Historia ya Yesu siyo halisi ilibuniwa na watu tofauti tofauti

Historia ya Yesu siyo halisi ilibuniwa na watu tofauti tofauti

Story ya Yesu

Mathayo anataja vizazi 26 Kati ya Yesu na Daudi, Luka hutaja vizazi 41. Mathayo anaanza kwa mtoto wa Daudi Solomon, wakati Luka anaanza kwa mtoto wa Daudi Nathan. Mathayo anasema Babu yake Yesu anaitwa Yakobo wakati Luka anasema babu yake Yesu Ni Heli. Cha kushangaza zaidi wamefuatilia vizazi vya Yosefu wakati Hana uhusiano na Yesu Kama kweli kazaliwa kwa bikira Mariam.

Mathayo 2:13-15 inasema Yesu alipelekwa Misri baada ya kuzaliwa. Luka 2:22-40 inasema walibaki Bethlehem, wakaenda Jerusalem na kurudi Nazareth, bila kutaja kwenda Misri.

Kifo Cha Yuda kinasemwa na Mathayo 27:5 kuwa alijinyonga Ila Matendo ya Mitume 1:18 inasema alianguka shambani na akafa.

Yohana 19:17 inatuambia alibeba msalaba wake, Marko 15:21-23 inasema Simoni alimbebea msalaba.
Kila kitabu Cha injili kinasema maneno ya Yesu ya mwisho tofauti Kila injili inachanganya tukio la kufufuka kwa Yesu. Marko 16:2 inasema ilikuwa asubuhi, Yohana 20:1 inasema ilikuwa usiku.

Mathayo 28:2 inasema alionekana malaika mmoja, Yohana 20:11-12 inasema malaika wawili. Marko 16:5 inasema mwanaume mmoja Luka 24:4 inasema wanaume wawili.

Hitimisho: Story ya Yesu inasemekana imeibiwa kutoka dini za kihindi, kipersia, kimisri, kigiriki na kirumi. Miungu yao mingi ilizaliwa December 25, ilizaliwa kutoka kwa Bikira, ilifanya miujiza, ilikufa na kufufuka.

Ina maanisha story ya Yesu sio original na iliundwa na watu tofauti tofauti ndo maana hata vitabu vya dini kuhusu yeye vinajichanganya kuhusu maisha yake yalivyokuwa. Kama ukristo mzima unategemea story hii na Ina makosa kihivi, je Biblia litakuwa neno halisi kutoka kwa Mungu au utunzi wa Binadamu?
Ukifuatilia kwa akili haya mambo unapotea mazima
 
Sasa hata kama hujui maana ya mfano basi wewe ni impossible. Ngoja nisipoteze muda wangu.
Mkuu upo DEEP sana na una hoja,usipuuzwe..hao jamaa achana nao,ni EMPTY BOXES...
 
Anayemkana Mola ni nyinyi mnaosema Yesu ni mungu
Wafilipi (2:5,6,7,8) lweni na nia iyo hiyo ndani yenu ambayo ilikuwamo pia ndani ya Kristo Yesu (6) ambaye yeye mwanzo alikuwa yu namna ya Mungu, naye hakuona kule kuwa sawa na Mungu ni kitu cha kushikamana nacho, (7) bali alijfanya kuwa hana utukufu, akatwaa namna ya mtumwa, akawa ana mfano wa wanadamu, (8)tena alipoonekana ana umbo kama mwanadamu, alijinyenyekeza akawa mtii hata mauti, naam mauti ya msalaba.
 
Wafilipi (2:5,6,7,8) lweni na nia iyo hiyo ndani yenu ambayo ilikuwamo pia ndani ya Kristo Yesu (6) ambaye yeye mwanzo alikuwa yu namna ya Mungu, naye hakuona kule kuwa sawa na Mungu ni kitu cha kushikamana nacho, (7) bali alijfanya kuwa hana utukufu, akatwaa namna ya mtumwa, akawa ana mfano wa wanadamu, (8)tena alipoonekana ana umbo kama mwanadamu, alijinyenyekeza akawa mtii hata mauti, naam mauti ya msalaba.

Paulo hakuwahi kukutana na Yesu maishani mwake.

Hii ni moja ya sababu kuu ya kutomwamini na kumwamini Paulo.

Kabla ya kujipa utume, jina lake lilikuwa Sauli na aliwahi kuwa muuaji wa waumini wa kweli.

Akiwa njiani kuelekea Damasko, akiwa kwenye mgawo wa kuwasumbua waamini wa kweli, anadai kuwa ameona maono ya Kristo, na baada ya hayo, alidai kwamba Yesu alimpa mamlaka ya kufundisha kwa jina lake.

Kuna matatizo mengi hapa.

Kwa vile hakuwahi kukutana na Yesu, akili ya kawaida inasema kwamba yeye hana uhusiano wowote na dini na tunaposoma anachosema tunakuta kwamba hakika yeye hana uhusiano wowote na dini ya kweli ya Nabii Yesu (amani iwe juu yake). .

Hebu tuangalie ono la Paulo anapolielezea kwa watu mbalimbali tofauti wa rangi tofauti.


1. Katika MATENDO 9:3, imeelezwa kwamba ni Paulo pekee aliyeanguka chini alipoona mwanga. Mstari wa 7 unasema kwamba wengine pamoja naye walisimama bila la kusema.

2. MATENDO 26:14 inasema WOTE walianguka chini.

3. MATENDO 9:7 inasema kwamba watu waliosafiri pamoja na Paulo hawakumwona mtu bali walisikia sauti.

4. MATENDO 22:9 inasema wale waliokuwa pamoja na Paulo waliona nuru lakini HAWAKUsikia sauti ya msemaji.

Hayo hapo juu ni mikanganyiko ya wazi na mtu ye yote angemkataa Paulo mara moja baada ya kusoma mistari hii.

Ikiwa huu ni uwongo wa wazi tu na Paulo amesahau aliposema nini, basi si kitu zaidi ya ujinga wake lakini ikiwa anatumia mbinu hii kwa makusudi kusimulia hadithi tofauti kwa watu tofauti, basi mbinu hii bado ingali ikitumiwa na wachungaji wa makanisa.

Mbinu kama hiyo imeweka msingi muhimu sana wa Kanisa, i.e. kupitisha njia inayomfaa mtu.

Sikukuu kama Krismasi; Halloween n.k hazina uhusiano wowote na Ukristo lakini Kanisa limeziingiza humo kwa kufuata nyayo za Paulo.

16 Hata kama mnakubali kwamba sikuwa mzigo kwenu, wengine watasema nilikuwa mjanja nikawanasa kwa hila.

( 2 WAKORINTHO 12:16 )


... na kwa hayo, anadanganya tena,


1 Thes. 2:3

"Kwa maana rufaa tunayotoa haitokani na makosa au nia chafu, wala hatujaribu kuwahadaa."



"Nasema kweli katika Kristo, sisemi uongo"

( Rum. 9:1, 1 Tim. 2:7 )

Paulo ameanzisha dhana hii ya kubadilika katika Ukristo na Kanisa. Aya hii pia inaelezea kuwepo kwa tovuti ya Answering-Islam na maeneo mengine yanayofanana na hayo ya chuki ambapo wanadanganya watu na bado wanafuata dini yao. Wanadanganya na kusema kwamba hawapendi tu mwanzilishi wao Paulo.


Paulo anapingana na mafundisho ya Nabii Isa (amani iwe juu yake).


Yesu anasema…


Msidhani ya kuwa nalikuja kuitangua torati au manabii; sikuja kutangua, bali kutimiliza. Kwa maana, amin, nawaambia, Mpaka mbingu na nchi zitakapoondoka, yodi moja wala nukta moja ya torati haitaondoka, hata yote yatimie. Yeyote atakayevunja mojawapo ya amri hizi zilizo ndogo na kuwafundisha watu hivyo ataitwa wa mwisho katika ufalme wa mbinguni. Kwa maana nawaambia nyinyi haki yenu isipozidi haki ya waandishi na Mafarisayo, hamtaingia kamwe katika ufalme wa mbinguni.

Mathayo 5:17-20


Paulo anasema...

'Wakristo' wamekufa kwa Sheria ya Mungu kupitia mwili wa Kristo.
( Warumi 7:14 )


Paulo ameharibu sheria.


Paulo ndiye mvumbuzi wa dhambi ya asili ( WARUMI 5:12, 1 WAKORINTHO 15:21-22 ).
 
Wafilipi (2:5,6,7,8) lweni na nia iyo hiyo ndani yenu ambayo ilikuwamo pia ndani ya Kristo Yesu (6) ambaye yeye mwanzo alikuwa yu namna ya Mungu, naye hakuona kule kuwa sawa na Mungu ni kitu cha kushikamana nacho, (7) bali alijfanya kuwa hana utukufu, akatwaa namna ya mtumwa, akawa ana mfano wa wanadamu, (8)tena alipoonekana ana umbo kama mwanadamu, alijinyenyekeza akawa mtii hata mauti, naam mauti ya msalaba.

Paulo anamkufuru Mungu


Kwa maana upumbavu wa Mungu una hekima zaidi ya hekima ya mwanadamu, na udhaifu wa Mungu una nguvu zaidi ya nguvu za wanadamu.

( 1 Wakorintho 1:25 )

Mambo ya Walawi 24:16

mtu ye yote atakayelikufuru jina la BWANA lazima auawe.


Yesu alisema...

Lakini mimi nawaambieni, yeyote anayemkasirikia ndugu yake atahukumiwa. Tena, yeyote anayemwambia ndugu yake, ‘Raca,’ anajibika mbele ya Baraza. Lakini yeyote anayesema, 'Mjinga wewe!' atakuwa katika hatari ya moto wa kuzimu.

( Mathayo 5:22 )

Paulo alisema…

“Wewe mpumbavu, ukipandacho hakiwi hai isipokuwa kikifa”
( 1 Kor. 15:36 )

Paulo aliamini Yesu alifufuka kutoka kwa wafu kama roho, si mwili wa nyama.

Hupandwa mwili wa asili, hufufuliwa mwili wa kiroho. Ikiwa kuna mwili wa asili, kuna mwili wa kiroho pia.
( 1 Wakorintho 15:44 )

Ndugu zangu, nawaambieni, nyama na damu haziwezi kuurithi ufalme wa Mungu, wala kuharibika kurithi kutoweza kuharibika.
( 1 Wakorintho 15:50 )

Ukweli ni kwamba Yesu alipaa Mbinguni katika mwili wa nyama (Luka 24:51).

Paulo alikanusha hadithi za Eliya na Eliza kufufua maiti kwa hali yao ya zamani (2Wafalme 17:20-23).

Pia anawakanusha Mitume. Kukanusha kwake hadithi hizi kunaonyesha kwamba alilichukulia Agano la Kale kuwa potovu kama hadithi za uwongo ndani yake.

Paulo analichukulia Agano la Kale kuwa potovu.

Anakanusha, Mungu, Yesu, Manabii wengine, anawapinga Barnaba na Petro kwa ukali kwa sababu wanafundisha hivi;

na

Wote wawili walifundisha Uislamu, hakuna uungu wa Yesu na hakuna kusulubiwa.

"Usinywe tena maji, bali tumia mvinyo kidogo, kwa ajili ya tumbo lako, na magonjwa yakupatayo mara kwa mara."
( 1 Tim. 5:23 )

Daktari Paulo anashauri, usinywe maji, kunywa divai tu.

Paulo anasema…

Rum. 12:14

"Wabarikini wanaowaudhi; barikini wala msiwalaani."

Lakini pia anasema…

Matendo 23:3

"Mungu atakupiga, wewe ukuta uliopakwa chokaa."
 
Paulo anamkufuru Mungu


Kwa maana upumbavu wa Mungu una hekima zaidi ya hekima ya mwanadamu, na udhaifu wa Mungu una nguvu zaidi ya nguvu za wanadamu.

( 1 Wakorintho 1:25 )

Mambo ya Walawi 24:16

mtu ye yote atakayelikufuru jina la BWANA lazima auawe.


Yesu alisema...

Lakini mimi nawaambieni, yeyote anayemkasirikia ndugu yake atahukumiwa. Tena, yeyote anayemwambia ndugu yake, ‘Raca,’ anajibika mbele ya Baraza. Lakini yeyote anayesema, 'Mjinga wewe!' atakuwa katika hatari ya moto wa kuzimu.

( Mathayo 5:22 )

Paulo alisema…

“Wewe mpumbavu, ukipandacho hakiwi hai isipokuwa kikifa”
( 1 Kor. 15:36 )

Paulo aliamini Yesu alifufuka kutoka kwa wafu kama roho, si mwili wa nyama.

Hupandwa mwili wa asili, hufufuliwa mwili wa kiroho. Ikiwa kuna mwili wa asili, kuna mwili wa kiroho pia.
( 1 Wakorintho 15:44 )

Ndugu zangu, nawaambieni, nyama na damu haziwezi kuurithi ufalme wa Mungu, wala kuharibika kurithi kutoweza kuharibika.
( 1 Wakorintho 15:50 )

Ukweli ni kwamba Yesu alipaa Mbinguni katika mwili wa nyama (Luka 24:51).

Paulo alikanusha hadithi za Eliya na Eliza kufufua maiti kwa hali yao ya zamani (2Wafalme 17:20-23).

Pia anawakanusha Mitume. Kukanusha kwake hadithi hizi kunaonyesha kwamba alilichukulia Agano la Kale kuwa potovu kama hadithi za uwongo ndani yake.

Paulo analichukulia Agano la Kale kuwa potovu.

Anakanusha, Mungu, Yesu, Manabii wengine, anawapinga Barnaba na Petro kwa ukali kwa sababu wanafundisha hivi;

na

Wote wawili walifundisha Uislamu, hakuna uungu wa Yesu na hakuna kusulubiwa.

"Usinywe tena maji, bali tumia mvinyo kidogo, kwa ajili ya tumbo lako, na magonjwa yakupatayo mara kwa mara."
( 1 Tim. 5:23 )

Daktari Paulo anashauri, usinywe maji, kunywa divai tu.

Paulo anasema…

Rum. 12:14

"Wabarikini wanaowaudhi; barikini wala msiwalaani."

Lakini pia anasema…

Matendo 23:3

"Mungu atakupiga, wewe ukuta uliopakwa chokaa."
2Petro (3:16)Vile Vile kama katika nyaraka zake zote pia, akitoa humo habari za mambo hayo, katika nyaraka hizo, yamo mambo ambayo ni vigumu kuelewa nayo, na mambo hayo watu wasio na elimu, wasio imara, huyapotoa, kama vile wayapotoavyo na maandiko mengine, kwa uvunjifu wao wenyewe, basi wapenzi, mkitaangulia kujua hayo, jilindeni nafsi zenu msije mkachukuliwa na kosa la hao wahalifu, mkaanguka na kuuacha uthibitifu wenu.
 
Ukiondoa mbingu na dunia nionyeshe kitu ambacho Mwenyezi Mungu hufanya bila kumhusisha mwanadamu. Mfano, kuzaliwa kwa watoto - tunasema ni Mwenyezi Mungu ndiye anayetutia roho, lakini mtoto anatokana na muunganiko wa mume na mke au mwanaume na mwanamke.

Nyumba ya ibada tunaiita 'nyumba ya Mungu' lakini inajengwa na binadamu. Sadaka tunasema ni ya Mungu, lakini inatolewa na kupewa wanadamu. Vitabu vitakatifu tunasema ni neno la Mungu, lakini vimeandikwa na binadamu.

Hata neno linaposomwa kanisani au mskitini tunasema ni neno la Mungu, lakini linasomwa na mwanadamu. Hivyo, katika mambo mengi Mungu anawashirikisha wanadamu katika kuifanya dunia iwe mahali pema zaidi. Kuna lugha ya kiteolojia inasema: "God did not create a perfect world, but a perfectable world" na ndiyo maana hatuna budi kutunza mazingira kwa kupanda miti na kupunguza uchafuzi wa mazingira, hewa na maji.

Tofauti unazoziona kwenye Biblia ni za kibinadamu/kimaandishi, lakini neno la Mungu ni timilifu maana linahusu 'saving justice, love of God and neighbour, forgiveness, compassion, salvation' na katika haya hakuna kilichokosewa. Hivyo, msingi wa biblia au focus yake ni "ukombozi wa mwanadamu" na siyo makabila mangapi au majina ya akina nani au sehemu gani.
Umejibu vema kabisa... Maana pamoja na utofauti wa wandishi.. Hoja ya wokovu imelindwa..sasa kama atasubiri mfanano wa maandiko ndio naamini atasubiri sanaaaa... Ila kweli Kwamba, YESU NI MWOKOZI NA KILA AAMINIE HATOHUKUMIWA, ASIEAMINI KESHA HUKUMIWA
 
2Petro (3:16)Vile Vile kama katika nyaraka zake zote pia, akitoa humo habari za mambo hayo, katika nyaraka hizo, yamo mambo ambayo ni vigumu kuelewa nayo, na mambo hayo watu wasio na elimu, wasio imara, huyapotoa, kama vile wayapotoavyo na maandiko mengine, kwa uvunjifu wao wenyewe, basi wapenzi, mkitaangulia kujua hayo, jilindeni nafsi zenu msije mkachukuliwa na kosa la hao wahalifu, mkaanguka na kuuacha uthibitifu wenu.

Wakristo wengi hawaelewi kwamba 2 Petro ni mojawapo ya vitabu vinavyojadiliwa sana katika kanuni za Agano Jipya.

Wasomi wachanganuzi wanaiona 2 Petro kuwa ilighushiwa na mwandishi wa baadaye aliyejifanya kuwa Petro (jina bandia = jina la uwongo) mwishoni mwa karne ya kwanza au mwanzoni mwa karne ya pili.

Mtindo na maneno ya 2 Petro ni tofauti kabisa na ile ya 1 Petro (kwa wasomi wachambuzi, hii inaonyesha hao ni waandishi wawili tofauti).

Petro anaelezewa kuwa "hajui kusoma na kuandika" (Matendo 4:13), na mwandishi wa 2 Petro anatumia maneno ya falsafa ya Kigiriki.

Kuna madai ya kutofautiana kwa kihistoria (rejeleo la barua ya Paulo kama Maandiko- 2 Petro 3:16).
 
Ukombozi ni zaidi ya fikira zako. Of course, huwezi kuona sense kama hujaelewa kitu. Kama hujafika "Soho" - ni moja ya sehemu maarufu sana jijini London - huwezi kuelewa wala kuelezea shughuli zinazoendelea huko. Huu ni mfano ninaoweza kukupa. Na wewe kama hujafikia level ya kuelewa au hutaki kuelewa, huwezi kuelewa.

Uandishi wa biblia uko kama waandishi wa habari wanavyoweza kuripoti tukio fulani. Mfano, imetokea ajali ya gari na kuna majeruhi 10 na waliopoteza maisha 3. Mwandishi A akifika sehemu ya ajali ataripoti kuna ajali imetokea sehemu X na kuna majeruhi 10 na waliopoteza maisha 3.

Mwandishi B ambaye amefika sehemu ya tukio na kukuta majeruhi na miili ya waliofariki imepelekwa hospitalini ataripoti kuwa kuna majeruhi wengine 3 waliofariki njiani, atasema ajali imetokea sehemu X waliofariki ni 6 na walionusurika ni 7. Angalia namba zimebadilika siyo kimakosa, bali kuendana na habari ilivyo kwa wakati huo na kama kuna mwandishi mwingine wa tatu atakayeenda sehemu ya tukio na kisha hospitalini na kukuta majeruhi wamesharuhusiwa kwenda nyumbani na ndugu wameshachukua miili ya wapendwa wao, naye taarifa yake itakuwa tofauti.

Tofauti hizi za namba na majina baadhi husema "waandishi wetu hawako serious". Lakini ukiangalia kila mwandishi aliripoti tukio kikamilifu kwa jinsi alivyopata taarifa za tukio lenyewe. Mfano, mwandishi wa kwanza hataongelea hospitali, daktari na nesi na mortuary. Lakini mwandishi wa pili ataongelea hayo pia. Mwandishi wa tatu yeye atategemea taarifa yake kwa madaktari na manesi.

Na kama kuna mwandishi wa nne huenda source ya taarifa yake atakuwa mwandishi mwenzake aliyefika sehemu ya ajali na kukuta majeruhi na waliopoteza maisha wakiwa bado sehemu ajali ilipotokea. Kama itakuwa hivyo, mwandishi huyu atatoa taarifa karibu inayofanana na mwandishi wa kwanza - maana anaweza hata kutaja namba za gari na jina la dereva, ambavyo kwa mwandishi wa nne hivi vitu kwake havitakuwa muhimu kwake. Sana sana anaweza kusema alipofika wodini walipolazwa majeruhi alikuta wodi ya wagonjwa imejaa, taarifa ambayo waandishi wengine hawatakuwa nayo pia.

Lakini pia kama waandishi hao watapeleka habari - mfano mmoja kwa wanafunzi wa chuo kikuu, mwingine kwa wakulima, mwingine kwa wavuvi na mwingine kwa wasanii kila mmoja atatumia msamiati au lugha inayoeleweka kwa wale anaowapelekea habari. Huu ni mfano (ingawa siyo mkamilifu) wa namna biblia ilivyoandikwa na tofauti za waandishi katika kuelezea habari wanazowasilisha siyo kosa/tatizo lao, bali ni aina ya habari ilivyopokelewa kutoka kwa chanzo cha habari na kuiweka katika lugha inayoeleweka kwa wale wanaopelekewa habari husika.

Matoleo ya Biblia ya Kingereza

Katika utangulizi wa toleo la Biblia linalotumika sana, la Revised Standard Version, mtunzi ameandika yafuatayo:

"Biblia ya Revised Standard Version, ni marekebisho yaliyoidhinishwa ya toleo la American Standard Version, lilochapwa 1901, na ambalo nalo pia lilikuwa ni marekebisho ya toleo la King James Version, lilochapwa 1611...

Toleo la King James Version lililazimika kushindana na Biblia ya Geneva Bible (1560) juu ya kutumiwa na watu wengi; lakini hatimaye lilienea, na kwa zaidi ya karne mbili na nusu hakuna tafsiri ya Biblia kwa Kingereza iliyoandikwa na kuidhinishwa.

Toleo la King James Version likawa ndilo "toleo lililoidhinishwa" kwa wanaoongea Kingereza...

Ndio, Toleo la King James Version lina dosari kubwa mno. Kufikia katikati ya karne ya kumi na tisa, maendeleo ya tafiti za Kibiblia vilevile kugunduliwa kwa miswada mingi ambayo ni ya kale zaidi kuliko ile iliyotegemewa na Toleo la King James Version, yamefanya toleo hilo kuwa ni wazi kuwa lina dosari nyingi na mbaya mno na kusababisha kuitishwa kufanyika marekebisho ya tafsiri ya kingereza.

Kazi ikafanywa, kwa idhini ya Kanisa la Uingereza, mwaka 1870.

Toleo la Biblia la English Revised Version lilichapwa mwaka 1881 – 1885; na Toleo la American Standard Version, lahaja zake zimejiingiza katika upendeleo wa wanazuoni wa Kimarekani walioshiriki katika kazi hiyo, nalo lilichapishwa mwaka 1901."

Toleo la King James Version la Agano Jipya liliegemea matini za kigiriki zilizovurugwa kimakosa, ikiwemo kujilimbikizia makosa ya karne ya kumi na nne ya kunukuu miswada.

Nalo kimsingi, lilikuwa ni matini ya Kigiriki ya Agano Jipya kama lilivyoandikwa na Beza, 1589, ambaye kwa ukaribu zaidi alifuata chapa hiyo ya Erasmus, 1516 – 1535, iliyoegemea juu ya miswada ya zama za kati. Mswada wa kwanza na ulio bora zaidi miongoni mwa miswada minane aliyoishirikisha ulikuwa ni wa karne ya kumi, naye akautumia kidogo mno mswada huo kwa sababu unatofautiana sana na matini za kawaida zilizopokelewa;

Beza alipata miswada miwili ya thamani kubwa mno, ikiwa ni ya karne ya tano na ya sita, lakini aliitumia kidogo mno kwa sababu inatofautiana na matini iliyochapwa ya Erasmus."

"... Toleo la American Standard Version lilipewa haki miliki ya kuzuia matini yake isibadilishwe bila idhini. Mnamo 1928 haki hiyo ilipatikana kutoka katika Baraza la Kimataifa la Elimu na Dini, na kwa hiyo likawekwa katika umiliki wa makanisa ya Marekani na Canada yaliyoshiriki katika baraza hilo kwa kupitia bodi zao za elimu na uchapaji.

Baraza hilo liliainisha kamati ya wasomi kusimamia matini ya ya Toleo la American Standard Version na kufanya uchunguzi na kujua kama marekebisho zaidi yanahitajika... [Baada ya miaka miwili] uamuzi ulifikiwa; nao ni kuwa; kunahitaji marekebisho kikamilifu katika toleo la 1901, ambalo litabakia kuwa lipo karibu na mapokeo ya Tyndale-King
James kama itakavyokuwa...

Mnamo 1937 na marekebisho yalipewa idhini kwa kura ya Baraza hilo."

"Wasomi thelathini na wawili walitumika kama wanakamati wa kamati iliyotakiwa kufanya marekebisho hayo, nao waliyalinda mabadiliko na kuishauri Bodi ya Ushauri ya wawakilishi hamsini wa madhehebu ili kushirikiana kufanya kazi hiyo... Toleo la Agano Jipya la Revised Standard Version lilichapwa mwaka 1946."

Toleo la Biblia la Revised Standard Version, linajumuisha Agano la Kale na Jipya, nalo lilichapwa mnamo Septemba 30, 1952, na likakubalika sana."

Katika Toleo la Biblia la Revised Standard Version, idadi kubwa ya mistari muhimu kutoka katika Toleo la King James Version ya Agano la Kale na Jipya, ambayo wasomi waliiona kuwa imeongezwa katika karne za baadaye, iliondoshwa kutoka katika matini na kuwekwa katika tanbihi.

Kwa mfano, kifungu maarufu sana katika Injili ya Yohana 8:7 kinachohusu mzinzi aliyetakiwa kupigwa mawe. Inasemakana Yesu amesema: "Nao walipozidi kumhoji, alijiinua, akawaambia, Yeye asiye na dhambi miongoni mwenu na awe wa kwanza wa kumtupia jiwe."

Tanbihi za Toleo la King James (1952) zinaeleza "Mamlaka za kale mno zinaondosha aya za 7:53 – 8:11"

Kwa kuwa mswada namba 1209 wa Vatikani na mswada wa Sinaitic ya tangu karne ya nne haina aya kumi na mbili hizo, wasomi wa Biblia wamefikia uamuzi wa kuwa maneno hayo hayatoki kwa Yesu.

Mfano mwingine ni kifungu kinachohusishwa na Yesu na kinachotumika kama ushahidi wa rejeo la Utatu katika Maandiko matakatifu.

Katika 1 Yohana 5:7, Inasemakana Yesu amesema: "Kuna watatu wanaoshuhudia huko mbinguni, Baba, Neno na Roho Mtakatifu: na watatu hawa ni mmoja"

Msomi maarufu sana wa Biblia, Benjamin Wilson, anaandika kuwa; maandiko haya yanayohusu "ushahidi wa mbinguni" hayamo katika mswada wowote wa Kigiriki ulioandikwa kabla ya karne ya kumi na tano!

Kwa hiyo, katika Toleo la Biblia la Revised Standard Version, mstari huu umefutwa na kutolewa katika matini tena bila ya kuwekewa tanbihi.

Hata hivyo, ili kuwe na idadi ya mistari iliyosawa baina ya Toleo la Biblia la Revised Standard Version, na ile ya Toleo la Biblia la King James Version, warejeaji wameugawa mstari wa sita na kuwa mistari miwili

Toleo la pili la tafsiri ya Agano Jipya (1971) limefaidika kwa tafiti za matini na isimu tangu lilipotolewa toleo la The Rivised Standard Version, kwanza lilitolewa mwaka 1946.

Kwa hiyo, baadhi ya vifungu vilivyofutwa zamani viliandikwa upya, na baadhi ya vifungu vilivyokubaliwa vilifutwa.

"Vifungu viwili, vya mwisho mrefu wa Marko (16:9-20) na kifungu cha mwanamke aliyekamatwa kwa uzinzi (Yohana
7:53 – 8:11), vilirejeshwa katika matini, zikitenganishwa kwa nafasi wazi na zikiambatana na nukuu za kauli taarifa...

Kukiwa na kuungwa mkono na miswada miwili, vifungu viwili, Luka 22:19b-20 na 24:51b, vilirejeshwa katika matini, na kifungu kimoja, Luka 22:43-44, kiliwekwa katika tanbihi, kama ni ibara katika Luka 12:39.
 
Wakristo wengi hawaelewi kwamba 2 Petro ni mojawapo ya vitabu vinavyojadiliwa sana katika kanuni za Agano Jipya.

Wasomi wachanganuzi wanaiona 2 Petro kuwa ilighushiwa na mwandishi wa baadaye aliyejifanya kuwa Petro (jina bandia = jina la uwongo) mwishoni mwa karne ya kwanza au mwanzoni mwa karne ya pili.

Mtindo na maneno ya 2 Petro ni tofauti kabisa na ile ya 1 Petro (kwa wasomi wachambuzi, hii inaonyesha hao ni waandishi wawili tofauti).

Petro anaelezewa kuwa "hajui kusoma na kuandika" (Matendo 4:13), na mwandishi wa 2 Petro anatumia maneno ya falsafa ya Kigiriki.

Kuna madai ya kutofautiana kwa kihistoria (rejeleo la barua ya Paulo kama Maandiko- 2 Petro 3:16).
2PETRO (2:20,21)Mkijua neno hili kwanza, ya kwamba hakuna unabii katika maandiko upatao kufasiriwa kama apendavyo mtu fulani. Maana unabii haukuletwa popote kwa mapenzi ya wanadamu, bali wanadamu walinena yaliyotoka kwa Mungu, wakiongozwa na roho mtakatifu.
 
Wakristo wengi hawaelewi kwamba 2 Petro ni mojawapo ya vitabu vinavyojadiliwa sana katika kanuni za Agano Jipya.

Wasomi wachanganuzi wanaiona 2 Petro kuwa ilighushiwa na mwandishi wa baadaye aliyejifanya kuwa Petro (jina bandia = jina la uwongo) mwishoni mwa karne ya kwanza au mwanzoni mwa karne ya pili.

Mtindo na maneno ya 2 Petro ni tofauti kabisa na ile ya 1 Petro (kwa wasomi wachambuzi, hii inaonyesha hao ni waandishi wawili tofauti).

Petro anaelezewa kuwa "hajui kusoma na kuandika" (Matendo 4:13), na mwandishi wa 2 Petro anatumia maneno ya falsafa ya Kigiriki.

Kuna madai ya kutofautiana kwa kihistoria (rejeleo la barua ya Paulo kama Maandiko- 2 Petro 3:16).
Mkuu Muhamad hakujua kusoma wala kuandika, ikiwa kutokujua kusoma ni kigezo, Quran isiaminiwe na waislamu? tusaidie.
 
Mkuu Muhamad hakujua kusoma wala kuandika, ikiwa kutokujua kusoma ni kigezo, Quran isiaminiwe na waislamu? tusaidie.

Muhammad SAW hakuandika Quran lakini tunaambiwa Peter aliandika 1 na 2 Peter
 
Back
Top Bottom