Uchaguzi 2020 Hivi hii Serikali inayodai inawatetea wanyonge, inawezaje kutapanya pesa kwa kusambaza mabango na "kuprint" T/shirt za kusambaza nchi nzima?

Uchaguzi 2020 Hivi hii Serikali inayodai inawatetea wanyonge, inawezaje kutapanya pesa kwa kusambaza mabango na "kuprint" T/shirt za kusambaza nchi nzima?

Mystery

JF-Expert Member
Joined
Mar 8, 2012
Posts
15,843
Reaction score
31,057
Kila unapotembea hivi sasa katika nchi hii utayaona mabango kwa maelfu, ya wagombea wa CCM yakiwa yamebandikwa sehemu mbalimbali za kuwanadi wagombea wao kwa uchaguzi mkuu ujao.

Vile vile katika kila mkutano wao wa kampeni, utaona mashabiki wao, wakiwemo watoto wadogo wanaosoma shule za msingi, wakiwa wamevakishwa sare za chama chao, yaani T/shirt na kofia, ambazo huwa wanapewa bure.

Sasa swali ninalojiuliza hivi sasa, hivi chama ambacho kiongozi wao mkuu, John Magufuli, huwa anajitanabaisha kuwa yeye ni mtetezi wa wanyonge, inakuwaje kifuje pesa kiasi hiki, kwa "kuprint" mabango ya wagombea wao kwa maelfu na maelfu, huku watoto wa shule za msingi, wakiwa wanakaa chini sakafuni, kwa ajili ya kukosa madawati?

Hivi unawezaje "kuprint" maelfu kwa maelfu ya T/shirt na kuwagawia bure mashabiki wenu, wakati hospitali nyingi nchini zikiwa hazina dawa muhimu za panadol?

Vile vile chama cha CCM kinaewezaje kusambaza bendera nchi nzima, na kuzitundika kwenye barabara zote kuu, wakati wanafunzi wa shule za msingi, wakiwa hawana hata uniform za kuvaa mashuleni kwao?

Imenenwa kuwa kupanga ni kuchagua, hivyo wanaccm wako tayari kufuja pesa hizo kwa mabilioni.na mabilioni, kwa ajili tu ya "kuprint" mabango ya wagombea wao, ambayo yamewagharimu mabilioni ya shilingi, wakati wafanyakazi wa Umma, hawajawaongezea mishahara yao, ambayo ni kwa mujibu wa sheria, kwa miaka 5 mfululizo, katika serikali hii ya awamu ya tano!

Kazi tunaachiwa watanzania katika uchaguzi mkuu huu ujao, aidha kuchagua chama ambacho kitaendelea kutupa mateso zaidi, kwa miaka mingine, au kuchagua chama ambacho kimetangaza neema, kwa wananchi wote wa nchi hii, kutokana na sera yake ya Uhuru, Haki na maendeleo ya watu.
 
Kila unapotembea hivi sasa katika nchi hii utayaona mabango kwa maelfu, ya wagombea wa CCM yakiwa yamebandikwa sehemu mbalimbali za kuwanadi wagombea wao kwa uchaguzi mkuu ujao..

Hizo pesa ni za CCM kwa hiyo matumizim wanaamuwa wao. Kumbuka pesa ya kuchukuwa fomu za kupendekezwa kugombea uraisi, ubunge, na udiwani inaenda kwenye mfuko wa chama. Hii ina maana chama kikiwa na wachukuwa fomu 100, kitaingiza sh millioni mia moja..huo ni uraisi tu.

CCM itakuwa imepata zaidi ya millioni 100 kwa uraisi tu. Chadema huenda millioni 4 n.k. CCM huenda kulikuwa na watia nia 500 au zaidi kwa ubunge, udiwnwani hunenda 2,000. Hizo zote pesa za chama. Ruzuku ya serkali inaenda na uwiano wa wabunge.

Hii ina maana CCM ina financial muscle hata bila vitega uchumi, baada ya CCM inafuatia CHADEMA sema tu CHADEMA financial displine & management yao ni ya ovyo.

Viongozi wakuu wachache wanaiona CHADEMA kama "cash cow" yao na hutumia mbinu mbalimbali za kiizi kuifuja pesa ya chama, tatizo ambalo CCM sasa limepunguwa lakini halijaisha.
 
Hizo pesa ni za CCM kwa hiyo matumizim wanaamuwa wao. Kumbuka pesa ya kuchukuwa fomu za kupendekezwa kugombea uraisi, ubunge, na udiwani inaenda kwenye mfuko wa chama...
Siyo kweli,

Unakumbuka maneno ya Katibu Mkuu wako Dkt Bashiru Ally?

Alikiri hadharani kuwa chama chake cha CCM kinatumia vyombo vyake vyote vya Dola, ili kuendelea kubaki madarakani.

Huwezi tofautisha chama dola na vyombo vyake vya dola, kwa hiyo chama hicho cha dola kinaweza hata "kujichotea" mabilioni kutoka kwenye Hazina yetu ya Taifa, kwa ajili ya matumizi ya chama chao.
 
Siyo kweli......................

Unakumbuka maneno ya Katibu Mkuu wako Dkt Bashiru Ally?

Alikiri hadharani kuwa chama chake cha CCM kinatumia vyombo vyake vyote vya Dola, ili kuendelea kubaki madarakani.......................

Huwezi tofautisha chama dola na vyombo vyake vya dola, kwa hiyo chama hicho cha dola kinaweza hata "kujichotea" mabilioni kutoka kwenye Hazina yetu ya Taifa, kwa ajili ya matumizi ya chama chao
Mfahamishe hiyooo
 
Hizo pesa ni za CCM kwa hiyo matumizim wanaamuwa wao. Kumbuka pesa ya kuchukuwa fomu za kupendekezwa kugombea uraisi, ubunge, na udiwani inaenda kwenye mfuko wa chama...
Sio pesa za CCM bali ni kodi za wananchi Magufuli anajichotea kama zs kwake binafsi kupitia kwa mpwa wake. Ndio maana aliondoa CAG muadilifu na kupachika jamaa yake
 
Hizo pesa ni za CCM kwa hiyo matumizim wanaamuwa wao. Kumbuka pesa ya kuchukuwa fomu za kupendekezwa kugombea uraisi, ubunge, na udiwani inaenda kwenye mfuko wa chama. Hii ina maana chama kikiwa na wachukuwa fomu 100, kitaingiza sh millioni mia moja..huo ni uraisi tu. CCM itakuwa imepata zaidi ya millioni 100 kwa uraisi tu. Chadema huenda millioni 4 n.k. CCM huenda kulikuwa na watia nia 500 au zaidi kwa ubunge, udiwnwani hunenda 2,000. Hizo zote pesa za chama. Ruzuku ya serkali inaenda na uwiano wa wabuinge. Hii ina maana ccm INA FINANCIAL MUSSLE hata bila vitega uchumi, baada ya CCM inafuatia CHADEMA sema tu CHADEMA financial displine & management yao ni ya ovyo. Viongozi wakuu wachache wanaiona CHADEMA kama "cash cow" yao na hutumia mbinu mbalimbali za kiizi kuifuja pesa ya chama, tatizo ambalo CCM sasa limepunguwa lakini halijaisha.
Mkuu kumbuka mkapa kwenye kitabu chake amekiri kuwapa CCM hela halafu wakatengeneza kashifa ya EPA
 
Siyo ivo tuu pexa za kuwalipa wasanii wap wanaotembea nao si bora wangetununulia hata madaw hospital in Amna af wanamzuia mzee ruge asigawe ubwabwa akat wap wanatembe a wasanii
 
Hayo mabango yamesambazwa na serikari au na chama?
Ulizeni ruzuku na michngo ya wabunge zililiwa na nani na kwa nini hazikufanya hiyo kazi ya mabango?
 
Hizo pesa ni za CCM kwa hiyo matumizim wanaamuwa wao. Kumbuka pesa ya kuchukuwa fomu za kupendekezwa kugombea uraisi, ubunge, na udiwani inaenda kwenye mfuko wa chama. Hii ina maana chama kikiwa na wachukuwa fomu 100, kitaingiza sh millioni mia moja..huo ni uraisi tu. CCM itakuwa imepata zaidi ya millioni 100 kwa uraisi tu. Chadema huenda millioni 4 n.k. CCM huenda kulikuwa na watia nia 500 au zaidi kwa ubunge, udiwnwani hunenda 2,000. Hizo zote pesa za chama. Ruzuku ya serkali inaenda na uwiano wa wabuinge. Hii ina maana ccm INA FINANCIAL MUSSLE hata bila vitega uchumi, baada ya CCM inafuatia CHADEMA sema tu CHADEMA financial displine & management yao ni ya ovyo. Viongozi wakuu wachache wanaiona CHADEMA kama "cash cow" yao na hutumia mbinu mbalimbali za kiizi kuifuja pesa ya chama, tatizo ambalo CCM sasa limepunguwa lakini halijaisha.
Hiyo siyo kweli Mkuu. Kama mtu ameweza kupora fedha za rambirambi ataachaje kupora fedha za Umm kwa manufaa yake binafsi na chama chake.

Tungekuelewa kama ungetuambia kuwa fedha zimetokana na fine kubwa waliotozwa Viongozi wa Chadema na Mahakama. Ama zilizotokana na Pre bargain kati ya DPP na Watuhumiwa waliobambikiwa kesi uhujumu uchumi. Ama zile walizoporwa Wafanyabiashara wamiliki halali wa Bureau de Change.

Vp kuhusu Shirika la Habari TBC linalotumiwa na Mgombea wa ccm ni mali ya chama?? Watz siyo vipofu wana macho na wanaona.
 
Hayo mabango yamesambazwa na serikari au na chama?
Ulizeni ruzuku na michngo ya wabunge zililiwa na nani na kwa nini hazikufanya hiyo kazi ya mabango?

Hayo mabango yamesambazwa na Serikali ya CCM.

Huwezi tofautisha kati ya chama dola na vyombo vyake vya dola.
 
Hayo mabango yamesambazwa na serikali ya CCM...............

Huwezi tofautisha kati ya chama dola na vyombo vyake vya dola.........
Kwani miaka ya nyuma mlipokuwa mnaweka mabango mlikuwa na dora au umechanganyikiwa
 
Lini vyama vya upinzani mtajielewa? Nampongeza Maalim Seif Sharif Hamadi, napenda anavyoongea kimkakati na kwa utulivu. Siasa ni hoja lakini hoja inatoka kwa mtu wa aina gani. Maalim Seif nakukubali, wewe umekomaa kifikra waelimishe wenzako wajielewe, waache mawenge.
 
Serikali inayotetea wanyonge haiwezi somesha namba wanyonge, hii ni serikali inayowanyonga wanyonge
 
"CCM itakuwa imepata zaidi ya millioni 100 kwa uraisi tu".

Ukiwa muongo uwe na kumbukumbu CCM kwenye ngazi ya urais iliprint fomu moja tu kwahiyo acha kuahalalisha wizi.
Hizo pesa ni za CCM kwa hiyo matumizim wanaamuwa wao. Kumbuka pesa ya kuchukuwa fomu za kupendekezwa kugombea uraisi, ubunge, na udiwani inaenda kwenye mfuko wa chama. Hii ina maana chama kikiwa na wachukuwa fomu 100, kitaingiza sh millioni mia moja..huo ni uraisi tu.

CCM itakuwa imepata zaidi ya millioni 100 kwa uraisi tu. Chadema huenda millioni 4 n.k. CCM huenda kulikuwa na watia nia 500 au zaidi kwa ubunge, udiwnwani hunenda 2,000. Hizo zote pesa za chama. Ruzuku ya serkali inaenda na uwiano wa wabuinge.

Hii ina maana ccm INA FINANCIAL MUSSLE hata bila vitega uchumi, baada ya CCM inafuatia CHADEMA sema tu CHADEMA financial displine & management yao ni ya ovyo.

Viongozi wakuu wachache wanaiona CHADEMA kama "cash cow" yao na hutumia mbinu mbalimbali za kiizi kuifuja pesa ya chama, tatizo ambalo CCM sasa limepunguwa lakini halijaisha.
 
Back
Top Bottom