Hivi hii ni sawa.? Naomba munisaidie

Hivi hii ni sawa.? Naomba munisaidie

situjadiriane

Member
Joined
Jan 5, 2023
Posts
41
Reaction score
49
Niliwahi kuandika hapa juu ya kinachoendelea katika baraza la La Ardhi wilaya mwanza
Nina Mambo mengi ambayo nitayaongea huko mbele baada ya kesi kuhukumiwa. Na ushahidi wetu uko kwenye sauti na message. Nitapenda viongozi wote wa selikari wanasheria. Mawaziri wote na kila kiongozi asikie rushwa inavyolazimishwa
Leo nataka kuuliza neno hili tulifungua kesi tukipinga kubomolewa maeneo yetu kwakuwa hatujawahi kuwa na kesi mahali popote. Hatujawahi kushitakiwa wala hatujawahi hukumiwa wala hakuna hukumu yoyote iliyotolewa juu ya maeneo yetu. Viwanja vyetu vimepimwa na kwazaidi ya miaka 20
tunalipa Kodi
Cha ajabu tuliowashitaki waligoma kufika mahakamani. Tumepeleka samasi Mara tano kwa mkono wa Dalali wa mahakama hawakuja. Hawa kujibu hata nots za wakili.
Kinacho nishangaza wanajua kila kinacho endelea. Wanajua tarehe ya hukumu na wanakueleza hukumu itakuwaje?
Swali nani natoa Siri za mahakama? Je nini kimejificha nyuma Yao. Wanajua je kila kitu wakati hawajawahi kuhudhuria hata kikao kimoja?
Wanajuaje kuwa watashinda kesi? Kiburi cha kutofika mahakani kujibu hoja wanakitoa wapi? Hayo majigambo yanatoka wapi kesi haijahukumiwa? Naomba kuwasilisha
 
Mimi Sheria sijui. Lakini hao jamaa kama Wana ukwasi ama Wana connection na viongozi wa serikali ama wao wenyewe ni viongozi Kwa Tz ya sa100 ushashindwa hta kabla ya kuendelea na kes. Pole sana
 
Back
Top Bottom