Hivi hawa ambao kila siku wanaporomosha Maghorofa ya Kupangisha DSM hali hii ngumu hawaioni au watapangisha Kuku?

Hivi hawa ambao kila siku wanaporomosha Maghorofa ya Kupangisha DSM hali hii ngumu hawaioni au watapangisha Kuku?

binadamu tunafanana kimaumbile ila tuna tofauti kubwa sana kwenye kufikiri we unaweza kuwa unaviona vyuma vilivyokaza Leo ila tuna wanaoona vyuma vitakavyolegea kesho na keshokutwa
 
Awamu hii wale waliogawanaga masandarusi wanasodoa tu mdogo mdogo, maisha yanasonga wakila zao popcorn huku wanawacheki wale mnaokula msoto mkilalamikia "eti vyuma vimekaza!"
Wamemtoa kafara mzee Ruhr na Singa singa
 
Kuna rafiki yangu kaajiriwa mwaka huu mwanzoni juzi amenunua Passo nikampigia kumpa hongera nikamwambia "Kaka naona mambo siyo magumu kabisa" akajibu "Nasikia sikia tu watu wanadai maisha magumu ila mi siamini" alinifurahisha sana.
Huyo mtu uskute katokea mpakan mwa Uganda aisee... Maana watu wa hzo sehem ni balaa
 
Tena kwa jeuri ananunua ghorofa/nyumba hata kumi haraf mabak anagawa bure ndo anapandsha mzgo wake, na kumbuka weng wanaobomolewa nyumb hawajeng tena Bali wanaishia kupanga, sasa kama amebomoa nyumb za kuish mfn kumi au ghorofa, i long view utagundua lazma kati ya waliobomolewa watarud kupanga direct au indirect, kwaio hata wasije kwake kuna mwingne aliebomoa huko nao watakuja kwa huyu na hawa wataenda kwa yule, Huo ndo mzunguko wa mambo, unageuzwa fursa au mtumwa bila kujijua

Hahaaaa na sisi wazee wa "Kwangu pakavu tia mchuzi" ndo tunaongozwa kwa kutumiwa zile msg za waganga "Mjukuu wangu nimekuagua umepata mali umenisahau"

Na ukiona zile msg zinakuandama hahaaaa my friend rud kwa wazee waulize umewakosea nini.....
 
Kwa wenye pesa/uchumi mzuri, huu ndio wakati hasa wa kuwekeza. Nakumbuka wakati wa recession huko Marekani real estates agencies nyingi zilipatwa na ukata, nyumba nyingi zilichukuliwa na mabenki kisa watu wameshindwa kulipa, baadhi ya benki zilikuwa liquidated lakini watu wa level ya kina Trump, Buffet, nk walizidi kuwekeza.

Nakumbuka kuangalia CNBC/CNN interview moja Warren Buffet akasema huu ndio wakati wa kununua, sio kuuza. Tunanunua mali za wale walioshindwa kujiendesha kwa bei ndogo, uchumi ukikaa sawa tutauza kwa faida kubwa.

Sasa kama wewe huna pesa saivi hata plot ya 20x20 tu ni mtihani, lakini viwanja vimeshuka bei, nyumba zinauzwa sana, wenye nazo wanaendelea kuwekeza.
 
Wenye hela bado wapo tu wengi tembea kwenye kumbi za starehe uone watu wanavyokula maisha
Kula maisha doesn't mean kwamba watu wana hela ni bac tyu kutoa stress mm mwenyew nina njaa kinoma ila weekend lzm unikute viti virefu nimevimbaaa
 
Wateja wapo

Hauhitaji uwe tajiri uishi sehemu nzuri.

Ni mipango tu.

Watu wanapoteza hela chingi kwenye mambo ya hovyo wanashindwa hata kulipa chapaa kukaa sehemu nzuri.

Mimi na partner wangu tunalipa $200 apartment tunakaa hapa Arusha.

Tunalipa chapaa sawa na lazima tuwe na budget ya rent.

Nani anamuda wa kupanga chumba na kuanza nunua vitu wakati anytime you may leave?

Apartment zinakuja nahuduma. Na hizi huduma ndiyo watu wanapenda.

Hapa ninakaa najisikia amani. Kidogo msongo wamawazo unapungua nafanya kazi kwa weledi.

Ni kujipanga na kukomaa tu.

Economy won't get better if you won't get better.

Binafsi huwa naona chumi za nchi za Afrika kila siku zinadidimia tu.

Ukiwa na chanzo kimoja cha mapato hata kama unaingiza chapaa nyingi upo hatarini tu.

Binafsi si tajiri lakini pia si mtu wa shida lukuki.

Najitahidi kuishi kwa budget.

Sehemu ya kuishi kwangu ni priority number one.

Kuliko nirent sehemu yenye mkusanyiko mkubwa wa watu bora nikaishi kwenye tent porini nje ya mji.
 
Katika Watanzania 500 badi 457 wanalia hali mbaya ya Uchumi a.k.a Vyuma Vimekaza halafu hapo hapo tena kuwa Watu wanathubutu kabisa Kujenga Maghorofa makubwa makubwa ya Kupangisha ( Apartments ) hivi humo wanategemea Kupangisha Binadamu au labda wataweka tu pengine ' Mifugo ' yao kama Kuku, Bata, Mbuzi na pengine hata Ng'ombe?

Kazi ipo hakyanani!

Nawasilisha.
Kujenga ndiyo biashara yao, na wao kukosa wateja wa kupanga vyuma vimekaza
 
Katika Watanzania 500 badi 457 wanalia hali mbaya ya Uchumi a.k.a Vyuma Vimekaza halafu hapo hapo tena kuwa Watu wanathubutu kabisa Kujenga Maghorofa makubwa makubwa ya Kupangisha ( Apartments ) hivi humo wanategemea Kupangisha Binadamu au labda wataweka tu pengine ' Mifugo ' yao kama Kuku, Bata, Mbuzi na pengine hata Ng'ombe?

Kazi ipo hakyanani!

Nawasilisha.
Mkuu,
Sema "NINA HALI NGUMU"
Usiseme " TUNA HALI NGUMU"
 
Back
Top Bottom