Duuu[emoji15] [emoji15] [emoji15] naomba asiniote kuna binti kafukuzwa kwao kijijini ni binti mdogo akiamka anasema fulani atakufa aipiti muda mwanakijiji anakufa mwisho wa siku alimtabiria mama yake ugonjwa uponi utakufa mama yake aikufika muda akafariki bibi na wajomba wakamfukuza akaja dar na kufanya kazi za ndani niliwai kuwa mdada wangu wakazi nilimuulizaga kisa cha kuja dar ndio akaniadithia nilifikiliaga mchawi kumbe Ni nguvu hii
Siwez sema ni uchawi ama sio uchawi.
Ukisoma katika 3:7 Hakika Bwana MUNGU hatafanya neno lolote; bila kuwafunulia watumishi wake manabii siri yake.
Hapa tunaona kuwa Mungu huwa anatujilisha hata mambo ya siri; huwa anafunulia watu wake
Yohana 16:13 Lakini yeye atakapokuja; huyo Roho wa kweli; atawaongoza awatie kwenye kweli yote;
Kwa maana hatanena kwa shauri lake mwenyewe; lakini yote atakayo yasikia atayanena; na mambo yajayo atawapasha habari yake
* hapa tunaona Roho Mtakatifu huwa anatupasha hata mambo yajayo na hanen ya kwake bali yale ya Mungu; ni msaidizi wetu.
Kwa upande wa wa Mungu aliye hai ipo hivyo.
Na Mungu ametupa mamlaka ya kufunga na kufungua. Ukisoma
mathayo 16:18 Nami( Yesu) nakuambia; Wewe ndiwe petro ( weka jina lako); na juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa langu; ( kanisa ni wewe) wala milango ya kuzimu haitalishinda .
19 Nami nimekupa wewe funguo za ufalme wa mbinguni; na lolote utakalolifunga duniani; litakuwa limefungwa mbinguni; na lolote utakalolifungua duniani; litakua limefunguliwa mbinguni.
* tunaona hapo kuwa vita vyetu kanisa yaan wewe kuwa ni zidi ya milango ya kuzima na vyote vinavyofanana hayo.
Tuna mamlaka ya kufungua na kufunga ; tuna mamlaka yote ya kubatilisha mambo mabaya yasitokee ktk ulimwengu wa kimwil .
Sababu mtu unapoota hicho kitu kinakua kimetendeka ktk ulimwengu wa roho; na matokeo ya ulimwengu wa kimwil yanatokana na ulimwengu wa kiroho.
Kwahiyo kama huyo binti angejua mapema kuwa mapema inatakiwa atangue abatilishe alichokiona na afunge huo mlango wa mauti na afungue huo mlango wa afya na uzima; mama yake asingekufa sababu tunayo funguo ya Damu Ya Yesu. Hii ni damu ya agano ambayo pia ni sadaka yaani pasaka wetu angekuwa na mamlaka ya kupaka hiyo damu katika hilo langu la mama yake sababu yeye amefanyika kuhani( kama kaokoka)
Ukisoma isaya 7:7 Bwana MUNGU amesema hivi; Neno hili halitasimama wala halitakua.
* unamamlaka yote yakubatilisha yaliyotokea ktk ulimwengu wa roho ili yasijihidhirishe ktk ulimwengu wa kimwili.
Wao wanaingia kwa damu za watu na wanyama lakin sisi tunaingia kwa kutumia damu ya Yesu.
Ktk kambi ya shetani.
Hata wao wana nguvu hizo hizo za kutabir kitu kikatokea; nacho kisikupe tabu sababu shetan anajua kucopy na kufuatisha vya MUNGU.
Kilichomshinda ni kuishika na ku copy ni Damu ya Yesu sababu ule ni uhai wa Mungu ndani yake.
Ukisoma mwanzo 7: 10 Basi Musa na Haruni wakaingia kwa Farao; wakafanya hivyo kama BWANA alivyo waambia; Haruni akaibwaga fimbo yake chini mbele ya farao; mbele ya watumishi wake ikawa nyoka.
11. Ndipo farao naye akawaita wenye akili na wachawi; na hao waganga wa Misri wakafanya vivyo kwa uganga wao.
13 wakabwaga chini kila mtu fimbo yake nazo zikawa nyoka; lakini Fimbo ya Haruni ikazimeza fimbo zao.
* Hapo unaona hata shetan ana nguvu za kucopy vitu vya MUNGU aliye hai ; lakini mwisho wa siku MUNGU anabaki kuwa mshindi tu.
Haijalishi mtu kaota kitu na kikatokea inategemea anatoka ktk kambi ipi? Ya Mungu au ya shetani?
Matokeo ya hivyo vitu utaviona kwa mtu yeyote yule.
Kama mtumishi anakutabiria halafu kitu kinatokea isikupe tabu; swal ni nguvu ipi anayo tumia ya Mungu ama siyo; kama ya Mungu utajua tu
Sababu lazima utafanya juhud ya kumtafuta Mungu binafsi; na kuomba mwenyewe; na sio kila kitu unamtegemea Mtu unamuabudu kuliko Mungu mwenyewe
Biblia inasema . amelaaniwa yule amtegemeaye mwanadamu;
Amfanya mwanadamu kuwa kinga yake ;Na moyoni mwake amemwacha Bwana ( Yeremia 17:5)
Mungu anataka tumuweke awe wa1 na sio wa mwisho.
Ukishindwa muulize yeye.
Tunahitaji macho ya rohoni zaid na si haya ya nyama.
Inaweza ikawa kuwa huyo bint anatumika na kambi ambayo sio lakin mwenyew hajijui. ( ulimwengu wa roho una vitu vingi sana kuliko tunavyo weza kuhisi sababu kuna vita hapo; kuna malango hapo shetan anataka lango na Mungu aliye hai anataka lango ; sasa inategemea nan kawahi lango ndio maana vita lazima iwepo; lango hilo hilo moja lapitisha kizur na kibaya.
Na kama shetan amekaa ktk hilo lango kwa haki kabisa kupitia huyo binti; Mungu hawez ingilia sababu kuna sheria ktk ulimwengu wa roho.
Ukitaka Mungu aingilie kati. Toba inahitajika ili Mungu amtoe adui kwenye lango ili akae yeye awe dereva; na dereva akiwa Mungu utaona matokeo yake ktk ulimwengu wa mwili.
Kwa imani yangu ni hivyo kwa uchache.