizi ya siku kwa siku ya ofisi ya TANU na yeye na Mzee Rupia, Abdul na Ally ndiye pia wakilipa bili zote za chakula na vinywaji katika kila shughuli ya TANU kwa siku za mwanzo hadi walipokuja kusaidiwa na Baraza la Wazee wa TANU mfadhili mkubwa akiwa Mshume Kiyate.
Si rahisi kusema fulani yeye alitoa zaidi ya fulani kwa kuwa wafadhili wa TANU wote walisaidiana.
Iko siku In Shaa Allah nitaeleza kisa cha ''sanduku la fedha la Bwana Abdul'' kama nilivyoelezwa na mkewe mama yetu Bi. Mwamvua.
Historia ya TANU ina mengi sana.
ila kumbuka azizi ally ndiye aliyekuwa tajiri zaidiPindisha maneno,refusha...Mfadhili mkuu wa TANU ni John Rupia,huo ni ukweli utasimama mpaka kiama unaochoma nyoyo yako kwasababu ya jina lake na dini yake.
kwenye Siku hizi huoni! kama FaizaFoxy husema shuleni mmesomea nini vile!?Ngongo,
Si kama watu wanaandika historia hizi ambazo hazikuwako kwa nia ya kumshusha Mwalimu Nyerere na sijui kwa nini uhisi hivyo, historia hizi zinaandikwa kwa kumamilisha historia ya Mwalimu mwenyewe.
Hakuna atakaeweza kubisha kuwa mchango wa Nyerere ulikuwa mkubwa na ikiwa yeyote awaye yule ataandika historia ya TANU na uhuru wa Tanganyika kwa nia ya kumdogosha kalamu yake haitafika popote pale.
Badala ya kuchukia kwa nini zinaandikwa historia za wazalendo wengine kama hii ya Ally Sykes iliyoandikwa na ndugu yetu Ramadhani ni wajibu wetu sisi kutia hima kila mwenye uwezo wa kutafiti na kuandika historia kama hizi akafanya hivyo.
Faiza naomba maelezo kidogo kuhusu yule sheikh binamiri,sijajua jina lake spelling zakeHistoria hiyo ni (taboo) kwa watu wa aina ya paschal mayalla inawauma sana kwani hawana cha kuhadithia cha wazee wao katika harakati za uhuru.
Hao wamekuta watu wamexhagua mchele wakaengua chuya wakatayarisha nyama wakasafisha viungo wakaandaa kuni, shaba na karamu ikaandaliwa. Wakatandikiwa wakala sasa wameshiba badala ya kusifia wapishi wanajisifia wao kuwa, aah pilau tumeikomesha. Hawana kheri hao ni kama punda tu ambao fadhila yao ni mateke.
Sifahamu kinachowauma ni nini? Kutajwa hao wazee waliokuwa mstari wa mbele kwenye harakati za Uhuru au Uislam wao?
Huyo paschal mayalla mwenyewe bila ukarimu wa Waislam wa Dar. Asingekuwa hapo alipo.
Labda awe amewasahau kina Abdallah Jabir na Shariff Mehboub Al Haddad na kina Alioki waliomtoa tongotongo za ushamba.
Kwahiyo unapata pesa kwa upotoshaji?Mikocheni,
Hajalazimishwa mtu chochote.
Nimeandika kitabu cha historia ya TANU watu wamekipenda na sasa tunakwenda toleo la nne.
Wengi mmeguswa na kitabu hiki mnakuja hapa Majlis kukipinga na ndiyo huu mjadala.
Kutokana na hii mijadala kitabu kimepata umaarufu mkubwa na mauzo yameongezeka sana.
niceNewazz,
Ndiyo historia ya TANU ilivyokuwa si kama mimi nimeitengeneza iwe hivyo.
La unadhani kuwa mimi nimeandika uongo fanya utafiti hata mdogo katika mikoa na uje na majibu.
Najua inawachoma wengi historia hii maana naona jinsi Majlis ilivyogeuka na watu sasa wananitukana.
Ukweli ni kuwa baada ya kuchapwa kitabu changu London (1998) publisher akakitangaza kwingi katika vyuo Ulaya na Marekani na hakika kitabu kimebadili historia nzima ya uhuru wa Tanganyika.
Kitabu hiki kikasababisha mimi kutiwa kwenye miradi miwili ya kuandika historia.
Mradi wa kwanza ulikuwa wa Oxford University Press, Nairobi na wa pili wa Harvard na Oxford University Press, New York.
Miradi yote hii imekamilika na vitabu vimechapwa na vinasomeshwa.
Nakumbuka katika mhadhara niliofanya Northwestern University, Chicago kuhusu Abdul Sykes na wazalendo wengine ambao historia zao zilikuwa zimefutika Mkuu wa Idara ya Historia ya Afrika Jonathon Glassman ambae ndiye aliyenialika, katika kutoa neno la shukurani mwisho wa mhadhara alisema kuwa hawakujua kuwa uhuru wa Tanganyika na Nyerere kuwa kiongozi kulichangiwa sana na wazalendo kama Hamza Mwapachu, Abdul Sykes, Sheikh Hassan bin Ameir na kuungwa mkono na Waislam.
Kwa kuwa ghadhabu ziko juu na siwezi kujibu matusi nimeacha kufanya majadiliano na hawa walioghadhibika kama njia ya kuepusha shari nitaendelea na wale ambao wana hamu ya kujifunza historia hii ambayo haikuwapo kabla.
Duduwasha,Kwahiyo unapata pesa kwa upotoshaji?
Proved,Hawa wazee kumbe walikuwa wakizungukana pia wao kwa wao? Ila unaposema baada ya uhuru hawa wasaliti waliachwa kufanya kazi na wale waliokuwa wanawahujumu inashangaza pia.
Wanalazimisha tuwatambue wehu wengine waliokuwa wanashinda kwenye bao wakati mwalimu yupo busy kuweka mikakati ya kuikomboa Nchi
Hawa wazee ni kuwaacha tu wanamatatizo mengi
Tatitzo kubwa ni udini umeathiri fahamu zao
Faiza naomba maelezo kidogo kuhusu yule sheikh binamiri,sijajua jina lake spelling zake
Pablo,Faiza naomba maelezo kidogo kuhusu yule sheikh binamiri,sijajua jina lake spelling zake
shukrani mama la mama FaizaHilo la Sheikh Hassan Bin Amir nnamwachia kaka yangu Allama Mohamed Said maana anamfahamu vizuri sana.
Allama nnaomba nisaidie kujibu hilo swali.
Mimi nnakuwekea clip utampata humo akielezewa...
Pablo,
Sheikh Hassan bin Ameir.
Ukitaka kumjua zaidi Maalim Faiza kaweka video clip.
Nami nakuongezea hapo chini:
MUFTI SHEIKH HASSAN BIN AMEIR (1880 - 1979)
Seminar on The Role of Educated Youth to Muslim Society 27 th February β 4 th March 2004 ORGANISED BY ZANZIBAR UNIVERS...mohamedsaidsalum.blogspot.com
Mokaze,Ni historia nzuri ya kisiasa na kidini "iliyofichwa" kuhusu Marhum Shk, Hassan bi Ameir.
Mungu amlaze peponi.
Nimefurahi sana kuona Lugha safi sana ya kiingereza imetumika kuelezea historia hiyo, dunia itajua japo sisi tumefunga macho na masikio. π€π»
Hili haliepukukiki, maana wapiginai na Uhuru wengi walikuwa waislam ,mfano akina mkwawa,kinjekitile, millambo nkMohamed Said , unafahamika unajadili kutokea wapi.... Angle moja waislam , hata hao uliowaandika ni mule mule waislam.. Kwani wasio waislam hawakufanya mchango..Hata kma utaweka majina machache bado mwisho wa siku miwani yako ni waislam. Hicho ndio hoja kuu.. Vua miwani hiyo..
mkuu wewe umesimuliwa na kusoma historia.Kwa hili la ufadhili nakubaliana na wewe hatuwezi ku quotify kwa kupitia viwango nani alitoa nini, lakini ndani ya wafadhili hao, kulikuwa na mfadhili mkubwa kabisa aliyetoa kitu kikubwa kuliko wote, bila hata kujitaja ni nani, huyu ni Mzee John Rupia, huyu ndie alitoa guarantee kwa Mwalimu kuacha kazi ya mshahara serikalini because he had a guarantee na the guarantor ni Mzee John Rupia.
Kitu ambacho nakubaliana na wewe ni thamani ya huo ufadhili, mfano kwa vile Mzee John Rupia ndio alikuwa tajiri kupita wote (hapa naomba msilete ubishi), thamani ya mchango wake hata akichangia shilingi milioni mia moja kati ya Bilioni moja na yule mama muuza maandazi aliyechangia thumuni kati Shilingi moja yake, yule mama ndio ametoa zaidi.
Kuna wachingiaji wa kuonekanika na invisible donors waliochagia pakubwa in kind kuliko hata nominal values, mfano aliyemfundisha Mama Maria kupika chapati na kuokoa fedha za kitafunio, ametoa mchango mkubwa kuliko yule anayemnunulia mkate.
P
aisee pascal mayalla hata nikimuangalia namuona kabisa ni mtupu katika mambo ya historia zetu kwani anaonekana ni mtu msomi wa historia kuliko uhalisia.Historia hiyo ni (taboo) kwa watu wa aina ya paschal mayalla inawauma sana kwani hawana cha kuhadithia cha wazee wao katika harakati za uhuru.
Hao wamekuta watu wamechagua mchele wakaengua chuya wakatayarisha nyama wakasafisha viungo wakaandaa kuni, shaba na karamu ikaandaliwa. Wakatandikiwa wakala sasa wameshiba badala ya kusifia wapishi wanajisifia wao kuwa, aah pilau tumeikomesha.
Hawana kheri hao, ni kama punda tu ambao fadhila yao ni mateke.
Sifahamu kinachowauma ni nini? Kutajwa hao wazee waliokuwa mstari wa mbele kwenye harakati za Uhuru au Uislam wao?
Huyo paschal mayalla mwenyewe bila ukarimu wa Waislam wa Dar. Asingekuwa hapo alipo.
Labda awe amewasahau kina Abdallah Jabir na Shariff Mehboub Al Haddad na kina Alioki waliomtoa tongotongo za ushamba.