Hivi Bunge la Tanzania linafanya kazi gani hasa?

Hivi Bunge la Tanzania linafanya kazi gani hasa?

MAHANJU

JF-Expert Member
Joined
Aug 26, 2014
Posts
5,252
Reaction score
8,003
Tunapojiita kua tuna bunge badala ya kufanya kazi ya kuishauri na kuisimamia serikali badala yake linafanya kazi ya kuitetea serikali ni hasara kwa taifa kupoteza mabilioni ya shilingi kuwalipa mishahara.

Mmekaa mnapitisha tozo ambazo ni maumivu kwa Watanzania tena kwa kishindo mnagonga meza. Mmetusaliti wapiga kura wenu kwa kiasi kikubwa na mimi kama kada mkongwe wa CCM ninaomba Mungu 90% ya wabunge msirudi bungeni 2025, mnakula mishahara isiyokuwa stahiki yenu.

Mnaona raha tu mnapitisha kitu mpaka watanzania wanapiga kelele na Mhe Rais anatoa maagizo anaona si sawa, ninyi hamna sifa kabisa za kua wawakilishi. Mlienda kumwakilisha nani Kama mnawageuka wapiga kura wenu?
 
Bunge letu ni la WAPIGAJI hakuna wanachofanya.

Kumuwakilisha mwananchi:----- Mambo mengi wanayoyapitisha mara zote wananchi wanayakataa ina maanisha Bunge ni Rubber Stamp ya mambo ya serikali.
 
Tunapojiita kua tuna bunge badala ya kufanya kazi ya kuishauri na kuisimamia serikali badala yake linafanya kazi ya kuitetea serikali ni hasara kwa taifa kupoteza mabilioni ya shilingi kuwalipa mishahara...
Bunge la Tanzania lingekataa kupitisha hiyo sheria ya utekeleza wa bajeti lingevunjwa na uchaguzi ungefanyika tena.
 
Waliposema wanaua upinzani mkashangilia tuisome namba sisi wapinzani wanaccm wanyamaze kabisaaaaa hizi tozo haziwahusu
 
kikubwa zaidi kwa mbunge ni ukomae kiganja kwa kupiga meza vingine kusifu kujipendekeza na kukejeli wenye maoni tofauti ni nyongeza tu
 
Kupiga meza na kumtukuza Rais, kwani kuna aliye wapigia kura?
 
Kwa mtazamo wangu, bunge hata lingefutwa sioni tatizo lolote zaidi ya kupata FAIDA zaidi, tutabana matumizi ya fedha nyingi sana ambazo zaweza kujenga hizo barabara za vijijini na hata bwawa la umeme na reli yetu ya umeme. Siioni value for money kwa bunge la Ndugai, halina maana yeyote
 
Metusaliti wapiga kura wenu kwa kiasi kikubwa na mimi kama kada mkongwe wa CCM ninaomba Mungu 90% ya wabunge msirudi bungeni 2025, mnakula mishahara isiyokuwa stahiki yenu.
Kada gani mkongwe halafu kichwani huna kitu?Unavyodai 2025 asilimia 90 wasirudi bungeni kwani hawa wa sasa hivi wana kibali cha wananchi?Kwani hili bunge la sasa hivi ni bunge la wananchi?Yaani namaanisha kwani wamechaguliwa na wananchi?
 
Tunapojiita kua tuna bunge badala ya kufanya kazi ya kuishauri na kuisimamia serikali badala yake linafanya kazi ya kuitetea serikali ni hasara kwa taifa kupoteza mabilioni ya shilingi kuwalipa mishahara...
Mkuu Tanzania hakuna Bunge,hilo ni genge la wahuni Shenz taipu wa CCM

Sent from my Infinix X688C using JamiiForums mobile app
 
Wengi hawatarudi bungeni baada ya 2025, maana aliyewaweka hayupo.
 
Back
Top Bottom