Hivi hizi hesabu toka JamiiForums zinaweza kuashiria tabia ya mchangiaji?

Bulldog yuko sahihi! tunapoongelea likes given hapo tunaangalia response za watu na kwa mtazamo wangu wote wenye likes given kidogo na kwa kuzingatia post zake hapo unapata jibu kwamba huyo mtu ni mchoyo au kinyume chake.

Mkuu, awali ya yote shukran kwa umakini mkubwa katika kuweka mada na mawazo yako. Kilicholeta msukumo wa kuanzisha mada mama ni kuwa nikikuta mtu ana postings 40,000, kisha ana Likes 850 huwa nachukulia kuwa huyu ni wale wanaoandika "ngoja waje...", "nimepotea...", "duh..." nk kifupi ni kuwa uzito wa mchango wake kama mtoa mada across hizo threads ni mdogo sana. Mimi namuona huyu kama mtu ambaye SIO SERIOUS hata kwenye mada nyeti. Namuona kama uwezo wake wa kupekua mambo na kuyaweka ili wengine wanufaike ni mdogo sana. Kifupi huyu ni Kilaza wa kutupa. Kisha napokuta mtu haswa mwenye ku-post mara nyingi na kusifiwa na kusomba Likes za watu across JF in thousands (mfano 19,000 likes) eti yeye ana Likes given 644, huwa naona huyu jamaa ni mbinafsi na hajali watu wengine na yuko pre-occupied na kutaka sifa. Singependa awe jirani yangu. Sitataja IDs lakini tembeleeni pages za vinara wa postings na kusomba likes za watu wakati mwingine kwa kigezo kuwa ni watetezi wa umma au makundi fulani kisha mfanye malinganisho. Wengi sio wenye hata kurudisha hisani kwa kuwatunuku mashabiki wao "likes". Hawa nawahisi kama watu wachoyo wapenda sifa na singependa wawe jirani zangu.

Lakini wapo wachangiaji ukipima Likes walizopewa na walizotoa unakuta ratio ya > 0.8, mfano rahisi ni kama kina Mamndenyi, Mkuu wa chuo, FaizaFoxy, na hata wewe mwenyewe wote wana ratio hadi 1.2 and above. Hawa nawaona kama ni watu kareem sana ambao ningependa sana wawe majirani zangu.

Njemba yoyote yenye ratio < 0.2 kama ni jirani itanifanya nijenge fence mapema (not really hahahahah).

In essence hii ndio spirit ya mada. Dada Mamndenyi, nina ushahidi wa ukarimu wako kwa hiyo huenda kigezo cha Likes Given/Received kipo sahihi.
 
Wickama jionee mwenyewe ulivyokuwa kauzu:

Join Date : 8th March 2009
Location : Donge, Tanga Mjini
Posts : 854
Rep Power : 4037
Likes Received 639
Likes Given 639

Hata mkuu wa kaya alisema ukitaka kula ni lazima na wewe uliwe.

Haki ya Mungu, Mamndenyi, umenichekesha kupita maelezo. Ila bwana nashukuru hata kunipa rank ya kitoweo maarufu kutoka the World's longest lake na Africa's deepest. Angalau nina value mezani pa mwenyeji. Pia ahsante sana kunijuza masuala ya "escrow". Shukran
 
Last edited by a moderator:

Nimekusoma.

hapo "ngoja waje" na "duh" pamenifurahisha sana. wengine husema "napita tu"

kiukweli hiyo ni element ya kilaza.
 
Nimekupata mkuu, ila nilichokuwa namaanisha kwa maana nyingine, mtu mmoja hawezi kutoa likes 2 kwa post moja, lakini mtu mmoja mwenye rep power kubwa akitoa rep power ina effect zaidi hata ya watu 100 wenye rep power ndogo... kwa hiyo kiwango cha kutoa likes kipo sawa kwa watu wote, tofauti na kiwango cha rep power... katika kutoa...
 

Kutotoa likes ni kujisahau, mimi ni mmoja wao. Najikuta napita tu na muda mwingi natumia app ya simu kwenye surfing.
 

Ndo tulivyoumbwa mkuu, wewe shukuru Mungu upo tofauti.
 

Safi sana mkuu. Mimi naona bora MMU kuliko chit chat au celebrity
 


Mkuu Wickama

Si Kweli Kwamba mwenye likes nyingi ndo anayetoa hoja za msingi sikubaliani kabisa na hilo. Kuna sababu kadhaa zinazofanya baadhi ya watu kuwa na likes nyingi nazo ni:

1.UMAARUFU
Umaarufu wa mimi bampami huwezi kuufananisha na wa dadaa Evelyn Salt, FaizaFoxy, MWANAKIjiji au mshana jr n.k Hao wakipost kitu lazima watapata likes nyingi kutokana na umaarufu wao.

2. USHABIKI
Kuna watu hutoa likes kiushabiki shabiki mfano hoja zinazohusiana na mapenzi hata kama hazina mantiki utaona watu wakikoment sana na kutoa likes. Sasa nenda kwenye nafasi za kazi umwone mtu anaomba msaada apate kazi uone kama atapata likes au replied nyingi.(mfano tu nimetoa)

3. (Ongezea kama umenielewa nlichokuwa nadefend)
 
Last edited by a moderator:
Sometimes likes hazitokani sana na point bali umepost nini,umechangia nini nanani ana mtazamo upi katika hicho ulichopost au kuchangia, lakini vilevile kuna wakati inabidi uwe mtu wa kiasi kwakuwa hujui nani ni nani kwasababu ya ID zetu, kuna watu walishawahi kunyambuana sana hapa jamvini halafu coicedence ikawakutanisha msibani kumbe ni ndugu kabisa, ishu kwamba walifahamianaje ni baada ya kila mmoja kuripoti msiba uje hapa jamvini
 
Kutotoa likes ni kujisahau, mimi ni mmoja wao. Najikuta napita tu na muda mwingi natumia app ya simu kwenye surfing.

Nimeona kwenye notification yako LIKES ulizopokea ni nyingi mno zaidi ya kiduchu ulizotoa, Download JF APP itakuwa kutoa LIKES ni kama kumsukuma mlevi unabofya tu
 
Nimeona kwenye notification yako LIKES ulizopokea ni nyingi mno zaidi ya kiduchu ulizotoa, Download JF APP itakuwa kutoa LIKES ni kama kumsukuma mlevi unabofya tu

Sawa mkuu, nitafanya hivyo
 
Kutotoa likes ni kujisahau, mimi ni mmoja wao. Najikuta napita tu na muda mwingi natumia app ya simu kwenye surfing.

Thank you for your concern. You may not be alone in a similar saga
 
Nimeona kwenye notification yako LIKES ulizopokea ni nyingi mno zaidi ya kiduchu ulizotoa, Download JF APP itakuwa kutoa LIKES ni kama kumsukuma mlevi unabofya tu

Mkuu mshana jr, hapo kwenye LIKEs nyingi za kupokea dhidi ya chache za kutoa ndipo nauliza jee panaweza kuashiria kuwa mtoa Likes Kiduchu huku kapokea nyingi kutoka kwa watu wengine kama ni bahili au mbinafsi? Hii ni ukiondoa sababu kama aliyotaja Bulldog, ya kujisahau?

Kwa mfano, nikigawa Likes given/Likes received zako napata ratio ya 0.955, kwangu mimi nakuhesabu kama mtu kareem sana ambaye ni mwepesi kurudisha hisani. Jee mwenye ratio ya 0.12 utamhesabu vipi?

cc bampami,
 
Last edited by a moderator:
Binafsi MTU akitoa just a simple fact katika jambo lolote hata LA kidini bila kujali liko opposite na imani yangu sio lazima nichangie. Natoa Like... Nasepa.
Mi sio mvivu kutoa like.

Manake kuna wakati nasoma idea ya MTU naisave jinsi alivyo jenga hoja. Hadi nacheka sometimes.
 

Mi ningependa nijikite hapo kwenye kutoa kiduchu, unajua mwanzoni hata mimi nilikuwa na hilo tatizo la kutoa likes hata rep power nilikuwa naona shida kweli kwasababu nilikuwa naipata JF kupitia browser mpaka siku moja memba mmoja akanisema

Sikutakata kuonana mjuaji nikajieleza tatizo langu nikasaidika, nikadownload JF APP, nakumbuka siku ya kwanza niligawa LIKES kama nagawa shekeli za eskoro

Lakini vilevile kuna watu wako arrogant, wanajiona wao ndio wao post zao ndio zimesheheni maarifa, hekima na elimu na za watu wengine ni za kijinga, kipuuzi au kitoto kwahiyo hazistahili likes, bali zake pekee ndio zinastahili kupata likes nyingi

Zaidi kuna watu wana rohombaya na choyo, kuipata LIKE yake mpaka umfurahishe hasa bila kujali ulichopost/changia kina mantiki au LA.....na wengine ni roho ya kwanini...!!! Yani kwanini nimpe Fulani LIKE yangu

Mwisho kwasababu nyingine zozote zile kuna watu wao macho yao yote yako kwenye NOTIFICATION BAR, nani ana LIKES NGAPI je kanizidi mimi ngapi, Huyo hupati yake ng'oti
 
Last edited by a moderator:
Lakini vilevile kuna watu wako arrogant, wanajiona wao ndio wao post zao ndio zimesheheni maarifa, hekima na elimu na za watu wengine ni za kijinga, kipuuzi au kitoto kwahiyo hazistahili likes, bali zake pekee ndio zinastahili kupata likes nyingi
mshana jr, nakuunga mkono sana kwenye uchambuzi huu. Mwenye muda atembelee baadhi ya pages za vinara wa kupost (kuwa wanatetea makundi au jamii fulani) au kujibizana na wana JF kwa niaba ya mwenzao. Tumia vigezo vya LIKEs GIVEN/LIKES RECIEVED you will be shocked. Kifupi ni kuwa wengi ni wabahili wa kuwapa wenzao hata "Likes".
 
Last edited by a moderator:

Mkuu kuna issue pia ya timing mtu umejiunga lini? kuna watu wakongwe humu 2007 so mchezo kwa kweli.
 
Mkuu kuna issue pia ya timing mtu umejiunga lini? kuna watu wakongwe humu 2007 so mchezo kwa kweli.

Umesema kweli. Hebu jaribisha kigezo cha Likes Given/Likes received. Kama ni mbahili/mchoyo pia utamgundua no matter alijiunga lini. Yupo mkongwe wa 2008, Likes received 4000 na ushee, likes given hazifiki 250, hii njemba ni bahili/mbinafsi hata kama inaandika lulu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…