Hitaji la ajira za kazi za ndani kwa watu wenye miaka 50+ linaongezeka

Hitaji la ajira za kazi za ndani kwa watu wenye miaka 50+ linaongezeka

Anita Kajembe

JF-Expert Member
Joined
Jun 29, 2021
Posts
215
Reaction score
487
Kuna kundi kubwa la watu wazima wanaotafuta kazi za ndani. Wengine ni kutokana na changamoto za maisha, kuachwa na mume, kufiwa, kupoteza ulivyonavyo na kubidi kuanza upya, haya yote si sababu ya kuanzisha uzi huu.

Watu wazima wengi wanajielewa, kazi umamwelekezi mara moja tu na huwa hawapendi kujivunjia heshima. Wengi hupenda uhuru wao, apate off mara moja kwa wiki hata kwenda kumsalimia binamu yake tu.

Jambo muhimu sana ni usalama wa ndoa. Unakuta mama huyu anawazidi wewe na mume wako umri. Baba hawezi kumgongea mlango usiku.

Changamoto nyingine ni sehemu ya kujistir. Wengi wetu mijini tunaishi kwa kubanana sana. Kupata chumba na kitanda kwa mama au baba huyu ni vigumu.

Watu wazima ni wazuri kwa usalama wa nyumba pia unaposafiri. Wengi hawakaribishi vijana wa mtaani wanaoweza kuwa vibaka.

Unapokutana na mtu mzima mwenye uhitaji wa ajira, fikiria kumpa nafasi.
 
Kuna kundi kubwa la watu wazima wanaotafuta kazi za ndani. Wengine ni kutokana na changamoto za maisha, kuachwa na mume, kufiwa, kupoteza ulivyonavyo na kubidi kuanza upya, haya yote si sababu ya kuanzisha uzi huu...
Mi kama Yupo huyo wa Miaka 50 kama Unamjua Namuhitaji Nitashukuru.

Sent from my SM-N900 using JamiiForums mobile app
 
Kuna kundi kubwa la watu wazima wanaotafuta kazi za ndani. Wengine ni kutokana na changamoto za maisha, kuachwa na mume, kufiwa, kupoteza ulivyonavyo na kubidi kuanza upya, haya yote si sababu ya kuanzisha uzi huu...
Kwa kweli sishauri kuajiri watu wa umri mkubwa, kwa sasa kuna mission nyingi za ibilisi ktk maisha ya watu.jirani alikuwa na mama wa makamo..kaja kugundua watoto ake wote wachawi, tena baada ya mateso makubwa ya ndoa, afya na uchumi. Kama unajiamini ajiri ila kama hauko ngangari ktk imani...jiandae kulia!!
 
Kuna kundi kubwa la watu wazima wanaotafuta kazi za ndani. Wengine ni kutokana na changamoto za maisha, kuachwa na mume, kufiwa, kupoteza ulivyonavyo na kubidi kuanza upya, haya yote si sababu ya kuanzisha uzi huu...
Mkuu, kampeni au?

Ila nakusaport. Mtu nzima mwanaume kwa kutunza mashamba na mifugo ni best. Utainjoi!
 
Kwa shughuli za ndani, kupika, usafi, nk, mwanamama ndiye anayefaa. Huwezi kuweka dume!
 
Kwa kweli sishauri kuajiri watu wa umri mkubwa, kwa sasa kuna mission nyingi za ibilisi ktk maisha ya watu.jirani alikuwa na mama wa makamo..kaja kugundua watoto ake wote wachawi, tena baada ya mateso makubwa ya ndoa, afya na uchumi. Kama unajiamini ajiri ila kama hauko ngangari ktk imani...jiandae kulia!!
Hii African Physics ni kikwazo katika maendeleo yetu.
 
ni kweli.

hata shule za awali za dini huwapa hawa kipaumbele kwenye upande wa kuhudumia watoto,usafi nk.
 
Back
Top Bottom