Hivi Bongo tunasoma ili iweje?

Hivi Bongo tunasoma ili iweje?

Tunasoma ili tujue kusoma, kuandika na kuhesabu basi.
 
Rich dad poor dad kitabu ambacho kina majawabu ya maswali yako yote.
Labda kwa faida ya wengi
Screenshot_20231004-113852.png
 
Wakuu habari,

Hivii Tanzania tuna soma ili iweje.Mataifa yote duniani elimu inatumika kumkomboa mwananchi kutoka mazingira duni na kuyaboresha , kuyatawala mazingira na si mazingira kumtawala mwanadamu.

Hapa nyumbani tuna baadhi ya vyuo venye kozi mbali mbali ambazo kwa macho ya nyama unaona zina tija lakini katika hali halisi vijana wanalalamika ajira hamna.

Na Wakati ajira zikionekana amna kuna utitiri wa mazao na rasilimali zinazolishwa Tanzania na kuuzwa njee kama malighafi na si bidhaa, nashindwa kuelewa sasa kama tuna wanafunzi wanaograduate kila siku na still amna innovations zinazotokana na elimu hizo au adaptation ya teknolojia kutoka nje ili kuongeza thamani malighafi zetu za ndani na ziuzwe njee kama bidhaa kamili sasa tunasoma na kutoa ela ndefu kwenye mikopo ili iweje?

Tanzania inajikuta katika changamoto kubwa za elimu na ajira, huku vyuo vikuu vikitakiwa kuwa injini ya mabadiliko ya kijamii na kiuchumi.

Hali hii inakinzana na dhima ya elimu duniani, ambayo ni kumkomboa mwananchi kutoka kwenye umaskini na kuboresha mazingira yake.

Vyuo vikuu nchini vinatoa kozi mbalimbali, lakini vijana wanalalamika kuhusu ukosefu wa ajira, wakati huo huo kuna utitiri wa malighafi zinazozalishwa Tanzania na kuuzwa nje kama malighafi tu, bila kuongeza thamani.

Kuna haja kubwa ya kubadilisha mfumo wa elimu ili kuchochea uvumbuzi na teknolojia, na kuongeza thamani ya malighafi za ndani ili ziuzwe nje kama bidhaa kamili.

Kutoa mikopo kwa wanafunzi ni hatua nzuri, lakini inapaswa kuelekezwa kwa njia ambayo itawawezesha kuanzisha miradi yao wenyewe na kuchangia katika maendeleo ya jamii.

Walimu wanapaswa kuwa mifano inayotoa mabadiliko ya kijamii, na elimu inayotolewa inapaswa kuhamasisha ujasiriamali na uvumbuzi.

Ni muhimu kuanzisha vituo vya uvumbuzi ndani ya vyuo vikuu ambavyo vitakuwa kazi yake kuvumbua majawabu ya changamoto za jamii kupitia wanafunzi wa taaluma husika.

Wanafunzi wanapaswa kupata fursa ya kutumia elimu yao kuleta mabadiliko katika jamii kwa kubuni suluhisho za changamoto za kitaifa na kimataifa.

Vyuo kama vile Chuo Kikuu cha Dodoma na Dar es Salaam vinaweza kuwa kiongozi katika kuleta mabadiliko ya kielimu na kijamii.

Elimu inapaswa kuwa chanzo cha tija na maendeleo, na wanafunzi wanapaswa kufundishwa kwa namna inayowawezesha kuwa nguvu ya mabadiliko katika jamii zao.

Tunapaswa kuwa na mtazamo mpya wa elimu na kuhakikisha inatoa thamani halisi kwa jamii yetu. Hii ndiyo njia ya kufikia lengo la kusoma ili kuwa na mabadiliko ya kweli nchini Tanzania na kuwa na vyuo vikuu vinavyochochea uvumbuzi na maendeleo endelevu..
Kusoma ni kitu personal sana cha mtu

Nachojua tunasoma tupate uelewa,kutanua uwezo wetu wa kufikiri na kupata majawabu mazuri na endelevu ya shida zetu kama wanadamu

Sasa kama unaenda kusoma kama somekind fulani hivi ya financial transaction au eti ili uweze kua mwanadamu wa kuajirika ufanyie kazi systems kama roboti,basi kuna tatizo mahali utakua hujui umekuja duniani kufanya nini hasa

Nachojua best skill to ever have ni to know how to make best decisions on everything!
 
Kusoma ni kitu personal sana cha mtu

Nachojua tunasoma tupate uelewa,kutanua uwezo wetu wa kufikiri na kupata majawabu mazuri na endelevu ya shida zetu kama wanadamu

Sasa kama unaenda kusoma kama somekind fulani hivi ya financial transaction au eti ili uweze kua mwanadamu wa kuajirika ufanyie kazi systems kama roboti,basi kuna tatizo mahali utakua hujui umekuja duniani kufanya nini hasa

Nachojua best skill to ever have ni to know how to make best decisions on everything!
wengi wanasoma kwasababu ya hii option ya pili, muuulize kijana kwa nini kozi hii na sio ile utaona jibu lake
 
wengi wanasoma kwasababu ya hii option ya pili, muuulize kijana kwa nini kozi hii na sio ile utaona jibu lake
Ndio maana wanaposhindwa maisha wanaanza kusingizia zile "elimu" zao walizonunua kama commodity dukani kwamba watapata faida wakija kuiuza

Wanachoshindwa kujua ni kwamba kupata mali na kupata elimu ni vitu viwili tofauti

Kupata elimu kama bidhaa eti ili uje uize baadae upate faida ni biashara ya ajabu maana kuna kupata hasara au faida,wakipata hasara wanaanza kulia

Kuliko kufanya hiyo biashara ni heri ufanye biashara ya kawaida kabisa ya kuuza tangible products kwa wanadamu wengine wakulipe

Watu wanatafuta uelewa na how to think effectively to help them to solve problems in their lives and not otherwise.

Getting money or not getting money is the by-product!
 
Ndio maana wanaposhindwa maisha wanaanza kusingizia zile "elimu" zao walizonunua kama commodity dukani kwamba watapata faida wakija kuiuza

Wanachoshindwa kujua ni kwamba kupata mali na kupata elimu ni vitu viwili tofauti

Kupata elimu kama bidhaa eti ili uje uize baadae upate faida ni biashara ya ajabu maana kuna kupata hasara au faida,wakipata hasara wanaanza kulia

Kuliko kufanya hiyo biashara ni heri ufanye biashara ya kawaida kabisa ya kuuza tangible products kwa wanadamu wengine wakulipe

Watu wanatafuta uelewa na how to think effectively to help them to solve problems in their lives and not otherwise.

Getting money or not getting money is the by-product!
Umeandika vyema
 
Mkuu sometimes nitakuwa nikikuita sana kwenye comments za watu wenye uhalisia wa jina lako
😆😆😆😆😆
🤓🤓🤓🤓🤓🤓🙌🙌🙌🙌🙌
Alafu mwenye jina nipo understanding kinoumaaaaaa
 
🤓🤓🤓🤓🤓🤓🙌🙌🙌🙌🙌
Alafu mwenye jina nipo understanding kinoumaaaaaa
Leo kazi yangu nikuwatafuta watu wote wenye haiba ya jina lako.
Usichukie wala kuchoka pale nikuitapo.
 
Leo kazi yangu nikuwatafuta watu wote wenye haiba ya jina lako.
Usichukie wala kuchoka pale nikuitapo.
Sawa sawa mkuu wee wabatize tuu.....
Kikosi jeshi. 07 🤓🤓🤓🤓🤓🤓🤓
 
Mawazo yako ni sehemu ya madhara ya kua na elimu duni, mtu wa kulaumu katika nchi hi ni mwl Nyerere, hakutaka kuelimisha wa Tanzania zaidi ya kuwapa basics za elimu tu.
Huyo Nyerere ameondoka madarakani lini?Kwa nini hamkubadilika kwa kuona ya kwake yaliwapotosha?Hapo mjinga na mwehu ni nani?
 
Mawazo yako ni sehemu ya madhara ya kua na elimu duni, mtu wa kulaumu katika nchi hi ni mwl Nyerere, hakutaka kuelimisha wa Tanzania zaidi ya kuwapa basics za elimu tu.
Wewe ndio huelewi hata Transition ya Elimu yetu

Mwl. Nyerere si ndiye aliyeleta Elimu ya Ujamaa na Kujitegemea?

Wakati wake si ndio tulipata Mabwana Shamba na Mabibi Shamba wabobezi, Ma carpenter wazuri, Washonaji wazuri wa nguo mpaka batiki

Si ndiye alisisitiza kuwepo na vyuo vya ufundi kina Arusha Tech, Mbeya Tech na Moshi Tech?

Angalia waliosoma Middle School walivyokuwa vizuri

Sasahv elimu ndio imekuwa hovyo
 
Back
Top Bottom