Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Dah kama Uko kwenye kichwa changu ..pale sinza kijiwe asikuambie mtu ..halafu masela na mamantilie hawana noma wala nini ..njo sasa huku karibu na ubungo mawasiliano Uko ndio balaa kwenye ile mitaro wanapitisha sijui nini ...kuna hewa nzito plus joto plus matatizo wooii..Ni kweli...
Ile barabara ya Sinza kijiweni kuelekea kwa mtogole inanuka mavi..nadhani wanapitisha maji ya chooni kwenye mtaro wa maji. Ndo Sinza kwa wajanja hiyo
Pembeni kuna chips tamu kinoma na chachandu ya ukwajuMaeneo ya sinza ndio balaa mkuu unaeza kudhani Uko chooni halafu mbaya zaidi wamamantilie wanauza chakula hapo hapo, wauza kahawa dah ni balaa hii dasalama yetu ..
Hahahaha ukichanganya na matunda ..bora ivyo vya kupikwa ..hayo matunda yanavyokatwa katwa halafu chini ya mitaro umo mizigo inapita tu kama kawaida unakula zako na harufu yako maisha yanaendelea.Pembeni kuna chips tamu kinoma na chachandu ya ukwaju
Huyu aende mkoani tu asituchoshe kwa kweli hahahaHamia mkoani mkuu utuachie dar yetu
Mkuu mimi nimekuelewa, na sina tatizo na hiyo observation yako, kwa sababu ni kweli once unapotoka nje ya Africa na kama umekaa kwa muda mrefu kidogo, ukishuka na kutoka tu hapo JNIA mfumo wako wa upumuaji unapata taarifa.Wakuu Kwema!
Aisee! Baada ya kutoka kuzurura huko Duniani, sitaki kupataja nisijeonekana najikosha hapa, na wenye nongwa zao na vijiba vya roho wasije nitolea mvuke wa ushubwada. Ila ifahamike tuu nimetoka huko Dunia ilipo.
Kwa kweli Dar inanuka vibaya mno. Inanuka vitu mfano wa mavi, sijasema ni mavi jamani Ila ni Kama hivyo.
Yaani Asilimia kubwa ya Maeneo yananuka chemba za maji taka. Nashindwa Kueleza hapa. Sitaki kugombana na wenye DAR Yao, sitaki kabisa. Maana najua wapo wanayoipenda, ikumbukwe siiongelei Jambo hili Kwa ni mbaya lakini naongea ili Jambo Fulani lifanyike.
Alafu ukiwaona wakazi wa Dar ni Kana kwamba hawaisikii hiyo harufu, pengine wamekuwa sehemu ya harufu yenyewe, sijasema watu wa DAR mnanuka chemba za maji taka [emoji2][emoji2][emoji2]. Maana wenye hasira hamkosekani.
Hata hivyo akili yangu ikanambia sio rahisi watu WA DAR kuisikia hiyo harufu mbaya ya mavi Kwa maana maisha yao ni yataabu Sana. Taabu zimeua mishipa ya Nostril ndani ya pua. Hawezi kunususa tena.
Hasa watu masikini wapanda Daladala, hawa ndio wanaoonja joto ya jiwe,hata hivyo wenyewe ni Kama joto Hilo hawalisikii kwani taabu imewafubaza na kuwafanya waone kila kitu Kama kipo Sawa.
Kipindi nasoma pale Udsm wala sikuwa najua DAR inanuka, nimekaa zaidi ya miaka mitano Kama sio sita sikuwa naona hizo harufu. Labda Maeneo ya Tandale huko na viunga vya makazi ya WALIA NA MUNGU watu fukara apeche Alolo.
Najiuliza niliwezaje kuishi miaka mitano kipindi kile?
Nafikiri serikali ipitie tena miundombinu ya taka hasa mitaro ya maji taka ili mji usiwe jiji la harufu mbaya.
Wananchi wa Dar nanyi mjitahidi kuwa wasafi hata Kama mmezoea harufu yenu mbaya kumbukeni wageni Kama Sisi tunaotoka Duniani tunakujaga pia kuwasalimu.
Muwe na Haya hata kidogo.
Taikon nitakuwa DAR Kwa wiki tatu mfululizo kabla sijaenda kudhuru Zanzibar nikielekea kuchumbia Visiwa vya Comoro.
Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Mkuu mimi nimekuelewa, na sina tatizo na hiyo observation yako, kwa sababu ni kweli once unapotoka nje ya Africa na kama umekaa kwa muda mrefu kidogo, ukishuka na kutoka tu hapo JNIA mfumo wako wa upumuaji unapata taarifa.
Hao wa hapo DSM washazoea kwa sababu hiyo harufu wako karibu nayo kwa muda mrefu kwa hiyo wamesha - merge nayo na hawahisi harufu yoyote tofauti tena.
Sisi tunaoishi huku Mikoani tuna harufu zetu pia kwa level za huku[emoji23], lakini uzuri wa huku hakuna misongamano
Wivu tu unakusumbua, au umetumwa na mabeberu, Macdm bwana!
Kuna siku Dar iliwahi kuacha kunuka? Ni moja ya Miji ya hovyo kuishi.
Mkiambiwa dhibitini ujenzi holela na kuzaana hovyo hamtaki,komaeni
Ukisikia paaaa ujue limempata.
Asante kwa kutuambia ukweli
Nafasi ya nini tena ndugu mwandishi, au nafasi ya kuwa shuhuda
Utakua unaishi karibu na chemba za Hospital moja wapo jijini
Mpaka papuchi siku hizi zinatoaa balaa
Kuna mitaa inanuka balaa.Leo nipo huku Kariakoo naomba nijifunze kunyamaza
Tunavumilia mengi mkuu ila ukweli hali yahewa nimbaya sana[emoji23][emoji23]
Kuna mitaa inanuka balaa.
Njoo Chanika upate hewa safi