Robert Heriel Mtibeli
JF-Expert Member
- Mar 24, 2018
- 28,297
- 68,017
Wakuu kwema!
Aisee! Baada ya kutoka kuzurura huko Duniani, sitaki kupataja nisijeonekana najikosha hapa, na wenye nongwa zao na vijiba vya roho wasije nitolea mvuke wa ushubwada. Ila ifahamike tuu nimetoka huko Dunia ilipo.
Kwa kweli Dar inanuka vibaya mno. Inanuka vitu mfano wa mavi, sijasema ni mavi jamani Ila ni kama hivyo.
Yaani Asilimia kubwa ya Maeneo yananuka chemba za maji taka. Nashindwa Kueleza hapa. Sitaki kugombana na wenye Dar yao, sitaki kabisa. Maana najua wapo wanayoipenda, ikumbukwe siiongelei Jambo hili Kwa ni mbaya lakini naongea ili Jambo Fulani lifanyike.
Halafu ukiwaona wakazi wa Dar ni Kana kwamba hawaisikii hiyo harufu, pengine wamekuwa sehemu ya harufu yenyewe, sijasema watu wa DAR mnanuka chemba za maji taka 😃😃😃. Maana wenye hasira hamkosekani.
Hata hivyo akili yangu ikanambia sio rahisi watu WA DAR kuisikia hiyo harufu mbaya ya mavi Kwa maana maisha yao ni ya taabu sana. Taabu zimeua mishipa ya Nostril ndani ya pua. Hawezi kunususa tena.
Hasa watu masikini wapanda Daladala, hawa ndio wanaoonja joto ya jiwe, hata hivyo wenyewe ni Kama joto Hilo hawalisikii kwani taabu imewafubaza na kuwafanya waone kila kitu Kama kipo Sawa.
Kipindi nasoma pale UDSM wala sikuwa najua Dar inanuka, nimekaa zaidi ya miaka mitano kama sio sita sikuwa naona hizo harufu. Labda Maeneo ya Tandale huko na viunga vya makazi ya WALIA NA MUNGU watu fukara apeche Alolo.
Najiuliza niliwezaje kuishi miaka mitano kipindi kile?
Nafikiri serikali ipitie tena miundombinu ya taka hasa mitaro ya maji taka ili mji usiwe jiji la harufu mbaya.
Wananchi wa Dar nanyi mjitahidi kuwa wasafi hata kama mmezoea harufu yenu mbaya kumbukeni wageni kama Sisi tunaotoka Duniani tunakujaga pia kuwasalimu.
Muwe na Haya hata kidogo.
Taikon nitakuwa DAR Kwa wiki tatu mfululizo kabla sijaenda kudhuru Zanzibar nikielekea kuchumbia Visiwa vya Comoro.
Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Aisee! Baada ya kutoka kuzurura huko Duniani, sitaki kupataja nisijeonekana najikosha hapa, na wenye nongwa zao na vijiba vya roho wasije nitolea mvuke wa ushubwada. Ila ifahamike tuu nimetoka huko Dunia ilipo.
Kwa kweli Dar inanuka vibaya mno. Inanuka vitu mfano wa mavi, sijasema ni mavi jamani Ila ni kama hivyo.
Yaani Asilimia kubwa ya Maeneo yananuka chemba za maji taka. Nashindwa Kueleza hapa. Sitaki kugombana na wenye Dar yao, sitaki kabisa. Maana najua wapo wanayoipenda, ikumbukwe siiongelei Jambo hili Kwa ni mbaya lakini naongea ili Jambo Fulani lifanyike.
Halafu ukiwaona wakazi wa Dar ni Kana kwamba hawaisikii hiyo harufu, pengine wamekuwa sehemu ya harufu yenyewe, sijasema watu wa DAR mnanuka chemba za maji taka 😃😃😃. Maana wenye hasira hamkosekani.
Hata hivyo akili yangu ikanambia sio rahisi watu WA DAR kuisikia hiyo harufu mbaya ya mavi Kwa maana maisha yao ni ya taabu sana. Taabu zimeua mishipa ya Nostril ndani ya pua. Hawezi kunususa tena.
Hasa watu masikini wapanda Daladala, hawa ndio wanaoonja joto ya jiwe, hata hivyo wenyewe ni Kama joto Hilo hawalisikii kwani taabu imewafubaza na kuwafanya waone kila kitu Kama kipo Sawa.
Kipindi nasoma pale UDSM wala sikuwa najua Dar inanuka, nimekaa zaidi ya miaka mitano kama sio sita sikuwa naona hizo harufu. Labda Maeneo ya Tandale huko na viunga vya makazi ya WALIA NA MUNGU watu fukara apeche Alolo.
Najiuliza niliwezaje kuishi miaka mitano kipindi kile?
Nafikiri serikali ipitie tena miundombinu ya taka hasa mitaro ya maji taka ili mji usiwe jiji la harufu mbaya.
Wananchi wa Dar nanyi mjitahidi kuwa wasafi hata kama mmezoea harufu yenu mbaya kumbukeni wageni kama Sisi tunaotoka Duniani tunakujaga pia kuwasalimu.
Muwe na Haya hata kidogo.
Taikon nitakuwa DAR Kwa wiki tatu mfululizo kabla sijaenda kudhuru Zanzibar nikielekea kuchumbia Visiwa vya Comoro.
Robert Heriel
Taikon wa Fasihi