Hivi Alliens wanakula chakula gani?

Hivi Alliens wanakula chakula gani?

Vitabu vya Mungu vinatuhusu sisi binadamu tunaoishi hii sayari tunayokanyaga na kuringia mafao, hao Alliens wenyewe maisha yao ni huko sayari zingine dunia hii siyo mahala pao!

Wanazaliwa kwa njia ya mbegu alafu wanakufa kama binadamu anavyokufa...

Mmmh!
Si umeona utata huo?
Kwani wao hawakuumbwa na Mungu?
Kwaiyo wao hawana hesabu?
Wao hawatendi uhalifu?
Hawatendi mema?
 
kwahiyo unamaanisha binadamu wa sasa watapotea na kuja wengine?

Hujanielewa Mokoyo. Nimemaanisha kama vile tunavyoaminishwa kua binaadamu alikua sokwe kitu ambacho hakiwezekani, ndio vile vile tunaaminishwa kuhusu allies, siamini kua viumbe hao wapo
 
Last edited by a moderator:
MPENZI msomaji ungana nami katika simulizi hii mpya ya kweli inayohusu viumbe wa ajabu waishio angani. Hawa wanasadikiwa kuimeza ndege ya malaysia. Ikiwa unafuatilia kuwa awali nliezea kuhusu theory ya Bermuda Triangle katika upotevu wa ndege hii, hapa basi utawasikia hawa viumbe wa ajabu kama vile biblia inavyosema kuna vile viumbe visivyoonekana kwa macho yetu lakini vipo. Haya twende pamoja. Kama ni msomaji wa vitabu vitakatifu, Mungu aliumba vitu vinavyoonekana na visivyoonekana. Inahisiwa kuwa visivyoonekana ni vingi kuliko vinavyoonekana.

Viumbe hao wa ajabu waishio angani wanaitwa Aliens. Wana muonekano kama binadamu isipokuwa hawafanani moja kwa moja na binadamu. Viumbe hao waliogundulika karne kadhaa zilizizopita wameshatengenezewa filamu nyingi na wasanii mbalimbali duniani (tutazichambua huko mbele). Aliens wapo wa rangi tofauti kama kijani, weupe, weusi, njano, zambarau na kila aina ya rangi. Inaaminika kuwa Aliens wanaoishi angani wana akili nyingi kuliko binadamu. Wana mfumo wa kompyuta uitwao Alien Software na wapo juu kiteknolojia kuliko binadamu, tatizo tu hawavai nguo! Ngoma nzito hapo mkuu ndo maana rubani wa MH370 flight alipampana vilivyo wale jamaa wakazima switchi za mawasiliano kama upepo vile upulizavyo mshumaa.

Tofauti na binadamu ambaye anafanya kazi kwa hatua moja kwenda nyingine, Aliens wao hufanya mambo kinyume kabisa. Kwa mfano wakitaka kusema ‘naomba maji’ husema ‘maji naomba’ yaani cha nyuma kinakwenda mbele na cha mbele kinarudi nyuma. Kama tunavyowashangaa, nao pia wanatushangaa na kutuona viumbe wa ajabu.

Wachambuzi wa mambo ya anga walishaandika ripoti nyingi kuhusu viumbe hao ambao huja duniani na kurudi angani. Swali ni je, viumbe hao wanaishi katika sayari gani? Wataalam hao wanalijibu swali hilo kwa kusema haijulikani moja kwa moja wanaishi sayari gani lakini kwa uhakika siyo kwenye mwezi (kumbuka mwezi siyo sayari). Inawezekana bado hujaelewa simulizi hii. Bermuda Triangle ni eneo la pembetatu la bahari lililopo kati ya nchi tatu katika Bahari ya Atlantiki. Miaka kadhaa huko nyuma viumbe hao waliwahi kutua eneo hilo na kuweka historia (nitaisimulia huko mbele). Eneo hili limeshapoteza ndege sita sasa na hazijawahi onekana tena ikiwamo ya juzi Boeing 777 Malaysian Airliness Flight.

Pia waliwahi kuonekana Kisiwa cha Bermuda pwani ya Mashariki mwa Marekani, Kisiwa cha Puerto Rico kilichopo Kaskazini mwa Carrebian na Fort Lauderdale huko Florida, Marekani. Umewahi kusikia vitu mbalimbali duniani vikisemekana vimepotea katika mazingira ya kutatanisha? Aliens wanahusishwa na upoteaji wa meli baharini hasa za mizigo huku watu wakiamini huwa zinazama lakini uchunguzi ukifanyika meli hizo huwa hazionekani hata ndani ya maji baharini. Msiba wa Boeing 777

Aliens wanatajwa kuhusika na upotevu wa watu duniani ikiaminika kuwa labda watu hao walikufa lakini ukweli ni kwamba huchukuliwa na viumbe hao. Ndege za kijeshi zimeripotiwa mara nyingi kupotea au kutokuonekana milele katika eneo la Bermuda Triangle ikieleza kuwa Aliens ndiyo wahusika wa upotevu huo.Ujio wa Aliens katika eneo la Bermuda Triangle ulisababisha kisiwa hicho kupata umaarufu duniani na kupewa jina la Devil’s Sea (Bahari ya Shetani) ambapo binadamu wamekuwa wakiamini au kujenga imani potofu kuwa shetani amekuwa na makazi katika eneo hilo na kuwapoteza wasafiri wa majini. Wengine huhisi ni ushirikina.

Wapo binadamu wanaoamini kuwa Aliens walikuwepo duniani tangu enzi hizo kabla ya binadamu na hawajaondoka.Si sehemu hizo pekee lakini wamekuwa wakitua maeneo mbalimbali duniani na kuna baadhi ya serikali duniani zinawajua. Wataalam wa anga wanadai Aliens wako mbali kimaendeleo na wanafanya wanavyotaka. Hivyo basi kuhusu hiyo ndege wao ndo wajua wataifanyaje na hao walokuwemo.
 
Google eti aliens wana exist.nijibu tafadhali maana kila kitu kinapatikana kwako
 
bila shaka abiria wa Malaysian Airline washafanywa kitoweo
 
Hivi ni vitu visivyotambulika vinavyopaa au kudondoka kutoka angani. Vitu hivi vinatajwa kuwa na uhusiano mkubwa na aliens na wanasayansi wa Kimarekani.
Hizi UFO zipo za aina mbili. Kuna zinazotoka katika uso wa dunia ambako kuna watu waliostaarabika. UFO nyingine ipo nje ya uso wa dunia inawezekana angani au katika sayari nyingine.
Ukiachilia mbali vimondo unaweza ukaona kitu kinang’aa angani na ghafla kikapotea kutokana na spidi yake. Hizo ndizo UFO.
Mara nyingi vitu hivi vimekuwa vikionekana katika rada za duniani akiwemo aliens maarufu waitwao Ashar Sheran na Valiant Thor kutoka Sayari ya Venus.
Inasemekana kuwa nchi zilizoendelea hasa Marekani huwa hawataki vitu kama UFO au hawa aliens wawe na ukjaribu na nchi masikini kwani nazo zitakuwa na nguvu ya kuzifikia au kuzipita kabisa.
Watu wengi hawafahamu kiundani kuhusu UFO. UFO ikipita kwa mdano Dar es Salaam, wakati wa shughuli za mchana inaweza kusababisha taharuki kwa watu na ajali nyingi kwa wakati mmoja.
Katika kutafuta undani juu ya mambo haya, mtunzi na mwandishi mashuhuri duniani, James Hadley Chase kupitia kitabu chake cha Dooms Day Conspiracy alijaribu kuelezea habari za hawa UFO vizuri, namna serikali kubwa zinavyoficha uwepo wa aliens na UFO kwa kuhofia kuzusha hofu kwa raia.
Ukweli utabaki palepale kuwa kuna viumbe wanaoishi nje ya dunia ambao wana teknolojia kubwa kuliko ya binadamu na kinachotokea mara kwa mara ni kwamba huwa vyombo vyao angani vinakuja duniani.
Unakumbuka kile chombo cha aliens kilichodondoka nchini Mexico? Ilisemekana kuwa kilipodondoka tu ndege za kijeshi za Kimarekani zilifika ndani ya muda mfupi ambapo wanasayansi walikibeba na kukipeleka makao yao makuu, NASA. Wanasayansi watano wa Marekani waliowahi kujishughulisha sana na utafiti juu hawa viumbe walifanikiwa kugundua lugha yao.
Mmoja wa wanasayansi hao alipojaribu kuvujisha siri katika vyombo vya habari, wanasayansi hao walipotea katika mazingira ya kutatanisha na hawakuonekana tena.
Nchi kubwa kama Urusi, Marekani, China, Uingereza na Japan zina hofu kubwa juu ya aliens kwamba wakipata nafasi ya kujitanua kiteknolojia hapa duniani itakuwa ndiyo mwisho wa ustaarabu wa binadamu ndiyo maana zinajitahidi sana kuzuia au kujipa wenyewe teknolojia yao ili itakapotokea aliens wakavamia duniani wao wawe tayari wamejiweka vizuri.

Na wewe ukaamini kama zuzu..
 
Vitabu vya Mungu vinatuhusu sisi binadamu tunaoishi hii sayari tunayokanyaga na kuringia mafao, hao Alliens wenyewe maisha yao ni huko sayari zingine dunia hii siyo mahala pao!

Wanazaliwa kwa njia ya mbegu alafu wanakufa kama binadamu anavyokufa...

Ha ha ha ha ha.....Dahhh!!! Hakuna Sayari inayo-support life zaidi ya Dunia hii....

Prove to me the existance of any planet other than Earth that support any kind of life...Ukiweza hapo sasa tutaweza ongea habari za hao Alliens.
 
zakuambiwa changanya na zakwako mkuu
internet inafundisha mengi na inadanganya mengi

Hakuna kitu kama hicho zaidi ya theories zilizozagaa kwenye website kibao tena zikiwa na picha na video
anyway amani unavyo amani

Watu wanaamini "true lies" za Internet...Kaazi kweli kweli..
 
Mkuu unaamini kuwa binadamu alikuwa sokwe?

Hakuna kitu ambacho sitakaa kuamini kama eti binadamu wakikuwa nyani tetete halafu nyani wenyewe walikuwa weusi sasa wazungu walitokea wapi? Au wazunhu walitokea kwa adam na hawa
 
thread nyingine bhana, full vichekesho hadi raha teh teh teh
 
Kuna maswali mengine ukijiuliza huwezi kupata jibu kabisa, kwa mfano mi huwa najiuliza kama bahari ingekuwa SUPU, chapati zingetosha kweli?
 
Kama wewe unaamini uwepo wa Mungu,malaika na majini,basi ujue Alliens wapo.Kama huamini,basi subiri siku utakayokubali kuamini.Then utajua alliens ni kiumbe gani.
 
Papa Mopao usiamini video za youtube,juzi nilikuwa napitia forum moja kuna jamaa alivujisha siri za NASA,kwamba alikuwa mtaalam wa kuedit video na kutumia photoshop,kwahiyo kazi yake huko NASA ilikuwa kutengeneza picha fake za huko space ili kuaminisha watu na kupima upepo unaendaje,kwahiyo usiamini youtube.
C.C utafiti
 
Last edited by a moderator:
Aisee, wanakula wanachokula si lazima kiwe kama chakula chetu. Kwanza hata wao maisha si lazima yawe kama yetu.
 
Papa Mopao usiamini video za youtube,juzi nilikuwa napitia forum moja kuna jamaa alivujisha siri za NASA,kwamba alikuwa mtaalam wa kuedit video na kutumia photoshop,kwahiyo kazi yake huko NASA ilikuwa kutengeneza picha fake za huko space ili kuaminisha watu na kupima upepo unaendaje,kwahiyo usiamini youtube.
C.C utafiti

Mkuu hawa watu wanachezea tu akili zetu hakula lolote. Mtu anaamini kila anachokiona google.com ndio chenyewe hakuna kabisa. Ni uwezo wao mkubwa wakutumia computer basi
 
Last edited by a moderator:
Kama sayari moja iitwayo dunia inaviumbe vya aina mbali mbali na sayari zipo zaidi ya bilions katika galaxies zingine tofauti na ya kwetu naimani kutakuwa na form of life in other planets too apart from being quite different from that of earth/ours or the same.
Mungu ameumba viumbe vinavyoonekana na visivyo onekana na vitabu vinaonesha haviko tu hapa, vingine viko ardhini na vingine vipo angani. Kwanini sasa tusijiulize swari rahisi tu kuwa je ''Hakuna uwezekano wa hizo sayari zingine kuwa na viumbe ambavyo sisi binaadamu hatuvioni kwa macho yetu ya kawaida?''
 
Back
Top Bottom