Historia ya Wanyakyusa kufahamika zaidi kuliko Wasafwa ambao ni wazawa halisi wa Jiji la Mbeya

Historia ya Wanyakyusa kufahamika zaidi kuliko Wasafwa ambao ni wazawa halisi wa Jiji la Mbeya

NetMaster

JF-Expert Member
Joined
Sep 12, 2022
Posts
1,454
Reaction score
4,925
Yani hii Tanzania ukienda mikoa nje ya Mbeya, ukiuliza jiji la Mbeya linakaliwa na kabila gani, fasta mtu anakujibu wanyakyusa lakini ukweli ni kwamba wasafwa ndio wenyeji wa kihistoria na hata hili jina la Mbeya lina asili ya neno la Kisafwa "Ibheya" ambayo maana yake ni chumvi, kilotokea nini hadi wasafwa wakapoteza utambulisho wao wa kufahamika kuwa wenyeji wa jiji hili ?

ni kwamba nchi ilipopata uhuru, Mbeya jiji ikapewa hadhi ya kuwa makao makuu ya mkoa wa Mbeya, wanyakyusa waliokuwa wilaya za karibu kama Rungwe na Kyela walianza kuja kwenye makao makuu ya kupata huduma za kijamii bora, kusoma, kufanya biashara, n.k.

Muda huo wakazi wa mbeya mjini wengi walikuwa ni wazawa ambao ni wasafwa, shida ikaja kwamba wasafwa wakiona wageni walikuwa hawataki kuchangamana na jamii zingine, ilikuwa ni kwa sababu za kulinda na kuzithamini zaidi tamaduni zao zisiingiliwe na makundi mengine, hivyo walikuwa wakiona kuna wageni wenye tamaduni tofauti, wao wanahamisha makazi kwenda sehem ambayo wapo peke yao. mji ulizidi kupanuka, wanyakyusa na wageni wengi zaidi walifikia Mbeya mjin, hii ilileta usumbufu kwa wasafwa kuhama hama mji unavyozidi kupanuka, ikafikia kipindi wengine wakaanza kukimbilia maeneo ya mbali zaidi milimani. Kwa wakati huu wote wanyakyusa na wageni wengine walifikia muafaka kwamba wasafwa wanahama kwasababu ni waoga, ila kwa uhalisia wasafwa walikuwa wana sababu zao za kitamaduni.

matokeo yake hapa mjini makabila ya ziada yaliyofika kama wanyiha, wandali, wakinga, wahehe, wangoni, wabena, n.k. wao wakawa wanajua huu mji ni wa wanyakyusa maana wakifika mjini wanakutana na wanyakyusa wengi, Pia wnyakyusa wengi waliwahi kutoka nje ya Mbeya kwenda mikoa mingine kikazi, kielimu, siasa, n.k. hivyo watu wa mikoa waliyofikia walijua Mbeya ni ya wanyakyusa. wakati huo wasafwa waliokuwa wenyeji original ilikuwa ngumu kuwajua sababu walikuwa wanaishi mbali ya mji na maeneo yasiyofikika kirahisi ikawa vigumu kwa watu wa mikoa mingine kuwajua.

Laiti wasafwa wangebaki kwenye huu mji huenda wangekuwa na maendeleo sana an kufahamika zaidi kuzidi wanyakyusa, mji huu ulikuwa ndio makao makuu ya mkoa wa Mbeya lakini hii bahati wakaichezea na. wasafwa waliletewa hivi vitu vizuri hapa mjini ila wakavikimbia.

-serikali ilijenga shule nyingi ila wasafwa walizikimbia, wakawaachia wanyakyusa na wageni wengine.

-Serikali na makampuni yalitoa nafasi za ajira lakini wasafwa walikuwa mbali, wanyakyusa na wageni walizifaidi

-mji ulianza kujaa na kukawa na fursa za biashara ambazo wasafwa wangeweza kupata pesa lakini kujitenga kwao kukaliacha soko wazi kwa wanyakyusa na wageni wengine.

-madaraka, vyeo na teuzi serikalini za kuongoza mji huu wakawaachia wanyakyusa na wageni wengine, nafasi hizi zilitumika na wanyakyusa kuwekana maofisini na kupeana vyeo.

-viwanja vingi waliviacha ama kuviuza na kukimbilia milimani kusiko hata na huduma za jamii, n.k. leo hii nyumba nyingi maeneo ya mjini ni za wanyakyusa japo kwa sikuhizi wageni wengine nao wanajenga sana,


Ni historia yenye kusikitisha ila ina funzo kubwa sana, mkataa kwao hugeuka mtumwa.

Mwisho kwa kuhitimisha naweza kutoa ushauri kwa wasafwa kwamba historia haiwezi kubadilika itabaki kwajili ya kujifunza lakini mnachoweza kubadilisha ni future kwa kuanza kutia bidii muda wa sasa (present)

- wasafwa mzingatieni sana elimu pambanieni na ikibidi mjinyime watoto wasome shule hasa za private na jumuia ya wazazi zilizojaa tele Mbeya jiji, mhakikishe watoto wafike vyuoni nanyi mjae jae maofisini na vyeo.

- mjipanue na kutafuta fursa mpya za kibiashara na kujiajiri, Mbeya ni jiji lina watu wengi wenye mahitaji mengi muangalie ni sehemu zipi mnaweza kuchota pesa.

- muwe na bidii ya kugombea nafasi mbalimbali za kisiasa na uongozi kwenye huu mji wenu, mpambanie nafasi za kupaza sauti ya kero zetu wageni wa mbeya na zenu wazawa halisi wa mbeya.

-msaidiane na kubebana ili walio chini nao wawe na maendeleo, roho za umimi na ubinafsi haziwezi leta maendeleo
 
images (16).jpeg
 
ni kwamba nchi ilipopata uhuru kulikuwa kuna wageni wengi walianza kuja na kuhamia hapa jijini kwenye makao makuu ya mkoa wetu wa Mbeya, wageni hawa kwa kiasi kikubwa walikuwa ni wanyakyusa, shida ikaja kwamba wasafwa wakiona wageni walikuwa hawataki kuchangamana nao walikuwa wanahamisha makazi kwenda sehem ambayo wapo peke yao, wanyakyusa walizidi kujaa hapa mjini na ikawa usumbufu kwa wasafwa kuhama hama ikafikia kipindi wengine wakaanza kukimbilia milimani waishi kivyao vyao.

matokeo yake hapa mjini makabila ya ziada yaliyokuja kama wanyiha, wandali, wakinga, wahehe, wangoni, wabena, n.k. wao wakawa wanajua huu mji ni wa wanyakyusa maana wasafwa wengi walikimbilia milimani ikawa vigumu kuwajua wao ndio wenye mji.

Laiti wasafwa wangebaki kwenye huu mji huenda wangekuwa na maendeleo sana kuzidi hata wanyakyusa, mji huu ulikuwa ndio makao makuu ya mkoa wa Mbeya lakini hii bahati wakaichezea na ni ngumu kurudi tena. wasafwa waliletewa hivi vitu vizuri hapa mjini ila wakavikimbia.
Karne hii watu bado wanazungumzia makabila,
 
Sokapo apa......mbeya yote yetu wanyakyusa.....[emoji23][emoji23][emoji23]
historia ina impact kubwa sana kwenye future, hawa wasafwa ndio ilibidi wawe na title yao ya kuwa wenyeji wa jiji lakini waliwaachia hio title wanyakyusa bure kabisa kwa kuwapisha wageni ili waishi peke yao sehemu za mbali.
 
Sababu kubwa ni kuwa wanyakyusa ni wengi. Na waliwahi kutoka nje ya mbeya.

Hivyo wakati wa kujitambulisha wakawa wanasema wanatokea Mbeya.

Kumbuka wanyakyusa ni wenyeji wa wilaya mbili.. RUNGWE na KYELA. Wasafwa ni wachache kwa ujumla wao. Hata huko milimani unakosema walikimbilia bado ni sehemu ya jiji.

Wakinga wana tabia ya kuitana na kushikana mikono ndugu.. Naona wametawala hiyo mbeya.
 
Sababu kubwa ni kuwa wanyakyusa ni wengi. Na waliwahi kutoka nje ya mbeya
Sababu kuu ni wasafwa kupenda kuishi peke yao, wao ndio walikuwa wenyeji wa jiji la Mneya, walipoona wageni wapya wanaanza kuja hasa wanyaki, wao wakawa wanaenda kuishi sehemu za mbali zisizo na wageni. wanyakyusa ni wazawa wa rungwe na kyela.

hadi leo sijajua hii strategy ya wasafwa walikuwa wanataka kufikia malengo gani, mji wako unaukimbia vipi yani
 
historia ina impact kubwa sana kwenye future, hawa wasafwa ndio ilibidi wawe na title yao ya kuwa wenyeji wa jiji lakini waliwaachia hio title wanyakyusa bure kabisa kwa kuwapisha wageni ili waishi peke yao sehemu za mbali.
Mkuu..... unadhani chambuko la wanyakyusa Ni wapi Kama siyo hapa mbeya[emoji23][emoji23]
 
Mbeya ni yetu sisi wanyakyusa....
wazawa watabaki kuwa wazawa mkuu, hata hili jina la Mbeya lina asili ya kisafwa, kule mteremko wa mbalizi na mlima wa nyoka, magari yanapopata sana ajali wanaofanya mila ni wasafwa, watu wakizama kule ziwa ngosi ni wasafwa ndio hufanya mila kuwapata, bila mila hamuwezi kuipata hio maiti. wasafwa walichokosea ni kukimbia maeneo wakiona wageni (hadi leo wanataniwa kwa jambo hili)

ila kwa idadi ya wakazi naweza kusema ni wanyakyusa japo nao wana kubarua kizito cha kujikwamua kiuchumi hasa kwenye utafutaji, wanyakyusa wengu ukifatilia wamejazana maeneo yenye maendeleo ya chini ama kawaida kama nzovwe, mamajoni, n.k. zile sehemu zenye maendeleo kama forest, block t, isyesye, n.k wamejazana wakinga pamoja na wageni wengine.

uzuri ni kwamba angalau wanyakyusa shule inawabeba wanapata ajira lakini sikuhizi kuna tatizi kubwa la ajira linalowalazimu vijana wageukie kujitafutia, ubaya ni kwamba kwenye utafutaji wa biashara na kujiajiri wanyakyus hapa wapo nyuma, ukifika sehemu kama mwanjelwa na kabwe maduka mengi yanamilikiwa na wakinga na wageni wengine.
 
wazawa watabaki kuwa wazawa mkuu, kule mteremko wa mbalizi na mlima wa nyoka, magari yanapopata sana ajali wanaofanya mila ni wasafwa, wasafwa walichokosea ni kukimbia maeneo wakiona wageni (huwa nacheka sana hapa)

ila kwa idadi ya wakazi naweza kusema ni wanyakyusa japo nao wamejazana maeneo ya nzovwe, mamajoni, n.k. zile sehemu zenye maendeleo kama forest, block t, isyesye, n.k wamejazana wakinga ambao ndio madoni wa jiji hilo oamoja na wageni wengine,
Nakumbuka ukiwa blot T Kutokea hapo fanya unakwenda shule ya sec ivumweee juu huko mlimani
Wasafwa walikuwa wengi huko milimani.....
Kitu kikubwa wasafwa walichonqcho ni uoga na upole
Hivi kwa sasa kuna Don mbeya msafwa

Ova
 
historia ina impact kubwa sana kwenye future, hawa wasafwa ndio ilibidi wawe na title yao ya kuwa wenyeji wa jiji lakini waliwaachia hio title wanyakyusa bure kabisa kwa kuwapisha wageni ili waishi peke yao sehemu za mbali.
Elimu pia iliwapitia kushoto

Ova
 
Nakumbuka ukiwa blot T Kutokea hapo fanya unakwenda shule ya sec ivumweee juu huko mlimani
Wasafwa walikuwa wengi huko milimani.....
Kitu kikubwa wasafwa walichonqcho ni uoga na upole
Hivi kwa sasa kuna Don mbeya msafwa

Ova
Kwa sasa jiji limepanuka sana limefikia mpaka sehemu walizohamiaga hapo zamani imesaidia nao wawe wanachangamana na wageni, wengine nao wameamua kurudi mjini kutoka huko milimani, mambo ya kukaa peke yao nadhani yaliwagharimu sana hivyo wameamua wajichanganye tu.

kuhusu uoga sidhani ila labda ni ile tabia yao ya kuhama kwenda kuishi kivyao ndio ilileta fikra hii, kwa upole naweza kubaliana na wewe huwaga hawana mambo ya vurugu.

Don wa kisafwa kwa hapa Mbeya sijamjua, kwa wanyakyusa wenye mendeleo angalau wapo wapo hasa walioajiriwa ila sijaona wa kufikia anga za madoni, Madoni wengi wa hapa Mbeya kwa sasa ni wakinga na wageni wengine wanaomiliki maduka makubwa, mahoteli, makampuni, viwanda, n. k
 
Kwa sasa jiji limepanuka sana limefikia mpaka sehemu walizohamiaga hapo zamani imesaidia nao wawe wanachangamana na wageni, wengine nao wameamua kurudi mjini kutoka huko milimani, mambo ya kukaa peke yao nadhani yaliwagharimu sana hivyo wameamua wajichanganye tu.

kuhusu uoga sidhani ila labda ni ile tabia yao ya kuhama kwenda kuishi kivyao ndio ilileta fikra hii, kwa upole naweza kubaliana na wewe huwaga hawana mambo ya vurugu.

Don wa kisafwa kwa hapa Mbeya sijamjua, hata wanyakyusa wapo wenye maendeleo hasa walioajiriwa ila kufikia levo za madon hapo sijaona, Madoni wengi wa hapa Mbeya kwa sasa ni wakinga na wageni wengine wanaomiliki maduka makubwa, mahoteli, makampuni, viwanda, n. k
Inasemekana mwenye Hotel ya silver stone tunduma ni mswafwa

Kuhusu madon mbeya toka kitambo ni wakinga hata hapo block t walijaa sana

Hivi eland Hotel bado ipo hapo block t

Ova
 
Sababu kubwa ni kuwa wanyakyusa ni wengi. Na waliwahi kutoka nje ya mbeya. Hivyo wakati wa kujitambulisha wakawa wanasema wanatokea Mbeya. Kumbuka wanyakyusa ni wenyeji wa wilaya mbili.. RUNGWE na KYELA.. wasafwa ni wachache kwa ujumla wao.. Hata huko milimani unakosema walikimbilia bado ni sehemu ya jiji. Wakinga wana tabia ya kuitana na kushikana mikono ndugu.. Naona wametawala hiyo mbeya.
wazawa watabaki kuwa wazawa mkuu, kule mteremko wa mbalizi na mlima wa nyoka, magari yanapopata sana ajali wanaofanya mila ni wasafwa, wasafwa walichokosea ni kukimbia maeneo wakiona wageni (hadi leo wanataniwa kwa jambo hili) ila kwa idadi ya wakazi naweza kusema ni wanyakyusa japo nao wana kubarua kizito cha kujikwamua kiuchumi hasa kwenye utafutaji, wanyakyusa wengu ukifatilia wamejazana maeneo yenye maendeleo ya chini ama kawaida kama nzovwe, mamajoni, n.k. zile sehemu zenye maendeleo kama forest, block t, isyesye, n.k wamejazana wakinga pamoja na wageni wengine. uzuri ni kwamba angalau wanyakyusa shule inawabeba wanapata ajira lakini sikuhizi kuna tatizi kubwa la ajira linalowalazimu vijana wageukie kujitafutia, ubaya ni kwamba kwenye utafutaji wa biashara na kujiajiri wanyakyus hapa wapo nyuma, ukifika sehemu kama mwanjelwa na kabwe maduka mengi yanamilikiwa na wakinga au wageni wa makabila ya kigeni,,, wanyakyusa wengi utawakuta nyuma ya soko wanauza maparachichi na baadhi mitumba.

Kusema wanyakyusa ndiyo wengi umetumia kigezo gani?🤔
 
Back
Top Bottom